Uchakachuaji Mafuta Unatumaliza Na Serikali Haifanyi Kitu

Lyambaa

Member
Dec 17, 2007
17
3
Suala la kuchakachua mafuta ni baya sana, tena ni uuwaji. Ni simu inayotuua kwa kufanya kazi taratibu. Kwanza mafuta bei juu. Halafu yamechakachuliwa. Hii maana yake inaua magari. Sina haja kuelezea athari zake kiuchumi kwa mtu na taifa. Serikali imebaki kushangaa tu na kusema wahusika watafutwe na kuchukuliwa hatua. Soma hii habari iliyotoka kwenye gazeti la nipashe.


PHP:
Waagizaji mafuta wawaumbua wachakachuaji
Na Joseph Mwendapole 
31st March 2011
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Mafuta (Ewura)

Waagizaji wa mafuta nchini wameieleza Kamati ya Nishati na Maduni kuwa wachakachuaji wa mafuta ni watu hatari na [COLOR="red"]wamekuwa wakilindwa na vigogo serikalini wanaonufaika na uchakachuaji huo kwa kuwa wanajulikana kwa majina[/COLOR].
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na wadau hao wa mafuta wakati wa kikao cha pamoja baina yao na kamati hiyo.
Walisema watu hao wana fedha nyingi kuliko kawaida na wamekuwa wakiwatishia maisha pindi wanapowakemea kuachana na vitendo hivyo.
[COLOR="red"]Mmoja wa waagizaji wa mafuta, Zacharia Hanspope, aliieleza kamati hiyo kuwa watu hao wanamtandao mkubwa ambao umeshindikana [/COLOR]kwa kuwa inaonekana wamekuwa wakiwahonga baadhi ya viongozi ili waendelee na biashara hiyo haramu.
Alisema wahusika wakuu wa vitendo hivyo ni madereva wa magari ya mafuta ambao wamekuwa wakilagaiwa na watu kuchakachua mafuta hayo na kuwalinda.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Mafuta (Ewura) Haruna Masebu, alikiri kuwa hilo ni tatizo kubwa ingawa wamekuwa wakijitahidi kukabiliana nalo.
“Kweli kufanya kazi kwenye sekta ya mafuta kuna changamoto nyingi na ni hatari sana, lakini pamoja na hayo tunaendelea kupambana, tumeshawaadhibu watu wengi waliokutwa na hatia na kila anayemjua mhusika wa vitendo hivi atuambie sisi hatutaacha kumwadhibu kwa kuwa wengi tumeshawadhibu hatumwogopi mtu,” alisema Masebu.
[COLOR="red"]Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Januari Makamba alihoji kwanini wahusika hawachukuliwi hatua kali wakati wanajulikana.[/COLOR]Alishauri serikali iweke mkazo kuwatafuta wahusika wa vitendo hivyo kwani licha ya kuharibu magari ya watu vinalitia aibu taifa.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Kigoma Malima, alisema tatizo hilo ni kubwa na Ewura wanapaswa kufanya jitihada zaidi kukabiliana na hali hiyo na ikishindwa ipeleke orodha ya wahalifu hao serikalini.
Mbunge wa Muleba Kaskazini (CCM), Charles Mwijage, alisema kwa kuwa wadau wakubwa wa uchakachuaji wanajulikana haoni sababu kwanini wasikamatwe na kuchukuliwa hatua kali.
Alisema kuna taarifa kuwa polisi wamekuwa wakiwalinda wahusika wa vitendo hivyo kwa kuwa wamekuwa wakinufaika nao.
Makamba alisema kupanda kwa bei ya mafuta kunasababishwa na tozo ya kodi kunakofanywa na taasisi nyingi, jambo ambalo linaendelea kumuumiza mlaji.
CHANZO: NIPASHE

Sasa mambo ninayoshindwa kuelewa:
1. Hao vigogo walio serikalini, wako juu ya mawaziri? makatibu wakuu wa wizara? Juu ya waziri mkuu? Yote tisa, kumi wako juu ya sheria?
2. Wanajulikana kwa majina, kwa hiyo tuwasujudie tuombe wapungeze ukali wa uchakachuaji. Maana serikali haiwezi, sababu ndio hao hao wanaoendeleza hiyo biashara.
3. Makamba anashauri serikali iweke mkazo, nani kwenye serikali afanye hivyo? wakati ameambiwa wanajulikana wanaofanya huo mchezo.

