Udini: Uchambuzi wa Mobhare Matinyi

Status
Not open for further replies.

TATIZO SI UISLAMU BALI UARABU WA GHUBA. Anayebisha hongera zake.


UTAMADUNI WA WAARABU WA GHUBA. Hakuna mwislamu anayeonewa wala
anayenyimwa shule.

Pamoja na kwamba Mwandishi M. Matinyi amefanya kazi nzuri kwenye uchambuzi wake hapo juu, lakini amekosea kabisa kwenye premise yake kuu kwamba tatizo ni "WAARABU WA GHUBA". Ameshindwa kuelezea tofauti ya msingi kati ya nchi kama "Moroko, Algeria, Tunisia, Misri na zile za Uturuki, Siria, Iraki na Yodani" ambazo hazina rasilimali ya mafuta, na kwa upande wa pili nchi zile anazoziita "nchi za ghuba" kama "Saudia Arabia, Yemeni, Kuwaiti, Omani, Katari, Imarata na Bahraini" ambazo zina utajiri mkubwa wa mafuta.

Ama baada ya kusema hayo, kwa ujumla utakuta kwamba nchi za Kiarabu za Ghuba zilizojaliwa mafuta, Wananchi wake wengi wameneemeka kiasi kwamba hawana haja kabisa ya kusoma (kwa maana ya elimu ya Kimagharibi au ya kisasa) ili waweze kuishi maisha ya raha na starehe bila kufanya kazi yoyote kwa sababu tu nchi hizi zina uwezo wa kuwalipa professionals kutoka nchi zenye Wasomi wengi (haswa zile za Kiislamu na za Kiarabu) wawafanyie kazi zote hata zile za kufikiri.

Lakini cha msingi ni kwamba utajiri wa mafuta wa nchi hizi uligundulika mwanzoni mwa karne iliyopita, ambayo ni zaidi ya karne mia moja tokea historia ya Waarabu wa Ghuba nchi za Afrika Masharaki na Kati ilipoanzia. Kwa hiyo kwa kweli mtazamo na uchambuzi wa Mwandishi kwamba Waislamu wa Tanzania hawajali elimu eti kutokana na influence ya "WAARABU WA GHUBA" una walakini kwa kukosa uchambuzi yakinifu wa sababu gani zinafanya "WAARABU WA GHUBA" kama tunavyowafahamu leo hii kukosa au kutokujali elimu ya kisasa, ilhali Mwandishi amekiri kwamba "WAARABU WA GHUBA" wa karne mia moja iliyopita walikuwa wakiongoza kwenye nyanja ya elimu ya kusoma na kuandika.
 
mapogolo

Damn you are good mambo yanaflow nimekukubali na uchambuzi wako , hivi ndio vitu tunavyotaka wachambuzi wenye mantiki

Pia nakumbuka kuna wakati Serikali ilipiga marufuku watu waliotoka seminary kuchaguliwa kwenda form V shule za serikali miaka ya 80s , maana walikuwa wanafaulu sana , nafikiri ni wakati wa Kighoma Malima sina uhakika maana walidai secondari za serikali wanajaa wakristo tuu,

Basi matokeo yake zile shule za seminary zikaanzisha form V na VI , basi fainali ikawa chuo kikuu darasa zima linajikuta liko chuo kikuu kutokana na ufauli

Kabla ya kukataza waseminary wasiende shule za serikali, watoto wengi waliomaliza seminary form 4 walikua wanashindwa kuhimili mikiki ya shule za serikali wengi walifeli hawakuzoe kusoma na njaa au bila vitabu au wanafunzi wengi darasani

Uamuzi huo wa wizara waliufanya kuwaongeza wakkristo chuo kikuu, maana sasa ni darasa zima lilikua linajikuta chuo kikuu na chuo wanaangalia matokeo, dhamira yao ya kuwa punguza form V na VI serikalini ndio ilichangia kupunguza idadi ya waisilamu chuo kikuu

Swala hivi siku hizi shuke binafsi wanachaguliwa kwenda high school serikalini ? Au bado ni seminary tuu wanazuiwa ?
 
Last edited by a moderator:
asalam aleikum

Walykum al salaam ... st ivuga nimeuliza swali halikujibiwa ... hivi kwanini kichwa cha habari kaandika udini? Udini ni nini? Je kuwa muislam au mtu akitaka kujadili uislam lazima aandike udini? Inaama udini ni uislam? Kama ameamuwa kuwachambua waislam amekosa title mpaka akatumia udini? Na mchumbuzi ni dini gani!? ...
 
...Pia Tanzania ikapata nafasi za masomo kwenye mataifa ya Misri, Algeria, Iran, na Uturuki, maalum kwa ajili ya waislamu tu. Marafiki zangu walikwenda huko na walinithibitishia kwamba hii ilikuwa maalum kwa waislamu tu.

