Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Kwenye Biblia katika kitabu cha Mwanzo, baada ya mwanadamu kuasi, alipewa hukumu iliyosema kwa jasho lako utaishi. ukiendelea kuisoma Biblia, kuna mpambanu mwing wa kuhusu ajira, ujira na hata wenye mali na wasio na mali, tajiri na masikini.
Katika agano jipya, kuna mfano wa waliopewa Talanta na wale waliozizalisha marudufu, walipewa motisha na yule aliyeilazia damu na kurudisha kile kile, akanyang'anywa alichokuwa nacho. Ama kuna hadithi ya wale walikwenda kazini asubuhi, na yule wa jioni lakini wakalipwa ujira ule ule. Zaidi kuna kauli inayosema mwenye nacho ataongezewa na asiyekuwa nacho atanyang'anywa.
Hata hivyo Biblia hii hii, inatoa utata pale inapozungumzia kuwa ni heri ya Ngamia kupita tundu la sindano kuliko tajiri kuingia mbinguni. Ama kuna ilee hadithi ya yule tajiri ambaye baada ya kujidundulizia aliamua kunywa mvinyo na kushereheka matunda ya kazi yake na kusema moyo wake upumzike na Israeli akauchukua uhai wake.
Sisi kama Taifa, mwaka 1967 tulilipokea Azimio la Arusha ambalo katika msisitizo wake, kuna lile linalosema kuwa binadamu wote sawa na linalosema kuwa lazima kuwe na uwiano wa kimapato.
Napenda nijengee hoja yangu kwa sisi kutathmini sehemu hii ya Azimio kama kipimio cha upotofu na udhaifu wa Azimio ambao ndio umezaa na kuendeleza Umasikini wa kipato na juhudi na maarifa kutokana na mapokeo hasi yaliyofanywa na jamii.
Aidha katika kufanya hivi, nafikiri Mwalimu Nyerere alilipuuzia lile ambalo Mkandara hulisema la Watu na Mazingira kwa mantiki ya kusema Mwalimu hakuwaelewa wafuasi wake na wananchi wa Tanzania iki kuhakikisha kuwa Azimio halikuleta utata au kujenga udhaifu wa kimapato na ufanisi katika ubunifu wa kazi na uzalishaji mali.
Kifupi ni kwamba pamoja na kwamba Azimio lilisema tunataka kujenga jamii na nchi yenye kujitegemea, matendo ya kiserikali na chama tawala yaliifanya Tanzania iwe nchi tegemezi na ndio mana mpaka leo hii imekuwa ni vigumu kwa Tanzania kujinasua kutoka Umasikini au Utegemezi na hasa kuwa na juhudi za kujikwamua kibinafsi na kwa ubunifu katika kuleta maendeleo ya uzalishaji mali na hivyo kuongezeka kwa kipato cha Mtanzania.
Nimeanza kwa kuleta mifano ya Biblia kwa kuwa ndani ya Biblia na Ukristo, tunaonyeshwa utata ambao upande mmoja unalaani vitendo vya matajiri, lakini kauli hizo zinapokelewa kama ni kulaani utajiri.
Azimio nalo lililaani si Matajiri pekee, bali hata Utajiri na kuufanya Utajiri kuwa ni Ufedhuli, Unyang'au na Unyama kwa kudai kuwa Utajiri ni sehemu ya Ubepari.
Nimemsoma Prof. Shivji hivi karibuni akitoa mada kuhusiana na Mwalimu Nyerere, napo nikaona tena yale yale maneno ya kulaani Utajiri na Uliberali kwa kuufanya ni sumu.
Sasa katika mfumo wowote kuna pande mbili, kwa madhumuni makubwa ya hoja yangu, palipo na Umasikini, lazima pawe na Utajiri. hivyo katika jamii, ni lazima kuwe na pande zote mbili za Matajiri na Masikini.
