Ufafanuzi: Majina John Heche Vs Wegesa Suguta

Ufafanuzi wako hakika unajitosheleza,labda pia kwa faida ya kufunzana katika jukwaa yapo mambo ya kueleweshana hasa tulikotoka,-ukiacha issue kama hii ya john heche kuwa na majina ya nyumbani utamaduni ambao ni mkubwa kwa makabila mengi tanzania,wapo pia wale waliosoma miaka ya nyuma kidogo kabla ya mfumo wa elimu ya sekondary kupanuka sana,ambapo nafasi za ufaulu zilikuwa finyu sana,na kujikuta mwanafunzi mmoja akifaulu katika darasa la watu mia moja,ikiwa ni sababu hasa ya kutokuwa na nafasi za shule za sekondary za kutosha,hii ilisababisha watu wengi kurudia madarasa ya shule za msingi kwa kupewa majina ya watu ambao mara nyingi walikuwa wakikataa shule,hivyo watu wengi waliosoma miaka ambayo ufaulu ulikuwa kwa kiwango kidogo,walipata kadhia hii ya kutumia majina ya watu wengine,hasa wale watu ambao familiya zao zilikuwa na msisitizo wa kusomesha watoto lakini hawana uwezo wa kuwapeleka private school ambazo pia zilikuwa chache,zaidi ya hapo nakupongeza kwa ufafanuzi mzuri wa john heche,ambao kwa sisi wengine tulijua ni majina yake rasmi,sema siasa za bongo lolote lile ni habari kama ambavyo hao wengine wanaambiwa wameiba majina ya watu,japo huko vyuoni wamesoma na watu.
 
Mkuu, taarifa imeeleweka, kwa sisi watu wa Mara hiyo ni kweli kabisa, hata mm nina majina kibao ya kizanaki na ya "kileo''. Hata Prof. MUhongo, Waziri wa Nishati na Madini, Jina lake la ubatizo ni Sospeter, lakini la Nyumbani ni Mwijarubhi. La baba yake ni Faru aka Muhongo Nyawayega. Kwa hiyo Shonza hapa huna jipya!
 
Mkuu mwita maranya hebu na wewe nyumbua hilo jina lako.
I thank you for nice ufafanuz kuhusu kamanda heche.
 
Ndugu wanaJF,

Nimelazimika kuanzisha thread hii kwa lengo moja tu la kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji wa jina la mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema unaofanywa na kundi la masalia kwa sababu maalum.

Mwishoni mwa mwaka jana TUNTEMEKE aliwahi kuibuka na madai kama haya kwamba John Heche anatumia cheti cha ndugu yake, na kwamba hakuwahi kusoma chuo kikuu cha mtakatifu augustino (SAUT) cha mwanza. Leo tena katika thread iliyoanzishwa na mwanamasalia aliyetimuliwa Chadema bi. Juliana Shonza amejitahidi sana kutumia jina la Wegesa Charles Suguta ama Wegesa Suguta.

Bila shaka ameamua kufanya hivyo kama muendelezo wa tuhuma walizozianzisha kundi la masalia kwa kutumia ID yao ya kundi ya Tuntemeke kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Hili kundi la PM7 linataka kumuonyesha John Heche kwamba naye amegushi jina kama walivyo baadhi ya viongozi wakubwa huko ccm (wafadhili wao). Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.

Sasa nirudi kwenye hoja ya msingi. Kawaida sisi wakurya hata kama umezaliwa mjini ama katika mazingira ya mbali na nyumbani/kijijini lazima unapewa jina la kikurya, kwahiyo kwa wakurya wengi wanakuwa na majina mawili ama matatu lakini yote yakiwa ya mtu mmoja.

Kwa mfano mwalimu Nyerere, majina yake ni Julius Kambarage Nyerere(Julius jina la kikristo). Kuna mwanae Charles Makongoro Nyerere (Charles jina la kikristo), kuna Dr. James Mnanka Wanyancha-mwenyekiti wa Road Fund (James jina la kikristo), Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (Ernest jina la kikristo), Jenerali mstaafu George Marwa Waitara (George jina la kikristo. Nadhani kwa kutaja hao wachache mnaweza kuona scenario ya majina ya kikurya, naamini kuna makabila mengine yenye utamaduni kama wa kwetu.