....Azania walikuwa na Mpemba aliyepata pointi SABA. Alikwenda tena Tambaza akawa nyuma yetu na akapata pointi TATU. Akaenda Ulaya. Hakunyimwa nafasi yoyote. Hao wanaonyimwa wako wapi?
Hizo nafasi za masomo katika nchi za Kiislamu miaka ya 90 hata huyo Mpemba wa pointi saba Azania pointi tatu Tambaza ni living proof ya nafasi hizo. Alienda kusoma Uturuki baada ya kidato cha sita kwa nafasi hizo hizo.

Pia, yeye ni ushahidi hai wa ukweli mwingine kuhusu jinsi Muungano ulivyowapa nafasi Wazanzibari, huyu Mpemba alisoma Mwananyamala Primary, halafu Azania na Tambaza. Sasa sijui kwa nini hakusoma Chake Chake primary au Wete sekondari. Si huku wananyimwa nafasi na makafiri? Kafiri mbaya kiatu chake dawa.
 
Njiwa
kama nimemuelewa vizuri mwandishi,

Mantiki na maudhui ya tafiti za mjadala, unajadili na kutoa vielelezo mbalimbali kuhusiana na sintofaham inayoendelea baina yetu watanzania. Mijadala ya kidini, wapo wanaoona mwalimu nyerere hakuwatendea haki, wapo wanaoona nyerere hakuwa na upande wowote aliwapenda wananchi wa din zote nk. Mijadala imeenda mbali kwamba waislam hawatendewi haki wakitoa malalamiko mengi mfano balaza la mitihani, uwiano wa kiuongozi nk.

Hivyo kwasababu amedadavua sintofaham hizi za kidini kwahakika title sahihi ambayo inatoa japo kwa untangulizi mjadala unahusu nini akapata hiyo.

Kwa upande wangu naona yuko sahih100%. Kichwa cha habari kitoe na kubeba maaana ya mjadala au kinachofuata.
 
Nakiri uwezo mkubwa wa Waislamu kielimu. Tambaza mwaka fulani kijana wa Kiislamu kwa jina la Mustafa Kudra ndio alikuwa kipanga form 4 atatoka na poit 7 lakini alipiga A 9!. Akarudi Tambaza PCM akapiga point 3!.

Mwaka wangu hapo Tambaza tulikuwa na vipanga watatu waislamu, Nia Sudi, somebody Issa na mwingine Mwinyimvua wote hao ni Wazaramo tena toka uswazi na familia duni!. Walipiga poit 7,8,9 na kutinga Kibaha na baadae UDSM, japo Nia Sudi safari ilikatikia njiani na kutangulia mbele ya haki!.

Wakati tukisoma Journalism pale TSJ ya enzi hizo, ilikuwa ni lazima uchukue idadi fulani ya wanafunzi kutoka Zanzibar, vipanga wetu darasani walikuwa ni wanafunzi kutoka Zanzibar na sasa ni wahadhiri wa vyuo vikuu!.

Nikiwa UD pale Law, kuna kipanga wa Kiislamu alitutangulia nikiishi nae Mabibo hostel, Alipiga GPA kali, akaunganisha LL.M na kubaki chuo sasa ameshapiga Ph.D na ni mhadhiri!.

Darasa letu tulikuwa na Waislamu kadhaa vipanga kutoka Zanzibar, japo mmoja alitumia boom kuoa mke wa kwanza 1st -year na mke wa pili 3rd -year alikuwa kipanga. Miongoni mwa vipanga waliobaki chuo mmoja ni Mwislamu saa hizi anamalizia Ph.D yake, hivyo naungana na mtoa mada kuwa tatizo sio Uislamu, tatizo ni watu wenyewe!.

Early civilization ilianzia dola la Axum enzi ya zama za mawe na chuma na usomi umeanzia Misri!.

Wakistu wengi hawajui Misri ilistaarabika miaka mingi kabla ya ulaya, hizi number na alphabeti tunazotumia ni za ki Misri, hata Yesu aliishi Misri tangu ana miaka 12 mpaka alipofika miaka 33 ndipo akarudi Israel.

Hakuna any details, alikuwa akifanya nini huku Misri ila inasemekana alikuwa akisoma na ni mwanachana wa kundi la Rosae Crusis wanaitwa Rosecrusians!. Kwa vile haijaandikwa kwenye Bibilia sio lazima tuiaminie sana ila habari ndio hiyo!.
 
Pasco
umechangia pakubwa mkuu, mimi kwa upande wangu nimekubali ndani ya jamii f tunajifunza na naelimika zaid.

