UDSM: Hawavumi, lakini wamo....

Hamna Faculty of ECSE.Mabadiliko ya muundo wa chuo yameondoa faculties.Ipo idara ya ECSE.Kirefu chake ni Electrical,Computer and Systems Engineering.
Kwanini watu hawagraduate in time?Zipo sababu kadhaa.Nitaeleza zile nilizoshuhudia kupitia marafiki ambao ni victims.

1.Hiyo iliyokuwa faculty imekuwa na tatizo la upungufu wa walimu kwa muda mrefu sana.Hii imesababisha baadhi ya wanafunzi wa shahada za uzamili kupewa majukumu makubwa.Upo mfano wa mtu aliyelazimika kufundisha kozi nzima mwanzo hadi mwisho(from lecturing,setting up and marking exams to results)

2.Njaa.Supervisors wana njaa....mishahara midogo.Hivyo wanatoa priority kwa consultancies and well funded researches kuliko supervision ya wanafunzi hao.Hili lina uhusiano na 1 hapo juu.Imagine kitivo kina uhaba wa walimu.Waliopo njaa kali.Idadi ya wanafunzi inaongezeka.Wakati huohuo wapo vijana wawili wanafanya masters.......kwanini wasifundishe ili supervisor apate muda wa kukimbizana na vijisenti mitaani?

3.Kutumiana.Yupo mwanafunzi wa masters mzuri.Anauwezo mkubwa.Hakika huyu ni wa msaada mkubwa sana kwa supervisor katika kazi zake be it research,consultancy or teaching.Kumruhusu huyu amalize masters yake mapema kutamkosesha supervisor cheap labour.

Mama Macha yupo.Kwa taarifa yako sasa amehamishiwa huko huko ECSE.Kama unamgwaya huyu usisogee ECSE kabsa ha ha haaa


BabaJ,

Asante sana kwa ufafanuzi. Hayo mabadiliko ya muundo wa kuondoa faculties nilikuwa sijayapata. Nilijua CoET ina faculties tatu ECSE, MECHE na CEBE??? ECSE ikiundwa na idara tatu tofauti.


Sasa kama hali ndiyo hivyo, hizo pesa zinazotoka kwa wafadhili zinatolewa tu alimradi zipo ama zina malengo gani? Mimi ningetegemea kwamba kila baada ya muda ni lazima ripoti ionyeshe ni wanafunzi wangapi wameweza kumaliza kutokana na scholarships hizo na pia research findings zao ziwasilishwe kwa wahusika katika muda uliowekwa. Sasa kama supervisor anaweza kuwa na mamlaka makubwa kiasi cha kuamua mwanafunzi amalize lini hata kama akisoma Master kwa miaka sita (badala ya 2 au 3), basi kuna tatizo kubwa sana hapo. Au hizo contracts kati ya mwanafunzi na chuo (c/o sponsor) hazionyeshi muda wa mwanafunzi kumaliza program yake?
 
Hamna Faculty of ECSE.Mabadiliko ya muundo wa chuo yameondoa faculties.Ipo idara ya ECSE.Kirefu chake ni Electrical,Computer and Systems Engineering.

Kwanini watu hawagraduate in time?Zipo sababu kadhaa.Nitaeleza zile nilizoshuhudia kupitia marafiki ambao ni victims.

1.Hiyo iliyokuwa faculty imekuwa na tatizo la upungufu wa walimu kwa muda mrefu sana.Hii imesababisha baadhi ya wanafunzi wa shahada za uzamili kupewa majukumu makubwa.Upo mfano wa mtu aliyelazimika kufundisha kozi nzima mwanzo hadi mwisho(from lecturing,setting up and marking exams to results)

2.Njaa.Supervisors wana njaa....mishahara midogo.Hivyo wanatoa priority kwa consultancies and well funded researches kuliko supervision ya wanafunzi hao.Hili lina uhusiano na 1 hapo juu.Imagine kitivo kina uhaba wa walimu.Waliopo njaa kali.Idadi ya wanafunzi inaongezeka.Wakati huohuo wapo vijana wawili wanafanya masters.......kwanini wasifundishe ili supervisor apate muda wa kukimbizana na vijisenti mitaani?

3.Kutumiana.Yupo mwanafunzi wa masters mzuri.Anauwezo mkubwa.Hakika huyu ni wa msaada mkubwa sana kwa supervisor katika kazi zake be it research,consultancy or teaching.Kumruhusu huyu amalize masters yake mapema kutamkosesha supervisor cheap labour.