Sasa nije kwa John Heche Suguta:
Jina lake la kikurya ni Wegesa na baba yake mzazi anaitwa Heche Suguta. Wegesa Heche Suguta jina lake la kikristo ni John, ndipo sasa unapata John Heche Suguta. Jina la kikristo la baba yake John Heche (Heche Suguta) ni Charles, ndipo sasa unapata Charles Heche Suguta.

Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.

Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.

John Heche aligombea na kushinda kiti cha udiwani Tarime mjini mwaka 2008 katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Chacha Wangwe, kwa kumshinda mbabe wa Tarime Bw. Peter Zakaria. Wakati huo alikuwa mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu augustino (SAUT) Mwanza. Kama angelikuwa anatumia majina ya bandia ama majina ya mtu mwingine bila shaka hilo lisingejificha wakati wa kampeni za uchaguzi.

Baada ya kusema hayo nadhani nime-clear doubts zilizokuwa zimeanza kujitokeza kwa baadhi ya watu hapa JF.

Nawatakia jioni njema.

Heshima Kubwa kwako Mwita

Nakushukuru sana kwa ufafanuzi huu uliojitosheleza nazungumza haya kutoka moyoni na sina unafki hata kidogo,kama nilivyosema toka awali mimi ni mimi George James Minja sina uhusiano na masalia wala PM7 sitetei kundi lolote wala sio MCCM nina kadi halali na iliyo hai ya CHADEMA.

Nakushukuru kwa sababu kama nilivyosema toka awali namkubali sana Heche na ufafanuzi niliokuwa nautaka ni wa muhimu ili kumuondoa kiongozi huyu na doubt yeyote.Lakini majibu waliyotoa wengi wanaojionyesha kama MaBAVICHASTIC wamenibeza na kuniita masalia jambo lililonisikitisha na kunifanya nione kama mnapoteza uwezo wa kuongoza na sasa mmekaa kama jeshi linalosubiri vita yaani kila anayehoji chochote anaitwa masalia au PM7,kitu ambacho vijana wengi wa BAVICHA hawajui ni kuwa BAVICHA ilichukua mchakato mrefu kuundwa na wengi tuliokuwepo wakati huo tumekaa nje kwa sababu ya majukumu au kuwa mbali na nyumbani.


sasa niingie kwenye hoja nyingine naomba kwa moyo hu huu mkubali na kukiri makosa kwenye barua ya kumfukuza Juliana Shoza,barua ambaya kicha cha habari kinasema KUFUKUZWA,haiwezekani ikaleta maana kwa watumiaji wa kiswahili kwa kusema KIKAO KIMEAZIMIA sii sawa na nitapinga daima kwani kwa mantiki ya Resolution haikubaliki kuseme TUMEDHAMIRIA AU TUMEAZIMIA hili ni kosa na lazima mkiri na msahihishe,CHADEMA kimebeba matumaini ya watanzania wote na tatizo kubwa Tanzania ni pamoja na mikataba mibovu sasa mkichukua nchi mnategemea hawa kina Deo ndio watakaosaini mikataba bila kuwa na hakika na tafsiri ya maneno??tutaendelea kuiuza nchi hii kwa vipande vya shilingi.


Masalia ni watu na waheshimiwe pia hata kama wamefukuzwa CHADEMA so wanyama au watu waliokosa sana,mbona wako watu wengi wanaasi vyama vyao na kuingia CDM je na wao wadhalilishwe kama wanyama??

