Ufisadi mkubwa wakithiri halmashauri ya kigoma vijijini

BRUCE LEE

JF-Expert Member
Dec 11, 2010
2,096
1,332
Habari za kazi na weekend ndugu zangu wana jamvi, kuna habari zakusikitisha sana kutoka katika vyanzo vinavyoaminika katika halmashauri hii ya kigoma, kiukweli halmashauri hii imekua ikitumika kama mradi wa vigogo kujipatia pesa za umma kwa maslahi yao binafsi, miradi mbalimbali ambayo inafadhiliwa na nchi mbalimbali imekua inaishia njiani na pesa zimekua zinaishia mifukoni mwa wakubwa hao, ifuatayo ni listi ya vinara wa ufisadi katika halmashauri hiyo
1. John Mongella bwana huyu amekua anatumia madaraka yake vibaya kuwanyanyasa wafanya kazi na pia yeye ndie mkuu wa wilaya na pia anashirikiana na baadhi ya vigogo kuhakikisha azma yao ya wizi wa rasilimali za taifa letu inakamilika.
DC huyu amekua akishirikiana na Charles Lembo ambae ni mratibu wa pembejeo na mbolea za ruzuku wilaya.. ndugu zangu watu hawa wamekua wakichakachua vocha za mbolea hiyo kwa muda mrefu na wamekuwa wakijipatia mamilioni ya shilingi. chakusikitisha takukuru habari hizi wanazijua lakini wamekua kimya muda mrefu na inaonekana huyu Mongela anaogopwa na pia ni mshirika wao.

kusema kweli mtu huyu ni kikwazo kwa maendeleo ya mkoa huo na hayo yote yanatokana na utawala mbaya wa kutowachagua viongozi waadilifu, watu wamekua wakimuogopa sana eti kisa katoka ukerewe na pia ana udugu na vigogo wakubwa serikalini.

2.Wambura huyu ni district treasurer mtu huyu nae ni mchakachuaji mkubwa pesa mbalimbali za umma na amekua mara kazaa akitaka mgao wa malipo ya vocha zilizo chakachuliwa na pia ni mnyanyasaji mkubwa hasa wa watumishi wenye vyeo vidogo.

3.Deogratius Sowoki huyu ni afisa elimu watu wazima, kwanza ana kashfa ya kuathirika na ukimwi pia ni mnyanyasaji sana wa kijinsia amekua akiwatumia wafanyakazi wenzake hasa walimu kingono pindi wanapohitaji huduma kutoka kwake, kiukweli watu wamekaa kimya na wengi hawana sauti ya kuongea ukweli dhidi ya mtu huyu pia amekua akichakachua hata pesa za marupurupu mbalimbali ya walimu kwa maslahi yake binafsi mpaka sasa amekwisha nunua gari aina ya noah na amefungua bar kubwa wakati hana biashara ya aina yoyote na thamani ya mali yake haiendani sambamba na mshahara wake.
4.Adam Abeid Misana. huyu ni district community development officer. bwana huyu amekua akitumia pesa za waathirika wa ukimwi ambazo zimekua zikitolewa na tacaids kwa ajili ya kuboresha hali ya maisha ya waathirika pamoja na kuwapatia huduma zingine za muhimu,ki ukweli pesa nyingi na miradi mingi ya waathirika haifanywi ipasavyo na pesa hizo zimekuwa zinaliwa vibaya na mtu huyu pamoja na washirika wake.
amekua na utamaduni wa kuwatishia maisha watu wanaomuhoji kuhusu matendo yake na pia ni mshirikina sana na amekua anatumia nguvu za giza kuwapumbaza watu na kuwatishia, amekua karibu sana na mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya anapenda kujipendekeza sana kwa wakubwa na kula nao pia anapenda sana madaraka.
5.kizenga ambae ni afisa ugavi huyu bwana ni mchakachuaji mkubwa wa tenda zinazo tolewa na amekua na tabia ya kuuza tenda hizo kwa watu anaowafahamu yeye ili apate cha juu na pia wengi wa watu hao hawana sifa wala kampuni za kufanyia kazi bali wamekua wakiazima kampuni za wengine ili kukamilisha kazi hizo pesa zinazotolewa haiendani sambamba na huduma za tenda hizo na hali hii inaodhoofisha maendeleo katika mkoa huu.
6 kamwela huyu ni afisa kilimo wa wilaya (daldo) huyu bwana amekua anaiba pesa nyingi sana za miradi ya dasip na dadip miradi hiyo inafadhiliwa na africa delevelopment bank na wahisani wengine na pesa pesa zote zimekuwa zikiishia mifukoni mwao.
kwa kifupi hawa ni wachache kati ya mafisadi wengi waliopo katika halmashauri hii tunaitaka serikali kwa kutumia tume ya maadili iwachunguze watu hawa pia tunawataka wabunge wa kigoma hasa zitto kabwe na kafulila pamoja na madiwani wafuatilie mambo hayo kwa umakini kama hawaoni sisi tuanaona na hatutaki habari za malimbano bungeni bali tunataka tuone utendaji wao katika kufuatilia maslahi ya watu waliowatuma kuwawakilisha bungeni.

asanteni sana tafadhali naomba kuwasilisha.
6.
 
Takukuru ni sehemu ya Vigogo kuwaweka watoto wao wasio na sifa ili wapate ajira. Kuna jamaa yangu nilisoma nae ni kilaza sana na form 6 alitoka na 0 sasa hivi yupo TAKUKURU Kigoma. nimegundua kitu kingine vigogo wengi wamewaficha watoto zao waliofeli kwenye mashirika mbalimbali yaliyopo Kigoma kwa sababu ni pembezoni mwa Nchi. Mtoto wa mheshimiwa John ane chill kwenye Gat. yupo PSPF Kigoma na wengine wengi tu wapo TRA na CRDB. Poleni sana wana Kigoma
JK aliwaahidi kua atigeuza Kigoma iwe kama DUBAI endeleeni kusubiria
 
Takukuru ni sehemu ya Vigogo kuwaweka watoto wao wasio na sifa ili wapate ajira. Kuna jamaa yangu nilisoma nae ni kilaza sana na form 6 alitoka na 0 sasa hivi yupo TAKUKURU Kigoma. nimegundua kitu kingine vigogo wengi wamewaficha watoto zao waliofeli kwenye mashirika mbalimbali yaliyopo Kigoma kwa sababu ni pembezoni mwa Nchi. Mtoto wa mheshimiwa John ane chill kwenye Gat. yupo PSPF Kigoma na wengine wengi tu wapo TRA na CRDB. Poleni sana wana Kigoma
JK aliwaahidi kua atigeuza Kigoma iwe kama DUBAI endeleeni kusubiria

Jamani hizi ahadi nyingine zina walakini.
 
Una mwandiko mbaya sana bana,hata mwalimu wako nadhani alikua ana kukosesha tu ingawa unaandika ya maana
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom