nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Waandishi Wetu Toleo la 262 10 Oct 2012
WAKATI Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Lawrence Mafuru, akisafishwa kutokana na uchunguzi uliofanyika katika benki hiyo kwa ridhaa ya Bodi ya Wakurugenzi, aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, William Mhando, ambaye naye alisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi, mambo yanazidi kumuelemea, Raia Mwema, limebaini.
Mhando na wenzake walisimamishwa kazi TANESCO ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zikiwamo za matumizi mabaya ya madaraka na hususan kuwapo kwa mgongano wa kimaslahi, uchunguzi ulioendeshwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambao umebaini mgongano wa maslahi kwa kiongozi huyo.
Kwa mujibu wa taarifa za uchunguzi huo uliodumu kwa miezi kadhaa sasa, Mhando amebainika kuwa na mgongano wa kimaslahi na Kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd.
Kwa mujibu wa nyaraka zilizopo, Mhando ameingia mkataba na MC Donald Live Line Technology Ltd, akipewa majukumu maalumu ndani ya kampuni hiyo. Mhando alipewa jukumu la kuitafutia miradi kampuni hiyo ndani ya shirika alilokuwa akiliongoza, TANESCO.
Tayari ripoti hiyo ya uchunguzi kutoka kwa CAG imekabidhiwa katika mamlaka serikalini, ikiwa ni pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, chini ya Mwenyekiti wake, Jenerali (mstaafu) Robert Mbona na Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka serikalini, taarifa ya uchunguzi huo inamuweka katika mazingira magumu zaidi Mhando ambaye, pamoja na baadhi ya wasaidizi wake, aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma za Shirika, Robert Shemhilu, Ofisa Mkuu wa Fedha, Lusekelo Kassanga na Meneja Mwandamizi katika Ununuzi, Harun Mattambo, wote walisimamishwa kazi kupisha uchunguzi huo.
Baada ya Mhando na wenzake kusimamishwa kazi aliyekuwa Mkurugenzi wa Masoko na Usambazaji, Felschami Mramba, alikaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa TANESCO.
Pamoja na kashfa hiyo ya MC Donald Live Line Technology Ltd uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwapo pia kwa kashfa nyingine ambayo pia inaonyesha matumizi mabaya ya madaraka, ikiwa nayo inathibitishwa na nyaraka, ikihusu kujipa kazi za shirika analoliongoza hivyo kujiingiza katika mgongano wa kimaslahi.
Kashfa hiyo ni ile iliyowahi kuandikwa na gazeti hili iliyohusu kuipa zabuni kampuni iliyohusishwa na mkewe.
Kwa mujibu wa nyaraka ambazo Raia Mwema imeziona kuhusiana na kashfa hizo, Mhando aliingia mkataba na Kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd akiwa na jukumu la ndani ya kampuni hiyo la utafutaji miradi ikiwamo ile ya TANESCO.
Kutokana na kuwapo kwa taarifa hizo zinazothibitishwa na nyaraka mbalimbali, mwandishi wetu aliwasiliana na Mhando ili kwanza kujua kama anaitambua kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd na kama anahusika nayo kwa kukabidhiwa jukumu la kuitafutia miradi kampuni hiyo binafsi.
Mhando alimjibu mwandishi wetu akisema; "Haya masuala yote ambayo unaniuliza yapo chini ya uchunguzi, kwa hiyo mimi siwezi kuyazungumzia kwa sababu yanachunguzwa."
Bodi ya TANESCO njia panda
Hata hivyo, huku ikiwa na taarifa hiyo tayari kwa kuipitia, Bodi ya TANESCO imejikuta ikiwa njia panda kwa baadhi ya wajumbe wake kuamua kutishia kujiuzulu; licha ya kutakiwa kukamilisha jukumu la kuhitimisha kazi ya kupitia taarifa hiyo ya uchunguzi dhidi ya menejimenti ya TANESCO iliyosimamishwa.
Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya bodi hiyo vinabainisha kuwa, mtafaruku huo umejitokeza kutokana na kauli iliyotolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle ambaye alinukuliwa na gazeti moja la kila siku akitangaza kusudio la uongozi wa wizara hiyo kuivunja Bodi ya TANESCO kutokana na kile alichokieleza dhamira ya uongozi wao, pale wizarani, kuhakikisha kwamba mgawo wa umeme hautokei tena.
Pamoja na kumaliza mgawo wa umeme, Maselle alinukuliwa akisema kwamba kukamilika kwa bomba la gesi hapo Machi mwakani na kuanza kutumika kwa gesi hiyo viwandani na majumbani kunahitaji bodi imara yenye weledi na uzalendo kwa nchi.
Kauli hiyo imechukuliwa kwa uzito na wajumbe wa bodi ya sasa kwamba uongozi wa wizara umewahukumu wao kuwa hawana weledi na si wazalendo kwa nchi yao, hivyo wakiamini lengo la kauli hiyo ni kuwadhalilisha.
"Yupi ni mzalendo kati ya Maselle aliyepewa unaibu waziri hivi karibuni na Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali Mboma aliyepigania nchi hii?" anahoji mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo na kuongeza:
"Hawa vijana wasilewe madaraka, huwezi kijana umepata unaibu waziri juzi tu unamwambia Jenerali Mboma eti hana uzalendo, hana weledi, hii si sawa. Ni kukosa adabu, huu si utamaduni wetu Waafrika."
Taarifa za ndani za bodi hiyo zinabainisha kuwa Jenerali Mboma, ambaye ni mwenyekiti wa bodi hiyo, pamoja na wajumbe wake wamekasirishwa na kauli ya Naibu Waziri huyo, na waliamua kujiuzulu siku ile ile taarifa za kauli ya Maselle zilipochapishwa gazetini.
Hata hivyo, kuwasilishwa kwa taarifa ya CAG ya uchunguzi kuhusu ufisadi ndani ya menejimenti ya shirika hilo uliiweka bodi hiyo njia panda baada ya kushauriwa kutochukua uamuzi wa kujiuzulu, na badala yake wamalizie kazi iliyopo mbele yao wakiwa kama mamlaka ya ajira ya menejimenti hiyo, na wao wakiwa ndiyo waliotoa maelekezo ya uchunguzi huo.
Raia Mwema ina taarifa za uhakika kuhusu kuwapo kwa uhusiano usioridhisha kati ya uongozi mpya wa wizara hiyo chini ya Waziri Prof. Muhongo na bodi iliyopo ya shirika hilo. Baadhi ya wajumbe wa bodi hiyo wanadai kutopewa ushirikiano na waziri huyo.
"Mara baada ya uteuzi wake, Mwenyekiti alienda wizarani kwa ajili ya kumpongeza, lakini waziri alipiga chenga, wakaenda na Katibu Mkuu wake pale TANESCO na kuzungumza na wafanyakazi, wakakusanya madai yao zikiwamo tuhuma dhidi ya Mkurugenzi Mhando, ndipo akatuita Dodoma na kutukabidhi tuzifanyie kazi," anasema mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo.
Hadi tunaenda mitamboni, bodi hiyo ilikuwa bado kutoa taarifa hiyo ya uchunguzi, na juhudi za kumpata Waziri Profesa Sospeter Muhongo na Naibu wake, Steven Masele hazikuzaa matunda.
- Bodi ya Jenerali Mbona yatishia kujiuzulu
- Bandari nako si shwari, mengine yafichuka
WAKATI Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Lawrence Mafuru, akisafishwa kutokana na uchunguzi uliofanyika katika benki hiyo kwa ridhaa ya Bodi ya Wakurugenzi, aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, William Mhando, ambaye naye alisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi, mambo yanazidi kumuelemea, Raia Mwema, limebaini.
Mhando na wenzake walisimamishwa kazi TANESCO ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zikiwamo za matumizi mabaya ya madaraka na hususan kuwapo kwa mgongano wa kimaslahi, uchunguzi ulioendeshwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambao umebaini mgongano wa maslahi kwa kiongozi huyo.
Kwa mujibu wa taarifa za uchunguzi huo uliodumu kwa miezi kadhaa sasa, Mhando amebainika kuwa na mgongano wa kimaslahi na Kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd.
Kwa mujibu wa nyaraka zilizopo, Mhando ameingia mkataba na MC Donald Live Line Technology Ltd, akipewa majukumu maalumu ndani ya kampuni hiyo. Mhando alipewa jukumu la kuitafutia miradi kampuni hiyo ndani ya shirika alilokuwa akiliongoza, TANESCO.
Tayari ripoti hiyo ya uchunguzi kutoka kwa CAG imekabidhiwa katika mamlaka serikalini, ikiwa ni pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, chini ya Mwenyekiti wake, Jenerali (mstaafu) Robert Mbona na Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka serikalini, taarifa ya uchunguzi huo inamuweka katika mazingira magumu zaidi Mhando ambaye, pamoja na baadhi ya wasaidizi wake, aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma za Shirika, Robert Shemhilu, Ofisa Mkuu wa Fedha, Lusekelo Kassanga na Meneja Mwandamizi katika Ununuzi, Harun Mattambo, wote walisimamishwa kazi kupisha uchunguzi huo.
Baada ya Mhando na wenzake kusimamishwa kazi aliyekuwa Mkurugenzi wa Masoko na Usambazaji, Felschami Mramba, alikaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa TANESCO.
Pamoja na kashfa hiyo ya MC Donald Live Line Technology Ltd uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwapo pia kwa kashfa nyingine ambayo pia inaonyesha matumizi mabaya ya madaraka, ikiwa nayo inathibitishwa na nyaraka, ikihusu kujipa kazi za shirika analoliongoza hivyo kujiingiza katika mgongano wa kimaslahi.
Kashfa hiyo ni ile iliyowahi kuandikwa na gazeti hili iliyohusu kuipa zabuni kampuni iliyohusishwa na mkewe.
Kwa mujibu wa nyaraka ambazo Raia Mwema imeziona kuhusiana na kashfa hizo, Mhando aliingia mkataba na Kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd akiwa na jukumu la ndani ya kampuni hiyo la utafutaji miradi ikiwamo ile ya TANESCO.
Kutokana na kuwapo kwa taarifa hizo zinazothibitishwa na nyaraka mbalimbali, mwandishi wetu aliwasiliana na Mhando ili kwanza kujua kama anaitambua kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd na kama anahusika nayo kwa kukabidhiwa jukumu la kuitafutia miradi kampuni hiyo binafsi.
Mhando alimjibu mwandishi wetu akisema; "Haya masuala yote ambayo unaniuliza yapo chini ya uchunguzi, kwa hiyo mimi siwezi kuyazungumzia kwa sababu yanachunguzwa."
Bodi ya TANESCO njia panda
Hata hivyo, huku ikiwa na taarifa hiyo tayari kwa kuipitia, Bodi ya TANESCO imejikuta ikiwa njia panda kwa baadhi ya wajumbe wake kuamua kutishia kujiuzulu; licha ya kutakiwa kukamilisha jukumu la kuhitimisha kazi ya kupitia taarifa hiyo ya uchunguzi dhidi ya menejimenti ya TANESCO iliyosimamishwa.
Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya bodi hiyo vinabainisha kuwa, mtafaruku huo umejitokeza kutokana na kauli iliyotolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle ambaye alinukuliwa na gazeti moja la kila siku akitangaza kusudio la uongozi wa wizara hiyo kuivunja Bodi ya TANESCO kutokana na kile alichokieleza dhamira ya uongozi wao, pale wizarani, kuhakikisha kwamba mgawo wa umeme hautokei tena.
Pamoja na kumaliza mgawo wa umeme, Maselle alinukuliwa akisema kwamba kukamilika kwa bomba la gesi hapo Machi mwakani na kuanza kutumika kwa gesi hiyo viwandani na majumbani kunahitaji bodi imara yenye weledi na uzalendo kwa nchi.
Kauli hiyo imechukuliwa kwa uzito na wajumbe wa bodi ya sasa kwamba uongozi wa wizara umewahukumu wao kuwa hawana weledi na si wazalendo kwa nchi yao, hivyo wakiamini lengo la kauli hiyo ni kuwadhalilisha.
"Yupi ni mzalendo kati ya Maselle aliyepewa unaibu waziri hivi karibuni na Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali Mboma aliyepigania nchi hii?" anahoji mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo na kuongeza:
"Hawa vijana wasilewe madaraka, huwezi kijana umepata unaibu waziri juzi tu unamwambia Jenerali Mboma eti hana uzalendo, hana weledi, hii si sawa. Ni kukosa adabu, huu si utamaduni wetu Waafrika."
Taarifa za ndani za bodi hiyo zinabainisha kuwa Jenerali Mboma, ambaye ni mwenyekiti wa bodi hiyo, pamoja na wajumbe wake wamekasirishwa na kauli ya Naibu Waziri huyo, na waliamua kujiuzulu siku ile ile taarifa za kauli ya Maselle zilipochapishwa gazetini.
Hata hivyo, kuwasilishwa kwa taarifa ya CAG ya uchunguzi kuhusu ufisadi ndani ya menejimenti ya shirika hilo uliiweka bodi hiyo njia panda baada ya kushauriwa kutochukua uamuzi wa kujiuzulu, na badala yake wamalizie kazi iliyopo mbele yao wakiwa kama mamlaka ya ajira ya menejimenti hiyo, na wao wakiwa ndiyo waliotoa maelekezo ya uchunguzi huo.
Raia Mwema ina taarifa za uhakika kuhusu kuwapo kwa uhusiano usioridhisha kati ya uongozi mpya wa wizara hiyo chini ya Waziri Prof. Muhongo na bodi iliyopo ya shirika hilo. Baadhi ya wajumbe wa bodi hiyo wanadai kutopewa ushirikiano na waziri huyo.
"Mara baada ya uteuzi wake, Mwenyekiti alienda wizarani kwa ajili ya kumpongeza, lakini waziri alipiga chenga, wakaenda na Katibu Mkuu wake pale TANESCO na kuzungumza na wafanyakazi, wakakusanya madai yao zikiwamo tuhuma dhidi ya Mkurugenzi Mhando, ndipo akatuita Dodoma na kutukabidhi tuzifanyie kazi," anasema mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo.
Hadi tunaenda mitamboni, bodi hiyo ilikuwa bado kutoa taarifa hiyo ya uchunguzi, na juhudi za kumpata Waziri Profesa Sospeter Muhongo na Naibu wake, Steven Masele hazikuzaa matunda.