Sasa tukisema kazi imewashinda, unajibiwa unahatarisha amani na utulivu nchini.
 
Week iliyopita nilitaka kuweka mafuta ktk kituo kimoja kinachotumia nembo ya BP jirani na tripple A.system ya kurefill gari ikareject..sasa kwa magari yasiyokuwa na system kama ile si ndo tunalishwa kerosene? Miezi sita engine haina uwezo tena imechoka inataka overhaul
 
Kansa ya taifa letu. Wachakachuaji wakuu ni vizito serikalini au katika biashara. Hawagusiki.
 
Habari hapa chini inaleta maswali zaidi.
Je Igunga kuwa kituo kikuu cha uchakachuaji kinamuhusu Mbunge wake?
Kwa nini hao Vigogo hawatajwi?
Inaonyesha Mwema, anayefagiliwa na watu si mwaminifu, mana anaongea na mtu halafu anawaarifu watuhumiwa, Kwa nini asijiuzulu?

Kipande cha habari hapo chini:

"Vituo vikuu vya uchakachuaji mafuta kwa kiwango cha kutisha hapa nchini ni Igunga (mkoani Tabora) na Gairo(Kilosa, mkoani Morogoro)," alisema Buba na kuwaacha wabunge wakiwa wameduwaa.

Wakati Buba akiendelea kufichua siri za mtandao huo na kueleza kila hatua ya itendaji wake wa kazi, mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, alisikika akisema chini chini, "wengine tumo humu humu, eee!"

Buba ambaye alionekana kuwa na dukuduku hilo kwa siku nyingi lakini alikosa jukwaa la kusemea, aliendelea kueleza kuwa ni vigumu kudhibiti tatizo hilo kwa kuwa wahusika wake ni vigogo wenye ushawishi mkubwa na ambao ni vigumu hata kutiwa mbaroni.

Kuonyesha uzito wa tatizo hilo, Buba alitoa mfano wa mkutano kati yao (Tatoa)na Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, ambao aliutumia kuwataja kwa majina vigogo hao lakini, dakika chache alipotoka nje, mmoja wao alimpigia simu na kumwambia, "sawa fitna zako nimezisikia."

Buba ambaye maelezo yake yaliamsha hisia kali kwa wabunge, alisema kitendo hicho kilimshtua lakini, kwa kuwa ni jasiri hakuogopa.

Aliongeza kwamba, taarifa hizi walizipeleka hadi Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) lakini hatua zinazochukuliwa ni ndogo.

"Tulisema sana, sasa ndiyo yakaja matukio kama ya Rwanda na gari la mheshimiwa Rais kujazwa mafuta machafu kule Moshi. Baada ya tukio mheshimiwa mmoja akatuita katika ofisi za Wizara ya Nishati na Madini na kutuambia; “ninyi mnasema sana, hebu tuelezeni, wabunge wanasubiri majibu bungeni."

Akielezea majibu walitoa, Buba alisema: "Sisi tulimwambia hivi, tuseme nini tena wakati tayari tulisema sana na kutoa hadi majina lakini, hayakufanyiwa kazi. Sasa leo gari la mheshimiwa Rais limejazwa mafuta machafu ndiyo mnastuka? Waheshimiwa hili ni tatizo kubwa la kitaifa.

Source: Mwananchi (today)
 
Nchi inaingia hasara ya bilioni 25-35 kwa muezi ikiwa ni pamoja na kuharibu magari ya watu. Imebainika kuwa huo ni mtandao mkubwa wa mafisadi ambao umeenea nchi nzima kwa sasa. Pamoja na polisi na vyombo vya serikali kuelezwa na wahusika juu ya mtandao huo na hata majina ya wahusika, hatua zozote zimeshindwa kuchukuliwa kwa kuwa wanaohusika ni 'vigogo na wenye ushawishi mkubwa serikalini'. Akitoa maelezo kwenye kamati ya bunge ya nishati na madini, mzee Buba
kwa kuonyesha uzito wa tatizo hilo,

"alitoa mfano wa mkutano kati yao (Tatoa)na Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, ambao aliutumia kuwataja kwa majina vigogo hao lakini, dakika chache alipotoka nje, mmoja wao alimpigia simu na kumwambia, "sawa fitna zako nimezisikia."....

