Posho City
JF-Expert Member
- Mar 15, 2012
- 646
- 415
Chuo kikuu cha Dodoma hadi sasa tangu chuo kifunguliwe tarehe 03/03/2012,kwa semista ya pili hawajatoa pesa za kujikimu kwa wanafunzi na hakuna taarifa rasmi wanatoa lini.Kumbuka mwezi wa kwanza walichelewesha hivyohivyo wanafunzi walipoandamana kwenda utawala,baada ya wiki moja wakafukuza wenzetu 29.bila sababu za msingi.Kuna TETES kuwa hela hizo zipo muda mrefu lakini wanafanya makusudi ili watu wagome wawafukuze wanaowaita wafuasi wa chadema.Lilitoka tangazo la waziri wa mikopo kuwa sababu za kuchelewa zipo nje ya uongozi wa chuo,akimaanisha ni tatizo la bodi ya mikopo,lakini iweje bodi hiyohiyo itoe hela udsm na kwingineko na isitoe kwa udom?!!!!Wakati huo huo wanatulazimisha tulipe ada na hela ya hostel.Tatizo pia hata serikali ya wanafunzi tuliyonayo ni ya kijinga isiyokuwa na upeo na wanaongoza kwa maelekezo ya Mlacha na Kikula.Kiuhalisai mfano huku kitivo cha elimu mimi nilipo hali ni mbaya na kumbuka hakunaga ustaarabu kwa mwenye njaa watu wameshaanza kusema wataingia barabarani liwalo na liwe.
HIYO NDO UDOM CHUO AMBACHO WANASIASA WALISEMA KITAKUWA BORA KULIKO VYOTE AFRIKA MASHARIKI,LAKINI KIUKWELI SIYO CHUO KIKUU NI CHUO KIKUBWA
HIYO NDO UDOM CHUO AMBACHO WANASIASA WALISEMA KITAKUWA BORA KULIKO VYOTE AFRIKA MASHARIKI,LAKINI KIUKWELI SIYO CHUO KIKUU NI CHUO KIKUBWA