Uchakachuaji huu wa kanuni za Bunge uliofanywa na CCM haukubaliki popote

Watanzania

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
727
42
Kabla hata hatujasahau uchakachuaji wa kura za uraisi wa JK, kura za wabunge wa CCM, umeya wa jiji la Arusha, CCM sasa wameendeleza kufuru ya uchakachuaji wa waziwazi wa kanuni za Bunge. Ukisoma kanuni za kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni huwezi kuja na tafsiri ya kambi rasmi eti maana yake ni vyama vyote vya upinzani kama alivyosikika Anna Makinda akitamka uchakachuaji huo.

Kanuni za bunge za kuunda kambi ya upinzani lazima zijitosheleze bila ya kujipinga zenyewe. Tangu mwanzo kanuni inaanza kwa kutoa mwongozo kuwa kambi rasmi ya upinzania itaundwa pale ambapo vyama vya upinzani vimefisha asilimia 12.5 ya wabunge wote. Na kwamba chama cha upinzania hakitakuwa na haki ya kuunda kambi ya upinzania hadi kiwe na wabunge wasiopungua asilimia 12.5. Na kwamba kama vyama viwili vinawabunge waliofikia asilimia 12.5, basi kile chenye wabunge wengi ndicho kitakachochagua kiongozi wa kambi ya upinzani na naibu wake. Kanuni inaeleza wazi kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani ndiye mwenye uwezo wa kuchagua wabunge wa chama chake au kambi rasmi ya upinzania kuwa wasemaji wa wizara.

Tafsiri ya kambi rasmi ya upinzani haiwezi kuwa ya vyama vyote ikiwa kuna chama kinajitosheleza kwa wabunge kuunda kambi ya upinzani. Tafsiri hii inaweza kutumika pale tu ambapo hakuna chama cha upinzani kina wabunge wanaofikia asilimia 12.5, ambapo vyama vinalazimika kujiunga pamoja na kufikisha asilimia 12.5. Lakini kama kuna chama cha upinzani kimefikisha aslimia 12.5 na kimevipita vyama vingine kwa idadi ya wabunge ndicho chenye haki ya kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni. Si haki, na uchakachuaji huu wa makusudi wa CCM na spika wa bunge Anna Makinda haukubaliki kabisa na ni juu ya Chadema na Watanzania kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu wa kulichezea bunge la Tanzania. Kutafsiri kanuni ya bunge kwa kupotosha wakati kanuni zinajieleza wazi ni uhaini mkubwa sana.

Chadema na Watanzania tuchukue hatua za haraka sana za kisiasa, kisheria n.k. leo hii na si kesho ili kulinda na kurudisha heshima ya bunge letu.

Kanuni za Kuunda kambi ya upinzania
14.
-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwa
chini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasili za Kanuni hii
zinazofuata.
(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi
ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na
mbili na nusu ya Wabunge wote.
(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya
Wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge
wote.
(4) Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimoja
ambavyo kila kimoja kina Wabunge asilimia kumi na mbili na nusu
au zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kuliko
vingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwili
au zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimia
kumi na mbili na nusu, Wabunge wa vyama vinavyohusika
watachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibu
watakaokubaliana wenyewe.
15
.-(1) Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi
ya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi wa
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
(2) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateua
Wabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi ya
Upinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi ya
Upinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.
 
Nchi yetu sasa imefikia mahali pabaya kwa habari ya msimamo. Watu wanaweza kutafsiri kama haina kichwa. Kila mara ule uadilifu wa kusimamia maneno yao umeondoka. Endapo hali itaendelea hivi basi imani kwa serikali itakuwa imekwisha. Nawashauri viongozi wa serikali na viongozi wa vyama vya siasa kusimamia maneno yao. Je sio Spika huyu huyu ambaye alisikika akisema juu ya kanuni kuwa haiwezekani kwa kambi ya upinzani kuwa na kambi mbili. Je kama spika akianza hivi na mapema imani ya wananchi kwa bunge itakuwaje?
Ni vizuri maslahi ya Taifa yakawa juu kuliko ya vyama. Unahitajika umakini katika kuisimamia serikali. Hakuna sababu ya kuhofu kwa chama cha upinzani makini kuwa viongozi wa kamati za bunge endapo maslahi ya tiafa niyo yaliyo juu.
 
