bushman
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,411
- 743
Mwishoni mwa wiki iliyopita Uongozi wa chuo iliwakamata wanafunzi wakiwa kwenye daladala ya ABIRIA pamoja na abiria wengine,wakaamulu gari liludi mpaka jengo kuu la utawala na kuanza kuwasachi wanafunzi hao wakakuta SKAFU za CHADEMA kwenye bahasha,wakanyang'anya vitambulisho vya chuo na kuwapiga picha kama MATEKA au WAHAINI na kuamuru wasimamishwe masomo kwa muda usiojulikana,Vijana wakapokea barua kwa masikitiko makubwa sana kwani walikuwa kwenye DALADALA kama abiria,hawakukodi basi kama wafuasi wa CHADEMA wengine walikuwa wanakwenda mjini kwenye mambo yao binafsi,wengine ni viongozi wa vikundi vya dini walikuwa wanakwenda kwenye mikutano yao,wengine hawajawahi kuwa wanachama hata wa CCM,WOTE WAKASIMAMISHWA.MY TAKE,HIVI MTU ALIYEPANDA DALADALA ANAKWENDA KUFANYA SIASA NJE YA CHUO ANAFANYA KOSA?2.KUWA MWANACHAMA WA CHADEMA UDOM NI UHAINI?3.KIGEZO GANI KILITUMIKA KUWAFUKUZA WANAFUNZI HAO WAKATI WAMEPANDA GARI YA ABIRIA?4.NAPE AMEKUJA MARA NGAPI KUFANYA SIASA UDOM? MWAKA 2010 MABASI YA CHUO YALITUMIWA NA CCM?