Ufafanuzi wa kilichotokea Uchaguzi Meya Mwanza...

Huyo Mkurugenzi mbona ni mtu wa ajabu. Yaani anakubali moja kwa moja haki ya Diwani Chagulani kupiga kura (baada ya kurudishiwa udiwani na mahakama, lakini hapo hapo akakwama katika kumruhusu Diwani Matata kugombea, kwa kuwa hakuteuliwa na chama (Chadema). Kama ni hivyo basi hata yule Chagulani hakuwa na haki ya kuruhusiwa kupiga kura, kwani alirudi katika udiwani kwa nguvu ya mahakama, na si ya Chama (Chadema).

Naona mawakili wa Chadema wanaaonza kusafisha bongo zao na kupeleka mahakamani suala la uchaguzi huo wa kihuni. Mimi nadhani haki lazima itafutwe mahakamni, maana CCM imezidi mno na umafia katika chaguzi hizi.
 
Huyo Mkurugenzi mbona ni mtu wa ajabu. Yaani anakubali moja kwa moja haki ya Diwani Chagulani kupiga kura (baada ya kurudishiwa udiwani na mahakama, lakini hapo hapo akakwama katika kumruhusu Diwani Matata kugombea, kwa kuwa hakuteuliwa na chama (Chadema). Kama ni hivyo basi hata yule Chagulani hakuwa na haki ya kuruhusiwa kupiga kura, kwani alirudi katika udiwani kwa nguvu ya mahakama, na si ya Chama (Chadema).

Naona mawakili wa Chadema wanaaonza kusafisha bongo zao na kupeleka mahakamani suala la uchaguzi huo wa kihuni. Mimi nadhani haki lazima itafutwe mahakamni, maana CCM imezidi mno na umafia katika chaguzi hizi.

Hapa patamu. hapa ndipo tungependa MM Mwanakijiji aje na nasaha zake.
 
itafikia wakati kabla ya kumpa mtu dhamana yakugombea kupitia cdm lazima tumchunguze kwa makini,mnakumbuka yalioyotokea arusha,na leo hii nimwanza
 
Kwa Mbunge wa viti maalum haina tatizo kwasababu yuko ndani ya mkoa huo huko kwa ninavyojua maana huwa ni wabunge wa mkoa siyo jimbo...lakini kwa diwani naona wamebaka kama walivyofanya Arusha..


Leo umekuwa mpoleee baada yakugaragazwa, hayo maneno jifarijini tu ila uchaguzi ulikuwa huru na haki, Slaa amewakimbia waandishi wa habari, ccm oyeeeeeeeeeeeeee
 
manispaa nayo huwa inachagua meyA
. umesahau hata jerry slaa ni meya wa ilala
 
Hawa makada wa CCM wanaojifanya kuwa ni watenda haki katika kusimamia chaguzi ni lazima watokomezwe katika Katiba mpya.

Taifa huru kamili la Watanzania baada ya 2015 lisiwe na mianya hii ya kijanja janja inayotumiwa na CCM kuendelea kushika dola bila ya mandate halali ya wananchi. Enough is enough.

halafu naunga mkono wazo kwa CDM kupeleke suala la uchaguzi huu mahakamani kuomba injunction ili utenguliwe wakati kesi ya msingi inasikilizwa.
 
Nilikuwa nasubiria kwa hamu tangia asubuhi post za wana cdm kuanza kujitetea baada yakupigwa dafrau hili la uchaguzi wa ccm , sasa ndio zinakuja. Na nashangaa mleta mada hii hajui kuwa meya ni wa Jiji la mwanza, ilemela ni manispaa itachagua mwenyekiti wa manispaa na sio meya. Cdm kubalini kushindwa uchemfu mmeufanya wenyewe na maamuzi ya kamati kuu yasiyo zingatia maslahi ya wana mwanza kwa kuwafukuza madiwani walio chaguliwa na wananchi, madhara yame mmeyaona.

Duh!Penye Blue hapo.....Wewe kweli ndo hujui Manispaa huwa haina mwenyekiti ila Meya...Niambie ni Manispaa gani Tanzania yenye Mwenyekiti...Unatakiwa kutofautisha kati ya halmashauri na manispaa....
 
Duh!Penye Blue hapo.....Wewe kweli ndo hujui Manispaa huwa haina mwenyekiti ila Meya...Niambie ni Manispaa gani Tanzania yenye Mwenyekiti...Unatakiwa kutofautisha kati ya halmashauri na manispaa....


