UDA imebinafsishwa ili iingie Biashara na DART - Siri ya kuuzwa Bei Chee

"An international review of paratransit regulation and integration experiences: Lessons for public transport system rationalisation and improvement in African cities: A Case Study of the Integrated Rapid Transit system in Cape Town and the Dar Es Salaam Rapid Transit project":http://www.vref.se/download/18.1166db0f120540fe049800010991/Mfinanga+-+An+international+review.pdf



Asante sana; unajua sijawahi kukaa na kulifikiria hili la UDA kwani nami kama wengine nilikubali maelezo ya kuwa UDA ilishindwa kuwahudumia watu wa Dar kwa kiwango cha kuridhisha. Niliposikia kuwaa shirika bado lipo na lina assets na linataka kuingizwa kwenye DART swali moja tu lilikuwepo - kwanini UDA haikugeuzwa DART? Ni maneno manne tu lakini bado sijapewa jibu la uhakika na la akili. Nimeamua na mimi kuridhisha udadisi wangu thanks. Mwenye document yoyote kuhusiana na UDA hadi ilipofika hapa naomba mnipatie.
 
Asante sana; unajua sijawahi kukaa na kulifikiria hili la UDA kwani nami kama wengine nilikubali maelezo ya kuwa UDA ilishindwa kuwahudumia watu wa Dar kwa kiwango cha kuridhisha. Niliposikia kuwaa shirika bado lipo na lina assets na linataka kuingizwa kwenye DART swali moja tu lilikuwepo - kwanini UDA haikugeuzwa DART? Ni maneno manne tu lakini bado sijapewa jibu la uhakika na la akili. Nimeamua na mimi kuridhisha udadisi wangu thanks. Mwenye document yoyote kuhusiana na UDA hadi ilipofika hapa naomba mnipatie.

Mkuu UDA kulikuwa hakuna tatizo. UDA, kama mashirika mengine ya umma, ilishindwa kufanya kazi tuu kutokana na ukiritimba uliokuwepo serikalini. UDA ilikuwa na planing nzuri ya usafiri. Makonda walikuwa well trained tofauti kabisa na wale wa Chai Maharage. Routes za UDA zilikuwa well planned (walikuwa hawakatishi safari hata kama basi ni tupu). Tatizo kubwa la UDA ni kwamba nauli zake zilikuwa zinapitishwa na baraza la mawaziri. Badala ya kupitisha nauli in a commercial way, serikali ilikuwa inaangalia tuu kama abiria wata afford hizo nauli. Maamuzi juu ya nauli yalikuwa yanatolewa na serikali bila kuangalia gharama za undeshaji.

Kwa mfano, zilipoanza daladala nauli zao zilikuwa shilingi tano, wakati UDA iliendelea ku charge shilingi moja mpaka moja unusu. Na daladala zilikuwa zinajaa japokuwa zilikuwa illegal wakati huo. Financial deficity ambayo ilitokana na maamuzi ya serikali, ndio yamefanya UDA iwe hapo ilipo. Unajua neno daladala limetokana na nini? Kwa sababu wakati hii biashara inaanza, exchange rate ya dola moja ya Kimarekani ilikuwa shilingi tano (dala).

Wakati huo daladala zilikuwa zina operate illegally mpaka mwaka 1983 ziliporuhusiwa rasmi ili ku comply na Economic Reform Programme (ERP). Tatizo kubwa lililofanywa ni ku legalise daladala bila kuziwekea regulations jinsi zitakavyofanya kazi, kuzitafutia route, n.k. Matokeo yake hata serikali ilipoanza kuziwekea regualations na routes, it was too late.

Utafiti uliyofanywa ndani ya Dar-es-Salaam Region Transport Licensing Authority (DRTLA), ambayo ina regulate daladala, unaonyesha kuna matatizo makubwa sana. Ukilinganisa na UDA, haina professional staff, qualified traffic inspectors or traffic planners. Pamoja na kwamba kuna regulations zinazodhibiti daladala, asilimia 30 tuu ya hizo daladala ni roadworthy. Hapo unajiuliza DRTLA inafanya nini? Future yake itakuwaje baada ya DART kuanza kazi?

