Ufafanuzi wa kilichotokea Uchaguzi Meya Mwanza...

wana JF,
Ilianzia kule Arusha mjini zilipofanyika hila za kuwanunua madiwani na walipogundulika mapema na kuchukuliwa hatua na chama basi CCM kwa kuwatumia viongozi wa halamashauri ya jiji wao ,basi mkurugenzi akaendelea kuwatambua kama madiwani halali ingawa wlikuwa
Tayari walikwishafukuzwa uanachama na inasemekana ccm ndio iliwashauri hata kwenda mahakamani,

Wakati hiyo kama haitoshi ccm kwa kuwatumia watendaji wake ikampokokonya mbunge wa CDM ubunge kwa mbinu za kesi batili,

Na kama vile hiyo haitoshi kwa kuwa uwanja wa NMC arusha uko katikati ya mji wa arusha na unaonekana kwa siku za hivi karibuni kuwa kama CDM SQUARE,CCM wameamuru mkurugenzi wa jiji la arusha ahamishie wamachinga pale ili kudhoofisha mikutano ya CDM kwa kuifanya ikose mahali rasmi pa kufanyia mikutano yake ambapo ni karibu na mji,na hili litaifanya CDM kulazimika kuomba uwanja wa Sheikh amri abeid ambao ni wa mpira na ni rahisi kuwafanyia mbinu chafu za kuwanyima nafasi ya kufanyia mikutano ya CDM pale. Mifano ya hili tumeiona mara kadhaa sehemu mbalimbali nchini hivi karibuni morogoro ikiwa mojawapo.

huko mwanza nako mchezo ni uleule
Kwanza baada ya kuona wamepoteza uongozi wa umeya wa jiji,wametumia mbinu ya kuligawa jiji na kuwa manispaa mbili ambazo ni Nyamagana na ilemela kitendo ambacho kimewagawa madiwani wa CDM katika makundi mawili na kudhoofisha wingi wa kura zao kwenye uchaguzi wa kumpata meya wa jiji.

Pia madiwani waliokuwa wamesimamishwa na CDM wakakimbilia mahakamani na kwa msaada wa ccm wakapewa barua za pingamizi harakaharaka nakurudi kushiriki uchaguzi na bila shaka wakaungana na wale wa CUFna kuipigia ccm kura ya umeya na hatimae kuwapa ushindi ccm.

Bado hiyo haikutosha wakalazimisha diwani aliyerudishwa na mahakama na kuomba agombee umeya CDM,chama kimekatalia lakini mkurugenzi ameahirisha uchaguzi wa ilemela tena kinyemela,

My take: ninauomba uongozi wa CDM mtafakari kwa kina muenendo huu na mchukuwe hatua ya kuwafahamisha wananchi kupitia mikutano ya hadhara pamoja na press comference na pia msisite kununua vipindi katika vyombo vya habari mbalimbali ili taarifa hizi ziwafikie wananchi katika muda muafaka,

Pia ni vema sasa chama kikawa na msemaji mkuu atakayehusika na uelimishaji umma kila linapotokea tukio muhimu basi wanachama na wananchi wapenda demokrasia wapate kujulishwa katika muda muafaka
PEOPLES POWER NEVER GIVE UP,MOVEMENT FOR CHANGE WE TRUST!
 
hii ndio tabu ya kumchukia mtu badala ya mfumo mtaendelea kuumia sana subirini 2015, kikwete anapita tu akija mnayempenda mtarudi CCM.
 
kinachonifurahisha cdm ni kuwa wewe km umechaguliwa kuwa kiongozi wa watu halafu unaleta mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya chama, unapumzishwa. hiyo ndo nidhamu ya chama.

inatujengea uzoefu wa kutovumilia makosa ya mtu once tumechukua nchi uchaguzi ujao. hizi ni challenges na vyama makini vilivyojipanga kuchukua nchi, hukutana na vitu km hivi.
 
ni wakati wa kubadilisha huu utaratibu wa kumpata meya kutoka huu mfumo wa kupigiwa kura na madiwani, iwe meya achaguliwe na wananchi sababu mfumo wa sasa umeweka maslahi ya chama mbele, pia huu mfumo si wa kidemokrasia kwasababu diwani analazimika kumpigia mtu wa chama chake hata kama ni mbovu

Mbaya zaidi chama ili ifanikiwe kushinda umeya inakwenda kuazima kura za madiwani wa chama kingine! Ingelikuwa ni wananchi tusingejua kuwa madiwani wa cuf wamewapigia kura ccm!
 
