Udanganyifu wa foreign investors-soma kwa makini

Kokolo

JF-Expert Member
Mar 20, 2008
1,768
2,766
Hawa Investors wakutoka nje ya nchi wanapokuja kuwekeza hapa Tanzania, utasikia amewekeza 100 billion. 400billion etc, kumbe mtaji wenyewe ni 10 million.

Mfano: Wale mashujaa wa Tarime walipoaribu vifaa vya wachimba madini mgodini ambavyo ni ( Wheel loader 988H, Drill Rig, and Shovel). Walisema thamani ya hivyo vifaa ni $16.6 million=17 billion Tshs.) Ebu angalia thamani yenyewe ya hivyo vifaa hapa Chini kwenye attachment.

Kwa nini hawasemi bei harisi ya vifaa, ni kutaka kutolipa kodi miaka na miaka, milele na milele. Je kuna faida gani ya kuwa na Investors hawa. na Kwa nini stamiko isipewe mitaji na kuchimba madini kawa hayo makampuni yanatumia wataalamu wetu sisi wenyewe, vifaa vya kukodi kwa nini stamiko isifanye kazi hiyo badala ya Mzungu toka Ulaya.

This Day "damaged equipment include a caterpillar loader worth $1.6m, two shovel machines valued at $7m and $4m respectively, and a drill rig worth $4m,"
 

Attachments

  • WHEEL LOADER 988-RIG-SHOVEL.pdf
    146.2 KB · Views: 179
Kokolo thanks for the good findings. Ni kwamba hawa wawekezaji wanakuja bila hata pesa yyoyote ya investment then nao wanaomba loans toka kwenye mabenki humu nchini. Nakubaliana na Kokolo kuwa mashine hizo wanunuliwe Stamico na serikali wataalam wa madini tunao hapa nchini hata kama atatoka nje ni kwa contract maalum full stop. Someone has to take action now for the betterment of all Tanzanians.
 
yote hiyo inachangiwa na 10%, ndio huwafundisha ujanja ilimradi nao waliohongwa wameshapata kitu. Sasa ni serikali gani itaambiwa kuwa tumewekeza kwa bilioni 40, nayo ikubali kibubusa bila hata kuchunguza. Ina maana tutadanganywa mpaka lini ama kuwaamini wawekezaji kila wasemalo. Ndio tatizo lakini, kama nchi imeoza toka chini, tutarajie nini?, ulizia mtu anapothaminiwa kutengeneza tu vyeti vya hospitali za serikali, uoanishe gharama atakayotoa na ile iliyoko ktk soko, ni udanganyifu mkubwa.
 
wizi mtupu!
ubinafsi, uchoyo, kutoweka maslahi ya taifa mbele ndio tabu yetu.
viongozi wetu wamekuwa watu wakufikiria leo tu.
lakini nashukuru mungu wenyewe wameanza kungia mkenge taratibu kwa kuruhusu utitili wa vyuo hata kama walimu hawatoshi ambao wengi wao wakimaliza wanategemea vyeti viwaajiri
hapo ndo patakuwa pazuri zaidi tutegemee fujo mtindo mmoja za watu kudai haki zao
ninachojua hata kama hawatapata elimu bora iliyokusudiwa kwa ajili ya mazingira magumu lakini uwezo wao wa kuelewa mambo utakuwa umeongezeka kamwe hawatakubali kuburuzwa is just matter of time!
hawawezi kukubali upumbafu huu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom