BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Friday, 18 September 2009
Na Mercy James
Majira
RAIS Jakaya Kikwete amesisitiza juhudi za pamoja za serikali yake kuvutia wawekezaji na kubainisha kuwa hakuna uchumi wa nchi yoyote duniani unaoweza kukua kwa uwekezaji wa serikali peke yake bila wawekezaji binafsi.
Aliyasema hayo jana Ikulu Dar es Salaam alipokutana na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali, Taasisi muhimu zinazohusu uwekezaji, wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Phillemon Luhanjo, katika mkutano wa kutathimini hali na kasi ya uwekezaji katika uchumi wa Tanzania.
Aliwataka maofisa wa Serikali yake kuchukua maamuzi ya haraka kutimiza mahitaji ya wawekezaji mara zinapojitokeza nafasi za wawekezaji kutaka kuja nchini.
"Uchumi huu wa kwetu hautakua bila wawekezaji, nchi yetu haiwezi kuendeshwa na uchumi wa serikali na hakuna uchumi wa nchi yoyote unaeza kukua kwa kutegemea uwekezaji wa umma pasipo kushirikisha wawekezaji binafsi,"alisema.
Aliwataka maofisa waandamizi wa serikali pamoja na taasisi za serikali kuchukua hatua za makusudi kuwezesha na siyo kuzuia uwekezaji katika uchumi wa nchi.
"Lazima tuwe na haraka katika kuvuta wawekezaji badala ya kuwa wazuiaji wa uwekezaji katika nchi yetu, nchi yetu inayo bahati kubwa ya Kijiografia na lazima tutumie fursa hiyo kuvuta watu kuja na kuwekeza katika uchumi wetu,"alisema .
Mkutano huo ulihudhuriwa makatibu wakuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Miundombinu, Wizara ya Sheria na Katiba, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Biashara, Viwanda, Masoko, Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Taasisi zilizowakilishwa ni pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
Na Mercy James
Majira
RAIS Jakaya Kikwete amesisitiza juhudi za pamoja za serikali yake kuvutia wawekezaji na kubainisha kuwa hakuna uchumi wa nchi yoyote duniani unaoweza kukua kwa uwekezaji wa serikali peke yake bila wawekezaji binafsi.
Aliyasema hayo jana Ikulu Dar es Salaam alipokutana na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali, Taasisi muhimu zinazohusu uwekezaji, wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Phillemon Luhanjo, katika mkutano wa kutathimini hali na kasi ya uwekezaji katika uchumi wa Tanzania.
Aliwataka maofisa wa Serikali yake kuchukua maamuzi ya haraka kutimiza mahitaji ya wawekezaji mara zinapojitokeza nafasi za wawekezaji kutaka kuja nchini.
"Uchumi huu wa kwetu hautakua bila wawekezaji, nchi yetu haiwezi kuendeshwa na uchumi wa serikali na hakuna uchumi wa nchi yoyote unaeza kukua kwa kutegemea uwekezaji wa umma pasipo kushirikisha wawekezaji binafsi,"alisema.
Aliwataka maofisa waandamizi wa serikali pamoja na taasisi za serikali kuchukua hatua za makusudi kuwezesha na siyo kuzuia uwekezaji katika uchumi wa nchi.
"Lazima tuwe na haraka katika kuvuta wawekezaji badala ya kuwa wazuiaji wa uwekezaji katika nchi yetu, nchi yetu inayo bahati kubwa ya Kijiografia na lazima tutumie fursa hiyo kuvuta watu kuja na kuwekeza katika uchumi wetu,"alisema .
Mkutano huo ulihudhuriwa makatibu wakuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Miundombinu, Wizara ya Sheria na Katiba, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Biashara, Viwanda, Masoko, Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Taasisi zilizowakilishwa ni pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
Last edited: