MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Waungwana,
Kuna mtu fulani aliniambia yafuatayo kuhusu mashindano ya ulimbwende ya Miss Tanzania.
1) Mashindano haya yanapokaribia kufikia hatua za mwisho yaani kabla ya kuingia Kambi Kuu, picha za walimbwende hao ambazo huwa zimepigwa katika hatua mbali mbali, hukusanywa na kuwekwa kwenye kitabu (catalogue) ambacho hutumwa kwa njia ya mtandao (Internet) kwa wateja ambao wako nje ya nchi.
2) Wateja hawa, kwa kiwango kikubwa, ni wazungu wenye uchu wa kuja kustarehe na hawa dada zetu, kwa malipo ya bei mbaya, ambayo huwa yanalipwa kabla ya wateja hawa kuingia nchini, wakiwa tayari wamekwishafanya "booking" ya kuchagua walimbwende watakaostarehe nao, wakati wakiwa "kambini" hoteli ya White Sands (ila mwaka jana, kama sikosei, kambi ilikuwa Paradise Resort ya Bagamoyo... ile iliyoungua/iliyounguzwa/iliyochomwa moto.....)
3) Wengi wa walimbwende ambao hulazimishwa (na hapa tunazungumzia suala la human trafficking au sexual slavery) kufanya vitendo vya ngono na wateja hawa kutoka ughaibuni pasi na wao kujipatia hata senti moja. Kila mshiriki anayeingia kwenye hatua hii ya mwisho hula kiapo cha kutotoa siri ya nini kinachotokea wakiwa "kambini", huku wakitishwa kama, iwapo watatoa siri, madhara makubwa yanaweza kuwafikia. Jambo hili limefanya ushahidi wa kina kuhusu ufisadi ngono huu kutopatikana, kwa kuwa, mpaka leo, hakuna mlimbwende hata mmoja aliyeweza kupata ujasiri wa kujitokeza na kuelezea yanayotokea.
Mimi ninauliza,
1) Kama haya ni kweli, je, kuna faida gani ya dada zetu kushiriki kwenye mashindano haya ambayo yanaonekana kuwa kichocheo cha maambukizi ya UKIMWI pamoja na magonjwa mengine ya zinaa?
2) Kama haya ni kweli, ile Sheria ya Sexual Offences Special Provisions Act (SOSPA) ya mwaka 2002, inafanya nini, isiwabane hao wanaoendesha ufisadi ngono huu?
Mtu aliyenieleza taarifa hizi (ni msiri, kwa kanuni ya uandishi wa habari siwezi kumtaja na sitamtaja... hata nikipelekwa jela) aliniambia kwamba, mawakala wa ngazi ya mikoa na kanda huwa wanashirikishwa kuendesha "minada ya siri" ambapo watu wanaotaka dada zetu hawa waweze kufikishwa "kambi kuu" huwa wanaendesha mnada huo kwa njia ya SMS, ambapo huwa wanawapigia kura washiriki wanaowataka "washinde" na kufikia ngazi ya "kumi bora", ili wakifika kwenye kambi kuu waweze kupatikana kwa ajili ya wateja hao kutoka ughaibuni. Kimsingi, biashara hii chafu inatambulika kwa jina la "sex tourism" lakini jina halali kabisa ni "sex slavery" au "human trafficking".
Wana JF, nawaombeni mchango wenu:
1) Nini kifanyike?
2) Nani abanwe?
3) Hatua gani za kisheria zifanyike?
Lakini kabla hamjafikia uamuzi wowote, jaribuni kufanya tathmini iwapo mashindano haya (zaidi ya "kuwaharibu" dada zetu kama akina Irene Uwoya na Wema Sepetu, kwa mfano.... najua hapa nitaulizwa "wameharibiwa" kwa namna gani... jibu mnalo!) yameleta mchango wa aina gani kwenye jamii ya Watanzania. Binafsi, mchango mkubwa ninaouona ni kwamba yamechangia kwa kiwango kikubwa katika kuporomoka kwa maadili ya Kitanzania. Hapo awali, kabla ya Miss Tanzania kuanza kuendeshwa, ilikuwa nadra sana kuweza kuyaona mapaja au sehemu kubwa ya miili/maungo ya akina dada zetu hawa, zikiwa wazi bila kufunikwa. Kile kipengele cha "vazi la ufukweni" (Je, ni msichana gani wa Kitanzania huwa anavaa mavazi kama yale akiwa "ufukweni"?) kimekuwa kisingizio cha kuwatembeza nusu uchi akina dada zetu.
Nadhani imetosha sasa. Natoa hoja: MISS TANZANIA IFUTWE! TOO MUCH DAMAGE HAS BEEN DONE.
Wenye kuunga mkono waseme NDIO na wasiounga mkono waseme HAPANA.
