Edwin Mtei
Senior Member
- Dec 13, 2008
- 181
- 342
Tanzania Bureau of Standards (Taasisi ya Ubora wa Bidhaa Tanzania) ina jukumu la kukagua na kudhibiti ubora wa bidhaa zinazozalishwa viwandani hapa nchini na hutoa vyeti (Certificates) kwa wazalishaji na kupiga mihuri zile bidhaa inazoridhika na ubora wake kabla ya kusambazwa kwa walaji au watumiaji. Naamini pia ni jukumu la TBS kuona kwamba bidhaa zinazoingizwa kutoka nje zinadhibitiwa.
Majukumu haya muhimu ya TBS yanapaswa kutekelezwa kabla bidhaa hazijaanza kusambazwa au kuuzwa reja reja kwa wananchi. Hata hivyo kumezuka mtindo wa wafanya biashara wengi kuuza bidhaa feki au bidhaa zenye ubora wa hali ya chini sana.
Huenda hali hii inatokana na maafisa wa TBS kutokuwa makini pale bidhaa zinazalishwa humu nchini. Kwa bidhaa zinazoingia toka nje, Idara ya Forodha na TBS wanatakiwa kuhakikisha ubora wa bidhaa hizo. Inakuwa ni fedhedha kwa Idara ya Serikali kutoza ushuru na kodi na TBS kuruhusu bidhaa ziingie, halafu zikifika dukani, Polisi wanazikamata na kuziteketeza eti kwa vile ni bidhaa feki.
Hali hii huenda ikatokana na tamaa ya wafanya biashara wenyewe kutaka kutajirika haraka haraka kwa kuuza bidhaa rahisi, au kutokuwa makini katika kuamua ni bidhaa zipi bora. Wenye tamaa hata kuagiza bidhaa mbovu au hafifu kwa bei ya chini maksudi ili waweze kuziuza kwa urahisi kwa vile wanajua wanunuzi wengi nchini kwetu wana uwezo mdogo kutokana na umaskini. Idara ya Forodha na TBS wahusishwe kikamilifu. Waagizaji wa bidhaa hafifu wasije wakatoa rushwa kwa maafisa wa TBS kupitishabidhaa zisizokidhi mahitaji na nyingine kuweza kuathiri afya na maisha ya wananchi.
Kumezuka mtindo wa viongozi wa Serikali katika ngazi za chini kuvamia maduka vijijini au hata mijini na kukamata bidhaa feki au bidhaa zenye ubora wa hali ya chini na kuamuru ziteketezwe. Wananchi kadhaa hushangilia wanapoona wafanya biashara wakitiwa mbaroni au bidhaa zao zikiteketezwa, wakiwalaumu kwamba ni wanyonyaji na mabepari.
Maoni yangu ni kwamba mtindo huu unaweza kutupeleka pabaya. Wafanya biashara vijijini ni watu muhimu wanaotoa huduma ambayo wanavijiji wanahitaji kwa karibu. Duka la kijijini ni mahala wanajamii wanapopata kwa karibu bidhaa au vifaa ambavyo wangelazimika kwenda mbali kuvipata. Hata katika miji, bidhaa au vifaa muhimu hupatikana toka maduka haya yanayotoa huduma za reja reja.
Kama bidhaa ni feki au zina ubora wa hali ya chini, ni kutokana na udhibiti usiokidhi mahitaji katika viwanda au bandarini wakati wa kuingiza bidhaa hizo. Kwa hiyo TBS na wakala wake wana wajibu wa kufanya kazi zaidi. Sina hakika Sheria inayohusu TBS inatumiwaje kudhibiti bidhaa hafifu au feki ambazo tayari zimekwishaingia katika maduka ya reja reja.
Hata hivyo, ili kuondoa uwezekano wa wafanya biashara kuonewa, nashauri TBS itoe maelekezo na utaratibu wa kufuata katika kushughulikia tatizo hili. Itambulike kwamba wenye maduka mijini na vijijini ni watu wanaotoa huduma muhimu, wengi wao wakiwa ni waadilifu. Ijulikane pia kunaweza kuwa na maafisa wenye choyo au wenye kutaka kulipa kisasi ambao wanaweza kuvamia maduka na kuteketeza mali kwa kisingizio kwamba ni feki.
Ijulikane pia kwamba bidhaa au vifaa vyote hata kama vina ubora wa chini vinanunuliwa wa wenye maduka, na kama vimetoka nje ya nchi, ni fedha zetu za kigeni zimetumika. Kabla ya kuviteketeza ni lazima turidhike kwamba ni kwa manufaa ya umma au la.
Ningependekeza kwamba bidhaa ambazo zinatumika kama chakula au dawa za binadamu au mifugo ambazo ni feki ziteketezwe bila kusita pale inapodhihirika hazifai. Hata bidhaa ambazo ni dawa za mimea au mbolea ambazo ni feki ziteketezwe. Lakini bidhaa ambazo ni vyombo vya matumizi yasioathiri afya mara moja, kama redio, TV sets, samani, mavazi n.k., waagizaji walazimishwe kuvirejesha kwa waliowauzia na kuwarudishia fedha zao.
Hapo awali, wakati nikiwa Gavana wa Benki Kuu, waagizaji wa bidhaa toka ngambo walikuwa wanatakiwa wafungue Letters of Credit katika benki yao ya biashara, na hiyo benki ilikuwa inaruhusiwa kupeleka fedha kwa muuzaji wa hizo bidhaa tu, pale zilipofika katika bandari yetu na kuruhusiwa na Idara ya Forodha kuingia nchini. Kama utaratibu huu ukizingatiwa, na kuhusisha TBS katika kukagua na kuthibitisha ubora wa bidhaa zinazoingia, basi tungelipia mali inayokidhi ubora tunaotaka tu. La sivyo bidhaa mbovu zingerudishwa zilikotoka, kwa vile hazitalipiwa.
Kuhusu ubora wa bidhaa tunazozalisha hapa nchini, bila shaka kama TBS na wenye kuzinunua toka viwandani au mahala popote zinapotengenezwa watakuwa makini, tutaepuka tatizo hili. Hasara kwa wafanya biashara pia itaepukwa.
Majukumu haya muhimu ya TBS yanapaswa kutekelezwa kabla bidhaa hazijaanza kusambazwa au kuuzwa reja reja kwa wananchi. Hata hivyo kumezuka mtindo wa wafanya biashara wengi kuuza bidhaa feki au bidhaa zenye ubora wa hali ya chini sana.
Huenda hali hii inatokana na maafisa wa TBS kutokuwa makini pale bidhaa zinazalishwa humu nchini. Kwa bidhaa zinazoingia toka nje, Idara ya Forodha na TBS wanatakiwa kuhakikisha ubora wa bidhaa hizo. Inakuwa ni fedhedha kwa Idara ya Serikali kutoza ushuru na kodi na TBS kuruhusu bidhaa ziingie, halafu zikifika dukani, Polisi wanazikamata na kuziteketeza eti kwa vile ni bidhaa feki.
Hali hii huenda ikatokana na tamaa ya wafanya biashara wenyewe kutaka kutajirika haraka haraka kwa kuuza bidhaa rahisi, au kutokuwa makini katika kuamua ni bidhaa zipi bora. Wenye tamaa hata kuagiza bidhaa mbovu au hafifu kwa bei ya chini maksudi ili waweze kuziuza kwa urahisi kwa vile wanajua wanunuzi wengi nchini kwetu wana uwezo mdogo kutokana na umaskini. Idara ya Forodha na TBS wahusishwe kikamilifu. Waagizaji wa bidhaa hafifu wasije wakatoa rushwa kwa maafisa wa TBS kupitishabidhaa zisizokidhi mahitaji na nyingine kuweza kuathiri afya na maisha ya wananchi.