Mama Macha yupo.Kwa taarifa yako sasa amehamishiwa huko huko ECSE.Kama unamgwaya huyu usisogee ECSE kabsa ha ha haaa

tunacho taka ni kuondoa bureaucrases ktk kazi sasa wewe unatetea kwamba ni bora supervisor amtumie mwanafunzi ktk issues zake na amcheleweshe kumaliza? huu ni upuuzi na haufai kutukuzwa.
 
Kimsingi ni kwamba, masurufu yake na wenzake, shemeji yangu huyu, yanatoka nje... siwezi kutaja nchi gani pia... lakini yanapitia mkono wa UD... na kumbukeni, hapo kuna "watu". Pesa ni shetani, ukiipitishia mkononi mwa mtu itapigwa panga.... na kweli, panga linapita hapo, mpaka fungu linapowafikia wanazuoni hao, linakuwa dogo kiasi cha kukatisha tamaa.

Wenyewe hawawezi kusema ukweli - kwa kuwa wahadhiri, wanaomega fungu hilo ndio wenye kushika mpini, wakati wanazuoni wameshika makali - kwani wakithubutu kulalamika, habari zitarudi UD, na wao watakuwa wamejiweka kwenye tafrani ya kunyimwa hata vyeti vyao, kwa kufelishwa mitihani MAKUSUDI!

Ninachouliza, hawa wahadhiri wanataka nini? Maisha yenyewe haya ni ya shida. Wanazuoni wamesoma, kwa shida, wamefaulu, wanastahili kupewa mafungu yao kwa asilimia 100! Wahadhiri wanalipwa mishahara lukuki, lakini wana tamaa kupita kiasi. Fedha za ufadhili zinatumwa kwa matumizi ya wanazuoni, hususan wanapofanya utafiti kwa ajili ya Shahada zao za Uzamili (Masters).

Je, hili, pamoja na lile za "maksi za chupi" yatakwisha lini?

Mwandishi wa mada hii naona amechanganya udaku na ukweli,


(a) Ukweli wake nimeuweka katika rangi ya buluu, na wala hauhitaji mjadala.

(b) Udaku nimeuweka katika rangi neykundu na ndio nitakaojadili kwa kifupi kama ifuatavyo:


  1. Pesa sa scholasrhip za wanafunzi hazipitii mikononi mwa wahadhiri; pesa hizi huja moja kwa moja hadi kwenye utawala wa chuo ambao unachukua sehemu ambayo ni haki yao, yaani karo na gharama zozote ambazo chuo kinamdai mwanafunzi, halafu zile za masurufu ya mwanafunzi anapewa mwenyewe. Ni kama ambavyo chuo kinavyofanya kwa hela zinazotoka serikalini kwa ajili ya wanafundi wa digrioi ya kwanza. Labda nimkumbukumbushewa mwandishi kuwa wahadhiri wa chuo kikuu wana majukumu matatu makuu: kufundisha, kufanya utafiti na kutoa huduma kwa jamii kulingana na taaluma zao. Jukumu hili la utafiti ni pana sana kwani linahusiaha mambo kama vile kuandika makala na kuzitoa ama kwenye mikutano na makongamano au kwenye majarida mbalimbali yanayohusiana na taaluma zao, kuandika vitabu, kutoa ushauri wa kitaaluma, na kuandika proposals (sijui kiswahili chake :confused:) za kutafuta pesa kwa ajili ya kusaidia tafiti zao. Pesa za utafiti zitokanazo na proposala hizo huweza kutumika pia kuwalipa wanafunzi mbalimbali wanaomsaidia kufanya utafiti wake. Mwanafunzi anayelipwa kutokana na pesa hzio hawezi kudai kuwa ana skolaship, bali yeye ni mwajiriwa wa kumsaidi mwalimu ambaye ndiye anayempangia malipo kulingana na uzito wa kazi yenyewe pamoja na bajeti yake. Usimamizi wa malipo hayo haufanywi na mhadhiri bali kuna ofisi nhuru inayosimamia pesa za wafadhili wa tafiti mablimbali chuoni. Kwa hiyo madai hayo kuwa wahadhiri wanachukua sehemu ya pesa za skolaship si kweli. Kama shemeji yake analipwa masurufu kutokana na pesa za utafiti alizonazo mhadhiri basi asilalamike.
  2. Hili la maksi za chupi ni jambo ambalo nimelisikia sana; watu wanaliongelea bila kutoa ushahidi wowote: kwa hiyo ni la kidaku, na kwa bahati mbaya mwandishi naye kanasa kwenye mtego huo wa udaku. Ninaweza kutoa maelezo mapana kuonyesha kuwa hii dhana ya maksi za chupi ni uwongo mkubwa sana, lakini kwa sasa hivi nitasema moja tu, kuwa chuo kikuu cha Dar es Salaam ni moja ya vyuo vichache ambavyo bado vinatumia external examiners kuhakiki na kuthibitisha uhalali wa maksi zitolewezo na wahadhiri kwenye mitihani ya mwisho. Maksi anazopata mwanafunzi huhakikishwa na huyu external examiner, kwa hiyo kama ni za chupi (kwa maana inayotumiwa na waenezaji wa uwongo huu) basi ni ina maana hata external examiner naye alitembea na msichana huyo jambo ambalo ni gumu sana hasa kwa vile hawa external examiners hutokea nchi za nje.
 
