JUMUIYA ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa), imeandaa kongamano la pili la Katiba ambalo pamoja na mambo mengine, litajadili muswada maalumu wa sheria unaopendekeza mabadiliko ya katiba ya Tanzania. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa Udasa na Mratibu wa Kongamano hilo, Dk Kitila Mkumbo, alisema muswada huo una upungufu mwingi ambao lazima uangaliwe kwa umakini.
Kwanza ni kwanini suala la tume apewe Rais, kwanini shughuli hii isifanywe na Bunge? Katika nchi za wenzetu kama Kenya, Ghana na Afrika kusini Bunge ndio limefanya hiyo shughuli, alisema Dk Kitila na kuongeza: Muswada unapendekeza tume iwe na watu 30, Kenya walikuwa na watu tisa tu, wakati mwingine mambo mazuri lazima tuyachukue kutoka kwa wenzetu, halafu haina ukomo wa kukusanya maoni na haiainishi moja kwa moja sifa za watu wanaotakiwa kuteuliwa kwenye tume.
Kutokana na hali hiyo, alisema upungufu huo na mwingine, utachambuliwa siku hiyo kuwapa wananchi uelewa kilichopo kwenye muswada huo. Kwenye kongamano hilo, wananchi na watoa mada watajikita zaidi kueleza maudhui ambayo yanatakiwa kubebwa kwenye katiba na kuainisha mambo yanatakiwa kuchukuliwa kutoka katiba ya sasa.
Naye Mwenyekiti wa Udasa, Dk Mshumbuzi Kibogoya, alisema watoa mada wakuu kwenye kongamano hilo litakalofanyika Jumamosi hii, ni Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samata na Mkurugenzi Mtendaji Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Francis Kiwanga.
Pia, vyama vya siasa vyenye wawakilishi Bungeni vimelikwa na vimethibitisha ushiriki wake, CCM kitawakilishwa na Makamu mwenyekiti wake, Pius Msekwa na Chadema kitawakilishwa na Mwanasheria wake, Mabele Marando. Kila chama kitapewa dakika kumi kutoa maoni yake na wananchi wengine watakaoshiriki wataruhusiwa kutoa maoni yao, alisema Dk Kibogoya.
Kwanza ni kwanini suala la tume apewe Rais, kwanini shughuli hii isifanywe na Bunge? Katika nchi za wenzetu kama Kenya, Ghana na Afrika kusini Bunge ndio limefanya hiyo shughuli, alisema Dk Kitila na kuongeza: Muswada unapendekeza tume iwe na watu 30, Kenya walikuwa na watu tisa tu, wakati mwingine mambo mazuri lazima tuyachukue kutoka kwa wenzetu, halafu haina ukomo wa kukusanya maoni na haiainishi moja kwa moja sifa za watu wanaotakiwa kuteuliwa kwenye tume.
Kutokana na hali hiyo, alisema upungufu huo na mwingine, utachambuliwa siku hiyo kuwapa wananchi uelewa kilichopo kwenye muswada huo. Kwenye kongamano hilo, wananchi na watoa mada watajikita zaidi kueleza maudhui ambayo yanatakiwa kubebwa kwenye katiba na kuainisha mambo yanatakiwa kuchukuliwa kutoka katiba ya sasa.
Naye Mwenyekiti wa Udasa, Dk Mshumbuzi Kibogoya, alisema watoa mada wakuu kwenye kongamano hilo litakalofanyika Jumamosi hii, ni Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samata na Mkurugenzi Mtendaji Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Francis Kiwanga.
Pia, vyama vya siasa vyenye wawakilishi Bungeni vimelikwa na vimethibitisha ushiriki wake, CCM kitawakilishwa na Makamu mwenyekiti wake, Pius Msekwa na Chadema kitawakilishwa na Mwanasheria wake, Mabele Marando. Kila chama kitapewa dakika kumi kutoa maoni yake na wananchi wengine watakaoshiriki wataruhusiwa kutoa maoni yao, alisema Dk Kibogoya.