Kumezuka mtindo wa viongozi wa Serikali katika ngazi za chini kuvamia maduka vijijini au hata mijini na kukamata bidhaa feki au bidhaa zenye ubora wa hali ya chini na kuamuru ziteketezwe. Wananchi kadhaa hushangilia wanapoona wafanya biashara wakitiwa mbaroni au bidhaa zao zikiteketezwa, wakiwalaumu kwamba ni wanyonyaji na mabepari.
Maoni yangu ni kwamba mtindo huu unaweza kutupeleka pabaya. Wafanya biashara vijijini ni watu muhimu wanaotoa huduma ambayo wanavijiji wanahitaji kwa karibu. Duka la kijijini ni mahala wanajamii wanapopata kwa karibu bidhaa au vifaa ambavyo wangelazimika kwenda mbali kuvipata. Hata katika miji, bidhaa au vifaa muhimu hupatikana toka maduka haya yanayotoa huduma za reja reja.
Kama bidhaa ni feki au zina ubora wa hali ya chini, ni kutokana na udhibiti usiokidhi mahitaji katika viwanda au bandarini wakati wa kuingiza bidhaa hizo. Kwa hiyo TBS na wakala wake wana wajibu wa kufanya kazi zaidi. Sina hakika Sheria inayohusu TBS inatumiwaje kudhibiti bidhaa hafifu au feki ambazo tayari zimekwishaingia katika maduka ya reja reja.
Hata hivyo, ili kuondoa uwezekano wa wafanya biashara kuonewa, nashauri TBS itoe maelekezo na utaratibu wa kufuata katika kushughulikia tatizo hili. Itambulike kwamba wenye maduka mijini na vijijini ni watu wanaotoa huduma muhimu, wengi wao wakiwa ni waadilifu. Ijulikane pia kunaweza kuwa na maafisa wenye choyo au wenye kutaka kulipa kisasi ambao wanaweza kuvamia maduka na kuteketeza mali kwa kisingizio kwamba ni feki.
Ijulikane pia kwamba bidhaa au vifaa vyote hata kama vina ubora wa chini vinanunuliwa wa wenye maduka, na kama vimetoka nje ya nchi, ni fedha zetu za kigeni zimetumika. Kabla ya kuviteketeza ni lazima turidhike kwamba ni kwa manufaa ya umma au la.
Ningependekeza kwamba bidhaa ambazo zinatumika kama chakula au dawa za binadamu au mifugo ambazo ni feki ziteketezwe bila kusita pale inapodhihirika hazifai. Hata bidhaa ambazo ni dawa za mimea au mbolea ambazo ni feki ziteketezwe. Lakini bidhaa ambazo ni vyombo vya matumizi yasioathiri afya mara moja, kama redio, TV sets, samani, mavazi n.k., waagizaji walazimishwe kuvirejesha kwa waliowauzia na kuwarudishia fedha zao.
Hapo awali, wakati nikiwa Gavana wa Benki Kuu, waagizaji wa bidhaa toka ngambo walikuwa wanatakiwa wafungue Letters of Credit katika benki yao ya biashara, na hiyo benki ilikuwa inaruhusiwa kupeleka fedha kwa muuzaji wa hizo bidhaa tu, pale zilipofika katika bandari yetu na kuruhusiwa na Idara ya Forodha kuingia nchini. Kama utaratibu huu ukizingatiwa, na kuhusisha TBS katika kukagua na kuthibitisha ubora wa bidhaa zinazoingia, basi tungelipia mali inayokidhi ubora tunaotaka tu. La sivyo bidhaa mbovu zingerudishwa zilikotoka, kwa vile hazitalipiwa.
Kuhusu ubora wa bidhaa tunazozalisha hapa nchini, bila shaka kama TBS na wenye kuzinunua toka viwandani au mahala popote zinapotengenezwa watakuwa makini, tutaepuka tatizo hili. Hasara kwa wafanya biashara pia itaepukwa.