Mimi hii post imezidi kutia machungu na inasikitisha sana, umenikumbusha kipindi nasoma hapo unakuta demu anafaulu kwa alama za mezani,anazirai kwenye chumba cha mtihani yaani paper imemuona,anatetemeka kama ameshikwa ugoni, matokeo yanatoka A,absolutely nonsense, ndo maana hata wasomi siku hizi makazini ni aibu tupu,Tubadilike wale tunaomba alama za mezani au degree za vichupi na maprof nao watende haki.
 
Leo nimepata habari za kusikitisha. Kuna shemeji yangu, anasomea Masters yake huko UDSM, zahama anazozikabili, kwa kweli, kama angekuwa mtu mwenye "munkari" wala asingemaliza masomo yake...

Taarifa nilizonazo ni kwamba, baada ya kumaliza Bachelors yake hapo UD alifanya kazi kama Graduate Teaching Assistant (wengine wanasema Assistant Lecturer-Trainee). Aliifanya kazi yake hiyo kwa ufanisi mkubwa, na kwa kuwa aligraduate top of his class, basi, kupata full academic scholarship (international) haikuwa ngumu sana kwake na wenzake. Siwezi kutaja yuko idara gani, kwa kuhofia yeye kufikwa na madhara ambayo yanaweza kuhatarisha mustakabali wake hapo UD.

Kimsingi ni kwamba, masurufu yake na wenzake, shemeji yangu huyu, yanatoka nje... siwezi kutaja nchi gani pia... lakini yanapitia mkono wa UD... na kumbukeni, hapo kuna "watu". Pesa ni shetani, ukiipitishia mkononi mwa mtu itapigwa panga.... na kweli, panga linapita hapo, mpaka fungu linapowafikia wanazuoni hao, linakuwa dogo kiasi cha kukatisha tamaa.

Wenyewe hawawezi kusema ukweli - kwa kuwa wahadhiri, wanaomega fungu hilo ndio wenye kushika mpini, wakati wanazuoni wameshika makali - kwani wakithubutu kulalamika, habari zitarudi UD, na wao watakuwa wamejiweka kwenye tafrani ya kunyimwa hata vyeti vyao, kwa kufelishwa mitihani MAKUSUDI!

Ninachouliza, hawa wahadhiri wanataka nini? Maisha yenyewe haya ni ya shida. Wanazuoni wamesoma, kwa shida, wamefaulu, wanastahili kupewa mafungu yao kwa asilimia 100! Wahadhiri wanalipwa mishahara lukuki, lakini wana tamaa kupita kiasi. Fedha za ufadhili zinatumwa kwa matumizi ya wanazuoni, hususan wanapofanya utafiti kwa ajili ya Shahada zao za Uzamili (Masters).

Je, hili, pamoja na lile za "maksi za chupi" yatakwisha lini?

Jamani, huu si ufisadi huu?

Kazi kwenu!

