TAASISI ya kimataifa inayojishughulisha na tafiti za Utawala Bora, Jopa ( JPF), imesema taifa litakumbwa na anguko la uchumi la asilimia tano katika mwaka huu wa fedha kutokana na tatizo la umeme nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa JPF, Praygod Mmasi, alieleza hayo hivi karibuni jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumzia utafiti waliofanya katika kipindi cha Januari hadi Machi 31, mwaka huu.
Alisema hali hiyo inatokana na shughuli zote za uzalishaji viwandani na zile za kijamii kuathirika kwa zaidi ya asilimia 75 kutokana na mgawo wa umeme.
Aidha, Mmasi alisema mabadiliko ya hali ya hewa na kushuka kwa thamani ya fedha ya Tanzania kwa zaidi ya asilimia tatu, ni miongoni mwa sababu ambazo zimesababisha mfumuko wa bei wa bidhaa zote za viwandani na vyakula.
Mmasi alisema wakati uchumi wa nchi ukiwa katika hali mbaya kwa kiwango hicho, serikali imekuwa ikitumia zaidi ya sh bilioni saba za bajeti yote ya nchi kwa matumizi ya kawaida ya serikali.
Aliongeza kuwa ni kiasi kidogo cha sh bilioni nne tu kimekuwa kikielekezwa katika shughuli za maendeleo.
Alisema kiini cha matatizo yote ya uchumi na utolewaji wa huduma za kijamii uliopo nchini leo ni matokeo ya anguko la utawala bora Tanzania na kushindwa kuwajibika kwa mamlaka ya wabunge
Source: Tanzania Daima.
Kuna siku za nyuma niliwahi kusema kwamba uchumi wa Tanzania ukuaji wake utakua kwa asilimia 4.5% mwaka huu na waziri wetu wa mapesa akasema uchumi unategemewa kukuwa kwa 7.8%. Je mheshimiwa waziri prediction zake za kukua kwa uchumi sasa ziko asilimia ngapi?
Mkurugenzi Mtendaji wa JPF, Praygod Mmasi, alieleza hayo hivi karibuni jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumzia utafiti waliofanya katika kipindi cha Januari hadi Machi 31, mwaka huu.
Alisema hali hiyo inatokana na shughuli zote za uzalishaji viwandani na zile za kijamii kuathirika kwa zaidi ya asilimia 75 kutokana na mgawo wa umeme.
Aidha, Mmasi alisema mabadiliko ya hali ya hewa na kushuka kwa thamani ya fedha ya Tanzania kwa zaidi ya asilimia tatu, ni miongoni mwa sababu ambazo zimesababisha mfumuko wa bei wa bidhaa zote za viwandani na vyakula.
Mmasi alisema wakati uchumi wa nchi ukiwa katika hali mbaya kwa kiwango hicho, serikali imekuwa ikitumia zaidi ya sh bilioni saba za bajeti yote ya nchi kwa matumizi ya kawaida ya serikali.
Aliongeza kuwa ni kiasi kidogo cha sh bilioni nne tu kimekuwa kikielekezwa katika shughuli za maendeleo.
Alisema kiini cha matatizo yote ya uchumi na utolewaji wa huduma za kijamii uliopo nchini leo ni matokeo ya anguko la utawala bora Tanzania na kushindwa kuwajibika kwa mamlaka ya wabunge
Source: Tanzania Daima.
Kuna siku za nyuma niliwahi kusema kwamba uchumi wa Tanzania ukuaji wake utakua kwa asilimia 4.5% mwaka huu na waziri wetu wa mapesa akasema uchumi unategemewa kukuwa kwa 7.8%. Je mheshimiwa waziri prediction zake za kukua kwa uchumi sasa ziko asilimia ngapi?