Mzee wa Gumzo
Senior Member
- Apr 21, 2008
- 197
- 5
Wakati nchi inapambana na vitendo viovu ukiwemo ufisadi na rushwa tunategemea taasisi zetu hasa za elimu ya chuo kikuu kuwa mstari wa mbele kukemea uovu huo na kuonesha mfano wa kuigwa na wanajamii wengine.
Hali inaonekana kuwa tofauti kabisa na ukweli huo.Chuo kikuu cha dar es salaam kimefunguliwa kwa muhula wa kwanza wa mwaka wa mpya wa masomo.Wanafunzi wengi wamekosa vyumba vya kulala katika mabweni ya liyopo eneo la chuo na hosteli ya mabibo.Imegundulika kuwa hali hiyo haitokani tu na uhaba wa vyumba kutokana na ongezeko la wanachuo bali kuna ufisadi wa hali ya juu.
Jana nilianza uchunguzi wangu na kufanikiwa kupata vyumba kumi na sita ambavyo vilikuwa vinauzwa na kiongozi wa DARUSO ambaye sikutajiwa jina.Nilitakiwa kulipia laki moja kwa chumba kimoja kilichopo mabibo hosteli na laki moja naishirini kwa chumba cha campus.Leo nimeendelea na uchunguzi kwa kujifanya mtafuta chumba.Nimefanikiwa kumpata mwanfunzi wa mwaka wa pili anauza vyumba viwili.vyote hivyo amepewa na kiongozi wa daruso atafute wateja wa chap chap.
Mbali na uchunguzi huu, kilio ni kikubwa sana kwa wanachuo waliokosa vyumba hasa pale wanapogundua kuwa vyumba vipo ila vimeshikiliwa na mafisadi wachache wanaoviuza kwa lengo la kujipatia fedha.
Rushwa na uchafu wa kila aina umekuwepo katika zoezi la kuwapatia vyumba wanachuo mlimani lakini siku zinavyokwenda linakuwa sugu.Haiingii akilini kama wanakuwepo viongozi wa wanafunzi wanashiriki kwenye ufisadi wa kutisha hivyo.Tuntengeneza kada ya viongozi wa namna gani kwa hapo baadae?.Jamii inayotarajiwa kuhudumiwa na watu kama hao itapona kweli?.Tuna haja gani kupambana na mafisadi wa kubwa wa EPA wakati vyuo vyetu vinatuzalishia mafisadi wenye digrii za kutungua?
Tatizo linaanzia UNIVERSITY STUDENTS ACCOMODATION BUREAU{USAB}Ni mamlaka yakusimamia suala la malazi lakini wanashindwa kuvalia njuga suala hili.Vilevile utawala wa chuo upo kimya wakati hali hii inajulikana wazi.
Tusiache kipele kikue na kugeuka donda ndugu.
Hali inaonekana kuwa tofauti kabisa na ukweli huo.Chuo kikuu cha dar es salaam kimefunguliwa kwa muhula wa kwanza wa mwaka wa mpya wa masomo.Wanafunzi wengi wamekosa vyumba vya kulala katika mabweni ya liyopo eneo la chuo na hosteli ya mabibo.Imegundulika kuwa hali hiyo haitokani tu na uhaba wa vyumba kutokana na ongezeko la wanachuo bali kuna ufisadi wa hali ya juu.
Jana nilianza uchunguzi wangu na kufanikiwa kupata vyumba kumi na sita ambavyo vilikuwa vinauzwa na kiongozi wa DARUSO ambaye sikutajiwa jina.Nilitakiwa kulipia laki moja kwa chumba kimoja kilichopo mabibo hosteli na laki moja naishirini kwa chumba cha campus.Leo nimeendelea na uchunguzi kwa kujifanya mtafuta chumba.Nimefanikiwa kumpata mwanfunzi wa mwaka wa pili anauza vyumba viwili.vyote hivyo amepewa na kiongozi wa daruso atafute wateja wa chap chap.
Mbali na uchunguzi huu, kilio ni kikubwa sana kwa wanachuo waliokosa vyumba hasa pale wanapogundua kuwa vyumba vipo ila vimeshikiliwa na mafisadi wachache wanaoviuza kwa lengo la kujipatia fedha.
Rushwa na uchafu wa kila aina umekuwepo katika zoezi la kuwapatia vyumba wanachuo mlimani lakini siku zinavyokwenda linakuwa sugu.Haiingii akilini kama wanakuwepo viongozi wa wanafunzi wanashiriki kwenye ufisadi wa kutisha hivyo.Tuntengeneza kada ya viongozi wa namna gani kwa hapo baadae?.Jamii inayotarajiwa kuhudumiwa na watu kama hao itapona kweli?.Tuna haja gani kupambana na mafisadi wa kubwa wa EPA wakati vyuo vyetu vinatuzalishia mafisadi wenye digrii za kutungua?
Tatizo linaanzia UNIVERSITY STUDENTS ACCOMODATION BUREAU{USAB}Ni mamlaka yakusimamia suala la malazi lakini wanashindwa kuvalia njuga suala hili.Vilevile utawala wa chuo upo kimya wakati hali hii inajulikana wazi.
Tusiache kipele kikue na kugeuka donda ndugu.