Hebu weka hesabu zako sawa aisee , umesema nyamagana ccm walikuwa 7, then wakahamisha viti maalum 1 kutoka ilemela kuja nyamagana, kwa maana hiyo jumla Yao hapa ni 8, ww hiyo hesabu ya 9 umenipata wapi, au hesabu ya mchina hiyo? Fafanua
 
CCM wameshindishwa na mbinu za kisiasa amabzo uhalali wake kisheria linabaki kuwa suala la wanasheria wanaojua taratiu zikoje.

Baada ya mgawanyo wa h/shauri ya jiji na kuwa na h/shauri ya jiji inayoundwa na jimbo la Nyamagana na halmashauri ya ilemela inayondwa na jimbo la ilemela mwezi Julai mwaka huu mgawanyo wa madiwai ulikuwa hivi kwa nyamagana

Chadema -wa kata 5, viti ,maalum 2. mbunge mmoja, jumla wanakuwa 8
CCM - wa kata 6, viti maalum 1 jumla wanakuwa 7
Cuf - wa kata 1, viti maalum 1

Ilemela

Chadema -- wak kata 6, viti maalum 2 mbunge 1 jumla wanakuwa 9
CCM - wa kata 3, viti maalum 2 na mbunge 1 (wa viti maalum) jumla wanakuwa 6
CUF - MBUNGE WA viti maalum 1

Kilchotokea kwenye uchaguzi ni CCM kuhamisha diwani mmoja wa viti maalum (kwa barua ya CCM kwenda kwa mkurugenzi wa jiji ya tarehe 14, Septemba, 2012) na mbunge wa viti maalum toka Ilemela kuja nyamagana na hivyo kuongeza idadi ya kura zao kuwa 9, wakati huo huo Chadema walishakuwa hawaihehabu kura ya Diwani wa Igoma Chagulani ambaye wamemfukuza uanachama akalejeshewa na mahakama wao wanapugukiwa na kura 1 zao zinabaki 7 , aliyepungua Chadema akiwapigia CCM wanakuwa na kura 10 dhid ya 7 za Chadema.

Lakini pia CUF walishakubaliana na chadema kuungana mkono, kwa hiyo kwa kura 2 za CUF Chadema wangekuwa na kura 9, lakini inaonekana ama mwana Chadema mmoja kapigia CCM au CUF mmoja kapigia CCM na kufanya matokeo ya kuwa kuwa 11 kwa CCM dhidi ya nane za Chadema.

Hiyo ndiyo hali halisi ya jinsi mahesau ya kura yalivyochezwa, kama kuna uhalali katika mchakato huo au la ni suala la wataalamu wa masuala haya kutujuza.

Hayo yakiendelea uchaguzi wa Meya wa Ilemela meahirshwa katika mazingira tata, baada ya Mkurugeni kusoma Amri ya Mahakama iliyopewa tafsiri na mwanasheria wa jiji kuwa inakifanya kikao hicho kuahirishwa kwa kuwa Diwani wa Chadema Matata (pia alifukuzwa uanachama pamoja na wa igoma na anaendelea na udiwani kwa amri ya makahama) kuleta pia barua ya kutaka atambuliwe kaa mgombea.

Ukazuka ubishi kidogo juu ya hoja ya mgombea kuteuliwa na chama, mkurugenzi wa jiji akasema hiyo siyo sheria ni mwogozo, na kwa kuwa sheria na mwongozo zikigongana sheria ndiyo inatamalaki hatakia aingie katka mgogoro wa tafsiri ya sheria, akaahirisha kikao bila hata madiwani kujadili hoja hiyo.

Kwa mujibu wa mwanasheria wa wa Chadema, pingamizi hilo lilikuwa linawarejeshea haki yao ya uanachama na hivyo kuendelea na udiwani wao, na kutaka matata asizuiliwe kuendelea na mchakato wa kuomba umeya, Kwa hiyo matata ameomba lakini hakuteuliwa na chama na mahakama haiwezi kuwalazmisha chama wateue mgombea kwa amri ya mahakama, anadhani ni uhuni tu na njama za kisiasa zimefanyika kuahirisha uchaguzi huo.
Nadhani kidogo piacha itaeleweka kwa wanjamvi juu ya nini hasa kimetokea.

