Sina shaka kabisa kwamba udiwani ni ngazi ya muhimu katika kuwakilisha mawazo ya wananchi katika vyombo vya kiutendaaji, hasa Wilayani na taifa kwa ujumla.Lakini sina hakika kama kiungo hiki muhimu kinapewa uzito unaostahili.Mara nyingi tumesikia madiwani ambao kama wamesoma ni kidogo sana.Diwani wangu ameishia darasa la tatu,tena alikimbia shule kwa sababu wakati fulani huko nyuma mzee Ruksa alipokuwa Rais, biashara ya fegi ilitamba sana.Akawa yeye ni muuza fegi kwenye mabasi na mdokozi mkubwa wa mizigo ya abiria.Mpaka leo fani ya wizi pamoja na udiwani wake hajaiacha.Pia ni mshirika mkubwa wa vijana wanaoshusha mizigo kwa njia ya kushangaza kigogo kwenye malori, maarufu kama "shushashusha".Sijui kama ndugu yangu Masha ana taarifa ya wizi huu wa aina yake!Yeye pia ni mnunuzi mkubwa wa bidhaa hizo za wizi.Madiwani wengi nchini wanatuhumiwa na vitendo vya ajabu ajabu kama hivi,ikionyesha wazi kwamba hatuko makini sana na ngazi hii muhimu sana ya uongozi. Nimetangulia kusema kwamba ngazi hii ni muhimu sana katika kuleta maendeleo ya wananchi.Siku zote nimejiuliza,hivi kweli mwenye elimu ya darasa la tatu anaweza kuchambua matatizo ya wanachi na kuyawakilisha kwenye vikao vya halimashauri kwa utekelezaji?Jamani hivi tuna kwenda wapi?Sidhani hata kama mtu kama huyu anajua kwa nini ni diwani.Karibu tunaingia katika uchaguzi wa 2010.Inabidi tuwe na mtizamo tofauti.Kazi ya udiwani sio ndogo,ina hitaji mtu mwenye ufahamu na anayeweza kuchambua mambo(diagnostic).Ni vema basi akawa mtu ambaye ana ufahamu mzuri,mwenye "proven intergrity",na ambae angalau ana Diploma,tena "inayofahamika" sio ya mtaani.