Kwa bahati mbaya mimi bado sijaelewa athari za mabadiliko ya tafsiri yaliyofanywa katika muktadha wa kanuni zenyewe. Mabadiliko hayo ya tafsiri yatainyima(yataipunguzia) CDM nini hasa yakisomwa pamoja na kanuni zenyewe?
 
Kwa bahati mbaya mimi bado sijaelewa athari za mabadiliko ya tafsiri yaliyofanywa katika muktadha wa kanuni zenyewe. Mabadiliko hayo ya tafsiri yatainyima(yataipunguzia) CDM nini hasa yakisomwa pamoja na kanuni zenyewe?

Mkuu uchakachuaji huu wa makusudi unataka kuwalazimisha Chadema bila hiari yao wawajumuishe vyama vingine kwenye kambi ya upinzani kinyume na kanuni zenyewe. Kwa kuwa Chadema wana asilimia 12.5 na imevipita vyama vingine, kanuni za bunge zinawaruhusu kuunda kambi ya upinzani bila kushirikisha vyama vingine. Lakini tafsiri ya CCM na Anna Makinda inapingana na kanuni zote.
 
Nchi yetu sasa imefikia mahali pabaya kwa habari ya msimamo. Watu wanaweza kutafsiri kama haina kichwa. Kila mara ule uadilifu wa kusimamia maneno yao umeondoka. Endapo hali itaendelea hivi basi imani kwa serikali itakuwa imekwisha. Nawashauri viongozi wa serikali na viongozi wa vyama vya siasa kusimamia maneno yao. Je sio Spika huyu huyu ambaye alisikika akisema juu ya kanuni kuwa haiwezekani kwa kambi ya upinzani kuwa na kambi mbili. Je kama spika akianza hivi na mapema imani ya wananchi kwa bunge itakuwaje?
Ni vizuri maslahi ya Taifa yakawa juu kuliko ya vyama. Unahitajika umakini katika kuisimamia serikali. Hakuna sababu ya kuhofu kwa chama cha upinzani makini kuwa viongozi wa kamati za bunge endapo maslahi ya tiafa niyo yaliyo juu.

Tatizo ni kwamba kanuni inachakachuliwa kwa manufaa ya CCM. Haikubaliki tafsiri ipingane na kanuni zingine
 
Angalizo: Hili suala la vyama lina walakini. Tanzania ya watu milioni 40, walio wanachama wa vyama vya siasa vyote hawafiki robo (yaani mil 10). Waheshimiwa wabunge wetu wajue wamechaguliwa na watanzania na watanzania wanataka maendeleo. Kwa mwendo huu nashawishika kuamini kwamba tunahitaji wagombea binafsi sasa ili kuondoa hili ombwe na jinamizi la uchama. Katiba mpya ikichelewa, misri inanukia.

Imezoeleka sasa kwamba kanuni au tafsiri zinaletwa sio kwa nia ya kusukuma maendeleo ya taifa bali kulinda aina fulani ya mfumo wanaotaka watawala....Chadema msikubali kuyumbishwa....kuna watu wenye akili timamu wanafuatilia kwa karibu...msichoke kusimama kwenye haki...siku moja watz watawakumbuka kama Mwalimu
 
Zamani nilifikiri bunge ndo mahali pekee pa kupatia haki za wananchi, i was so wrong. they are self centred sana na wako kufanya lolote kwa maslahi yao tuu, kweli duniani hakuna haki. niko so demoralized.
 
".........Ukisoma kanuni za kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni huwezi kuja na tafsiri ya kambi rasmi eti maana yake ni vyama vyote vya upinzani kama alivyosikika Anna Makinda akitamka uchakachuaji huo....."

