Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Hebu tuwekeni siasa ya vyama kando tuilijadili hili swala kwa undani. Huyu mwanamke Mange Kimambi amekuwa akikurupuka na shutuma lukuki. Amesema mengi sana kuhusiana na kifo cha kanumba. Kawashambulia viongozi wa CHADEMA, Kasema hajawahi kumuona kanumba wala kuangalia movies zake. Yaani amesema mengi sana ya kichochezi
Mange Kimambi lazima ashirikiane na serikali kuhusiana na kifo cha Kanumba. Hii ni kwa sababu, siku Kanumba alipofariki, usiku huo huo aliandika kwenye blog yake kwamba, Mpenzi wa Kanumba Lulu ndiye aliyempa Kanumba sumu. Jana karudi na tafsiri nyingine akidai kwamba, Lulu hakuuwa kwa kusudia bali alitumiwa na Ray kutokana na upelelezi wake akishirikiana na Hoysterbay Police. Tunaiomba serikali hasa polisi na mahakam zishirikiane naye huyu mwanamke, kwa maana ameshaingilia uchunguzi wao.
Ameingilia hadi mahakama kwa kutoa hukumu kwamba kuna watu,mtu (Ray) waliomtumia Lulu kumuua Kanumba kabla hata mahakama haijaanza kesi. Ina maana kwamba, anawafahamu au anafahamu mengi ambayo sisi hatuyajui na hata vyombo vya dola haviyajui. Kwa hiyo kama serikali ipo kweli, huyu mwanammke asiachwe huru hadi uchunguzi ukamilike. Ni maoni yangu
Mange Kimambi lazima ashirikiane na serikali kuhusiana na kifo cha Kanumba. Hii ni kwa sababu, siku Kanumba alipofariki, usiku huo huo aliandika kwenye blog yake kwamba, Mpenzi wa Kanumba Lulu ndiye aliyempa Kanumba sumu. Jana karudi na tafsiri nyingine akidai kwamba, Lulu hakuuwa kwa kusudia bali alitumiwa na Ray kutokana na upelelezi wake akishirikiana na Hoysterbay Police. Tunaiomba serikali hasa polisi na mahakam zishirikiane naye huyu mwanamke, kwa maana ameshaingilia uchunguzi wao.
Ameingilia hadi mahakama kwa kutoa hukumu kwamba kuna watu,mtu (Ray) waliomtumia Lulu kumuua Kanumba kabla hata mahakama haijaanza kesi. Ina maana kwamba, anawafahamu au anafahamu mengi ambayo sisi hatuyajui na hata vyombo vya dola haviyajui. Kwa hiyo kama serikali ipo kweli, huyu mwanammke asiachwe huru hadi uchunguzi ukamilike. Ni maoni yangu