SOURCE: Kamnada Deus Bugaywa-Mchambuzi Raia Mwema
mkuu asante kwa taarifa hiyo, naona hawa jamaa wanataka yatokee ya Arusha, sasa wanapanga mbinu kwa Ilemela na diyo sababu ya kuahirisha uchagizi huo
 
Hiyo sababu ya kuahirisha uchaguzi wa ilemela ndiyo itakayowaumbua CCM na Mkurugenzi wao. Mkurugenzi kakubali kwamba Diwani Matata hana chama, basi ilikuwaje alimkubali Chagulani kushiriki kupiga kura? Kwa nini asitumie kigezo hicho hicho cha alichomkatalia Matata?

Ikumbukwe kwamba katika chaguzi sifa zote mbili lazima zizingatiwe - sifa ya kupiga kura na sifa ya kupigiwa kura. Huwezi kuikubali moja na nyingine ukaikataa.

Lakini wataalamu wa sheria wafafanue hili, na naomba wachangiaji wajikite katika subject hii tu.

Nawasilisha.
 
Pingamizi liwekwe kwa sababu hizi njama njama zikiruhusiwa kuendelea hatutafika ina maana TAMISEMI walipitisha huo uamuzi sasa kesi ianzie hapo
 
mkuu asante kwa taarifa hiyo, naona hawa jamaa wanataka yatokee ya Arusha, sasa wanapanga mbinu kwa Ilemela na diyo sababu ya kuahirisha uchagizi huo

Yah -- la Ilemela limewakalia pabaya, ndiyo maana wanahaha kulitafutia namna. After all si wao ndiyo wanaopanga kila kitu? -- the one=man show halafu eti wanasema huu ndiyo ukuaji wa demokrasia.
 
Mmekumbuka shuka wakati kumekucha?wakati nyie mnalalamika,wenzenu watakuwa bize kutekeleza ilani yao ya uchaguzi ili 2015 warudishe kata zote pamoja na hayo majimbo mawili
 
Chadema kubalini matokeo, angalia hata mwandishi anasema walikubaliana na cuf sasa hajui nani kati ya cuf au cdm kapigia ccm. Sasa wanaobisha naona mmezoea tu kusema. Sio kila mwanchi anachukia ccm. Hata iyo mnayoita nguvu ya umma si kwa chadema pekee. Muwe waelewa muda mwingine mazingira yanafanya mambo ya ajabu.
Pili kila wakati ccm wakifukuzana au wakikosana mnaona madhara yake. Sasa mnashangaa nini kwa kwa cdm mmegombana tegemeeni mnayoyaona ccm.
Tatu poleni na kubalini ukweli. Sasa ninyi chadema si mlizoea kutoka nje sasa leo imekuaje. Mmelewa sifa.
 
Heheeeeee!!!! CCM wamelinukisha huko tena Mwanza! hawa wajamaa ni mwisho, pole pole wanatupeleka katika kuchapana!
 
Chadema kubalini matokeo, angalia hata mwandishi anasema walikubaliana na cuf sasa hajui nani kati ya cuf au cdm kapigia ccm. Sasa wanaobisha naona mmezoea tu kusema. Sio kila mwanchi anachukia ccm. Hata iyo mnayoita nguvu ya umma si kwa chadema pekee. Muwe waelewa muda mwingine mazingira yanafanya mambo ya ajabu.
Pili kila wakati ccm wakifukuzana au wakikosana mnaona madhara yake. Sasa mnashangaa nini kwa kwa cdm mmegombana tegemeeni mnayoyaona ccm.
Tatu poleni na kubalini ukweli. Sasa ninyi chadema si mlizoea kutoka nje sasa leo imekuaje. Mmelewa sifa.

Sikubaliani na wewe unaetaka daima kusukumiszia uchafu chini ya zulia! Nyie magamba mmezoea hivyo! kama vile la Arusha, hili pia lazima kieleweke.

Unanichoma kisu halafu unaniambia nikubali tu matokeo? Tell that to the mountains!
 
Mmekumbuka shuka wakati kumekucha?wakati nyie mnalalamika,wenzenu watakuwa bize kutekeleza ilani yao ya uchaguzi ili 2015 warudishe kata zote pamoja na hayo majimbo mawili

Naapa hilo halitafanyika, huijui CDM wewe! Uharamia wa aina hii lazima uwe na mwisho.
 
Hata kama kuna umafia, tulitegemea chadema inteligence kujua hizi mbinu.... kwahiyo kitendo cha kushindwa kujiandaa kwa haya kimeboa

hata mfanyeje hili ni doa
 
Back
Top Bottom