Huyo mama hawatendei haki akina mama wengine wanaowakilishwa na jinsia yake maana ana-paint picha kwamba
1. akina mama ni watu wa kukurupuka na kutoa maamuzi wakipewa nafasi kubwa kitu macho si kweli..

2. Anatoa picha kwamba akina mama si watumakini kitu ambacho si kweli hasa ukizingatia kazi na majambozi ya Mdee...

3. Anatoa picha kwamba akina mama kazi yao kubwa ni kuwafurahisha akina baba ili wasiendelee kugombana na kusahu kwamba kazi aliyopewa ina nafasi ya kumpa uraisi kama (God Forbid) raisi wa nchi akifariki gafla...
4. Anapingana na kauli yake mwenyewe kwamba jambo ambalo halina maslahi kwa taifa halipaswi kuchukua muda wa bunge maana ni sisi tax payers tunaowalipa siku zote kwa kazi za kipuuzi kama hizi za kutafsiri kanuni na taratibu zilizopitishwa na zililokubalika na bunge la 9

5. Labda atuambie tangu lini sisi wapiga kura tuliwatuma kwenda kubadlisha kanuni na sio kutunga sheria na za kuwabana mafisadi?

Akina mama popote pale mlipo amkeni na mkemeeni kama shetani anavyokemea na akina kakobe vinginevyo mama huyo anaiwekea jinsia yenu matatani katika kushika nyadhifa kubwa kama akina Tibaijuka... MSIPOAMUKA siku mkitaka kugombea uraisi tutawapinga kwa sababu ya mambo ya akina makinda..
 
Nashindwa hata kuelezea nilivyokerwa na jambo hili, najiuliza kila mara kwanini CCM hawana aibu kiasi hicho na kwanini wanatudharau namna hiyo? Wanafikiri watanzania wote ni bendera fuata upepo kama wanachama wao? kwamba hatuna uwezo wa kufikiri au ni ulevi wa madaraka ndio unawasumbua... hivi hii idea kwanini hawakuitoa wakati CHADEMA ina wanawabunge wachache, nawaunga mkono kwa 100% CHADEMA kwa walichokifanya ila sijui nitoe mchango gani kuhakikisha CCM hawafanikiwi kwa walichopanga. Sijui lini na sisi tutakuwa majasiri kama wenzetu wa Tunisia na Misri...
 
Wakati tuliokuwa tukiusubiri kuona CCM wanavyojarbu kuupiga vita upinzani mahiri wa CHADEMA ni sasa, nadhani watanzania wale wote wanaotaka kufahamu nyendo na matendo yanayotendwa na CCM kila siku, jana wameshuhudia ni kitu gani kimeanza, Mimi nachoomba kwa wana JF na watanzania wote kufaham ni kwamba madai yote yanayotafutwa na CCM kutaka vyama vyote pinzani kujiunga si kwa nia nzuri, wamejaribu hata kuchakachua na kuongeza kanuni ambazo hata hazikuwepo wakidhania kuwa CHADEMA hawatoona. Na tufahamu kuwa CCM na CUF ni kitu kimoja mpaka sasa kwa hiyo wanajaribu kuingiza mashushu na wasaliti kupitia shati la Upinzani, Chonde chonde CHADEMA kataeni hiyo sumu!!!!, hata kwa kuandamana mjengoni huko huko, bunge ni la kwetu wananchi na wala si la CCM na CUF, pigeni ngumi hizo meza mpaka zipasuke lakini kieleweke!!!,. Wasomeni machoni mwao kuna tabasam la kinafiki! huo urafiki wa kutaka kutujengea uadui ndani yetu hatuutaki hatuutaki!!, Halafu kwa nini wanatudharau kiasi hichoo? wapuuzi kweli!, hivi wanadhania kuwa mpaka tukaamua kufanya hivyo tulikuwa hatujui kuwa tunazuia nini na ni kwa sababu gani, mi nawashauri CCM wajinge na CUF kwani ni ndugu tayari useme tu walikuwa hawajafahamiana coz dingi yao alichelewa kuwatambulisha!!, ni vyama viwili tayari vilivyoko madarakani, wakifanya hivyo watuache, kisha CHADEMA itajiunga na vyama pinzani vingine viliyobaki. kama si hivyo CHADEMA endelei kuwa CHADEMA hivyo hivyo, ukizingatia si nyie bali ni umma mkubwa wa watanzania uliopo nyuma yenu, tafadhrini sana CCM na CUF waacheni hao wawakilishi wetu, la sivyo wote tutaingia bungeni coz mmeshindwa kuwasikiliza na kuwatii wao.CHADEMA kuweni makini na huyo mama, naye ni kibaraka wa ccm na CUF, kwani hatumwamini kuwa ataisimamia haki kama inavyotakiwa, lakini kwa muundo wa Tundu Lisu, atajiuzuru ngazi hiyo wakati akienda kutibiwa PRESHA hukoooo!! Big up Tundu, tunakukubali, endelea kupiga hizo meza, but kuwa makini coz ipo day waweza kushtakiwa kuwa umeua kwa kumsababishia presha huyo mama!!, coz hayuko fresh kiafya, lakini usijali coz kayataka mwenyewe!! RAi yangu kwa vyama vingine tofauti na hivi vyama viwil tawala ni kwamba anakayetaka kwenda nasi na auvue na kuupiga vita huo uovu kwanza!!.
 
".........Ukisoma kanuni za kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni huwezi kuja na tafsiri ya kambi rasmi eti maana yake ni vyama vyote vya upinzani kama alivyosikika Anna Makinda akitamka uchakachuaji huo....."

Huyo mama hawatendei haki akina mama wengine wanaowakilishwa na jinsia yake maana ana-paint picha kwamba
1. akina mama ni watu wa kukurupuka na kutoa maamuzi wakipewa nafasi kubwa kitu macho si kweli..

2. Anatoa picha kwamba akina mama si watumakini kitu ambacho si kweli hasa ukizingatia kazi na majambozi ya Mdee...

3. Anatoa picha kwamba akina mama kazi yao kubwa ni kuwafurahisha akina baba ili wasiendelee kugombana na kusahu kwamba kazi aliyopewa ina nafasi ya kumpa uraisi kama (God Forbid) raisi wa nchi akifariki gafla...
4. Anapingana na kauli yake mwenyewe kwamba jambo ambalo halina maslahi kwa taifa halipaswi kuchukua muda wa bunge maana ni sisi tax payers tunaowalipa siku zote kwa kazi za kipuuzi kama hizi za kutafsiri kanuni na taratibu zilizopitishwa na zililokubalika na bunge la 9

5. Labda atuambie tangu lini sisi wapiga kura tuliwatuma kwenda kubadlisha kanuni na sio kutunga sheria na za kuwabana mafisadi?

Akina mama popote pale mlipo amkeni na mkemeeni kama shetani anavyokemea na akina kakobe vinginevyo mama huyo anaiwekea jinsia yenu matatani katika kushika nyadhifa kubwa kama akina Tibaijuka... MSIPOAMUKA siku mkitaka kugombea uraisi tutawapinga kwa sababu ya mambo ya akina makinda..

Huyu mama anashangaza sana. Hajui umuhimu wa nafasi yake ya kulinda hadhi ya bunge na ofisi ya Uspika. Mimi hata sijui CCM na Anna Makinda wametumia ufahamu wa kutoka sayari gani. Yaani chama ambacho hakina haki ya kuunda kambi rasmi ya bunge eti kijumuishwe kwenye kambi hiyo kinyume cha kanuni ni ajabu kabisa. Iweje chama chenye wabunge pungufu ya asilimia 12.5 kijumuishwe kwenye kambi rasmi ya bunge wakati kanuni zinakataa? CCM sasa mnaipeleka nchi wapi hata kuchezeachezea bunge?
 
