Ni zipi sababu za msingi zinazoifanya serikali iendelee kuwalea wachakachaji wa pembejeo za kilimo? Mchakachuaji wa pembejeo za kilimo kwangu mimi ni mhujumu uchumi namba moja na anastahili kutupwa gerezani mara moja anapobainika na si kunyang'anjwa leseni ambayo anaweza kuomba na kupata nyingine hata kwa kupitia kwa rafiki yake. Kimsingi kumyanyang'a leseni mhujumu uchumi sio adhabu ni upuuzi mtupu. Nisaidieni kiwazo ndugu zangu na hapohapo muishauri serikali yetu namna bora ya kuwashughulikia wahujumu uchumi kupitia pembejeo za kilimo ambao wengi wao walituhujumu msimu ulipita wanafahamika.