Ufisadi Halmashauri Ya Wilaya Karagwe -jembe La Mkono Km 30

Kamakabuzi

JF-Expert Member
Dec 3, 2007
2,861
1,302
Juzi juzi nilikuwa matembezini katika wilaya ya Karagwe. Kilichonishangaza ni kukuta barabara kati ya makao makuu ya wilaya na tarafa moja ya nyabionza, umbali wa zaidi ya km 30, inatengenezwa kwa jembe la mkono. Hivi kweli uhalali uko wapi. Je ina maana fedha zilizotolewa hazitoshi kutumia catepillar?

Kioja hicho kinazidi unapokuta watengenezaji wanalima nyasi za pembeni mwa barabara na kuzifukia kwenye mashimo yaliyo katikati ya barabara. Matokeo yake yakipita magari mawili, shimo linarudi palepale, lakini mhusika ameshatengeneza!
Pia utakuta halitengenezwi tuta la barabara kiasi cha kuwezesha maji ya mvua yatiririke kwenda pemebeni, hivyo mvua ikinyesha maji huzoa tena hata huo udongo kidogo waliouweka kwa jembe la mkono, mfano mzuri ni sehemu inayoitwa Bigoro.

Kuna siku wananchi waliona gari la Tanroads mkoa wa Kagera, wakajisemea moyoni kuwa sasa huyu mkandarasi atakoma maana wenye barabara wameona upuuzi anaoufanya - lakini wapi - anaendelea vilevile.

Naendelea kutafuta kiasi cha fedha kilichotengwa kwa barabara hiyo, ila kwa vile nilikuwa nimeenda kutembea huko, inakuwa vigumu. Wana JF kama kuna anayeweza kukipata kwa haraka, atujulishe.
 
Juzi juzi nilikuwa matembezini katika wilaya ya Karagwe. Kilichonishangaza ni kukuta barabara kati ya makao makuu ya wilaya na tarafa moja ya nyabionza, umbali wa zaidi ya km 30, inatengenezwa kwa jembe la mkono. Hivi kweli uhalali uko wapi. Je ina maana fedha zilizotolewa hazitoshi kutumia catepillar?

Kioja hicho kinazidi unapokuta watengenezaji wanalima nyasi za pembeni mwa barabara na kuzifukia kwenye mashimo yaliyo katikati ya barabara. Matokeo yake yakipita magari mawili, shimo linarudi palepale, lakini mhusika ameshatengeneza!
Pia utakuta halitengenezwi tuta la barabara kiasi cha kuwezesha maji ya mvua yatiririke kwenda pemebeni, hivyo mvua ikinyesha maji huzoa tena hata huo udongo kidogo waliouweka kwa jembe la mkono, mfano mzuri ni sehemu inayoitwa Bigoro.

Kuna siku wananchi waliona gari la Tanroads mkoa wa Kagera, wakajisemea moyoni kuwa sasa huyu mkandarasi atakoma maana wenye barabara wameona upuuzi anaoufanya - lakini wapi - anaendelea vilevile.

Naendelea kutafuta kiasi cha fedha kilichotengwa kwa barabara hiyo, ila kwa vile nilikuwa nimeenda kutembea huko, inakuwa vigumu. Wana JF kama kuna anayeweza kukipata kwa haraka, atujulishe.

Mambo mengine hata yanatia uchungu kuyasoma jamani...
 
Back
Top Bottom