ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Miongoni mwa masharti ya kujiunga na shahada ya Uzamili katika vyuo vingi vya nje (Ulaya, Marekani na kwingineko) ni kuwa na uthibitisho wa kujua lugha ya Kiingereza kwa usahihi. Katika hili unapaswa pamoja na cheti chako cha shahada ya kwanza, transcipts nk, uwasilishe cheti cha masomo ya Lugha ya Kiingereza.
Japo kuwa Kiingereza ndio lugha ya kufundishia Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na moja ya kozi ya lazima ukiwa hapo ni somo la mawasiliano (communication Skills), unapotaka kupata uthibitisho wa chuo Kikuu cha Dare es salaam (UDSM), inaoneka kuwa chuo hicho kupitia Idara yake ya Lugha kinatoa tena kwa gharama ya zaidi ya Tshs. 10, 000 Cheti cha kinachoitwa " Certificate of Proficiency in English" (CPE).
Kwa wale ambao wamewahi kupata cheti hicho kwa kweli unaweza kuona ni bishara ya kitapeli inafanyika hapo, kwani kwa mtazamo halisi, cheti hicho ambacho binafsi nilikipata kwa zaidi ya Tshs, 15, 000 ni kijikaratasi tu cha "A4" ambacho kinatolewa na Idara ya "Foreign Languages & Linguistics" na kimesainiwa na kimegongwa muhuri wa "rubbers stamp" na "Coordinator - Communication Skills Unit". pia, binafsi hata nilipolipia, fedha nilitoa kwa Katibu mhtasi (sekretari) na kupewa risiti ya "pay cash" isiyo na nembo yeyote ya UDSM...
Cha ajabu, tofauti na cheti cha shahada na Transcript ambavyo unaweza kutoa na kutuma nakala kivuli kwa kila chuo unachoomba, hiki cha kujua Kiingereza cha UDSM inabidi uwe na nakala halisi (orignal copy) kwa kuwa kwenye kila cheti wanaandika "Only orignal copies with official stamp should be considered genuine" yaani wakimaanisha hako ka "rubber stamp" ka Mratibu wa Kitengo cha Lugha ndo jenuini yenyewe.
na UDSM wanataka ulipie fedha kila nakala watakayokupa. Cha kusikitisha zaidi, cheti hicho cha UDSM kimekataliwa na zaidi ya vyuo vitatu kuwa hakina hadhi yeyote ya kuthibitisha uwezo wa kujua kiingereza. Hivyo kulazimika kuchukua masomo ya Lugha yanayotolewa na British Council.
Ninachojiuliza, hivi ni kwanini ikiwa mtu umesoma hapo UDSM na kufuzu vizuri somo la "Communication Skills" bado chuo kna shindwa kukusaidia na badala yake kuachia huu uhuni wa baadhi ya walimu wa Idara ya Lugha kujipatia fedha kupitia hivi vyeti ambavyo pangine havimsaidii mhusika au kwa muonekano haviwezi kuwa na gharama kubwa ya zaidi ya Tshs. 10, 000??.
Ni kama ka ufisadi fulani hivi!!.
Japo kuwa Kiingereza ndio lugha ya kufundishia Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na moja ya kozi ya lazima ukiwa hapo ni somo la mawasiliano (communication Skills), unapotaka kupata uthibitisho wa chuo Kikuu cha Dare es salaam (UDSM), inaoneka kuwa chuo hicho kupitia Idara yake ya Lugha kinatoa tena kwa gharama ya zaidi ya Tshs. 10, 000 Cheti cha kinachoitwa " Certificate of Proficiency in English" (CPE).
Kwa wale ambao wamewahi kupata cheti hicho kwa kweli unaweza kuona ni bishara ya kitapeli inafanyika hapo, kwani kwa mtazamo halisi, cheti hicho ambacho binafsi nilikipata kwa zaidi ya Tshs, 15, 000 ni kijikaratasi tu cha "A4" ambacho kinatolewa na Idara ya "Foreign Languages & Linguistics" na kimesainiwa na kimegongwa muhuri wa "rubbers stamp" na "Coordinator - Communication Skills Unit". pia, binafsi hata nilipolipia, fedha nilitoa kwa Katibu mhtasi (sekretari) na kupewa risiti ya "pay cash" isiyo na nembo yeyote ya UDSM...
Cha ajabu, tofauti na cheti cha shahada na Transcript ambavyo unaweza kutoa na kutuma nakala kivuli kwa kila chuo unachoomba, hiki cha kujua Kiingereza cha UDSM inabidi uwe na nakala halisi (orignal copy) kwa kuwa kwenye kila cheti wanaandika "Only orignal copies with official stamp should be considered genuine" yaani wakimaanisha hako ka "rubber stamp" ka Mratibu wa Kitengo cha Lugha ndo jenuini yenyewe.
na UDSM wanataka ulipie fedha kila nakala watakayokupa. Cha kusikitisha zaidi, cheti hicho cha UDSM kimekataliwa na zaidi ya vyuo vitatu kuwa hakina hadhi yeyote ya kuthibitisha uwezo wa kujua kiingereza. Hivyo kulazimika kuchukua masomo ya Lugha yanayotolewa na British Council.
Ninachojiuliza, hivi ni kwanini ikiwa mtu umesoma hapo UDSM na kufuzu vizuri somo la "Communication Skills" bado chuo kna shindwa kukusaidia na badala yake kuachia huu uhuni wa baadhi ya walimu wa Idara ya Lugha kujipatia fedha kupitia hivi vyeti ambavyo pangine havimsaidii mhusika au kwa muonekano haviwezi kuwa na gharama kubwa ya zaidi ya Tshs. 10, 000??.
Ni kama ka ufisadi fulani hivi!!.