Naomba wenye data, facts au historia zaidi waendelee kutujuza pengine tutafumbua macho na masikio na kuutokomeza huu usintofaham na adui udini anayetunyemelea kwa kasi kututenganisha hapa tanzania.
 
Mr Mutinyi amegusia eneo zuri sana la tamaduni na maendeleo..naweka thread yangu inalenga katika hili
 
mwarabu na mzungu walileta dini zao ili kutuogopesha na kutugawa ili wabebe resourse zetu vizuri na walifanikiwa sana hadi sasa hivi ina work out ..

hii ni kweli kabisa mkuu, mpaka sasa tayari wanakomba rasilimali zetu za kutosha, wanasubiri tukianza kushikana mashati na kukatana mapanga, wationgezee silaha huku wao wakipata nafasi ya kuiba kwa masaa 24 wakati huo. ila sisi hatuoni hilo tunachoona ni kuwa HUssein ananionea, au jackson anapendelewa!! ajabu yenyewe tunachukiana wakati hatujuani na si ndugu, na wala hatukai pamoja!! ila tu kwa sababu watu wawili watatu wanatuchochea tuchukiane, kwa kutushawishi kuwa fulani anaonewa..... ni wakati wa kuamka sasa watanzania!!
 
Naposoma habari kama hii ndipo huelewa kwamba Watanzania bado tuna safari ndefu sana katika hata kutambua Uhuru wetu. Mtu kweli anaandika habari za elimu kwa kuonmyesha jinsi wakoloni walivyojenga shule zao, iwe mzungu au mwarabu inahusiana nini na wewe mwananchi ulotawaliwa. Ni sawa na Barricks wanavyoiba dhahabu yetu wakitujengea shule na zahanati mnawasifia saana sijui na wao tutasema wakristu au waislaam.

Jamani jamani Watanzania wenzangu, Mna UHuru kamili na uhuru huu haukuja kwa Wakristu wala Waislaam na swala la kuendelea kusema makanisa yalifanya hivi ama vile ni mwanza wa kukujenga wewe ufikirie Udini. haiwezekani mtu aamke asubuhi na kupanga mambo yote yaliyofanywa na kanisa ktk shughuli za serikali akaona ubora wa kanisa lake au wazungu ambao wamekutawala. Kaa kuna tatizo lizungumziwe tatizo lilipo na sii kutafuta sababu za kupamba kuwepo kwa tatizo hilo.

Nimekwisha sema sana na nitarudia kusema tena na tena.. Tuna tatizo la kimfumo nchini Tanzania na hili ndilo limejenga hisia hizi chafu za kikoloni maana hata Mjarumani leo husema yeye alikuwa mbora zaidi alitujengea reli, kuleta mazao ya fedha kama katani, kahawa na chai lakini kwa faida yake mwenyewe. Bila yeye tusingekuwa na shule wala zahanati, haya ni matusi kwetu wala sii majisifu yenye kuthaminika..

Mfumo ELIMU na AFYA ni mbovu na haufai, serikali inatakiwa kuuchukua jukumu hilo na shule au Hospital zote za makanisa na waislaam ziwe PRIVATE na zijiendeshe zenyewe maana hupata misaada toka nchi za nje na muundo wake hufuata vyanzo vya wawekezaji wake. Swala la kuweka mamlaka ya ELIMU juu ya chombo cha dini ndiko kunakosababisha malalamiko yote haya na inaweza kuepukika. Hakuna Ulazima wa Makanisa kuwa mbia na serikali isipokuwa makanisa waruhusiwe kujenga shule na Hopital sehemu zozote watakazopenda na kuomba kibali maana hii ni biashara na mwenye mali ana haki ya kutafuta sehemu na soko la wahitaji. Lakini sio tena asaidiwe kuendesha huduma hii, hapo tena ushindani unaondoka na inafanya wananchi kuendelea kuwa wahitaji omba omba na mwenye nguvu ya kauli ni mwenye mali badala ya Mteja.

Serikali ivunje muafaka na ushirikiano wake na vyombo vyote vya kidini na badala yake iunde idara na mashirika yanayosimamiwa na serikali hata kama waajiriwa wote watakuwa Wakristu haijalishi. Kwani Lowassa anafanya Ufisadi kwa sababu yeye ni Mkristu au Rostam, Chenge na wengineo. Huwezi kutumia majina ya watu kwa kutafsiri matendo yao kuhusiana na imani za dini. haya ni makosa na Upumbavu mkubwa sana. Elimu ya Uraia inatakiwa, na mwanzo ni muundo wa serikali yenyewe.
 
mwarabu na mzungu walileta dini zao ili kutuogopesha na kutugawa ili wabebe resourse zetu vizuri na walifanikiwa sana hadi sasa hivi ina work out ..