Vituo vikuu vya uchakachuaji mafuta kwa kiwango cha kutisha hapa nchini ni Igunga (mkoani Tabora) na Gairo(Kilosa, mkoani Morogoro)," alisema Buba na kuwaacha wabunge wakiwa wameduwaa".

soma zaidi hapa: Vigogo watajwa mtandao wa uchakachuaji mafuta

my take:
Kila sehemu palipo na mtandao wa kutisha wa ufisadi wa mabilioni ya fedha za kitanzania-fisadi rostam aziz yupo!!! imefika wakati akamatwe na mtandao wao kwa sheria za uhujumu uchumi wa nchi kulinusuru taifa, vinginevyo... tunatwanga maji kwenye kinu!!!
 
Hawa watu hawana huruma hata kidogo na umaskini wa watanzania. Sioni namana tutakavyoondoa umaskini na watu hao wangalipo. Dawa iliyopo lazima watu wasacrifice kuwaondoa kwa gharama yeyote ile. kwa mfumo uliopo bado wataendelea kupeta. Usalama wa taifa mko wapi mtunusuru?
 
Vigogo watajwa mtandao wa uchakachuaji mafuta

Ramadhan Semtawa na
Patricia Kimelemeta

SAKATA la uchakachuaji mafuta jana lilitikisa kikao cha Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na kusababisha kikao hicho kuunda kamati ndogo ya uchunguzi baada ya kuelezwa kuwa vigogo ndio wanaounda mtandao huo.

Mjadala huo ulianzia katika Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, ambako Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Wasafirishaji Mizigo (Tatoa), Fulgance Buba, alieleza kwa undani ukubwa wa tatizo hilo na kutaja maeneo yanakoendeshwa biashara hiyo haramu.

"Vituo vikuu vya uchakachuaji mafuta kwa kiwango cha kutisha hapa nchini ni Igunga (mkoani Tabora) na Gairo(Kilosa, mkoani Morogoro)," alisema Buba na kuwaacha wabunge wakiwa wameduwaa.

Wakati Buba akiendelea kufichua siri za mtandao huo na kueleza kila hatua ya itendaji wake wa kazi, mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, alisikika akisema chini chini, "wengine tumo humu humu, eee!"

Buba ambaye alionekana kuwa na dukuduku hilo kwa siku nyingi lakini alikosa jukwaa la kusemea, aliendelea kueleza kuwa ni vigumu kudhibiti tatizo hilo kwa kuwa wahusika wake ni vigogo wenye ushawishi mkubwa na ambao ni vigumu hata kutiwa mbaroni.

Kuonyesha uzito wa tatizo hilo, Buba alitoa mfano wa mkutano kati yao (Tatoa)na Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, ambao aliutumia kuwataja kwa majina vigogo hao lakini, dakika chache alipotoka nje, mmoja wao alimpigia simu na kumwambia, "sawa fitna zako nimezisikia."

Buba ambaye maelezo yake yaliamsha hisia kali kwa wabunge, alisema kitendo hicho kilimshtua lakini, kwa kuwa ni jasiri hakuogopa.

Aliongeza kwamba, taarifa hizi walizipeleka hadi Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) lakini hatua zinazochukuliwa ni ndogo.

"Tulisema sana, sasa ndiyo yakaja matukio kama ya Rwanda na gari la mheshimiwa Rais kujazwa mafuta machafu kule Moshi. Baada ya tukio mheshimiwa mmoja akatuita katika ofisi za Wizara ya Nishati na Madini na kutuambia; “ninyi mnasema sana, hebu tuelezeni, wabunge wanasubiri majibu bungeni."

Akielezea majibu walitoa, Buba alisema: "Sisi tulimwambia hivi, tuseme nini tena wakati tayari tulisema sana na kutoa hadi majina lakini, hayakufanyiwa kazi. Sasa leo gari la mheshimiwa Rais limejazwa mafuta machafu ndiyo mnastuka? Waheshimiwa hili ni tatizo kubwa la kitaifa."

Aliweka bayana kwamba, kama tatizo hilo halitafanyiwa kazi kwa haraka, mtandao huo utaua uchumi wa nchi kutokana na TRA kupoteza mabilioni ya shilingi kila mwezi.

"Hili ni janga la kitaifa kwa kweli. Mtandao ni mkubwa umesambaa nchi nzima, hivi vituo mnavyoviona njia nzima kuanzia hapa Dar es Salaam hadi Kibaha mnadhani kuna biashara kubwa, baadhi vinafanya kazi hiyo," alisisitiza.

