Leo imenibidi niandike kitu hii kutokana na hali halisi ya Tanzania na pengine kuwatatiza wengi kuelewa kwa sababu ya kichwa cha mada hii. Nimetafakari sana hali halisi ya Tanzania na kusema kweli imenishinda hata kumeza kwa sababu nilipokuwa Bongo nilikutana na wafanyabiashara wengi ambao wamekubali matokeo ya hali halisi hivyo kuendesha biashara zao ktk misingi ya kuwa Ufisadi sio tatizo bali uzalishaji ndio tatizo!..
Kwa wenye Mashule, Hospital, Daladala, Bodaboda, maduka, Mahotel, viwanda, mashirka ya kutoa huduma wote hawa wanaelewa wazi kwamba mali zao zinaibiwa na wafanyakazi. Wanaendesha biashara zao wakijua kuna asilimia fulani ya kuibiwa na wafanyakazi walowaajili, hivyo kinachotakiwa ni kuongeza uzalishaji zaidi ili kufidia kiasi kile unachoibiwa na waajiriwa.. Na kibaya zaidi ni kwamba kama huwezi kuvumilia kuibiwa basi huwezi kufanya biashara Tanzania. Hii ndio hali halisi na imekubaliwa na wafanyabiashara wote. Wizi ni utamaduni unaokubalika na hakuna uwajibikaji kutokana na wizi wa ndani..
Kuna rafiki yangu ana Restaurant yeye huibiwa nyama toka ktk friji yake, hivyo hununua kilo 60 akijua kati ya hizo kilo 5 zitaibiwana wafanyakazi, mwingine ana Bar anajua wafanyakazi huingiza pombe zao wakaziuza kabla ya mauzo yake lakini maadam mwisho wa siku wanaleta millioni 1 ya mauzo inatosha. Daladala vile vile dereva hupumzisha gari na akasema leo mauzo mabaya kwa sababu alikamatwa na traffic Polisi wakati haikutokea hivyo.Hii ndio Tanzania yangu..
Kitaifa sasa tunawakuta viongozi wakiiba mabillioni ya fedha pasi kuwajibika kwa sababu mfumo wa utendaji kazi ni ule ule wenye shida la kutoharamisha wizi. Kwa hali yoyote ile serikali itaibiwa kwa sababu wananchi wenyewe wameupitisha wizi kuwa ni ujanja wa kuishi mjini. Ni utamaduni unaokubalika maadam hukamatwi kwa sababu inatakiwa ushahidi wa kumkamata mwizi na nyama mkononi ndio unaweza kumtuhumu mtu na hata kumfikisha mahakamani lakini sii swala la kuhesabu zimeibiwa kilo ngapi kuwa ushahidi wa kuibiwa. Wenyewe wanasema ulomkamata na ngozi ndiye aliyeiba ng'ombe!
Kwa hiyo, katika mazingira haya ya kutatatisha watu wengi sana waanaamini Tatizo la nchi yetu sio UFISADI, huwezi kukomesha wizi wala kuwajibisha watu kama suluhisho isipokuwa ni kuongeza Uzalishaji kufidia kiwango cha wizi ili faida unayokusudia ipatikane ktk ujenzi wa Taifa letu. Tumeibiwa sana toka ubinafsishaji wa viwanfda na mashirika, uuzaji wa nyumba za serikali, mikataba ya uwekezaji toka IPTL, Rada, Madini na kadhalika. Wahusika wa wizi na ufisadi huu hawaonekani kuwa na makosa kutokana na utamaduni wetu wa kutojali mwizi ambaye hana ngozi .. Sasa kilichobakia ni Ardhi maana tumesha ibiwa kote na hali ya uchumi wetu unazidi kudumaa na kuwa sugu - Wanasema ati ili tuendelee nguvu na juhudi kubwa zaidi inatakiwa kulijaza pakacha linalovuja!
Je, kuna ukweli kwamba uchumi wetu umedumaa kwa sababu - Ufisadi sio tatizo bali tatizo ni Uzalishaji mdogo?
Kwa wenye Mashule, Hospital, Daladala, Bodaboda, maduka, Mahotel, viwanda, mashirka ya kutoa huduma wote hawa wanaelewa wazi kwamba mali zao zinaibiwa na wafanyakazi. Wanaendesha biashara zao wakijua kuna asilimia fulani ya kuibiwa na wafanyakazi walowaajili, hivyo kinachotakiwa ni kuongeza uzalishaji zaidi ili kufidia kiasi kile unachoibiwa na waajiriwa.. Na kibaya zaidi ni kwamba kama huwezi kuvumilia kuibiwa basi huwezi kufanya biashara Tanzania. Hii ndio hali halisi na imekubaliwa na wafanyabiashara wote. Wizi ni utamaduni unaokubalika na hakuna uwajibikaji kutokana na wizi wa ndani..
Kuna rafiki yangu ana Restaurant yeye huibiwa nyama toka ktk friji yake, hivyo hununua kilo 60 akijua kati ya hizo kilo 5 zitaibiwana wafanyakazi, mwingine ana Bar anajua wafanyakazi huingiza pombe zao wakaziuza kabla ya mauzo yake lakini maadam mwisho wa siku wanaleta millioni 1 ya mauzo inatosha. Daladala vile vile dereva hupumzisha gari na akasema leo mauzo mabaya kwa sababu alikamatwa na traffic Polisi wakati haikutokea hivyo.Hii ndio Tanzania yangu..
Kitaifa sasa tunawakuta viongozi wakiiba mabillioni ya fedha pasi kuwajibika kwa sababu mfumo wa utendaji kazi ni ule ule wenye shida la kutoharamisha wizi. Kwa hali yoyote ile serikali itaibiwa kwa sababu wananchi wenyewe wameupitisha wizi kuwa ni ujanja wa kuishi mjini. Ni utamaduni unaokubalika maadam hukamatwi kwa sababu inatakiwa ushahidi wa kumkamata mwizi na nyama mkononi ndio unaweza kumtuhumu mtu na hata kumfikisha mahakamani lakini sii swala la kuhesabu zimeibiwa kilo ngapi kuwa ushahidi wa kuibiwa. Wenyewe wanasema ulomkamata na ngozi ndiye aliyeiba ng'ombe!
Kwa hiyo, katika mazingira haya ya kutatatisha watu wengi sana waanaamini Tatizo la nchi yetu sio UFISADI, huwezi kukomesha wizi wala kuwajibisha watu kama suluhisho isipokuwa ni kuongeza Uzalishaji kufidia kiwango cha wizi ili faida unayokusudia ipatikane ktk ujenzi wa Taifa letu. Tumeibiwa sana toka ubinafsishaji wa viwanfda na mashirika, uuzaji wa nyumba za serikali, mikataba ya uwekezaji toka IPTL, Rada, Madini na kadhalika. Wahusika wa wizi na ufisadi huu hawaonekani kuwa na makosa kutokana na utamaduni wetu wa kutojali mwizi ambaye hana ngozi .. Sasa kilichobakia ni Ardhi maana tumesha ibiwa kote na hali ya uchumi wetu unazidi kudumaa na kuwa sugu - Wanasema ati ili tuendelee nguvu na juhudi kubwa zaidi inatakiwa kulijaza pakacha linalovuja!
Je, kuna ukweli kwamba uchumi wetu umedumaa kwa sababu - Ufisadi sio tatizo bali tatizo ni Uzalishaji mdogo?