Ufisadi mwingine wa kutisha serkalini

Mawenzi

JF-Expert Member
Sep 21, 2010
1,251
345
Kama mjuavyo wanaJF, Nane Nane mwaka inafanyika Dom kitaifa. Hata mwaka jana na mwaka juzi ilifanyika hapahapa. Nia ya maonyesho haya ni kujaribu kukuza kilimo kwa wakulima kuonyesha walimacho/waffugacho. Na pia wafugaji/wakulima wanabadilishana mawazo/ujuzi. Makampuni na maduka yanayojishughulisha na haya mambo yapata fursa ya kutangaza/kuuza bidhaa zao. maonyesho haya yako chini ya wwizara zinazojishughulisha na kilimo/ufugaji/uvuvi.

Sasa cha kushangaza ni kwamba serkali yote sasa hivi imehamia Dom. Hata wizara zisizojishughulisha na sekta hizi zipo hapa. kila wizara inawakilishwa na wafanyakazi wengi walioshonewa uniform/suit za bei mbaya. Ukichukulia kuwa wizara zote na watu wengi ziko Dom kwenye bunge, basi ni dhahiri kuwa pesa inayotumika kuwaweka watu hawa hapa Dom ni nyingi sana.

Hivi wizara zifuatazo zina uhusiano gani na kilimo/ufugaji/uvuvi kiasi cha kuhusika kwenye maonyesho haya: Ofisi ya Rais, Waziri Mkuu, Mambo ya Ndani, Afya, Jinsia na Watoto, Kazi, Ulinzi, -----------------, etc,etc???

Kwa mtazamo wangu, huu ni ufisadi mkubwa sana unaofanywa wazi wazi.

Nawasilisha
 
Duh! Mkuu soma kwanza majukumu ya Wizara ulizotaja ili uboreshe hoja yako.
 
mimi nilifungua thread kwa hamu kubwa kuona kilichopo!kumbe ni yale tuliyoyazoea!siku hz ndio deal lililobakia kumalizia mafungu ya budget.
 
Back
Top Bottom