Kutajwa kwa mtandao huo kunakuja katika kipindi ambacho Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekuwa ikirushiwa lawama na wadau kuwa ni sehemu ya tatizo kutokana na baadhi ya maafisa wake kuhusika na ulaji rushwa.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk Abdalla Kigoda, alisema tatizo ni kubwa lakini, akaitaka Tatoa waisaidie kamati kwa kufanya uchambuzi wa kina kuona hasara na faida ya kuondolewa kodi ya mafuta ya taa, kama inaweza kweli kupunguza tatizo hilo.

Baadaye mjadala huo ulihamia kwenye kamati ya Kamati ya Kudumu ya Bunge Nishati na Madini, ambako wajumbe walikubaliana kuunda kamati ndogo ya kuchunguza tatizo hilo linalodaiwa kuisababishia Serikali hasara ya Sh35 bilioni kwa mwezi.

Hata hivyo, ndani ya Kamati ya Nishati na Madini, TRA ilivutana na wadau baada ya kujaribu kutoa taarifa zilizodaiwa kuwa za uongo ambazo zilipingwa na wadau, baada ya kupunguza hasara inayotokana na tatizo la uchakachuaji mafuta hadi Sh25 bilioni kwa mwezi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Januari Makamba, alisema kamati hiyo ndogo itafanya kazi katika kipindi cha mwezi mmoja na itawasilisha ripoti yake kwa wajumbe wa kamati yake ili waweze kuijadili kabla ya Mkutano wa Bunge la Bajeti utakaonza Juni mwaka huu.

Makamba alifafanua kuwa, kamati hiyo itafanya kazi kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kuangalia chanzo cha tatizo la uchakachuaji wa mafuta kuanzia yanakotoka hadi yanapomfikia mtumiaji.

“Tatizo la uchakachuaji mafuta ni kubwa na tayari limeisababishia serikali hasara kubwa, hivyo tumepanga kuhakikisha kuwa tunalimaliza. Ili kufanikisha kazi hiyo tumeunda kamati ndogo ya kufuatilia,” alisema Makamba.
Makamba alifahamisha asilimia 10 ya ushuru wa Serikali inatokana na mafuta hayo.

Makamba alieleza kuwa kutokana na hali hiyo kamati hiyo itaanza kuangalia mfumo unaotumika wa kusafirisha mafuta, sehemu yanakohifadhiwa na maeneo mengine ili kuhakikisha kuwa wanajua chanzo cha tatizo hilo.

Kwa mujibu wa Makamba, uchakachuaji mafuta unasababisha hasara si kwa Serikali tu, bali hata watumiaji wa mafuta wakiwemo wafanyabiashara ya usafiri kutokana na kuharibikiwa magari yao na kupanda kwa gharama za uendeshaji.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, kamati iliyoundwa itaongozwa na Charles Mwijage (Muleba Kaskazini) akiwa mwenyekiti. Wajumbe wakiwa Khalfan Aeshi (Sumbawanga), Mariamu Kisangi (Viti maalum Dar es Salaam), Yusuph Nassir (Bukene), Seleman Nchambi (Kishapu) na Ally Mbarouk(Wete).
 
Mzee kila kitu kipo wazi tatizo nani(panya) wa kumfunga paka kengele!!
 
Last Tuesday, African leaders once again proved to the world that they are useless as far as serious global issues are concerned, when they failed to attend the crucial London Summit to chart the way forward in the much-anticipated post-Gaddafi Libya.
The main reason given by the African Union officials was simply characterised as “organisational.”

At least, Africa was invited to the London Summit, but the continent was not invited to other meetings. Let us look at some examples.
On March 19, moments before the start of the bombing of strategic Libyan targets, world leaders gathered in Paris to fine tune their mission against the brutal regime of Colonel Muammar Gaddafi. Africa was absent.

When the United Nations Security Council (UNSC) passed Resolution 1973, on March 17, three African states, which are non-permanent members of the council –Gabon, Nigeria, and South Africa –, voted for it but nobody felt their weight.

As it appeared days after the start of the military operation in Libya, at least South Africa showed that it didn’t know what it was voting for when President Jacob Zuma condemned the air raids on Libya. Gabon and Nigeria went completely silent as if somebody had coerced them to support the resolution.

On February 26, all the African members of the United Nations supported the Security Council’s Resolution 1970 to impose sanctions against the Libyan authorities. The sanctions, included an arms embargo, freezing of assets owned by individual members of the regime, and referring the Libyan case to the International Criminal Court (ICC).