./Mwana wa Haki
Kuna mtu fulani aliniambia yafuatayo kuhusu mashindano ya ulimbwende ya Miss Tanzania.
1) Mashindano haya yanapokaribia kufikia hatua za mwisho yaani kabla ya kuingia Kambi Kuu, picha za walimbwende hao ambazo huwa zimepigwa katika hatua mbali mbali, hukusanywa na kuwekwa kwenye kitabu (catalogue) ambacho hutumwa kwa njia ya mtandao (Internet) kwa wateja ambao wako nje ya nchi.
2) Wateja hawa, kwa kiwango kikubwa, ni wazungu wenye uchu wa kuja kustarehe na hawa dada zetu, kwa malipo ya bei mbaya, ambayo huwa yanalipwa kabla ya wateja hawa kuingia nchini, wakiwa tayari wamekwishafanya "booking" ya kuchagua walimbwende watakaostarehe nao, wakati wakiwa "kambini" hoteli ya White Sands (ila mwaka jana, kama sikosei, kambi ilikuwa Paradise Resort ya Bagamoyo... ile iliyoungua/iliyounguzwa/iliyochomwa moto.....)
3) Wengi wa walimbwende ambao hulazimishwa (na hapa tunazungumzia suala la human trafficking au sexual slavery) kufanya vitendo vya ngono na wateja hawa kutoka ughaibuni pasi na wao kujipatia hata senti moja. Kila mshiriki anayeingia kwenye hatua hii ya mwisho hula kiapo cha kutotoa siri ya nini kinachotokea wakiwa "kambini", huku wakitishwa kama, iwapo watatoa siri, madhara makubwa yanaweza kuwafikia. Jambo hili limefanya ushahidi wa kina kuhusu ufisadi ngono huu kutopatikana, kwa kuwa, mpaka leo, hakuna mlimbwende hata mmoja aliyeweza kupata ujasiri wa kujitokeza na kuelezea yanayotokea.
Mimi ninauliza,
1) Kama haya ni kweli, je, kuna faida gani ya dada zetu kushiriki kwenye mashindano haya ambayo yanaonekana kuwa kichocheo cha maambukizi ya UKIMWI pamoja na magonjwa mengine ya zinaa?
2) Kama haya ni kweli, ile Sheria ya Sexual Offences Special Provisions Act (SOSPA) ya mwaka 2002, inafanya nini, isiwabane hao wanaoendesha ufisadi ngono huu?
Mtu aliyenieleza taarifa hizi (ni msiri, kwa kanuni ya uandishi wa habari siwezi kumtaja na sitamtaja... hata nikipelekwa jela) aliniambia kwamba, mawakala wa ngazi ya mikoa na kanda huwa wanashirikishwa kuendesha "minada ya siri" ambapo watu wanaotaka dada zetu hawa waweze kufikishwa "kambi kuu" huwa wanaendesha mnada huo kwa njia ya SMS, ambapo huwa wanawapigia kura washiriki wanaowataka "washinde" na kufikia ngazi ya "kumi bora", ili wakifika kwenye kambi kuu waweze kupatikana kwa ajili ya wateja hao kutoka ughaibuni. Kimsingi, biashara hii chafu inatambulika kwa jina la "sex tourism" lakini jina halali kabisa ni "sex slavery" au "human trafficking".
Wana JF, nawaombeni mchango wenu:
1) Nini kifanyike?
2) Nani abanwe?
3) Hatua gani za kisheria zifanyike?
Lakini kabla hamjafikia uamuzi wowote, jaribuni kufanya tathmini iwapo mashindano haya (zaidi ya "kuwaharibu" dada zetu kama akina Irene Uwoya na Wema Sepetu, kwa mfano.... najua hapa nitaulizwa "wameharibiwa" kwa namna gani... jibu mnalo!) yameleta mchango wa aina gani kwenye jamii ya Watanzania. Binafsi, mchango mkubwa ninaouona ni kwamba yamechangia kwa kiwango kikubwa katika kuporomoka kwa maadili ya Kitanzania. Hapo awali, kabla ya Miss Tanzania kuanza kuendeshwa, ilikuwa nadra sana kuweza kuyaona mapaja au sehemu kubwa ya miili/maungo ya akina dada zetu hawa, zikiwa wazi bila kufunikwa. Kile kipengele cha "vazi la ufukweni" (Je, ni msichana gani wa Kitanzania huwa anavaa mavazi kama yale akiwa "ufukweni"?) kimekuwa kisingizio cha kuwatembeza nusu uchi akina dada zetu.
Nadhani imetosha sasa. Natoa hoja: MISS TANZANIA IFUTWE! TOO MUCH DAMAGE HAS BEEN DONE.
Wenye kuunga mkono waseme NDIO na wasiounga mkono waseme HAPANA.
./Mwana wa Haki