./Mwana wa Haki

NA BADO, ntasema zaidi.... vitisho havintishi.... kwani kufa si WAJIBU tu? Niogope? Nyoooooooooooo!
ee bwana umenikuna mno na post yako, huo mchezo uko sehemu nyingi mno! kwanza mpe pole huyo shemeji yako mwambie hii ndo nchi ya wadanganyika ambao hawajui kudai haki,wao kila kitu husema "tunamwachia MUNGU" huku wakiumia na kupata tabu zisizo na msingi. kuna bosi mmoja wa tanroad niliongea naye akaniambia eti kama barara itagharimu milioni kumi basi ili kufikia kiwango hicho hulazimika kukiongezea mara tatu zaidi ili hata wakipigapiga panga wapate kiasi hicho, kweli huo ni ufisadi lakini huu ndo ukomo wake kwani vijana NGUVU TUNAZO, UWEZO TUNAO, NA NIA TUNAYO kwa nini tusiwakomeshe? tuamke jamani.
 
Mheshimiwa spika naomba sasa nieleze kisa kinacho fanana na hicho na hapa sita ficha. Pale UDSM, college of Engineering & Technology hayo yamefanyika kwa vijana waliokuwa wanasoma masters ya materilas engineering under the sponsorship of Swedish people (SIDA-Sarec).

Kuna pia wale wamesoma masters za electrical engineering, wote pesa ilikuwa inatoka sweden ikionyesha walipwe dola 300 za marekani na hapa tunazungumza mwaka 2002 lakini walikuwa wanalipwa kiwango cha UDSM ambacho kilikuwa ni shs. 150 000/-. Ukiwauliza kwa nini wazungu wale wanapokuja mbona hamlalamiki wanasema Dr. Tesha atatumaliza.

Hivi kumbe Engineering bado wanamchezo huu?, kuna jamaa yangu alikuwa anasoma Civil Eng. miaka hiyo, sasa kuna pesa za project ya mwaka wa mwisho sijui kama bado zipo. Hela ile watu walikuwa wanatakiwa kulipwa kama laki nne hivi, regardless unafanyia watu. Jamaa alikuwa anafanyia Dar, alikuwa ananilalamikia bwenini project cordinator wao Msambichaka alikuwa anawabana, yaani nauli unatakiwa kuonesha ticketi za daladala ili aku-refund hela ya nauli jamaa alizichanga akaambulia shs 3,000 tu maana nauli ilikuwa mia kipindi hicho.

Haya mambo kwa UDSM ni possible hasa kwenye vitivo vyenye shule ambayo haitabiriki, ni lazima utoe shingo yango ya kwa prof, vinginevyo humalizi shule utakuwa-discontinued tu.
 
Kichuguu

Maksi za chupi ni sawa na rushwa. Hivi ushawahi kumwona au kusikia msichana "aliyemegwa" (samahani kwa usemi wa kihuni.... Mhe. Spika, naomba kuongea hovyo hovyo!) na mhadhiri akikubali kwamba ni kweli "alimegwa" na kupewa "maksi za chupi"? Hii ni sawa na kumwona au kusikia "trafiki" akikubali kwamba pale Kabuku alipewa elfu 10 na konda wa basi la Mohammed Trans...

Niseme zaidi?

Usijifanye HUIJUI NJI HII!

./Mwana wa Haki
 
Ok, sawa, pesa zapitia kwenye "Department", na wanapiga mapanga yao.... kinachobakia ni kiduchu ile mbaya.... kwani, mtu ukipewa "scholarship" maana yake nini haswa? Mpaka na "tuition fees" unakatwa pia? "Research grant" je? Kama hesabu haitoshi, hiyo "research" utaifanya kwa fungu lipi?

"Maksi za chupi"? Hili mbona ni la toka 90s? Au wewe hukusoma au hukuwa na ndugu wa kike waliosoma UD? Waulize... utabaki mdomo wazi!

./Mwana wa Haki
 
Mwandishi wa mada hii naona amechanganya udaku na ukweli,


(a) Ukweli wake nimeuweka katika rangi ya buluu, na wala hauhitaji mjadala.

