Udaktari wa JK ni wa hii hapa

sijuikitu

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
286
12
Wengi wanaona JK ana uDakta feki....ila sio feki, ni udaktari wa ukweli kabisa....Yeye kama Dakta JK ni mwalimu. Na kwa sasa anatufundisha sisi watanzania.

Anatufundisha umuhimu wa kupiga kura. Kwa sababu miaka ya nyuma tulikuwa tunadharau kura zetu, ameamua kutuonyesha ukichezea kura yako matokeo yake ni nini.

Naamini watu watakao piga kura 2015 watakuwa weengii sanaaaa. Na akimaliza muda wake itabidi tumpe uprofesa kabisa, maana hili somo la sasa hata kulidesea sio lazima, linaeleweka na kusahau ni vigumu.

1. utasahauje mabomu? (mara ya kwanza ilikuwa bahati mbaya, hatuihesabii)
2. mgao wa umeme (pia mara ya kwanza ilikuwa bahati mbaya mvua hazikunyesha)
3. DOWANS (pia mara ya kwanza "richmond" ilikuwa bahati mbaya)
4 ......list ni ndefu na najua watanzania wote wanaijua kama hesabu za kuzidisha moja mara moja moja, moja mara mbili mbili, moja mara tatu tatu......


Huu ndio mwaka 2010....bado kuna 2011, 2012, 2013, 2014...na hata 2015 (uchaguzi ni october mjue.....na JK ameshatuonyesha kuwa ndani ya miezi minne tu mambo mengi yanaweza kutokea including watu wakatae kupigwa picha)
 
Back
Top Bottom