UDSM hali si shwari

Mzee wa Gumzo

Senior Member
Apr 21, 2008
197
5
Jamani mzee wa gumzo hapa nilipo sina amani,hali siyo shwari kabisa hapa mlimani panapojulikana kuwa kitovu cha wanazuoni (sijui kama bado ndivyo au la).Hali bado ni wasiwasi tangu jana mchana.Yaani ni vurugu mtindi mmoja.

Kama hauna habari pengine nikupashe tu kuwa jana hali ya mgomo na maandamano ambavyo vilikuwepo hapa tangu wiki iliyopita jana viliingia katika hatua mbaya baada ya askari wa kutuliza ghasia maarufu kama FFU kumwagwa chuoni wakiwa na gari lao la maji ya kuwasha na kutimuana na wanachuo wenye ghadhabu.

Jana tu wnafunzi 39 walitiwa mbaroni na askari huku polisi wawili wakijeruhiwa,mmoja kwa kupigwa na kukatwa mguu kwa chupa na mwingine akivunjika mguu.

Leo taarifa zimesambaa kuwa wanafunzi watatu wamefariki kufuatia sakata la jana.Bado mpaka sasa hivi hazijadhibitishwa ila niandikapo haya maandamano makubwa ya wasomi wa mlimani yamepamba moto.Nyimbo zinazoimbwa leo siyo zile za kimapinduzi walizozoea kama "solidarity forever" na "kama siyo nguvu zako mwalimu Nyerere...".Leo hapa kama vile kuna maombolezo.Wasomi wanaimba nyimbo tulizozoea kuzisikia msibani kama vile "Haleluya tutaonana mbinguni","nenda nenda kapumzike" n.k.

Kama hiyo haitoshi wamebeba na msalaba uliotengenezwa kwa matawi ya mti.Kama nilivyosema hali bado ni tete na sisi tulio kwenye ofisi tumefunga milango kwa hofu ya kutokea vurugu kama jana.

Hatujui mabosi wa chuo wanajipanga vipi ila wasomi wameapa kuendelea na maandamano mpaka kieleweke.
Hatuna hakika kama kweli kuna vifo vimetokea ila muda siyo muda tutajua.

Pengine umefika wakati sasa jamii tujiulize kuna nini chuo kikuu cha dar es salaam,kila semester migomo,maandamano...mjadala huooooo waungwana.

Mzee wenu sijui nitatokavipi humu ofisini leo
 
loh kunawanafunzi waliouawa!!! hii inatokea Tanzania (kisiwa cha amani) it is difficult to believe.
 
Kuna Wengine Walibakwa Usiku

Du Mkuu shy hivi hizi habari ni za kweli? kwani nasikiliza BBC muda huu (Internet), Mkandara na Dkt wa Mwananyamala wanasema hakuna aliyekufa. Wanadai huyo mjamzito ni mzima na hakuna madai ya ubakaji yaliyo ripotiwa au hata BBC ni kimeo siku hizi?
 
Du Mkuu shy hivi hizi habari ni za kweli? kwani nasikiliza BBC muda huu (Internet), Mkandara na Dkt wa Mwananyamala wanasema hakuna aliyekufa. Wanadai huyo mjamzito ni mzima na hakuna madai ya ubakaji yaliyo ripotiwa au hata BBC ni kimeo siku hizi?

Huyu shy ni kimeo kweli, mara kasema wamekufa wanafunzi watatu mara wamebakwa tueleze vizuri hizo habari zako hacha utani kwenye vitu sensitive kama kifo.
 
Wanafunzi walikuwa na jazba wakasambaza uvumi kuwa kuna wanafunzi wamekufa.Siyo kweli ila ni matokeo ya hasira na jazba.Hii haikubaliki katika jamii,kudanganya kuwa wamekufa watu?tuna presha zetu wengine
 
Hawa vijana siku hizi 'kunji' zao hazifanikiwi; labda irudishwe ile sheria ya kupitia JKT kabla ya chuo vinginevyo tutaendelea kushuhudia migomo isiyopangiliwa vizuri
 
Hawa vijana siku hizi 'kunji' zao hazifanikiwi; labda irudishwe ile sheria ya kupitia JKT kabla ya chuo vinginevyo tutaendelea kushuhudia migomo isiyopangiliwa vizuri

Point.

Ukiangalia sana utakuta makunji yao ni ya jazba tuu hamna strategies. Halafu na Mukandara utadhani hajaenda nae JKT. May be hajui utawala , au ni dikteta. Pengine hafai kuongaza taasisi kama hii. Naye yuko kama hao vijana tu .

Rudisheni JKT , hamna discpline vyouni wala ujasiri wa akili . ujasiri wao ni wa uoga kabisa. Taifa kama hilo ni failure in future.
 
Back
Top Bottom