(b) Udaku nimeuweka katika rangi neykundu na ndio nitakaojadili kwa kifupi kama ifuatavyo:


  1. Pesa sa scholasrhip za wanafunzi hazipitii mikononi mwa wahadhiri; pesa hizi huja moja kwa moja hadi kwenye utawala wa chuo ambao unachukua sehemu ambayo ni haki yao, yaani karo na gharama zozote ambazo chuo kinamdai mwanafunzi, halafu zile za masurufu ya mwanafunzi anapewa mwenyewe. Ni kama ambavyo chuo kinavyofanya kwa hela zinazotoka serikalini kwa ajili ya wanafundi wa digrioi ya kwanza. Labda nimkumbukumbushewa mwandishi kuwa wahadhiri wa chuo kikuu wana majukumu matatu makuu: kufundisha, kufanya utafiti na kutoa huduma kwa jamii kulingana na taaluma zao. Jukumu hili la utafiti ni pana sana kwani linahusiaha mambo kama vile kuandika makala na kuzitoa ama kwenye mikutano na makongamano au kwenye majarida mbalimbali yanayohusiana na taaluma zao, kuandika vitabu, kutoa ushauri wa kitaaluma, na kuandika proposals (sijui kiswahili chake :confused:) za kutafuta pesa kwa ajili ya kusaidia tafiti zao. Pesa za utafiti zitokanazo na proposala hizo huweza kutumika pia kuwalipa wanafunzi mbalimbali wanaomsaidia kufanya utafiti wake. Mwanafunzi anayelipwa kutokana na pesa hzio hawezi kudai kuwa ana skolaship, bali yeye ni mwajiriwa wa kumsaidi mwalimu ambaye ndiye anayempangia malipo kulingana na uzito wa kazi yenyewe pamoja na bajeti yake. Usimamizi wa malipo hayo haufanywi na mhadhiri bali kuna ofisi nhuru inayosimamia pesa za wafadhili wa tafiti mablimbali chuoni. Kwa hiyo madai hayo kuwa wahadhiri wanachukua sehemu ya pesa za skolaship si kweli. Kama shemeji yake analipwa masurufu kutokana na pesa za utafiti alizonazo mhadhiri basi asilalamike.
  2. Hili la maksi za chupi ni jambo ambalo nimelisikia sana; watu wanaliongelea bila kutoa ushahidi wowote: kwa hiyo ni la kidaku, na kwa bahati mbaya mwandishi naye kanasa kwenye mtego huo wa udaku. Ninaweza kutoa maelezo mapana kuonyesha kuwa hii dhana ya maksi za chupi ni uwongo mkubwa sana, lakini kwa sasa hivi nitasema moja tu, kuwa chuo kikuu cha Dar es Salaam ni moja ya vyuo vichache ambavyo bado vinatumia external examiners kuhakiki na kuthibitisha uhalali wa maksi zitolewezo na wahadhiri kwenye mitihani ya mwisho. Maksi anazopata mwanafunzi huhakikishwa na huyu external examiner, kwa hiyo kama ni za chupi (kwa maana inayotumiwa na waenezaji wa uwongo huu) basi ni ina maana hata external examiner naye alitembea na msichana huyo jambo ambalo ni gumu sana hasa kwa vile hawa external examiners hutokea nchi za nje.

Suala la maksi za chupi siyo la kiudaku; haya mambo yaliwahi kutokea katika baadhi ya idara hapo UDSM na hadi wasichana waliohusika ndiyo waliitoa hewani baada ya kukorofishana wao kwa wao. Kama sikosei walikuwa Engineering. Ila cha muhimu hapa siyo vizuri kugeneralize kwamba UDSM kuna maksi za chupi. Ni kwa cases chache kama hizo ambako walimu husika ni wachafu wa kimaadili.

External examiner siyo rahisi kugundua mchezo huo. Kwani watagunduaje kama mtihani uli-leak?

Pili, kuna continuous assessment ambayo inaplay part katika ufaulu wa mwanafunzi. External examiners wao wana-assess final exams tu. Kwa hiyo kuna uwezekano wa mwanafunzi kupendelewa kupitia category hii pia (continous assessment: tests, homeworks, etc).

Kuna lecturer mmoja (sasa marehemu) hapo UDSM ambaye alikuwa akiuza mitihani kwa kumtumia mke wake. External examiners hawakuwahi kuligundua hili hadi pale wanafunzi wenyewe waliokuwa wakiuziwa mitihani walipoamua kumchoma kwa Utawala wa Chuo naye akasimamishwa kazi kabla ya kufukuzwa kabisa.

Sasa katika kesi kama hiyo, mtu hauwezi uka-generalize kwamba UDSM wanauza mitihani. Vivyo hivyo na suala la maksi za chupi.
 
tunacho taka ni kuondoa bureaucrases ktk kazi sasa wewe unatetea kwamba ni bora supervisor amtumie mwanafunzi ktk issues zake na amcheleweshe kumaliza? huu ni upuuzi na haufai kutukuzwa.