Kuna watu toka Dar City Council walitembelea jiji la Bogota nchini Colombia mwaka mwaka 2002 na inasemekana kuwa DART itafuata plan ya Bogota (BRT). Baada ya DART ku take off, kuna senior officers wawili wa DART walitembelea jiji la Miami Marekani sasa sijui kama wameamua kutofuata plan ya Bogota. The Institute for Transportation and Development Policy (ITDP) ilitengeneza plan ya kuboresha usafiri Dar Es Salaam. Plan yao ina incorporate streests, shared streets and pedestrian streets ili kuwe na nafasi ya kutosha kwa magari na pedestrians. Sijui kama hii itakuwa implemented.
 
EMT.. nimeuliza hivyo kwa sababu inaonekana public transportation tunaingalia kwa kutumia prism ya faida. Hivi ni lazima UDA iwe kampuni ya kutengeneza faida badala ya huduma tu na faida isiwe katika fedha za nauli bali katika huduma inayotoa? Kwa mfano, kama UDA linaweza kusafirisha watu milioni 2 kwa mwaka, hawa watu wanachangia uchumi vipi katika shughuli zao mbalimbali?

Ukifikiria utaona kuwa hata bei kupangwa na cabinet kwangu haikuwa tatizo kabisa - hapa Detroit na maeneo mengine ya US yenye public (owned and operated) transit system bei haipangwi na soko bali na city councils au bodi na huwa imebakia hivyo kwa muda mrefu sana. Wanaangalia faida nje ya kuuza tiketi na miji hutenga fedha za kuhudumia hizo public transit. Nadhani kosa kubwa ni kwamba hatukutaka kutoa ruzuku kwenye vyombo hivi vya umma lakini tunatoa ruzuku ya mabilioni ya fedha kila mwezi kwa vyama vya siasa ili vitutawale!

Wenyewe tunafikiria ndio ubepari kumbe siyo ubepari ni ujinga tu. I really mean it.
 
Hapo sasa ulipaswa kuanzia na siyo kulete porojo kwa jambo usilolijua.Kwanza nimekujibu kwanini UDA imebinafsishwa ni kwamba ilishindwa kujiendesha kibiashara kwa sababu ya ushidani huria wa usafiri wa jijini, Mfumo wa UDA haukutoa nafasi ya kubadilika kutoka mfumo wa zamani wa kiuendeshaji na mfumo wa soko huria. UDA haikuchukua role za DART kwa sababu za kimuundo na mfumo wa uendeshaji ni tofauti kabisa.
DART Agency is a government entity established by GN No.120 of 25th May, 2007 under the Executive Agency Act No. 30 of 1997 and its subsequent amendments. The key role of the DART Agency is to establish and operate the Bus Rapid Transit (BRT) system for Dar es Salaam. The Agency aims at achieving the following objectives;
a) Establish and operate Bus Rapid Transit (BRT) system for Dar es Salaam, branded Dar Rapid Transit – DART,
b) Ensure orderly floor of traffic on urban streets and roads and
c) Ensure effective Management of the Agency.
The Agency operates under the guidance of the Prime Minister’s Office, Regional Administration and Local Government – PMO-RALG

Aim
The DART aims at “effectively planning, coordinating and facilitating the provision of urban transport facilities and services and ensuring improved traffic management in Dar es Salaam”. Hili halikuwa lengo la UDA

Mwanakijiji wewe ni mchokozi wa mada tuu, Ambaye mara nyingi unakuja na fact fake kuwahaadaa wa-JF kwamba umefanyia research yale unayoongelea,Yamkini mimi binafsi nimekuwanisoma thread nyingi zako ukweli ni asimia chache sana uongo ndo unachukua zamu kubwa zaidi .Kama yule Waziri fulani katika serikali ya JK atatoaaga figures kweli kweli kumbe asilia kubwa ya tarakimu anazowaeleza watu majukwaani ni uongo uliopitiliza,Sasa na wewe una kasumba hiyo.Ukweli umejidhihirisha katika thread hii.Mwana JF Kiroroma amekushushua kwa fact zako ulizoziweka asubuhi ya leo.

