Ngagarupalu
Senior Member
- Oct 13, 2012
- 156
- 57
Nchi ya Tanzania inakadiliwa kuwa na idadi watu wapatao million 44 ( japo tunasubiri matokeo ya sensa ya 2012 yenye utata). Nchi hii inakadiriwa kuwa na makabila yapatayo 121 au zaidi. Ina madhehebu ya dini yasipungua 50 ( yakigawanywa kwenye makundi makuu matatu, ukristo, uislam, na upagani. Ingawa ndani ya haya makundi kuna madhehebu isiyopungua matano.
Makundi mawaili ya uislam na ukristo yamekuwa kwenye malumbano kwa muda sasa na kujiona kama yapo juu hata ya sheria na kama yenyewe ndo yana mungu wao, yana haki ya kuwambia wengine ubaya wao, uzuri wa mungu wao, kushiriki kutunga sheria za nchi, pengine kuzingatia dini zao na hata kutaka kuchukua dola na kuongoza, na hivyo kusahau kuwepo kwa makundi mengine, na hata kusahau ndani yao kuna madhehebu mengine tena yanayotofautiana.
Pamoja na kuwepo kwa makabila yanayozidi 100, bado ukabila umeshindwa kujipenyeza kwa nguvu zaidi, na hata kutia chuki dhidi ya kabila jingine, japo ukabila nao hauwezi kuachwa nje kama mdudu nyemelezi kwenye taifa changa. Leo nitaongela udini sababu ndo umepanda chart hadi leo kuwa gumzo, na kuleta matukio tofauti ndani ya nchi ambayo wengine waliamini ni kiswa cha amani.
Udini umetoka wapi?
Kabla ya miaka ya 80, hapakuwepo na udini, ila tulipo anza kusonga mbele tunaona udini unapata kazi, miaka ya tisini, ulianza, pale tuliposema watu waende shule na mavazi tofauti (tukizingatia dini zao) ingawa hilo wengine waliona halina tabu, ila liliwatofatisha wanafunzi na kuwafanya wawe na makundi tofauti, pengine sababu ya mavazi yao.
Pili, idadi ya watu imeongezeka , na fursa kutokuongezeka kuendana na ongezeko la idadi ya watu. Hii imesababisha watu kutafuta upendeleo kwa njia mbadala, na moja ni dini kutimika, na ukabila japo bado upo chini ya dini.
Tatu, uchumi wan chi haukui na kutoa fursa sawa kwa wote, kwa mfano shule nzuri zimekuwa za gharama sana, kuhitimu chuo kikuu haisaidii au haihakikishi upatikanaji wa kazi, na maisha bora, ajira mpya ni chache, hivyo kuwa nakundi la watu wanelimu ya nchini na kati bila shughuli maalum za kufanya. Hili kundi ni rahisi kulishawishi kwa lugha yoyte ile lugha yoyote kwa gharama nafuu.
Nne, idadi ya watu kuingia kwenye dini na kuitumia kama ngazi, kufadhili, kudhulumu, etc na kujipatia umaarufu kumbe nia yao ni kwenda kwenye madaraka na kushika dola, kundi hili ni baya sana, kwani hupandikiza chuki dhidi ya kundi la dini nyingine.
Tano, wanasiasa kujipambanunua kwa kulinda na kutetea kundi flani la dini flani, wakati mwingine kupeleka malalamiko yao na maonyo yao ya kisiasa kwenye majukwaa ya dini.
Sita, viongosi wa dini kuingilia na kusemea serikali katika kujitanabaisha kuwa iko (haiko) upande wake bila kujadili na kundi jingine la dini/dhebu
Saba, serikali kushindwa kutoa nafasi kwa viongozi wa dini na madhehebu kukutana kwa pamamoja, ( na kama inafanya hivyo viongozi hawaleti taarifa sahihi kwa waumini wao) Viongozi wa dini wanapaswa kutoa mawazo yao kwa serikali kwa niaba ya waumini wao kwenye vikao maalum, ikiwa ni kukutana na serikali kwa muda mwafaka, na kufanya makubaliano ya pamoja.