Mkulu tuko pamoja katika kupambana na urasimu(hivi ndio byurokrasi eeeh?).Wala siutetei kabisa.Read between those lines.Nimejaribu kueleza nilichopata kutoka kwa wahanga wa urasimu huo.
 
Hivi kwanini ham-binafsishi vyuo vyenyewe? Yaani kwa maisha ya kitanzania, elimu ya VETA tu inatosha.
 
Hapana, huu pia ni upotoshaji. Kuna tofauti kubwa sana kati ya scholarship ya sida/SAREC na mashirika mengine kama DAAD. Moja ya tofauti ni kwamba DAAD wanatoa scholarship kwa mwanafunzi mmojammoja (individual support), wakati sida/SAREC wao wanatoa scholarship kwa taasisi (institutional support) for specific activity. Kwa hiyo hela ya scholarship inatolewa kwa chuo, na chuo ndiyo inaamua kinatoa shilingi ngapi kwa kila mwanafunzi kwa mujibu wa mwongozo uliopo katika prospectus.

Ufafanuzi mwingine muhimu wa kuzingatia ni kwamba kiwango cha pesa kinachoonyeshwa kwa mwanafunzi haimanisha kwamba yote ni kwa ajili ya 'stipend'; katika hizohizo kuna sehemu ina-cover administrative costs, etc. Sasa mambo kama haya wanafunzi wetu wa uzamili wangekuwa wanauliza wangekuwa wanapata ufafanuzi kirahisi kabisa. Sasa kama wanaogopa kuuliza, then ni vigumu sana kujua ukweli watabaki ku-speculate!

PS: Mimi naeleza haya kwa sababu mie pia nilisoma masters yangu kwa scholarship yangu hiyo, japokuwa ilikuwa ni enzi hizo kabla ya hiyo sh 150,000/=. Sisi tulikuwa wafuatiliaji; tulifahamu ni kiasi gani sida/SAREC wanatoa, na kiasi gani kinapaswa kwenda moja kwa moja kwa mwanafunzi (yaani direct student costs)-we got the answers because we did not fear to ask!

JF kuna watu wa kila aina ila tatizo kuna watu wakishaanzisha hoja wanalazimisha kutoelewa mpaka mwisho. Naungana kabisa na Mr.Mkumbo kwamba hela iliyotolewa Chuoni wanafunzi hulipwa kutokana na jinsi prospectus inavyoeleza. Tatizo baadhi ya wanafunzi hawasomi hata prospectus zao kama zimesemaje wakisikia uvumi basi wanakomaa nao mpaka mtaani na kwenye club za Pombe kuanzisha topic ya siku. Tuwe na tabia ya kusoma Terms of Reference vyuoni/kazini ili tusije tukaaibika na hoja zetu ambazo maelezo yapo wazi kwenye documents tulizokwishapewa awali.
 
Mh! Nani asili yao kusoma aisee? Mbona unataka kutuangusha blaza tunakutegemea utuokoe kumbe mwenzetu unaelekea kukata tamaa hivyo? Kaza buti twende blaza. Tutafika tu,mdogomdogo kaka!
 
JF kuna watu wa kila aina ila tatizo kuna watu wakishaanzisha hoja wanalazimisha kutoelewa mpaka mwisho. Naungana kabisa na Mr.Mkumbo kwamba hela iliyotolewa Chuoni wanafunzi hulipwa kutokana na jinsi prospectus inavyoeleza. Tatizo baadhi ya wanafunzi hawasomi hata prospectus zao kama zimesemaje wakisikia uvumi basi wanakomaa nao mpaka mtaani na kwenye club za Pombe kuanzisha topic ya siku. Tuwe na tabia ya kusoma Terms of Reference vyuoni/kazini ili tusije tukaaibika na hoja zetu ambazo maelezo yapo wazi kwenye documents tulizokwishapewa awali.