Hiyo ni hakika mkuu! Dini ni utamaduni tu. Walitukuta na utamaduni wetu wa kuabudu jua na mibuyu wao wakauuita wa kishenzi wakatuletea utamaduni wao wa kishenzi wa kuabudu kisichoonekana. Lengo lao watutawale vyema na kutuibia huku sisi tukipewa hofu?
 
Huwezi kutenga dini ya Islam na utamaduni wa kiarabu! Utamaduni wa kiislamu upo ndani ya islam na islam ipo ndani ya utamaduni wa kiislamu kiasi huwezi kuona tofauti. Lugha, mavazi, tabia, mila, desturi, malezi, makuzi ya watoto n.k ni lazima viwe vya kiarabu kwa muislamu la sivyo hatakuwa mwislamu. Kule Ghuba ni matajiri sana na hawataki kufanya kazi. Wanakaa na kucheza bao na karata kwa kuwa hata hivyo hupewa ruzuku ya kuishi kutoka serikali kwa sababu ya utajiri wa mafuta. Maeneo ambapo kua waislamu wengi kama huku Pwani ya Afrika mashariki tabia ni hiyohiyo kwa kuwa imo ndani ya utamaduni wa Waarabu na utamaduni wao ni sehemu ya dini na dini ni sehemu ya utamaduni wao. Boko Haram kule Nigeria wanauwa watu kwa kuwa wanapinga elimu hii ya kawaida wanayoita ya magharibi. Wao wanataka ile ya kiarabu, inayofundishwa kiarabu katika viwango vya Uarabu! Waislamu wasioshika fika utamaduni wa kiarabu wananyanyapaliwa kuwa sio waislamu halisi! Wewe kama huvai kanzu na barghashia hata kama unaswali msikitini mara 5 kwa siku sio muislamu ila pandikizi la tamaduni ya magharibi!
 
Nimekuwa nikiisoma hii habari na kuirudia na kuirudia na kugundua kwamba unatoa majawabu kwa maswali mengi.
 
Hivi Mobhare Mathinyi na yule M.M Mwanakijiji Mwandishi maarufu wa makala magazetini sio mtu na pacha wake kweli? Just thinking aloud!
 
Nakiri uwezo mkubwa wa Waislamu kielimu. Tambaza mwaka fulani kijana wa Kiislamu kwa jina la Mustafa Kudra ndio alikuwa kipanga form 4 atatoka na poit 7 lakini alipiga A 9!. Akarudi Tambaza PCM akapiga point 3!.

Mwaka wangu hapo Tambaza tulikuwa na vipanga watatu waislamu, Nia Sudi, somebody Issa na mwingine Mwinyimvua wote hao ni Wazaramo tena toka uswazi na familia duni!. Walipiga poit 7,8,9 na kutinga Kibaha na baadae UDSM, japo Nia Sudi safari ilikatikia njiani na kutangulia mbele ya haki!.

Wakati tukisoma Journalism pale TSJ ya enzi hizo, ilikuwa ni lazima uchukue idadi fulani ya wanafunzi kutoka Zanzibar, vipanga wetu darasani walikuwa ni wanafunzi kutoka Zanzibar na sasa ni wahadhiri wa vyuo vikuu!.

Nikiwa UD pale Law, kuna kipanga wa Kiislamu alitutangulia nikiishi nae Mabibo hostel, Alipiga GPA kali, akaunganisha LL.M na kubaki chuo sasa ameshapiga Ph.D na ni mhadhiri!.

Darasa letu tulikuwa na Waislamu kadhaa vipanga kutoka Zanzibar, japo mmoja alitumia boom kuoa mke wa kwanza 1st -year na mke wa pili 3rd -year alikuwa kipanga. Miongoni mwa vipanga waliobaki chuo mmoja ni Mwislamu saa hizi anamalizia Ph.D yake, hivyo naungana na mtoa mada kuwa tatizo sio Uislamu, tatizo ni watu wenyewe!.

Early civilization ilianzia dola la Axum enzi ya zama za mawe na chuma na usomi umeanzia Misri!.

Wakistu wengi hawajui Misri ilistaarabika miaka mingi kabla ya ulaya, hizi number na alphabeti tunazotumia ni za ki Misri, hata Yesu aliishi Misri tangu ana miaka 12 mpaka alipofika miaka 33 ndipo akarudi Israel.

Hakuna any details, alikuwa akifanya nini huku Misri ila inasemekana alikuwa akisoma na ni mwanachana wa kundi la Rosae Crusis wanaitwa Rosecrusians!. Kwa vile haijaandikwa kwenye Bibilia sio lazima tuiaminie sana ila habari ndio hiyo!.
Good Pasco, you have managed to count Bright moslems simply because Bright Christians are uncountable! Thanx kwa andiko lako
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom