uchungu wa uzazi bwana balaaa..!

david mkwizu

Member
Jul 31, 2011
29
9
jamaa mmoja alienda kumpeleka mke wake hospitalini ili kujifungua...! kwakweli mama alikua kwenye hali mbaya sana ya uchungu.... walipofika dr akawaambia ametengeneza mashine ambayo inaweza kuhamisha uchungu wa mama kwenda kwa baba.. yule jamaa akakubali kuhamishiwa uchungu.. dr akamwambia kwa wanaume wanaoanza kuitumia mashine hii wanaanza kuhamishiwa uchungu kwa asilimia kumi tu ya uchungu wa mama..! jamaa baada ya kusisitiza sana ahamishiwe uchungu kutokana na upendo aliokua nao kwa mkewe basi dr akahamisha 10%

akamuuliza jamaa kua anajisikiaje..? jamaa akasema anajisikia safi tu.. na jamaa akamwambia dr kwakua ninajisikia vizuri tu hebu ongeza tena kwa sababu kwa kweli ninaona mke wangu anapata nafuu kidogo.. dr akaongeza mpaka 50%.. na baada ya kumuuliza jamaa kua anajisikiaje..! jamaa alionekana bado yupo safi tu..! jamaa akamwambia dr hebu ongeza mpaka asilimia mia moja kabisa ili mama asipate shida ninakusihi sana dr..! dr akaongeza mpaka 100%...

yule mama akajifungua bila matatizo kabisa... waliporudi nyumbani wakakuta mlinzi getini yuko hoi karibu na kufa..!
 
Sio mbaya saana! Namwachia mlinz mke wa bure kwan mapenz kwa uyo mke yapo kwa mlinz sio mm
 
kila mla vya wenzake na vyake huliwa, wewe hujawahi kula vya wenzio?????
 
Nilidhani baada ya mama kujifungua uchungu uliisha? Sasa mlinzi inawezekana alikuwa amehamishiwa uchungu toka kwa mama mtarajiwa mwingine pia. Milinzi noma.Anyway it is funny.
 
Back
Top Bottom