Nimejiuliza hili swali sina majibu ya uhakika.
CUF na CCM wamekuwa na Umoja usioelezeka kwenye masuala mbalimbali ya Utawala wa Taifa hili. Kimsingi maamuzi yao yamekuwa yakiwa kwenye Jihad kuu ya kupingana na CHADEMA kwa nguvu zote.
Sera za CHADEMA ziko tofauti sana na CUF na CCM. Kitendo cha Vyama hivi viwili CUF na CCM kuungana kwenye Maamuzi Muhimu ya kitaifa inaonyesha mkanganyiko mkubwa kwenye Demokrasia. Haijulikani bado kama CUF ni chama cha Upinzani au ni Chama Dada cha CCM. CUF imeungana na CCM kuipiga vita CHADEMA popote nwenye ngazi mbali mbali.

Nimejiuliza hivi haya wanayofanya ni kwa faida za nani?.

wewe jamaa mbona mjinga sana?
Ujerumani kuna serikali ya mseto, uingereza kuna serikali ya mseto, israel kuna serikali ya mseto, ugiriki kuna serikali ya mseto, lebanon kuna serikali ya mseto, kenya na zimbabwe pia. Sasa unaona ajabu cuf na ccm kuunda serikali zanzibar?

Hebu wacha ushamba huo usikae vichakani kula panzi tu njoo utembee zanzibar uone watu walivyostaarabika ili upunguze fikra potofu.

Punguza ubinafsi, choyo na chuki na utambue tu kua ni sisi wananchi wa zanzibar kupitia njia ya kidemokrasi 64.3% tulipiga kura ya kukubali mfumo wa serikali ya umoja wa kitaifa. Na hata chadema kama wana ubavu wa kupata alau jimbo moja zanzibar nanyi mutashirikishwa. Lkn kwa sasa musitegemee huruma bila ya kufanya kazi.
 
CCM wameshindishwa na mbinu za kisiasa amabzo uhalali wake kisheria linabaki kuwa suala la wanasheria wanaojua taratiu zikoje.

Baada ya mgawanyo wa h/shauri ya jiji na kuwa na h/shauri ya jiji inayoundwa na jimbo la Nyamagana na halmashauri ya ilemela inayondwa na jimbo la ilemela mwezi Julai mwaka huu mgawanyo wa madiwai ulikuwa hivi kwa nyamagana

Chadema -wa kata 5, viti ,maalum 2. mbunge mmoja, jumla wanakuwa 8
CCM - wa kata 6, viti maalum 1 jumla wanakuwa 7
Cuf - wa kata 1, viti maalum 1

Ilemela

Chadema -- wak kata 6, viti maalum 2 mbunge 1 jumla wanakuwa 9
CCM - wa kata 3, viti maalum 2 na mbunge 1 (wa viti maalum) jumla wanakuwa 6
CUF - MBUNGE WA viti maalum 1

Kilchotokea kwenye uchaguzi ni CCM kuhamisha diwani mmoja wa viti maalum (kwa barua ya CCM kwenda kwa mkurugenzi wa jiji ya tarehe 14, Septemba, 2012) na mbunge wa viti maalum toka Ilemela kuja nyamagana na hivyo kuongeza idadi ya kura zao kuwa 9, wakati huo huo Chadema walishakuwa hawaihehabu kura ya Diwani wa Igoma Chagulani ambaye wamemfukuza uanachama akalejeshewa na mahakama wao wanapugukiwa na kura 1 zao zinabaki 7 , aliyepungua Chadema akiwapigia CCM wanakuwa na kura 10 dhid ya 7 za Chadema.

Lakini pia CUF walishakubaliana na chadema kuungana mkono, kwa hiyo kwa kura 2 za CUF Chadema wangekuwa na kura 9, lakini inaonekana ama mwana Chadema mmoja kapigia CCM au CUF mmoja kapigia CCM na kufanya matokeo ya kuwa kuwa 11 kwa CCM dhidi ya nane za Chadema.

