Sungurampole
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 984
- 205
JK anapolinganisha Uchumi wa nchi EAC
1. Mbona anakwepa kuelezea kwanini Rwanda wanaofanya vizuri?
2. Anasema sisi ndiyo tunasupply wenzetu na chakula. Iweje basi anayemlisha mwenzake awe na hali mbaya hata kuliko anayelishwa? Au hatuwauzii tunawapa bure?
3. Anasema ili kupambana na kushuka kwa dhamani ya shilingi tunadhibiti fedha za kigeni kweli hiyo? Mbona tunaona uholela usiyo kifani- Bureau de change hadi vichochoroni huku ndiko kudhibiti fedha za kigeni?hivi hizi bureau zinalenga kujibu hitaji gani la mtanzania wa kawaida zaidi ya kuvuruga suppy -demand ya fedha za kigeni - kichekesho ukitaka kununua $ 500 kulipia masomo nje kupitia benki unaulizwa maswali lukuki, japo nchi hiyohiyo ukitaka $10,000 za kwenda kutanua Kempsiki serengeti unapata bureau ndani ya dakika.
4. Unasema tunaathiriwa na kupanda kwa kwa mafuta bei ya mafuta? Sawa mbona hutuambii pia tunaathirikaje na kupanda kwa bei ya dhahabu ambayo mauzo ya Tz yanaongezeka kila kukicha? Hivi haya ndiyo yanayofanya shilingi iporomoke au? Hiki kiini macho mbona huwaelezi wazee?
5. Unazungumzia waziri kukuta sukari yetu supermarket za nchi jirani -ina maana tumeingiza forex nyingi au?
Kuhusu mchakato wa katiba mpya
Hukuhitaji kuanza na kuorodhesha katiba za nyuma kwani ukiwa safarini majuu huku wataalamu walikwisha waeleza kwa ufasaha mkubwa watanzania wote (siyo wazee wa CCM tu) kuhusu hilo. Uchambuzi wao ulikuwa mpana hata kufikia kutaja washiriki walivyopatikana na tafsiri ya kilichopatikana, uhalali wake kwa maana ya kisheria na hata legitimacy yake. Waliweza kufafanua kwa nini leo tunachokitaka ni TOFAUTI. Hivi umefuatiliwa mijadala iliyoendeshwa hapa bara na visiwani kuhusu mchakato huu?
Wewe umeeleza walivyofanya wengine na kutumia hii kuhalalisha na wewe kuiga (hili la kujilinganisha siku zote linakuangusha, unapenda sana- Mzee wa 'Business as Usual -BAU').
Nakumbuka ukiwahutubia hao wazee uliwahi kusema kuwa Tz ilimshinda hata Nyerere, Mwinyi na Mkapa. Swali ni je, kwa hiyo na wewe tuendelee kukuacha wakati tunaona wazi unashindwa? Tusitake kurebisha ili aje anayejiamini kuweza na sio anatetea kushindwa kwake kwa kuwasema waliopita?
ULICHOSAHAU KIKUBWA KABISA NI KUWA SAFARI HII SISI TUNATAKA KATIBA YA WATANZANIA (WANANCHI)
Ungelielewa hili tu ungejua ili upate hii katiba ya tofauti wewe unatakiwa utofautiane na waliotangulia.
Au unaamini katika maajabu kuwa utachemsha upate omlet?
1. Mbona anakwepa kuelezea kwanini Rwanda wanaofanya vizuri?
2. Anasema sisi ndiyo tunasupply wenzetu na chakula. Iweje basi anayemlisha mwenzake awe na hali mbaya hata kuliko anayelishwa? Au hatuwauzii tunawapa bure?
3. Anasema ili kupambana na kushuka kwa dhamani ya shilingi tunadhibiti fedha za kigeni kweli hiyo? Mbona tunaona uholela usiyo kifani- Bureau de change hadi vichochoroni huku ndiko kudhibiti fedha za kigeni?hivi hizi bureau zinalenga kujibu hitaji gani la mtanzania wa kawaida zaidi ya kuvuruga suppy -demand ya fedha za kigeni - kichekesho ukitaka kununua $ 500 kulipia masomo nje kupitia benki unaulizwa maswali lukuki, japo nchi hiyohiyo ukitaka $10,000 za kwenda kutanua Kempsiki serengeti unapata bureau ndani ya dakika.
4. Unasema tunaathiriwa na kupanda kwa kwa mafuta bei ya mafuta? Sawa mbona hutuambii pia tunaathirikaje na kupanda kwa bei ya dhahabu ambayo mauzo ya Tz yanaongezeka kila kukicha? Hivi haya ndiyo yanayofanya shilingi iporomoke au? Hiki kiini macho mbona huwaelezi wazee?
5. Unazungumzia waziri kukuta sukari yetu supermarket za nchi jirani -ina maana tumeingiza forex nyingi au?
Kuhusu mchakato wa katiba mpya
Hukuhitaji kuanza na kuorodhesha katiba za nyuma kwani ukiwa safarini majuu huku wataalamu walikwisha waeleza kwa ufasaha mkubwa watanzania wote (siyo wazee wa CCM tu) kuhusu hilo. Uchambuzi wao ulikuwa mpana hata kufikia kutaja washiriki walivyopatikana na tafsiri ya kilichopatikana, uhalali wake kwa maana ya kisheria na hata legitimacy yake. Waliweza kufafanua kwa nini leo tunachokitaka ni TOFAUTI. Hivi umefuatiliwa mijadala iliyoendeshwa hapa bara na visiwani kuhusu mchakato huu?
Wewe umeeleza walivyofanya wengine na kutumia hii kuhalalisha na wewe kuiga (hili la kujilinganisha siku zote linakuangusha, unapenda sana- Mzee wa 'Business as Usual -BAU').
Nakumbuka ukiwahutubia hao wazee uliwahi kusema kuwa Tz ilimshinda hata Nyerere, Mwinyi na Mkapa. Swali ni je, kwa hiyo na wewe tuendelee kukuacha wakati tunaona wazi unashindwa? Tusitake kurebisha ili aje anayejiamini kuweza na sio anatetea kushindwa kwake kwa kuwasema waliopita?
ULICHOSAHAU KIKUBWA KABISA NI KUWA SAFARI HII SISI TUNATAKA KATIBA YA WATANZANIA (WANANCHI)
Ungelielewa hili tu ungejua ili upate hii katiba ya tofauti wewe unatakiwa utofautiane na waliotangulia.
Au unaamini katika maajabu kuwa utachemsha upate omlet?