Nane, serikali kushindwa kutoa sera na mwongozo kwa makundi madogo (unadvantaged group) haya ni yale ya wasio waislam wala wakristo, ni wapagani, dini za asili na hata wasio abudu. Kundi hili kubwa lenye watu wengi limeachwa nje na hata halina mwakilishi na wala halipewi fursa ya kuwepo, tunaomba litambuliwe, maana mm hujiuliza kama, kiongosi wetu hatokani na uislam na ukristo ataapa kwa kushika nini?, ( mfumo useme na siyo katiba maana hiyo ya wote wenye na wasiyo na dini)
Tisa, migogoro isiyo isha ndani ya dini hizi. Dini hizi kubwa zenye wafuasi wengi zina migogoro kila siku. Vikundi vya uasi ndani ya dini hizi, vikundi vya wpigania haki ndani ya dini, vikundi vya wana mageuzi huleta migogolo kila kukicha. Migogoro hii isipopata ufumbuzi ndani basi hutoka nje na kuwa kero kwa waumini wenyewe na kwa waumini wa dini zingine. Vikundi hivi, vya wanamaombi, siasa kali, imani kali etc huanza kuongelea siasa kugawa watu na hata kuunganisha mapinduzi ndani na nje ya nyumba za ibada.
Kumi, kuwepo kwa kundi kubwa ambalo linapenda dini, lakini halijapta muda wa kuisoma na kuilewa dini, hili kundi limekuwa ni kama bendera kufuata upepo, kiongozi akisema haliwezi kupambanua hata kidogo. Waumini wengi wamekuwa si wasomi wazuri wa vitabu vya dini bali wasikilizaji, na hivyo kupokea upotoshaji kirahisi zaidi.
Kumi na moja, baadhi ya viongozi wa dini hawana wito, wanamapinduzi, wamechoshwa na mfumo wa sisa, uchumi, na maendeleo ya nchi. Hili kundi halina mbadala ila kutumia nyumba ya ibada, kutaka kuleta mapinduzi hadi ya kisias, kiuchumi, kisheria n.k wao Rais, IGP, Sheikh, Askofu, Waziri etc siyo muhimu, maneno yao chuki tu, wakichanganya na mahubiri wanapotosha waumini wao, maana wao wamejaa visasi na uhasi.
Hitimisho!!
Kuwepo na mjadala mkubwa watu wajifunze siyo tu dini bali hata vyanzo vya dini hizi, hivi mkwawa, mirambo, etc walikuwa dini gani? Kabla ya warabu na wazungu, wazee waliomba mvua wapi? Je hizi dini zina husiana na tamani za wketu au wageni waliozileta? Hivi ukiua watu wote wasio dini yako utahubiri nani? Hivi ni bora kuingiza watu kundi mwako au kuwa ua
Nitakuja na suluhisho la udini kwenye Taifa maskini. Ingawa umaskini ni chanzo kikubwa cha udini, ukabila na machafuko mbalimbali.
Makundi mawaili ya uislam na ukristo yamekuwa kwenye malumbano kwa muda sasa na kujiona kama yapo juu hata ya sheria na kama yenyewe ndo yana mungu wao, yana haki ya kuwambia wengine ubaya wao, uzuri wa mungu wao, kushiriki kutunga sheria za nchi, pengine kuzingatia dini zao na hata kutaka kuchukua dola na kuongoza, na hivyo kusahau kuwepo kwa makundi mengine, na hata kusahau ndani yao kuna madhehebu mengine tena yanayotofautiana.
Pamoja na kuwepo kwa makabila yanayozidi 100, bado ukabila umeshindwa kujipenyeza kwa nguvu zaidi, na hata kutia chuki dhidi ya kabila jingine, japo ukabila nao hauwezi kuachwa nje kama mdudu nyemelezi kwenye taifa changa. Leo nitaongela udini sababu ndo umepanda chart hadi leo kuwa gumzo, na kuleta matukio tofauti ndani ya nchi ambayo wengine waliamini ni kiswa cha amani.
Udini umetoka wapi?
Kabla ya miaka ya 80, hapakuwepo na udini, ila tulipo anza kusonga mbele tunaona udini unapata kazi, miaka ya tisini, ulianza, pale tuliposema watu waende shule na mavazi tofauti (tukizingatia dini zao) ingawa hilo wengine waliona halina tabu, ila liliwatofatisha wanafunzi na kuwafanya wawe na makundi tofauti, pengine sababu ya mavazi yao.
Pili, idadi ya watu imeongezeka , na fursa kutokuongezeka kuendana na ongezeko la idadi ya watu. Hii imesababisha watu kutafuta upendeleo kwa njia mbadala, na moja ni dini kutimika, na ukabila japo bado upo chini ya dini.
Tatu, uchumi wan chi haukui na kutoa fursa sawa kwa wote, kwa mfano shule nzuri zimekuwa za gharama sana, kuhitimu chuo kikuu haisaidii au haihakikishi upatikanaji wa kazi, na maisha bora, ajira mpya ni chache, hivyo kuwa nakundi la watu wanelimu ya nchini na kati bila shughuli maalum za kufanya. Hili kundi ni rahisi kulishawishi kwa lugha yoyte ile lugha yoyote kwa gharama nafuu.
Nne, idadi ya watu kuingia kwenye dini na kuitumia kama ngazi, kufadhili, kudhulumu, etc na kujipatia umaarufu kumbe nia yao ni kwenda kwenye madaraka na kushika dola, kundi hili ni baya sana, kwani hupandikiza chuki dhidi ya kundi la dini nyingine.
Tano, wanasiasa kujipambanunua kwa kulinda na kutetea kundi flani la dini flani, wakati mwingine kupeleka malalamiko yao na maonyo yao ya kisiasa kwenye majukwaa ya dini.
Sita, viongosi wa dini kuingilia na kusemea serikali katika kujitanabaisha kuwa iko (haiko) upande wake bila kujadili na kundi jingine la dini/dhebu
Saba, serikali kushindwa kutoa nafasi kwa viongozi wa dini na madhehebu kukutana kwa pamamoja, ( na kama inafanya hivyo viongozi hawaleti taarifa sahihi kwa waumini wao) Viongozi wa dini wanapaswa kutoa mawazo yao kwa serikali kwa niaba ya waumini wao kwenye vikao maalum, ikiwa ni kukutana na serikali kwa muda mwafaka, na kufanya makubaliano ya pamoja.
Nane, serikali kushindwa kutoa sera na mwongozo kwa makundi madogo (unadvantaged group) haya ni yale ya wasio waislam wala wakristo, ni wapagani, dini za asili na hata wasio abudu. Kundi hili kubwa lenye watu wengi limeachwa nje na hata halina mwakilishi na wala halipewi fursa ya kuwepo, tunaomba litambuliwe, maana mm hujiuliza kama, kiongosi wetu hatokani na uislam na ukristo ataapa kwa kushika nini?, ( mfumo useme na siyo katiba maana hiyo ya wote wenye na wasiyo na dini)
Tisa, migogoro isiyo isha ndani ya dini hizi. Dini hizi kubwa zenye wafuasi wengi zina migogoro kila siku. Vikundi vya uasi ndani ya dini hizi, vikundi vya wpigania haki ndani ya dini, vikundi vya wana mageuzi huleta migogolo kila kukicha. Migogoro hii isipopata ufumbuzi ndani basi hutoka nje na kuwa kero kwa waumini wenyewe na kwa waumini wa dini zingine. Vikundi hivi, vya wanamaombi, siasa kali, imani kali etc huanza kuongelea siasa kugawa watu na hata kuunganisha mapinduzi ndani na nje ya nyumba za ibada.
Kumi, kuwepo kwa kundi kubwa ambalo linapenda dini, lakini halijapta muda wa kuisoma na kuilewa dini, hili kundi limekuwa ni kama bendera kufuata upepo, kiongozi akisema haliwezi kupambanua hata kidogo. Waumini wengi wamekuwa si wasomi wazuri wa vitabu vya dini bali wasikilizaji, na hivyo kupokea upotoshaji kirahisi zaidi.
Kumi na moja, baadhi ya viongozi wa dini hawana wito, wanamapinduzi, wamechoshwa na mfumo wa sisa, uchumi, na maendeleo ya nchi. Hili kundi halina mbadala ila kutumia nyumba ya ibada, kutaka kuleta mapinduzi hadi ya kisias, kiuchumi, kisheria n.k wao Rais, IGP, Sheikh, Askofu, Waziri etc siyo muhimu, maneno yao chuki tu, wakichanganya na mahubiri wanapotosha waumini wao, maana wao wamejaa visasi na uhasi.
Hitimisho!!
Kuwepo na mjadala mkubwa watu wajifunze siyo tu dini bali hata vyanzo vya dini hizi, hivi mkwawa, mirambo, etc walikuwa dini gani? Kabla ya warabu na wazungu, wazee waliomba mvua wapi? Je hizi dini zina husiana na tamani za wketu au wageni waliozileta? Hivi ukiua watu wote wasio dini yako utahubiri nani? Hivi ni bora kuingiza watu kundi mwako au kuwa ua
Nitakuja na suluhisho la udini kwenye Taifa maskini. Ingawa umaskini ni chanzo kikubwa cha udini, ukabila na machafuko mbalimbali.