Ukweli ni kwamba sikubaliani na masalia hata kidogo na ningeshangaa sana kama wasingefukuzwa kwani binafsi niliona mnachelewa kuwafukuza kwani walikuwa wamefanya kazi ya CCM vya kutosha lakini msiwe wanafki kila mtu hapa J na kila mahali tunajua kuwa ZITTO ZUBERI KABWE ametajwa mara nyingi kama kiongozi wa masalia kwa nini hafukuzwi??kwa nini haitwi na kuhojiwa na kama haji kwenye vikao kwa nini asifukuzwe moja kwa moja yeye ninani au yuko juu ya sheria hili ni tatizo na hapa tunaona kuwa CDM inawatu wanaoogopwa na kuachwa.

Ben Saanane alisema hapa Zitto,Drogba,Dogo au Presda ndio mdhamini mkuu wa PM7 kwa nini hachukuliwi hatua.


BAVICHA lazima muwe makini katika kuchagua viongozi mtu mjinga kama Juliana Shoza,Mchange na wale wajinga wao wote hawastahili hata kugombea ujumbe wa tawi kuna mamilioni ya watanzania wenye uwezo wa kuongoza na ni wanachama wa cdm kwa nini mnawapa mamlaka watu wasio hata na mwelekeo,wajinga wapuuzi waisojua hata maana ya uhuru wa maoni,uchafu alioandika Juliana hapa kwa muda wote ningalikuwa Heche au Mbowe ningeshamfungulia mashtaka ya defamation nyie mmekaa kimya badala yake mnakuja kupambana na sisi tunaohoji ili kukisaidia chama chetu

Mwisho,CHADEMA ni cham chetu kama nyie mmekikuta kiko juu sio kwa sababu tuliokikuza tulikuwa wajinga na waandishi wa barua zisizoeleweka tulikuwa na mikakati imara ndio maana kimekua na nyie mnatakiwa kufanya kwa nafasi yenu kuendelea kukikuza na siku mkishindwa na kama mnavyoonekana sasa mnayumba wenyewe tutarudi kukisimamisha tena.

Ahsanteni
 
Siku ya kufa nyani miti yote huteleza, masalia wanatapatapa tu, wanashindwa kuelewa kuna watu waliosoma na heche wamo katika chama na humu JF wapo wengi tu. Uchu wa madaraka unawasumbua.

Mie mmoja wapo ambaye namjua Heche kwa mda mrefu kwa kusoma nae,na pia nje ya shule. Maranya kakopi na kupesti niliyotaka kuyasema juu ya Heche. Hata mie jina nililotumia nilipokuwa nasoma shule ya msìngi Mugumu, sio nililolitumia Kiagata sekondari baada ya kujiunga shuleni hapo. Hiyo si hoja ya kung'ang'ania. Mijitu inayokosa sera huishia kuingia katika siasa nyepesi kabisa kama hawa PM7!
 
Kwa mfano mimi naitwa
Wambura Mugwisha Misana au Benaire Wambura David Mugwisha Abel Misana.....yaani Benaire,David na Abel ni majina ya ubatizo.....
Asante
 
Wakirya si wezi wa ngombe.sasa heche akitumia.akiazima jina la mtumwingine kuna ubaya gani usipotoshe nimeka na wakurya na nimeoa hakuna hilo inalotetea ndugu kokaragosi
 
mbona mnajibu vitu vdogo na kuacha mambo makubwa yaliyohojiwa na Shonza?
hebu tupeni ufafanuzi juu ya vifungu alivyolalamikia Shonza kwamba vmekiukwa! hebu tuambieni vigezo vilivyotumika kumwadhibu Shonza na kumuacha Mamuya wakati wote hawakuhudhuria kikao, hebu tuambieni juu ya mshahara wa Heche na kwann kodi ya nyumba yake inatoka kwa katibu mkuu?
hebu tufafanulieni juu ya gari la BAVICHA na dreva wake.
CHHADEMA acheni kujibu hoja nyepesi na zisizohitaji kujibiwa wakat kuna hoja znahtaj majibu yenu na hapo sijawauliza kwann hamjamfukuza Zitto kwa sababu najua Zitto sio BAVICHA!