Wewe na Kitila Mkumbo mnabadili hoja, mnatengeneza hoja yenu halafu mnaizungumzia hiyo hoja yenu mpya. Na kwa hakika mtakuwa mko sawa mpaka pale mtakaporudi kwenye hoja ya msingi. ( [ame=http://en.wikipedia.org/wiki/Straw_man]Straw man - Wikipedia, the free encyclopedia[/ame] )

Argument ya kwamba mtu afuatilie kwa undani anatakiwa alipwe kiasi gani na akikuta tofauti ndio alalamike ni argument ya nzurii kabisa. Ila sidhani kama ni relevant kwenye hili. Kuna uwezekano kukawa na watu wanalalamika, ila tu hawajajua kwamba wanacholipwa ndicho wanachostahili. Sawa! Huu ni upande mmoja wa shilingi. Na hawa watu wanakiwa wakae kimya.

Upande mwingine wa shilingi ni kwamba yawezekana kuna wanaojua wanatakiwa walipwe kiasi gani na hawalipwi hivyo. Na upande huu ndio ambao unazungumziwa.

Ku-prove kwamba kuna uwezekano, ka mfano kamoja kanatosha. Ku-prove kwaba hakuna uwezekano wa jambo flani, mantiki inadai kamfano kako hakatoshi, hata kama wewe ndio muhusika na shahidi mkuu katika hako ka mfano. Na mantiki inadai kama unataka ku-prove kwamba hakuna uwezekano kwa kutumia mifano, inabidi uweze kupitia kila case na kuonesha kwamba kila moja ya hizo case zinasupport argument yako.

Sasa wewe kama hujawahi kupigwa panga kihivyo, au hujawahi kusikia rafiki yako wa karibu kapigwa panga kihivyo, utakuwa sawa ukisema huamini kwamba hiyo kitu inatokea. Lakini ukisema kwamba unajua kwamba hiyo kitu haitokei, pengine waweza kuwa sawa. Lakini utaweza kuridhisha mantiki pale tu utakapoweza kuonyesha kwamba taratibu za utoaji wa hizo pesa haziruhusu kamwe mtu kupigwa panga kihivyo, na uweze kuonyesha kwamba hakuna mianya inayoruhusu hivyo kamwe. Na haitoshi kusema tu kwamba kuna taratibu, kwa sababu hata kule jikoni BOT taratibu zipo na watu wamekomba vijisent kama kawa.

Hata mimi nawaheshimu sana wale ma-prof na ma daktari wetu. Lakini ntakuwa nadanganya kusema kwamba naamini kwamba wote ni watu safi na hakuna hata mmoja wao mwenye vitamaa flani hivi. Vitamaa ambavyo vitasababisha akipata mwanya wa kubamiza atabamiza, au akikuta kuna jinsi ya kubana wanafunzi wake ili yeye ale chajuu atabana.


Hebu nisaidie kitu kimoja. Hivi hiyo prospectus inasema mwanafunzi wa engineering anatakiwa alipwe kiasi gani kwa ajili ya final year project. Kama haisemi then argument yako ya kwamba "wanaolalamika wanatakiwa wasome prospectus" inakuwa imekufa. Kama inasema, then nenda kawaulize pale kama ndicho wanacholipwa, na uwaulize huwa wanalipwaje. Sisemi kwamba wanaibiwa, kwa sababu sijui. Ila tu nadhani ukifanya hivyo utaelewa kwamba majibu marahisi marahisi kama "watu hawasomi prospectus" yanaweza yakawa si majibu sahihi. Na pengine unakuwa sahihi zaidi ukisema "sijui".
 
Wewe na Kitila Mkumbo mnabadili hoja, mnatengeneza hoja yenu halafu mnaizungumzia hiyo hoja yenu mpya. Na kwa hakika mtakuwa mko sawa mpaka pale mtakaporudi kwenye hoja ya msingi. ( Straw man - Wikipedia, the free encyclopedia )

Argument ya kwamba mtu afuatilie kwa undani anatakiwa alipwe kiasi gani na akikuta tofauti ndio alalamike ni argument ya nzurii kabisa. Ila sidhani kama ni relevant kwenye hili. Kuna uwezekano kukawa na watu wanalalamika, ila tu hawajajua kwamba wanacholipwa ndicho wanachostahili. Sawa! Huu ni upande mmoja wa shilingi. Na hawa watu wanakiwa wakae kimya.

Upande mwingine wa shilingi ni kwamba yawezekana kuna wanaojua wanatakiwa walipwe kiasi gani na hawalipwi hivyo. Na upande huu ndio ambao unazungumziwa.