Hiyo ndiyo hali halisi ya jinsi mahesau ya kura yalivyochezwa, kama kuna uhalali katika mchakato huo au la ni suala la wataalamu wa masuala haya kutujuza.

Hayo yakiendelea uchaguzi wa Meya wa Ilemela meahirshwa katika mazingira tata, baada ya Mkurugeni kusoma Amri ya Mahakama iliyopewa tafsiri na mwanasheria wa jiji kuwa inakifanya kikao hicho kuahirishwa kwa kuwa Diwani wa Chadema Matata (pia alifukuzwa uanachama pamoja na wa igoma na anaendelea na udiwani kwa amri ya makahama) kuleta pia barua ya kutaka atambuliwe kaa mgombea.

Ukazuka ubishi kidogo juu ya hoja ya mgombea kuteuliwa na chama, mkurugenzi wa jiji akasema hiyo siyo sheria ni mwogozo, na kwa kuwa sheria na mwongozo zikigongana sheria ndiyo inatamalaki hatakia aingie katka mgogoro wa tafsiri ya sheria, akaahirisha kikao bila hata madiwani kujadili hoja hiyo.

Kwa mujibu wa mwanasheria wa wa Chadema, pingamizi hilo lilikuwa linawarejeshea haki yao ya uanachama na hivyo kuendelea na udiwani wao, na kutaka matata asizuiliwe kuendelea na mchakato wa kuomba umeya, Kwa hiyo matata ameomba lakini hakuteuliwa na chama na mahakama haiwezi kuwalazmisha chama wateue mgombea kwa amri ya mahakama, anadhani ni uhuni tu na njama za kisiasa zimefanyika kuahirisha uchaguzi huo.
Nadhani kidogo piacha itaeleweka kwa wanjamvi juu ya nini hasa kimetokea.

SOURCE: Kamnada Deus Bugaywa-Mchambuzi Raia Mwema

Asante sana mkuu. Umenifumbua macho
 
mkuu uko sawa kabisa. Tukubali kabisa kushindwa kwa chadema asilimia kubwa kunachangiwa na chedema wenyewe... Wakati ccm walienda kwa hesabu sisi tulienda kwa huruma kutoka cuf na kwa bahati itokee ccm.!

Na mgogoro wa mwanza haukuanza leo kuchelewa kutatatua migogoro ya kiuongozi kutakukost sana nashauri kuwe kuna taratibu ya kutatua matatizo ya uongozi once yanapoanza.
 
Kweli kabisa maana kama ingekuwa ni uchu wa umayer basi madiwani wasinge fukuzwa.

Huu ndio utumishi ulio tukuka kwani kulea maovu ni kukiua chama!

Big up cdm

kinachonifurahisha cdm ni kuwa wewe km umechaguliwa kuwa kiongozi wa watu halafu unaleta mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya chama, unapumzishwa. hiyo ndo nidhamu ya chama.

inatujengea uzoefu wa kutovumilia makosa ya mtu once tumechukua nchi uchaguzi ujao. hizi ni challenges na vyama makini vilivyojipanga kuchukua nchi, hukutana na vitu km hivi.
 
Seif Abalhassan

UFAFANUZI KILICHOTOKEA KWENYE UCHAGUZI WA UMEYA WA JIJI LA MWANZA KATI YA CCM NA CHADEMA.

Mgombea wa kiti cha umeya katika Halmashauri ya jiji la Mwanza kupitia CCM na diwani wa kata ya Mkolani Ndg Stanslaus Mabula, ameshinda kiti cha Umeya wa Halmashauri ya Nyamagana kwa jumla ya kura 11 dhidi ya mgombea wa CHADEMA diwani wa kata ya Mahina Ndg Charles Chibara aliyepata kura 8.

CCM wameshindishwa na mbinu za kisiasa amabzo uhalali wake kisheria linabaki kuwa suala la wanasheria wanaojua taratibu zikoje kutufafanulia.