Ebu jibu swali moja muhimu hapa nani atakuwa operator wa mabasi ya DART
 
Hapo sasa ulipaswa kuanzia na siyo kulete porojo kwa jambo usilolijua.Kwanza nimekujibu kwanini UDA imebinafsishwa ni kwamba ilishindwa kujiendesha kibiashara kwa sababu ya ushidani huria wa usafiri wa jijini, Mfumo wa UDA haukutoa nafasi ya kubadilika kutoka mfumo wa zamani wa kiuendeshaji na mfumo wa soko huria. UDA haikuchukua role za DART kwa sababu za kimuundo na mfumo wa uendeshaji ni tofauti kabisa.
DART Agency is a government entity established by GN No.120 of 25th May, 2007 under the Executive Agency Act No. 30 of 1997 and its subsequent amendments. The key role of the DART Agency is to establish and operate the Bus Rapid Transit (BRT) system for Dar es Salaam. The Agency aims at achieving the following objectives;
a) Establish and operate Bus Rapid Transit (BRT) system for Dar es Salaam, branded Dar Rapid Transit – DART,
b) Ensure orderly floor of traffic on urban streets and roads and
c) Ensure effective Management of the Agency.
The Agency operates under the guidance of the Prime Minister’s Office, Regional Administration and Local Government – PMO-RALG

Aim
The DART aims at “effectively planning, coordinating and facilitating the provision of urban transport facilities and services and ensuring improved traffic management in Dar es Salaam”. Hili halikuwa lengo la UDA

Mzee wa taaluma ebu twambie nani anakuja kuendesha mabasi ya DART?
 
We Kiroroma,

Hivi unafahamu ni mara ngapi mashirika ya umma yanakwamishwa makusudi ili yaonekane hayafai kujimudu ili yaende kwa bei che.
Tena mwekezaji si wakati wote ananua kwa bei chee tunayoisikia sie. Hapo ameshakamuliwa 10% nyingi na ma directors, makatibu wakuu. Na wizara ya uchukuzi ndio bingwa wa hizi 10%.
Kwa hiyo unayosema kuwa UDA ilishindwa ni sawa kwa macho ya wengi but ukweli ni most likely it was purposely sabotaged to fail, just like so many other mashirika ya umma.

Nawakilisha

Mzee Avatar yako inapereka mbali
 
EMT.. nimeuliza hivyo kwa sababu inaonekana public transportation tunaingalia kwa kutumia prism ya faida. Hivi ni lazima UDA iwe kampuni ya kutengeneza faida badala ya huduma tu na faida isiwe katika fedha za nauli bali katika huduma inayotoa? Kwa mfano, kama UDA linaweza kusafirisha watu milioni 2 kwa mwaka, hawa watu wanachangia uchumi vipi katika shughuli zao mbalimbali?

Ukifikiria utaona kuwa hata bei kupangwa na cabinet kwangu haikuwa tatizo kabisa - hapa Detroit na maeneo mengine ya US yenye public (owned and operated) transit system bei haipangwi na soko bali na city councils au bodi na huwa imebakia hivyo kwa muda mrefu sana. Wanaangalia faida nje ya kuuza tiketi na miji hutenga fedha za kuhudumia hizo public transit. Nadhani kosa kubwa ni kwamba hatukutaka kutoa ruzuku kwenye vyombo hivi vya umma lakini tunatoa ruzuku ya mabilioni ya fedha kila mwezi kwa vyama vya siasa ili vitutawale!

Wenyewe tunafikiria ndio ubepari kumbe siyo ubepari ni ujinga tu. I really mean it.

Nafikiri hilo ndilo tatizo la daladala Dar Es Es Salaam. They are run on profit. Inaonekana pia waliokimbilia kuwekeza UDA wanaangalia profit zaidi. Hata they DART inaonekana kama itakuwa ni profit based kwa sababu private companies will be invited to place their bids. Matokeao yake matatizo yatakuwa yale yale kwa sababu makampuni yatakayoshinda tenda aims yake itakuwa ni kumiximize faida. Kwa kawaida public transport inakuwa funded na nauli za abiria. Pia transit operators au transit authority zinaweza kupata subsidies kwenye kodi na subsidies nyingine toka serikalini. Matangazo pia ni sehemu ya income. Pia nafikiri UDA inamiliki ardhi kibao ambayo inaweza kutumika kama miradi kupata fedha za kuendesha hayo mabasi. Kituo cha mabasi cha Ubungo na stendi ya Zamani ya Kisutu zinamilikiwa na nani? Tatizo kubwa tulilo nalo ni ubaridhifu ndani ya vyombo kama hivi.
 
Kumbe kuna watu wengi wenye uchungu na UDA - nyaraka zinatiririka kwenye mail box yangu hadi nasikia kizunguzungu. Nilisema baada ya PPF sikutaka kuingia kwenye haya mambo tena lakini it is almost impossible to resist the temptation. Nashangaa haya mambo walitakiwa wabunge ndio wapatiwe!!! grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr halafu wamebakia kulilia posho!! screw 'em!

Nimeongeza hiyo brochure hapo juu kuhusu UDA kumbe kulikuwa na mpango wa kupata Soft Loan ya kununua mabasi 150? Kweli watu wa Dar wana matatizo.
 
Mwalimu alishindwa kuizuia NBC isibinafsishwe mbele ya chaguo lake mwenyewe Mkapa, sidhani kuna shirika la UMMA litabaki wakubwa hawa wakishaamua kuliuza au kuuziana.
 
Hivi Kiroromo amekwenda watu yeye alionekana kujuwa usahihi wa kuuzwa kwa UDA lakini soon akatoweka nao?
 
Kumbe kuna watu wengi wenye uchungu na UDA - nyaraka zinatiririka kwenye mail box yangu hadi nasikia kizunguzungu. Nilisema baada ya PPF sikutaka kuingia kwenye haya mambo tena lakini it is almost impossible to resist the temptation. Nashangaa haya mambo walitakiwa wabunge ndio wapatiwe!!! grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr halafu wamebakia kulilia posho!! screw 'em!

Nimeongeza hiyo brochure hapo juu kuhusu UDA kumbe kulikuwa na mpango wa kupata Soft Loan ya kununua mabasi 150? Kweli watu wa Dar wana matatizo.

Tuwekee basi hizo info. Kumbe UDA ina karakana nzuri inayoweza kutengeneza hata bodi za mabasi. Ina vitega uchumi vizuri tuu vinavyofanya UDA iweze kutoa huduma ya usafiri kwenye project ya DART. Lakini kuuza nusu ya shirika kwa kampuni binafisi ina maana kuwa, UDA itakuwa inaendeshwa kibiashara. Huu mkopo nafuuu kutoka Korea ulichukuliwa lini? B'se kuna taarifa kuwa UDA ilishawahi kuomba mkopo CRDB wakatoswa.
 
Tuwekee basi hizo info. Kumbe UDA ina karakana nzuri inayoweza kutengeneza hata bodi za mabasi. Ina vitega uchumi vizuri tuu vinavyofanya UDA iweze kutoa huduma ya usafiri kwenye project ya DART. Lakini kuuza nusu ya shirika kwa kampuni binafisi ina maana kuwa, UDA itakuwa inaendeshwa kibiashara. Huu mkopo nafuuu kutoka Korea ulichukuliwa lini? B'se kuna taarifa kuwa UDA ilishawahi kuomba mkopo CRDB wakatoswa.

ndio hivyo; unajua mafisadi huwa wanaona mbali sana; wanapanga move zao kama maili 100 kabla. Wako kama tai wawindaji. Panya anaweza hata asijue kuna tai angani wakati tai ameshampiga jicho. UDA ilihitaji kubadilishwa tu kuwa chombo cha usafiri Dar - lengo ambalo ndilo liliunda. DART wala haikuwa na ulazima wowote! Sasa ili ujue move yenyewe ni kuwa badala ya kuifanya DART iwe kweli Transit system -- na mabaasi yake, karakana, na muundo wake wameamua kuifanya DART iwe ni kutengeneza hizo barabara na kuzisimamia kampuni nyingine "binafsi".

Unfortunately, wasingeweza kufanya hivyo UDA ikiwa ni taasisi huru yenye uwezo. So wakaamua kuiuza UDA badala ya kuiwezesha halafu hiyo UDA itakuja na kuingia mkataba na DART na itaanza kutengeneza hela kama ina akili mbovu. Halafu upande mwingine wanasema wenye kampuni ya daladala wajiunge na kuunda kampuni moja - guess ni kina nani watanufaika siyo wale wenye vijidaladala vidogo? Ooh nooo makampuni makubwa ya usafiri.
 
Jamani.. naona nimemiss swali kuhus UDA na DART; nimeona sehemu ya mwisho waziri akijibu na inaonekana ni Mnyika aliuliza.. any details?
 
Wenyewe kina nani?



Kwanini?



Kwanini?




Sasa wewe sema ukweli. Kwanini UDA imebinafsishwa na kwanini UDA haikuchukua majukumu ya DART au DART nayo itakuja kubinafsishwa?