Nakubaliana na wewe kwa % zote badala kujibu hoja kama hizo wanajiridhisha na majina kweli hili ni dema akili zinavuja
 
Mkuu George J Minja umeandika baadhi ya vitu vya msingi sana lakini umevi-dilute kwa kuweka hoja nyepesi sana mwishoni.
Kwanza umeandika ukini-address mimi juu ya barua ya shonza as if mimi ndiye munishi.
Pili unasema hiki chama tumekikuta hapo kilipo kwakuwa mlifanya kazi kubwa na imara ya kukijenga. Je una uhakika kwamba ulinitangulia kujiunga Chadema? Je una uhakika kwamba contribution yako ni kubwa kuliko mimi ama wanachama wengine waliojunga baada yako?
Hii tabia ya kujikweza na kujiona bora zaidi ya wengine ndio inakufanya ushambuliwe na wadau hapa JF halafu unabaki kulalamika.

Mwisho, siamini kama wewe ni mwanachadema kadri ninavyokusoma katikati ya mistari. Nisingekuwa natumia simu ningekuonyesha contradictions zinazokubainisha kuwa wewe si mwenzetu!
 
Last edited by a moderator:
Mwanzoni nilikuwa naona kama Bavicha wamechukua hatua kali mno kwa Shonza and Co. ila kwa hoja za kipuuzi za leo alizotoa huyu Dada nashauri Kamati Kuu ibariki maamuzi magumu ya Bavicha ili huyu Dada ahamie NCCR au CHAUMMA haraka sana. Ni kirusi kibaya sana
 
Sasa tumegundua Kumbe Dada Juliana alikuwa hamjui vizuri mwenyekiti wake. Kama atakuwa mwerevu japo kidogo basi ataweza kuwa amejifunza kitu kutokana na ufafanuzi huu ili siku nyingine asitumike vibaya. Kutokana na umri wake, bado ananafasi ya kujifunza na kuwa mwanasiasa mzuri Kama atajirekebisha.
 
Mkuu George J Minja umeandika baadhi ya vitu vya msingi sana lakini umevi-dilute kwa kuweka hoja nyepesi sana mwishoni.
Kwanza umeandika ukini-address mimi juu ya barua ya shonza as if mimi ndiye munishi.
Pili unasema hiki chama tumekikuta hapo kilipo kwakuwa mlifanya kazi kubwa na imara ya kukijenga. Je una uhakika kwamba ulinitangulia kujiunga Chadema? Je una uhakika kwamba contribution yako ni kubwa kuliko mimi ama wanachama wengine waliojunga baada yako?
Hii tabia ya kujikweza na kujiona bora zaidi ya wengine ndio inakufanya ushambuliwe na wadau hapa JF halafu unabaki kulalamika.

Mwisho, siamini kama wewe ni mwanachadema kadri ninavyokusoma katikati ya mistari. Nisingekuwa natumia simu ningekuonyesha contradictions zinazokubainisha kuwa wewe si mwenzetu!

Mkuu Maranya Huyo ni M23 NA NI KONDOO ALIE JIVIKA NGOZI YA MBWA MWITU, MNAFIKI MKUBWA SANA HUYO
 
Heshima Kubwa kwako Mwita

Nakushukuru sana kwa ufafanuzi huu uliojitosheleza nazungumza haya kutoka moyoni na sina unafki hata kidogo,kama nilivyosema toka awali mimi ni mimi George James Minja sina uhusiano na masalia wala PM7 sitetei kundi lolote wala sio MCCM nina kadi halali na iliyo hai ya CHADEMA.