No single African country had the guts to defend Col Gaddafi. No African country came out to condemn Col Gaddafi’s violent repression of civilian protesters. So Africans remained in the middle ground.
On March 19, the same day the Paris Summit was held, the AU High Level ad hoc committee on Libya met in Nouakchott. The committee brought together leaders from Republic of Congo, Mali, Mauritania, South Africa and Uganda. Nobody around the world cared about this stuff.

On March 25, the AU convened a consultative meeting on the situation in Libya in Addis Ababa. The diplomatic gathering brought together the ad hoc committee, 15 member states of the AU Peace and Security Council, six countries neighbouring Libya, and three African members of the UNSC.

Because the AU is unconfident, it had to invite all the five permanent members of the UNSC, 12 countries from around the globe, the UN, European Union, League of Arab States, and the Organisation of Islamic Conference, turning the summit into a diplomatic rally.

The Africans in the Addis Ababa meeting agreed on a peaceful solution to the crisis, but it was too little too late as nobody around the world had the time to listen to the murderers in Tripoli who had started to push for talks after disobeying their own cease-fire plea.

Surprisingly, when an opportunity to present the AU case before the world arrived in London, the Africans couldn’t agree on how to do it.
In fact, a day before the London Summit, I had an opportunity to attend President Barack Obama’s speech at the National Defence University in Washington DC in which many regions of the world were mentioned in relation to the conflict in Libya, but Africa was not one of them.

I felt so bad when President Obama gave an example of delayed action by the international community in the Bosnia and Herzegovina conflict in 1995 but forgot to mention the international community’s inaction in the 1994 Rwandan genocide. Compared to the Bosnian conflict death toll, about 200,000, the Rwandan genocide claimed an estimated 800,000 lives. Africa is unimportant.

In Paris, 18 nations, the EU, Arab League and the UN participated, while in London, 36 nations, the EU, Nato, OIC, Arab League and the UN attended. The AU was absent.

If we can’t agree on a clear-cut issue such as uniting against the brutal regime in Tripoli, then why should the world bother about us?
We had the Rwandan genocide in the heart of our continent, and we did nothing for three months. Only Tanzania opened its doors to the fleeing Rwandans but the rest kept quiet. The same story has repeated itself several times in every corner of the continent. Even when Tunisia and Egypt were about to explode, Africa was silent.

That’s Africa, the continent that prompted The Economist to write in February 2010: “If the African Union had allowed Muammar Qaddafi, Libya’s clown of a leader, to chair the continental body for another year, as he apparently desired, the rest of the world would rightly have consigned it to the dustbin of comic diplomacy.”

Africans, we need to get serious, if we want the world to recognise us.
 
Igunga, Igunga kwanini lakini??? Yaani nadhani mwalimu anageuka kaburini akisikia Igunga na Monduli...
 
RA is everywhere ktk kila nyanja ya uchumi wa nchi....... na sasa Gairo, mwarabu mwenzie Shabiby nae anaibuka. Tanzania hii, nahisi tushanunuliwa wote nasi hatujui tu.................. Kwa hawezi uwawa huyu for the sake of more than 42mil Tanzanians?
 
Last Tuesday, African leaders once again proved to the world that they are useless as far as serious global issues are concerned, when they failed to attend the crucial London Summit to chart the way forward in the much-anticipated post-Gaddafi Libya.
The main reason given by the African Union officials was simply characterised as "organisational."

At least, Africa was invited to the London Summit, but the continent was not invited to other meetings. Let us look at some examples.
On March 19, moments before the start of the bombing of strategic Libyan targets, world leaders gathered in Paris to fine tune their mission against the brutal regime of Colonel Muammar Gaddafi. Africa was absent.

When the United Nations Security Council (UNSC) passed Resolution 1973, on March 17, three African states, which are non-permanent members of the council –Gabon, Nigeria, and South Africa –, voted for it but nobody felt their weight.

As it appeared days after the start of the military operation in Libya, at least South Africa showed that it didn't know what it was voting for when President Jacob Zuma condemned the air raids on Libya. Gabon and Nigeria went completely silent as if somebody had coerced them to support the resolution.

On February 26, all the African members of the United Nations supported the Security Council's Resolution 1970 to impose sanctions against the Libyan authorities. The sanctions, included an arms embargo, freezing of assets owned by individual members of the regime, and referring the Libyan case to the International Criminal Court (ICC).