MKJJ nadhani watunga sera na wanaozisimamia nchi hii wangekuwa wanaanza na maswali haya rahisi na ya msingi kabisa tusingekuwa na huu ubinafsishaji usiokuwa na kichwa wala miguu.
  • Hivi kwa nini watu hawataki kujiuliza sababu za msingi zinazopelekea haya mashirika ya umma yote yawe "yanakufa" na mara tu "yanapokufa" watu wanakimbilia kununua hisa kwa ajili ya kuendesha mashirika mfu/marehemu?. Why?
  • Ni nini hicho ambacho mtanzania huyu akiwa serikalini hawezi kukifanya kuendeleza mashirika lakini mara anapokuwa "mbinafsi" akakabidhiwa shirika lililokufa anakuwa mahiri wa kulifufua na kuliendesha kwa faida?
  • Kwa nini idara za serikali zinashindwa kulipa bili za umeme wakati kila mwaka kuna fungu la bajeti ya umeme linapitishwa na bunge?
  • Kwa nini nyumba za serikali ziliachwa mpaka zikaharibika na kujengewa hoja kuwa ni mzigo ziuzwe wakati miaka yote mafungu ya kuzikarabati yalikuwa yakipitishwa na kutumika?
  • Kama tunakubaliana kuwa mashirika ya serikali hayawezi kufikia malengo yake ya kuanzishwa ni nini kinatufanya tuamini kuwa serikali ile ile iliyoshindwa kusimamia mashirika haya ili yafikie malengo yake inaweza kusimamia mambo mengine ya kitaifa kama kuinua uchumi wa nchi, kuondoa janga la umeme, kuondoa njaa na kudhibiti mfumko wa bei?
  • Hivi kwa kufuata mantiki hiyo hiyo potofu ya ubinafsishaji kwa nini hawa viongozi wa serikali hawajengi hoja kuwa serikali kuu (kwa maana ya Ikulu, Wizara na Idara za serikali) imeshindwa kujiendesha na kufikia malengo yake na hivyo tuibinafsishe kwa wawekezaji wa kigeni toka ulaya, marekani au asia tutakuwa tumekosea?
Just thinking aloud!
 
MKJJ nadhani watunga sera na wanaozisimamia nchi hii wangekuwa wanaanza na maswali haya rahisi na ya msingi kabisa tusingekuwa na huu ubinafsishaji usiokuwa na kichwa wala miguu.
  • Hivi kwa nini watu hawataki kujiuliza sababu za msingi zinazopelekea haya mashirika ya umma yote yawe "yanakufa" na mara tu "yanapokufa" watu wanakimbilia kununua hisa kwa ajili ya kuendesha mashirika mfu/marehemu?. Why?
  • Ni nini hicho ambacho mtanzania huyu akiwa serikalini hawezi kukifanya kuendeleza mashirika lakini mara anapokuwa "mbinafsi" akakabidhiwa shirika lililokufa anakuwa mahiri wa kulifufua na kuliendesha kwa faida?
  • Kwa nini idara za serikali zinashindwa kulipa bili za umeme wakati kila mwaka kuna fungu la bajeti ya umeme linapitishwa na bunge?
  • Kwa nini nyumba za serikali ziliachwa mpaka zikaharibika na kujengewa hoja kuwa ni mzigo ziuzwe wakati miaka yote mafungu ya kuzikarabati yalikuwa yakipitishwa na kutumika?
  • Kama tunakubaliana kuwa mashirika ya serikali hayawezi kufikia malengo yake ya kuanzishwa ni nini kinatufanya tuamini kuwa serikali ile ile iliyoshindwa kusimamia mashirika haya ili yafikie malengo yake inaweza kusimamia mambo mengine ya kitaifa kama kuinua uchumi wa nchi, kuondoa janga la umeme, kuondoa njaa na kudhibiti mfumko wa bei?
  • Hivi kwa kufuata mantiki hiyo hiyo potofu ya ubinafsishaji kwa nini hawa viongozi wa serikali hawajengi hoja kuwa serikali kuu (kwa maana ya Ikulu, Wizara na Idara za serikali) imeshindwa kujiendesha na kufikia malengo yake na hivyo tuibinafsishe kwa wawekezaji wa kigeni toka ulaya, marekani au asia tutakuwa tumekosea?
Just thinking aloud!

maswali yako haya nimeyapenda; ningefurahi kusikia waziri mmoja anaulizwa.
 
Back
Top Bottom