Nakushukuru kwa sababu kama nilivyosema toka awali namkubali sana Heche na ufafanuzi niliokuwa nautaka ni wa muhimu ili kumuondoa kiongozi huyu na doubt yeyote.Lakini majibu waliyotoa wengi wanaojionyesha kama MaBAVICHASTIC wamenibeza na kuniita masalia jambo lililonisikitisha na kunifanya nione kama mnapoteza uwezo wa kuongoza na sasa mmekaa kama jeshi linalosubiri vita yaani kila anayehoji chochote anaitwa masalia au PM7,kitu ambacho vijana wengi wa BAVICHA hawajui ni kuwa BAVICHA ilichukua mchakato mrefu kuundwa na wengi tuliokuwepo wakati huo tumekaa nje kwa sababu ya majukumu au kuwa mbali na nyumbani.


sasa niingie kwenye hoja nyingine naomba kwa moyo hu huu mkubali na kukiri makosa kwenye barua ya kumfukuza Juliana Shoza,barua ambaya kicha cha habari kinasema KUFUKUZWA,haiwezekani ikaleta maana kwa watumiaji wa kiswahili kwa kusema KIKAO KIMEAZIMIA sii sawa na nitapinga daima kwani kwa mantiki ya Resolution haikubaliki kuseme TUMEDHAMIRIA AU TUMEAZIMIA hili ni kosa na lazima mkiri na msahihishe,CHADEMA kimebeba matumaini ya watanzania wote na tatizo kubwa Tanzania ni pamoja na mikataba mibovu sasa mkichukua nchi mnategemea hawa kina Deo ndio watakaosaini mikataba bila kuwa na hakika na tafsiri ya maneno??tutaendelea kuiuza nchi hii kwa vipande vya shilingi.


Masalia ni watu na waheshimiwe pia hata kama wamefukuzwa CHADEMA so wanyama au watu waliokosa sana,mbona wako watu wengi wanaasi vyama vyao na kuingia CDM je na wao wadhalilishwe kama wanyama??

Ukweli ni kwamba sikubaliani na masalia hata kidogo na ningeshangaa sana kama wasingefukuzwa kwani binafsi niliona mnachelewa kuwafukuza kwani walikuwa wamefanya kazi ya CCM vya kutosha lakini msiwe wanafki kila mtu hapa J na kila mahali tunajua kuwa ZITTO ZUBERI KABWE ametajwa mara nyingi kama kiongozi wa masalia kwa nini hafukuzwi??kwa nini haitwi na kuhojiwa na kama haji kwenye vikao kwa nini asifukuzwe moja kwa moja yeye ninani au yuko juu ya sheria hili ni tatizo na hapa tunaona kuwa CDM inawatu wanaoogopwa na kuachwa.

Ben Saanane alisema hapa Zitto,Drogba,Dogo au Presda ndio mdhamini mkuu wa PM7 kwa nini hachukuliwi hatua.


BAVICHA lazima muwe makini katika kuchagua viongozi mtu mjinga kama Juliana Shoza,Mchange na wale wajinga wao wote hawastahili hata kugombea ujumbe wa tawi kuna mamilioni ya watanzania wenye uwezo wa kuongoza na ni wanachama wa cdm kwa nini mnawapa mamlaka watu wasio hata na mwelekeo,wajinga wapuuzi waisojua hata maana ya uhuru wa maoni,uchafu alioandika Juliana hapa kwa muda wote ningalikuwa Heche au Mbowe ningeshamfungulia mashtaka ya defamation nyie mmekaa kimya badala yake mnakuja kupambana na sisi tunaohoji ili kukisaidia chama chetu

Mwisho,CHADEMA ni cham chetu kama nyie mmekikuta kiko juu sio kwa sababu tuliokikuza tulikuwa wajinga na waandishi wa barua zisizoeleweka tulikuwa na mikakati imara ndio maana kimekua na nyie mnatakiwa kufanya kwa nafasi yenu kuendelea kukikuza na siku mkishindwa na kama mnavyoonekana sasa mnayumba wenyewe tutarudi kukisimamisha tena.

Ahsanteni

Tangu nianze kutumia hili Jukwaa sijawahi kutana na Mtu mnafiki kama wewe, yaani kwa kifupi wewe ni wa Kwanza kabisa kukutana naye humu, wewe ni mnafiki mkubwa kabisa kuliko wanafiki wote hapa DUNIANI
 
Ndugu wanaJF,

Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.

.

Hivi majina yaliyomulikwa hapo juu yamewahi kutolewa ufafanuzi kama huu, kama upo mniibulie plz
 
Back
Top Bottom