Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Madai ya Chuo Kikuu cha Dodoma naweza kusema ni sawa mafisadi wanaotafuta njia za mkato kujinufaisha katika maisha yao. Haiingii akilini mwangu na sioni msukumo wa kudai kila mwanachuo apate laptop computer na kama kuna aliyewaahidia ni itikadi za siasa za kufikirika na wala si za kutekelezeka.
Ningesoma shule na chuo nchini Tanzania tu ningehadaika kwamba labda hayo madai ni ya msingi kwa wanachuo. Lakini uzoefu wangu kitaifa na kimataifa jinsi mfumo wa mahitaji ya kielimu vyuoni hilo la Chuo Kikuu cha Dodoma ni jipya na la pekee kabisa. Labda kuna kitu kingine nyuma yake, lakini kama dai la msingi laptop computer ni hadithi ya kufikirika isiyotekelezeka.
Vyuo vyote duniani hata katika mataifa tajiri kunakuwa na computer laboratory ambayo ni huru kwa kila mwanafunzi kutumia. Tena katika mataifa tajiri gharama za uendeshaji laboratory vyuoni huingizwa katika gharama za ada ya chuo na zinaonyeshwa wazi katika mchanganua wa general exp. and credit hour tuition fee. Mwanachuo aingiapo computer lab anakuwa na kitambulisho kinachomruhusu kutumia computer lab maana yake amelipia fee, kama hakulipia computer lab hakuna kitambulisho cha kumhalalisha kuingia computer lab. Hali kama hiyo Tanzania tungewapiga mawe viongozi.
Mwanafunzi binafsi kuwa na computer ni jukumu la mwanafunzi mwenyewe, mlezi au mzazi wake ndio wenye kubeba gharama, na wala sio chuo. Sasa hilo la Chuo Kikuu cha Dodoma kudai kila mwanafunzi apewe laptop computer na chuo au serikali ni kali ya mwaka na ni mzigo ambao chuo au serikali haiwezi kubeba gharama hizo.
Kuna mambo ya msingi ya kusikiliza na kukubali, lakini katika hili hapana, ni nje kabisa ya taratibu ya vyuo, na ni jambo la kuwazika kwa wenye upeo mdogo hitaji lisilotekelezeka. Bora waangalie mambo mengine ya msingi badala ya kupoteza muda na kudai personal laptop computer kutoka serikalini. Wanapoteza muda wao wa kusoma ndio maana baadaye tutapata viongozi vilaza kama tunavyoshuhudia siku hizi.
Ningesoma shule na chuo nchini Tanzania tu ningehadaika kwamba labda hayo madai ni ya msingi kwa wanachuo. Lakini uzoefu wangu kitaifa na kimataifa jinsi mfumo wa mahitaji ya kielimu vyuoni hilo la Chuo Kikuu cha Dodoma ni jipya na la pekee kabisa. Labda kuna kitu kingine nyuma yake, lakini kama dai la msingi laptop computer ni hadithi ya kufikirika isiyotekelezeka.
Vyuo vyote duniani hata katika mataifa tajiri kunakuwa na computer laboratory ambayo ni huru kwa kila mwanafunzi kutumia. Tena katika mataifa tajiri gharama za uendeshaji laboratory vyuoni huingizwa katika gharama za ada ya chuo na zinaonyeshwa wazi katika mchanganua wa general exp. and credit hour tuition fee. Mwanachuo aingiapo computer lab anakuwa na kitambulisho kinachomruhusu kutumia computer lab maana yake amelipia fee, kama hakulipia computer lab hakuna kitambulisho cha kumhalalisha kuingia computer lab. Hali kama hiyo Tanzania tungewapiga mawe viongozi.
Mwanafunzi binafsi kuwa na computer ni jukumu la mwanafunzi mwenyewe, mlezi au mzazi wake ndio wenye kubeba gharama, na wala sio chuo. Sasa hilo la Chuo Kikuu cha Dodoma kudai kila mwanafunzi apewe laptop computer na chuo au serikali ni kali ya mwaka na ni mzigo ambao chuo au serikali haiwezi kubeba gharama hizo.
Kuna mambo ya msingi ya kusikiliza na kukubali, lakini katika hili hapana, ni nje kabisa ya taratibu ya vyuo, na ni jambo la kuwazika kwa wenye upeo mdogo hitaji lisilotekelezeka. Bora waangalie mambo mengine ya msingi badala ya kupoteza muda na kudai personal laptop computer kutoka serikalini. Wanapoteza muda wao wa kusoma ndio maana baadaye tutapata viongozi vilaza kama tunavyoshuhudia siku hizi.