Baada ya mgawanyo wa Halmashauri ya jiji la Mwanza na kuwa na halmashauri ya jiji inayoundwa na Majimbo mawili, kulipatikana Halmashauri ya Nyamagana inayoundwa na Jimbo la Nyamagana na halmashauri ya ilemela inayondwa na jimbo la Ilemelai.

Mgawanyo huo ulifanyika Mwezi Julai mwaka huu ambapo Mgawanyo wa Madiwani ukabaki ifuatavyo;

NYAMAGANA.

CHADEMA - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 5, MADIWANI WA VITI MAALUM - 2, MBUNGE - 1. JUMLA CHADEMA WANAKUWA NA WAJUMBE 8 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

CCM - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 6, MADIWANI WA VITI MAALUM - 1, MBUNGE - 0. JUMLA CCM WANAKUWA NA WAJUMBE 7 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

CUF - DIWANI WA KUCHAGULIWA -1, DIWANI VITI MAALUM -1, MBUNGE 0. JUMLA WANAKUWA NA WAJUMBE WAWILI WA BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

ILEMELA.

CHADEMA - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 6, MADIWANI WA VITI MAALUM - 2, MBUNGE - 1. JUMLA CHADEMA WANAKUWA NA WAJUMBE 9 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA ILEMELA.

CCM - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 3, MADIWANI WA VITI MAALUM - 2, MBUNGE - 1. JUMLA CCM WANAKUWA NA WAJUMBE 6 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA ILEMELA.

CUF - DIWANI WA KUCHAGULIWA - 0, DIWANI VITI MAALUM - 0, MBUNGE 1. JUMLA WANAKUWA NA WAJUMBE WAWILI WA BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA ILEMELA.

SIASA NI MIPANGO - MBINU ZA CCM HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

Kilichotokea ni CCM kuhamisha Diwani Mmoja wa Viti Maalum na Mbunge Mmoja wa viti maalum (kwa barua yao kwenda ya tarehe 14, Septemba, 2012 kwa mkurugenzi wa Jiji) kutoka Halmashauri ya Ilemela kuja Halmashauri ya Nyamagana na hivyo kuongeza idadi ya kura zao kuwa 9.

Wakati huo huo Chadema walishakuwa hawaihehabu kura ya Diwani wao wa Kata ya Igoma Bwana Chagulani Adams ambaye wamemfukuza/wamemvua Uanachama na amerejeshwa na mahakama Barazani wakati akisubiri kusikilizwa kwa kesi yake aliyoifungua kupinga kuvuliwa Uanachama, Hivyo kuwafanya Chadema wao wapungukiwe na Mjumbe Mmoja na hivyo kubaki na Wajumbe 7 .

Matokeo mara baada ya Kura kupigwa ni kuwa CCM walipata kura 11 na Chadema walipata Kura 8 na hivyo CCM kuwa Washindi wa Kiti cha Umeya wa Halmashauri ya Nyamagana.

HISIA/DHANA.

Kulingana na Tathmini hiyo hapo juu kumezuka dhana na hisia kuwa Kura zilipigwa ifuatavyo:

CCM: Walipata kura zote za Wajumbe wao 9 NA PIA WAKAPATA NYONGEZA YA KURA 2 ZA WAJUMBE WA CHADEMA.
CCM: Walipata kura zote za Wajumbe wao 9 NA PIA WAKAPATA NYONGEZA YA KURA 2 ZA WAJUMBE WA CUF.
CCM: Walipata kura zote za Wajumbe wao 9 NA PIA WAKAPATA NYONGEZA YA KURA 2 ZA MJUMBE MMOJA WA CHADEMA NA MJUMBE MMOJA WA CUF.

MUAFAKA WA CHADEMA B/CCM B (CUF) NA CHADEMA.

Pamoja na kuitwa CCM B kwa kuwa na MUAFAKA na CCM kule Zanzibar Lakini pia CUF walipata jina jipya la CHADEMA B kwa kuwa na Muafaka na Chadema ambapo walikubaliana kuungana mkono katika Uchaguzi huo.

Kamati ya utendaji ya Chadema Nyamagana, kushirikiana na kamati za madiwani wa Chadema zilikamilisha mchakato wa kupata Mgombeawa nafasi ya Umeya mara baada ya Diwani wa Kata ya Maina, Charles Chibara, kupitishwa kuwa mgombea Umeya wa Halamashauri Hiyo.

Chadema walifanya makubaliano na chama cha CUF ili wapate wingi wa kura na kumpitisha Diwani wa CUF Kata ya Mirongo Daudi Mkama, kuwa mgombea wa nafasi ya Naibu Meya.

CUF wanadai walitekeleza Makubaliano yao na Chadema na hivyo kura zao zote 2 waliipigia Chadema na hivyo kuonyesha kuwa Chadema walipata Kura 7 kutoka kwa Wajumbe wake Halali (Ukimuondoa "Diwani wa Mahakama" Chagulani Adams).

Ni vigumu kuthibitisha Uhalali wa Madai ya Cuf kupiga Kura zao 2 kwa Chadema kama ambavyo ni vigumu kuthibitisha Kinyume chake, AKILI KUMKICHWA.

MWARI ALALA ILEMELA.

Hayo yakiendelea uchaguzi wa Meya wa Ilemela umeahirshwa katika mazingira tata, baada ya Mkurugeni kusoma Amri ya Mahakama iliyopewa tafsiri na Mwanasheria wa jiji kuwa inakifanya kikao hicho kuahirishwa kwa kuwa "Diwani wa Chadema wa Mahakama" wa Kata ya Kitangiri Bwana Matata (ambaye naye pia alifukuzwa/alivuliwa Uanachama pamoja na yule Diwani wa Igoma na anaendelea na Udiwani kwa Amri ya Makahama) kuleta Barua ya kutaka atambuliwe kama Mgombea.

Ukazuka ubishi kidogo juu ya hoja ya Mgombea kuteuliwa na chama, Mkurugenzi wa Jiji akasema hiyo siyo sheria ni mwogozo, na kwa kuwa sheria na mwongozo zikigongana sheria ndiyo inatamalaki hataki aingie katka Mgogoro wa Tafsiri ya Sheria, Hivyo akaamua kuaghirisha Kikao.

HOJA YA KISHERIA YA CHADEMA.

Kwa mujibu wa mwanasheria wa wa Chadema, pingamizi hilo la Mahakama juu ya Chadema kumvua Uanachama Diwani Matata lilikuwa linamrejeshea Diwani huyo haki yake ya Uanachama na hivyo kuendelea na Udiwani wake, na kutaka matata asizuiliwe kuendelea na mchakato wa kuomba Umeya.

Mwanasheria huyo aliendelea kusema kuwa kwa mantiki hiyo Matata ameomba uteuzi wa Chama lakini hakuteuliwa na Chama na hivyo Mahakama haiwezi kuwalazmisha chama wateue mgombea kwa Amri ya Mahakama. Yeye anaamini ni uhuni tu na njama za kisiasa zimefanyika kuaghirisha uchaguzi huo.

USHAURI HURU WA KISHERIA.

Bado nawasiliana na Wanasheria Mbalimbali ili kupata Ushauri huru wa Kisheria juu ya Suala hili.

HONGERA WASHINDI, ASHINDWAE PIA NI MUME.

Nichukue Fursa hii kuwapongeza CCM KWA uSHINDI WAO, Hongereni sana. Poleni sana Chadema na pia Poleni sana CCM B/CHADEMA B (CUF).
 
hii ndio tabu ya kumchukia mtu badala ya mfumo mtaendelea kuumia sana subirini 2015, kikwete anapita tu akija mnayempenda mtarudi CCM.

Busara imenifanya nikuheshimu! Other ways, watu kama hawa wanatakiwa kutumia akili badala ya kinyesi kufikiri!
 
mkuu nisaidie kura za wazi zinapigwa kwenye mazigira gani.?
Mazingira ya wazi,ikiwa na maana kwamba kuna uwezekano wa kufahamu ni diwani yupi wa chadema(kama ni kweli) alimpigia mgombea wa ccm.

