masingo sharili
Member
- Mar 18, 2011
- 63
- 12
Miaka michache iliyopita tangu kuanzishwa kwa chuo kikuu cha dodoma, wanafunzi wengi wa chuo hicho walihusishwa na chama tawala yaani ccm. Lakini siku za hivi karibuni idadi kubwa ya wanafunzi wa chuo hicho wameudhihirishia uma wa watanzania kuwa ni wana mapinduzi wa kweli. Mfano siku moja kabla ya uzinduzi wa sherehe za kuzaliwa kwa ccm mjini dodoma gari lililofika kutangaza chuoni hapo lilizuiliwa kwa ghadhabu na baadhi ya wanafunzi. Hata hivyo siku ya sherehe walijitokeza wanafunzi wachache sana na kuzomewa na idadi kubwa ya wanafunzi hapo chuoni. Simaanishi kuwa kuisaliti ccm ndio kuwa mwanamapinduzi... La hasha, kimsingi wanafunzi wa vyuo vikuu wanatakiwa kuwa wachambuzi wa mambo zaidi ya vyama vya siasa kwa manufaa ya taifa. Hata hivyo kwa msomi wa chuo kikuu kuhusishwa na ccm ya leo ni aibu kubwa kutokana na chama hicho kuwa chanzo cha umasikini mkubwa ndani ya tanzania.