No single African country had the guts to defend Col Gaddafi. No African country came out to condemn Col Gaddafi's violent repression of civilian protesters. So Africans remained in the middle ground.
On March 19, the same day the Paris Summit was held, the AU High Level ad hoc committee on Libya met in Nouakchott. The committee brought together leaders from Republic of Congo, Mali, Mauritania, South Africa and Uganda. Nobody around the world cared about this stuff.

On March 25, the AU convened a consultative meeting on the situation in Libya in Addis Ababa. The diplomatic gathering brought together the ad hoc committee, 15 member states of the AU Peace and Security Council, six countries neighbouring Libya, and three African members of the UNSC.

Because the AU is unconfident, it had to invite all the five permanent members of the UNSC, 12 countries from around the globe, the UN, European Union, League of Arab States, and the Organisation of Islamic Conference, turning the summit into a diplomatic rally.

The Africans in the Addis Ababa meeting agreed on a peaceful solution to the crisis, but it was too little too late as nobody around the world had the time to listen to the murderers in Tripoli who had started to push for talks after disobeying their own cease-fire plea.

Surprisingly, when an opportunity to present the AU case before the world arrived in London, the Africans couldn't agree on how to do it.
In fact, a day before the London Summit, I had an opportunity to attend President Barack Obama's speech at the National Defence University in Washington DC in which many regions of the world were mentioned in relation to the conflict in Libya, but Africa was not one of them.

I felt so bad when President Obama gave an example of delayed action by the international community in the Bosnia and Herzegovina conflict in 1995 but forgot to mention the international community's inaction in the 1994 Rwandan genocide. Compared to the Bosnian conflict death toll, about 200,000, the Rwandan genocide claimed an estimated 800,000 lives. Africa is unimportant.

In Paris, 18 nations, the EU, Arab League and the UN participated, while in London, 36 nations, the EU, Nato, OIC, Arab League and the UN attended. The AU was absent.

If we can't agree on a clear-cut issue such as uniting against the brutal regime in Tripoli, then why should the world bother about us?
We had the Rwandan genocide in the heart of our continent, and we did nothing for three months. Only Tanzania opened its doors to the fleeing Rwandans but the rest kept quiet. The same story has repeated itself several times in every corner of the continent. Even when Tunisia and Egypt were about to explode, Africa was silent.

That's Africa, the continent that prompted The Economist to write in February 2010: "If the African Union had allowed Muammar Qaddafi, Libya's clown of a leader, to chair the continental body for another year, as he apparently desired, the rest of the world would rightly have consigned it to the dustbin of comic diplomacy."

Africans, we need to get serious, if we want the world to recognise us.

Gadhaffi bribes a lot of African leaders; he was also part of leaders wanted to pay Mugabe out of his presidency now fire is on him... GREADY
 
Si hata gari ya mkulu "dk' ilizimika kwa mafuta ya kuchakachuliwa.Tuwe tu wapole labda nature itaamua,serikali ilishashindwa/fumbia macho.
 
RA is everywhere ktk kila nyanja ya uchumi wa nchi....... na sasa Gairo, mwarabu mwenzie Shabiby nae anaibuka. Tanzania hii, nahisi tushanunuliwa wote nasi hatujui tu.................. Kwa hawezi uwawa huyu for the sake of more than 42mil Tanzanians?
Nchi hii hatuna viongozi kabisa. Kwa nini lakini wote wako kimya?
 
Uchakachuaji hauwezi kwisha mpaka CCM itakapo toka madarakani. Wachakachaji wote ni wafadhili wa CCM amini usiamini ndivyo ilivyo.
 
Tuwaache waheshimiwa wafanye kazi yao.Kwa uchache wameweza kutajana Mungu awape na awazidishie moyo huyo amen.
 
hivi wana jf mnajua hata tembo Wetu wanauliwa na hawa waheshimiwa?magari ya stk ndiyo yanabeba nyara hizo kwa hawa watu wanaojiita watanzania wenye asili ya arab,asia
 
hivi wana jf mnajua hata tembo Wetu wanauliwa na hawa waheshimiwa?magari ya stk ndiyo yanabeba nyara hizo kwa hawa watu wanaojiita watanzania wenye asili ya arab,asia

malizia na asili zingine ukiachia hapo unapotosha ukwelli, japo usemayo ni sehemu ya ukweli, nilishawahi kuonyeshwa matajiri wakubwa sana wa maeneo yanayozunguka mji wa Liwale ambao wanatajirika kwa kuuza nyara.
 
Back
Top Bottom