Lakini sisi tunadai hilo si sahihi, ni lazima tuwe na jamii ya kati ambayo si Tajiri sana wala Masikini sana ili kujenga jamii yenye nguvu na kujitegemea.
Hata hivyo Azimio katika sehemu hii ninayonukuu hapa chini, ni wazi lilikatisha ule mwendo na mwenendo wa Watanzania kuwa Wabunifu kwa kushuhudia Utajiri kuwa ni sumu badala ya kushuhudia vitendo dhalilishwaji kuwa ni uovu.
Kama Azimio lisingepiga vita Utajiri na badala yake likajijenga kwa kupiga vita vitendo vya kidhalimu na udhulumu, leo hii tungekuwa tumepiga hatua ya kuondokana na Umasikini.
Ilikuwa ni makosa kwa Azimio kutoa tamko ambalo lilidumaza maendeleo ya viwanda na ustawi wa Watu binafsi kama Wazalishaji huru kwa kutamka kuwa kuhodhi mali au kujizalishia kwa ziada ni sumu na si sahihi katika mfumo wa Kijamaa.
Azimio lilizungumzia pato la haki, lakini pato la haki kutokana na kazi bado halijaweza kupatikana kwa Mtanzania kutokana na Serikali na Chama kuingilia kati mfumo wa Uzalishaji mali kwa kisingizio cha kujenga Ujamaa, bila kutafakari kuwa Serikali haiwezi kuwa mzalishaji mali, mtunga sheria, mdhibiti sheria na mkusanyaji wa mapato.
Ama pale Azimio lilipotoa kauli la kudai hakuna tabaka la Wafanyakazi na Wanaofanyiwa kazi (waajiri), kauli hiyo ilipokelewa kinyume na Watanzania na ndio maana hata leo hii, pamoja na Tanzania kujitahidi kuingia katika mfumo wa Uchumi huria au wa Kibepari, bado kuna msuguano wa kifikra wa kuona wanaoajiri wafanyakazi hasa katika sekta binafsi kuwa ni wahujumu na ni mabepari ambao ni sumu tuliyoitolea ushuhuda kwenye Azimio la Arusha na azma yetu ya kujenga jamii ya kijamaa na kujitegemea.
Kingine kibaya zaidi ni kile cha kuondoa ushindani katika sekta za uzalilshaji mali kwa kuhakikisha kuwa kila kitu kinadhibitiwa na Serikali badala ya kuhakikisha kuwa sheria na Kanuni ambazo zingemlinda kila mtu, kuanzia mtumia bidhaa, mzalishaji wa idhaa, mwajiriwa na mwajiri vinakuwa bayana na haki inatumika katika kuhakikisha hakuna uonevu na dhuluma.
Basi ni vema tukalirudia Azimio kwa kunyoosha udhaifu na mapokeo potofu ambayo yametudumaza si kifikra tuu bali hata kwa vitendo na kutufikisha hapa tulipo.
FULL VERSION ya Azimio - https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=44703&d=1325749444
Katika agano jipya, kuna mfano wa waliopewa Talanta na wale waliozizalisha marudufu, walipewa motisha na yule aliyeilazia damu na kurudisha kile kile, akanyang'anywa alichokuwa nacho. Ama kuna hadithi ya wale walikwenda kazini asubuhi, na yule wa jioni lakini wakalipwa ujira ule ule. Zaidi kuna kauli inayosema mwenye nacho ataongezewa na asiyekuwa nacho atanyang'anywa.
Hata hivyo Biblia hii hii, inatoa utata pale inapozungumzia kuwa ni heri ya Ngamia kupita tundu la sindano kuliko tajiri kuingia mbinguni. Ama kuna ilee hadithi ya yule tajiri ambaye baada ya kujidundulizia aliamua kunywa mvinyo na kushereheka matunda ya kazi yake na kusema moyo wake upumzike na Israeli akauchukua uhai wake.
Sisi kama Taifa, mwaka 1967 tulilipokea Azimio la Arusha ambalo katika msisitizo wake, kuna lile linalosema kuwa binadamu wote sawa na linalosema kuwa lazima kuwe na uwiano wa kimapato.
Napenda nijengee hoja yangu kwa sisi kutathmini sehemu hii ya Azimio kama kipimio cha upotofu na udhaifu wa Azimio ambao ndio umezaa na kuendeleza Umasikini wa kipato na juhudi na maarifa kutokana na mapokeo hasi yaliyofanywa na jamii.
Aidha katika kufanya hivi, nafikiri Mwalimu Nyerere alilipuuzia lile ambalo Mkandara hulisema la Watu na Mazingira kwa mantiki ya kusema Mwalimu hakuwaelewa wafuasi wake na wananchi wa Tanzania iki kuhakikisha kuwa Azimio halikuleta utata au kujenga udhaifu wa kimapato na ufanisi katika ubunifu wa kazi na uzalishaji mali.
Kifupi ni kwamba pamoja na kwamba Azimio lilisema tunataka kujenga jamii na nchi yenye kujitegemea, matendo ya kiserikali na chama tawala yaliifanya Tanzania iwe nchi tegemezi na ndio mana mpaka leo hii imekuwa ni vigumu kwa Tanzania kujinasua kutoka Umasikini au Utegemezi na hasa kuwa na juhudi za kujikwamua kibinafsi na kwa ubunifu katika kuleta maendeleo ya uzalishaji mali na hivyo kuongezeka kwa kipato cha Mtanzania.
Nimeanza kwa kuleta mifano ya Biblia kwa kuwa ndani ya Biblia na Ukristo, tunaonyeshwa utata ambao upande mmoja unalaani vitendo vya matajiri, lakini kauli hizo zinapokelewa kama ni kulaani utajiri.
Azimio nalo lililaani si Matajiri pekee, bali hata Utajiri na kuufanya Utajiri kuwa ni Ufedhuli, Unyang'au na Unyama kwa kudai kuwa Utajiri ni sehemu ya Ubepari.
Nimemsoma Prof. Shivji hivi karibuni akitoa mada kuhusiana na Mwalimu Nyerere, napo nikaona tena yale yale maneno ya kulaani Utajiri na Uliberali kwa kuufanya ni sumu.
Sasa katika mfumo wowote kuna pande mbili, kwa madhumuni makubwa ya hoja yangu, palipo na Umasikini, lazima pawe na Utajiri. hivyo katika jamii, ni lazima kuwe na pande zote mbili za Matajiri na Masikini.
Lakini sisi tunadai hilo si sahihi, ni lazima tuwe na jamii ya kati ambayo si Tajiri sana wala Masikini sana ili kujenga jamii yenye nguvu na kujitegemea.
Hata hivyo Azimio katika sehemu hii ninayonukuu hapa chini, ni wazi lilikatisha ule mwendo na mwenendo wa Watanzania kuwa Wabunifu kwa kushuhudia Utajiri kuwa ni sumu badala ya kushuhudia vitendo dhalilishwaji kuwa ni uovu.
Kama Azimio lisingepiga vita Utajiri na badala yake likajijenga kwa kupiga vita vitendo vya kidhalimu na udhulumu, leo hii tungekuwa tumepiga hatua ya kuondokana na Umasikini.
Ilikuwa ni makosa kwa Azimio kutoa tamko ambalo lilidumaza maendeleo ya viwanda na ustawi wa Watu binafsi kama Wazalishaji huru kwa kutamka kuwa kuhodhi mali au kujizalishia kwa ziada ni sumu na si sahihi katika mfumo wa Kijamaa.
Azimio lilizungumzia pato la haki, lakini pato la haki kutokana na kazi bado halijaweza kupatikana kwa Mtanzania kutokana na Serikali na Chama kuingilia kati mfumo wa Uzalishaji mali kwa kisingizio cha kujenga Ujamaa, bila kutafakari kuwa Serikali haiwezi kuwa mzalishaji mali, mtunga sheria, mdhibiti sheria na mkusanyaji wa mapato.