Ku-prove kwamba kuna uwezekano, ka mfano kamoja kanatosha. Ku-prove kwaba hakuna uwezekano wa jambo flani, mantiki inadai kamfano kako hakatoshi, hata kama wewe ndio muhusika na shahidi mkuu katika hako ka mfano. Na mantiki inadai kama unataka ku-prove kwamba hakuna uwezekano kwa kutumia mifano, inabidi uweze kupitia kila case na kuonesha kwamba kila moja ya hizo case zinasupport argument yako.

Sasa wewe kama hujawahi kupigwa panga kihivyo, au hujawahi kusikia rafiki yako wa karibu kapigwa panga kihivyo, utakuwa sawa ukisema huamini kwamba hiyo kitu inatokea. Lakini ukisema kwamba unajua kwamba hiyo kitu haitokei, pengine waweza kuwa sawa. Lakini utaweza kuridhisha mantiki pale tu utakapoweza kuonyesha kwamba taratibu za utoaji wa hizo pesa haziruhusu kamwe mtu kupigwa panga kihivyo, na uweze kuonyesha kwamba hakuna mianya inayoruhusu hivyo kamwe. Na haitoshi kusema tu kwamba kuna taratibu, kwa sababu hata kule jikoni BOT taratibu zipo na watu wamekomba vijisent kama kawa.

Hata mimi nawaheshimu sana wale ma-prof na ma daktari wetu. Lakini ntakuwa nadanganya kusema kwamba naamini kwamba wote ni watu safi na hakuna hata mmoja wao mwenye vitamaa flani hivi. Vitamaa ambavyo vitasababisha akipata mwanya wa kubamiza atabamiza, au akikuta kuna jinsi ya kubana wanafunzi wake ili yeye ale chajuu atabana.


Hebu nisaidie kitu kimoja. Hivi hiyo prospectus inasema mwanafunzi wa engineering anatakiwa alipwe kiasi gani kwa ajili ya final year project. Kama haisemi then argument yako ya kwamba "wanaolalamika wanatakiwa wasome prospectus" inakuwa imekufa. Kama inasema, then nenda kawaulize pale kama ndicho wanacholipwa, na uwaulize huwa wanalipwaje. Sisemi kwamba wanaibiwa, kwa sababu sijui. Ila tu nadhani ukifanya hivyo utaelewa kwamba majibu marahisi marahisi kama "watu hawasomi prospectus" yanaweza yakawa si majibu sahihi. Na pengine unakuwa sahihi zaidi ukisema "sijui".

hapa UDSM kuna matatizo makubwa sana katika matumizi ya pesa,
watu wafanye vi interview kwa wanafunzi wa MSc na PhD wataaambiwa hivyo.
tatizo la kuibiwa lipo na pia kutopata pesa kwa wakati ndiyo kubwa zaidi, kuna wanafunzi wengi research zao zimesimama wakisubili pesa wakati tayari zilikuwa budgeted for.
hiyo ya kumcheleweshea mtu pesa yake ni wizi
(justice delayed is justice denied)
 
[/kuwa chuo kikuu cha Dar es Salaam ni moja ya vyuo vichache ambavyo bado vinatumia external examiners kuhakiki na kuthibitisha uhalali wa maksi zitolewezo na wahadhiri kwenye mitihani ya mwisho. Maksi anazopata mwanafunzi huhakikishwa na huyu external examiner, kwa hiyo kama ni za chupi (kwa maana inayotumiwa na waenezaji wa uwongo huu) basi ni ina maana hata external examiner naye alitembea na msichana huyo jambo ambalo ni gumu sana hasa kwa vile hawa external examiners hutokea nchi za nje.]
[/LIST]

Kuhusu external examiners. Ninachofahamu ni kwamba external xaminer akija chuoni huwa hawapitii kazi zote za wanafunzi, hii itakua mzigo mkubwa sana na kama mumuegundua huwa hawakai mda mrefu. Hebu fikiria idadi ya wanafunzi wote waliopo pale chuo mitihani yao yote ipitiwe mmojammoja. Wanachofany ni kupitia mitihani za wale walipata maksi za juu sana na wale walipewa maksi za chini sana kisha wanatoa ripoti yao. Kwahiyo naungana na mdau aliyesema uwezekano wa kuweko maksi za chupi kutolewa upo, kwani mwanafunzi anaweza pewa maksi za kati ambazo external huwa hawazipitii.
 
Back
Top Bottom