SOKON 1
JF-Expert Member
- Dec 28, 2010
- 1,134
- 331
<br />Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Prof Idrissa Kikula ameiambia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii kuwa sasa hawatakuwa na Msamaha kwa wale wote wanaotumiwa na vyama vya siasa kusababisha migomo ndani ya UDOM,amesema kuna wanafunzi wengine wapo kwa maslahi ya vyama vya siasa hatawavumilia bila kuangalia wanatoka chama gani! Amewaomba Wabunge waelewe kuwa Udom ni sehemu ya elimu sio uwanja wa wanasiasa kuja kupotosha vijana na kusababisha migomo isiyokuwa ya lazima!<br />
My take: Naunga mkono wanafunzi wadai haki kwa mambo yanayowahusu na sio kupotoshwa na wanasiasa!
<br />
Nape alipokuja kukaguwa majengo ya chuo Udom je alikuja kufanya nini? Pia mabus ya chuo kutumika kubeba wanachama wa ccm je hao ndio wenye maalaka, wafuasi wa ccm kutumia madarasa ya vyuo kufanya mikutano yao na kugawa tshrt za ccm chuoni, Pro Kikula fungua macho acha kutuweka gizani natambua vyote unavifahamu ila kwa mapenzi yako umeamua kukaa kimya!
Ila tupo tunasubiria utekelezaji.