Ama pale Azimio lilipotoa kauli la kudai hakuna tabaka la Wafanyakazi na Wanaofanyiwa kazi (waajiri), kauli hiyo ilipokelewa kinyume na Watanzania na ndio maana hata leo hii, pamoja na Tanzania kujitahidi kuingia katika mfumo wa Uchumi huria au wa Kibepari, bado kuna msuguano wa kifikra wa kuona wanaoajiri wafanyakazi hasa katika sekta binafsi kuwa ni wahujumu na ni mabepari ambao ni sumu tuliyoitolea ushuhuda kwenye Azimio la Arusha na azma yetu ya kujenga jamii ya kijamaa na kujitegemea.
Kingine kibaya zaidi ni kile cha kuondoa ushindani katika sekta za uzalilshaji mali kwa kuhakikisha kuwa kila kitu kinadhibitiwa na Serikali badala ya kuhakikisha kuwa sheria na Kanuni ambazo zingemlinda kila mtu, kuanzia mtumia bidhaa, mzalishaji wa idhaa, mwajiriwa na mwajiri vinakuwa bayana na haki inatumika katika kuhakikisha hakuna uonevu na dhuluma.
Basi ni vema tukalirudia Azimio kwa kunyoosha udhaifu na mapokeo potofu ambayo yametudumaza si kifikra tuu bali hata kwa vitendo na kutufikisha hapa tulipo.
Nchi yenye Ujamaa kamili ni nchi ya wafanyakazi:
haina ubepari wala ukabaila.
Haina tabaka mbii za watu: tabaka ya chini ya watu wanaoishi kwa kufanya kazi, na tabaka ya juu ya watu wanaoishi kwa kufanyiwa kazi.
Katika nchi ya Ujamaa kamili mtu hamnyonyi mtu, bali kila awezaye kufanya kazi hufanya kazi, na kila mfanya kazi hupata pato la haki kwa kazi aifanyayo na wala mapato ya wafanyakazi mbali mbali hayapitani mno.
Katika nchi ya Ujamaa kamili watu peke yao ambao huishi kwa jasho la wenzao, na ni haki yao kuishi kwa jasho la wenzao ni watoto wadogo, wazee wasiojiweza, vilema na wale ambao, kwa muda, Jumuiya imeshindwa kuwapatia kazi yo yote ya kujipatia riziki kwa nguvu zao wenyewe.
Nchi yetu ni nchi ya Wakulima na Wafanya kazi, lakini si nchi ya Ujamaa kamili. Ina misingi ya ubepari na ukabaila na vishawishi vyake. Misingi hii ya ubepari na ukabaila yaweza ikapanuka na kuenea.
Namna ya pekee ya kujenga na kudumisha ujamaa ni kuthibitisha kuwa njia kuu zote za uchumi wa nchi yetu zinatawaliwa na kumilikiwa na Wakulima na Wafanyakazi wenyewe kwa kutumia vyombo vya Serikali yao na Vyama vyao vya Ushirika. Pia ni lazima kuthibitisha kuwa Chama kinachotawala ni Chama cha wakulima na wafanyakazi.
Njia kuu za Uchumi ni kama vile ardhi, misitu, madini, maji, mafuta na nguvu za umeme; njia za habari, njia za usafirishaji; mabenki, na bima; biashara na nchi za kigeni na biashara za jumla; viwanda vya chuma, mashini, silaha, magari, simenti, mboleo; nguo, na kiwanda cho chote kikubwa ambacho kinategemewa na sehemu kubwa ya watu katika kupata riziki zao au kinachotegemewa na viwanda vingine; mashamba makubwa na hasa yale yanayotoa mazao ya lazima katika viwanda vikubwa.
FULL VERSION ya Azimio - https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=44703&d=1325749444