Nimemaliza degree yangu ya kwanza mwaka 2006 katika chuo kikuu cha mlimani, Ninajaribu kuendelea na shahada ya pili, moja kati ya mahitaji ya chuo ninachoomba ni kwamba nipeleke barua kutoka chuo nilichosoma kuthibitisha kwamba degree yangu ilifundishwa kwa kingereza, na kama degree yangu haikufundishwa kwa kingereza basi inabidi nipeleke cheti kuthibitisha nimejifunza kingereza, hiki cheti kinajulikana kama TOEFL.
Sasa, kwa hali ya kawaida, kwa sababu degree yangu ilifundishwa kwa kingereza ilikua rahisi tu kupeleka barua kutoka chuo changu. Nikafunga safari hadi mlimani na nikaelekezwa niende kumuona Mr Mwetemi (ni Dr au Prof sikumbuki, enzi tunasoma tulikua tunamuita Don King kutokana na style yake ya nywele), nilipofika ofisini kwake nikakuta msg mlangoni kwake kwamba yuko hospitali na kama mtu ana shida ya kiofisi aende kwa secretary ofisi namba 7.
Hapo ofisi namba 7 ndio nilipokuta vituko. Kwanza yule mama akakataa katakata kuandika barua, ila akaniambia wao huwa wana vimitihani vyao (mradi wao) ambapo natakiwa kulipa elfu 40, ila kama ninataka sana hiyo barua basi nilipe hiyo 40 halafu yeye atanifanyia huo mpango, niwe kama nimefanya mtihani, atanijazia hiyo marks sijui A tupu sijui nini (anajua mwenyewe alitaka ajaze nini) halafu nitapata hicho cheti chao na barua ninayoitaka
HAPA NDIPO CHUO CHETU Kilipofika!
Sasa, kwa hali ya kawaida, kwa sababu degree yangu ilifundishwa kwa kingereza ilikua rahisi tu kupeleka barua kutoka chuo changu. Nikafunga safari hadi mlimani na nikaelekezwa niende kumuona Mr Mwetemi (ni Dr au Prof sikumbuki, enzi tunasoma tulikua tunamuita Don King kutokana na style yake ya nywele), nilipofika ofisini kwake nikakuta msg mlangoni kwake kwamba yuko hospitali na kama mtu ana shida ya kiofisi aende kwa secretary ofisi namba 7.
Hapo ofisi namba 7 ndio nilipokuta vituko. Kwanza yule mama akakataa katakata kuandika barua, ila akaniambia wao huwa wana vimitihani vyao (mradi wao) ambapo natakiwa kulipa elfu 40, ila kama ninataka sana hiyo barua basi nilipe hiyo 40 halafu yeye atanifanyia huo mpango, niwe kama nimefanya mtihani, atanijazia hiyo marks sijui A tupu sijui nini (anajua mwenyewe alitaka ajaze nini) halafu nitapata hicho cheti chao na barua ninayoitaka
HAPA NDIPO CHUO CHETU Kilipofika!