Kwa mfano marekani,kwenye electoral college,kama elector wa lets say democrats,akampigia kura mgombea wa republican,basi democrats wanaruhusiwaa kisheria kupinga hilo.(Kwenye baadhi ya states)
 
kinachonifurahisha cdm ni kuwa wewe km umechaguliwa kuwa kiongozi wa watu halafu unaleta mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya chama, unapumzishwa. hiyo ndo nidhamu ya chama.

inatujengea uzoefu wa kutovumilia makosa ya mtu once tumechukua nchi uchaguzi ujao. hizi ni challenges na vyama makini vilivyojipanga kuchukua nchi, hukutana na vitu km hivi.

Yo damn right mkuu, maadili ya chama kwanza mambo mengine baadae.
 
images
images

Makubaliano ya Chadema na CUF kusafisha njia ya kupitisha Meya wa Chadema na Kaimu CUF ndoa yao ya mkeka imekuja kutalikiwa na sintofahamu ya kinachoendelea Arusha hali halisi inaweza kusomeka hivyo kutokana na kurushiana makombora mazito ya kutuhumiana kwa vurugu za Arusha ambazo zilisababisha mtafaruku dhidi ya CUF kuituhumu Chadema kuvuruga misafara yao.

Tofauti zinazojitokeza sasa hivi Huko Arusha ni dalili tosha kwamba adui mkubwa wa vyama vya upinzani nchini ametumia ufa huo kumrudisha ndani mwandani wake aliyeelekea kuvutiwa na mwingine mpya, lakini kabla hawajavishana pete amemwahi na kumrudisha ndani kwa mtindo wa kiaina.

Tatizo linalokuja kuonekana wazi ambalo tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa ni pale CCM inapotumia mfumo wa Mwingireza wa
divide and rule. Vyama vya upinzani vimeonekana kutafuta suluhisho la kufanya pamoja inapohitajika kupata kura. Hali ya kujenga kuungana kiitikadi kwa upeo wa muda mrefu ili kuwaletea ushindi dhidi ya CCM umekuwa mgumu kwa vile mwendelezo wa kuungana kwa msimu ili kukusanya kura ndio mwanya ambao CCM inatumia kunyakua ushindi kama ilivyotokea sasa huko Mwanza.

Naam, vyama vya upinzani ukata ndio unaovitavuna, wakati vyanzo vya mapato ni kidogo, matokeo CCM rahisi kuwahadaa wenye njaa ili kujirudishia himaya ili kuzidi kujenga hoja ya kujiaminisha nguvu bado wanayo.

Yeah, ubinafsi nao ukipata nafasi sisi tupate vyote matokeo ndio haya, wenzetu Kenya Mwai Kibaki asingekuwa flexable na wenzake katu KANU isingesambaratika tuonavyo leo. Kuna ya kujifunza kutokana na haya ili kukuza demokrasia nchini, kwani siasa za leo zinaendeshwa kisayansi kuliko wentu tufikiriavyo.
 
wewe jamaa mbona mjinga sana?
Ujerumani kuna serikali ya mseto, uingereza kuna serikali ya mseto, israel kuna serikali ya mseto, ugiriki kuna serikali ya mseto, lebanon kuna serikali ya mseto, kenya na zimbabwe pia. Sasa unaona ajabu cuf na ccm kuunda serikali zanzibar?

Hebu wacha ushamba huo usikae vichakani kula panzi tu njoo utembee zanzibar uone watu walivyostaarabika ili upunguze fikra potofu.

Punguza ubinafsi, choyo na chuki na utambue tu kua ni sisi wananchi wa zanzibar kupitia njia ya kidemokrasi 64.3% tulipiga kura ya kukubali mfumo wa serikali ya umoja wa kitaifa. Na hata chadema kama wana ubavu wa kupata alau jimbo moja zanzibar nanyi mutashirikishwa. Lkn kwa sasa musitegemee huruma bila ya kufanya kazi.

Wewe ndi mshamba umekalia uzanziari wenu huko na Jussa wenu aliyewahi kusema mlipoteza jimbo kwa ajili lilikuwa na wakristo wengi
Acha sias zetu wabara tuzijadili huku huku bara nyie endeleeni na fungate salama
 
madiwani wa chadema walikuwa 7 na wamepata kura 8, hii moja imetoka wapi? kuna diwani mmoja wa chadema kapigia kura CCM japo CUF kuwapigia kura cdm.
 
Back
Top Bottom