chadema mliamua kubagua sasa mmebaguliwa. mizee mizima hovyo

nimelipenda hilo la waturudi kwenye posho wana madeni benki
 
Kabla hata hatujasahau uchakachuaji wa kura za uraisi wa JK, kura za wabunge wa CCM, umeya wa jiji la Arusha, CCM sasa wameendeleza kufuru ya uchakachuaji wa waziwazi wa kanuni za Bunge. Ukisoma kanuni za kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni huwezi kuja na tafsiri ya kambi rasmi eti maana yake ni vyama vyote vya upinzani kama alivyosikika Anna Makinda akitamka uchakachuaji huo.

Kanuni za bunge za kuunda kambi ya upinzani lazima zijitosheleze bila ya kujipinga zenyewe. Tangu mwanzo kanuni inaanza kwa kutoa mwongozo kuwa kambi rasmi ya upinzania itaundwa pale ambapo vyama vya upinzani vimefisha asilimia 12.5 ya wabunge wote. Na kwamba chama cha upinzania hakitakuwa na haki ya kuunda kambi ya upinzania hadi kiwe na wabunge wasiopungua asilimia 12.5. Na kwamba kama vyama viwili vinawabunge waliofikia asilimia 12.5, basi kile chenye wabunge wengi ndicho kitakachochagua kiongozi wa kambi ya upinzani na naibu wake. Kanuni inaeleza wazi kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani ndiye mwenye uwezo wa kuchagua wabunge wa chama chake au kambi rasmi ya upinzania kuwa wasemaji wa wizara.

Tafsiri ya kambi rasmi ya upinzani haiwezi kuwa ya vyama vyote ikiwa kuna chama kinajitosheleza kwa wabunge kuunda kambi ya upinzani. Tafsiri hii inaweza kutumika pale tu ambapo hakuna chama cha upinzani kina wabunge wanaofikia asilimia 12.5, ambapo vyama vinalazimika kujiunga pamoja na kufikisha asilimia 12.5. Lakini kama kuna chama cha upinzani kimefikisha aslimia 12.5 na kimevipita vyama vingine kwa idadi ya wabunge ndicho chenye haki ya kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni. Si haki, na uchakachuaji huu wa makusudi wa CCM na spika wa bunge Anna Makinda haukubaliki kabisa na ni juu ya Chadema na Watanzania kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu wa kulichezea bunge la Tanzania. Kutafsiri kanuni ya bunge kwa kupotosha wakati kanuni zinajieleza wazi ni uhaini mkubwa sana.

Chadema na Watanzania tuchukue hatua za haraka sana za kisiasa, kisheria n.k. leo hii na si kesho ili kulinda na kurudisha heshima ya bunge letu.

Kanuni za Kuunda kambi ya upinzania
14.
-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwa
chini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasili za Kanuni hii
zinazofuata.
(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi
ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na
mbili na nusu ya Wabunge wote.
(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya
Wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge
wote.
(4) Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimoja
ambavyo kila kimoja kina Wabunge asilimia kumi na mbili na nusu
au zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kuliko
vingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwili
au zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimia
kumi na mbili na nusu, Wabunge wa vyama vinavyohusika
watachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibu
watakaokubaliana wenyewe.
15
.-(1) Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi
ya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi wa
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
(2) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateua
Wabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi ya
Upinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi ya
Upinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.

Ahsante sana ndugu yagu. lakini kumbuka Pia Spika ana nafasi nzito katika kubalisha kanuni za Bunge.

Pitia kanuni ya Kifungu cha 152 (3) ambacho kinasema bayana kuwa Spika akishauriana na kamati ya kanuni za Bunge atakuwa na madaraka ya kuzifanyia marekebisho au mabadiliko, nyongeza za kanuni za bunge kulingana na mahitaji ya wakati, kadri atakavyoona inafaa.


Kwa msingi huo Sasa ni wakati muafaka kuondoa Hilo neno RASMI ili kuwepo na uakilishi mahiri wa upinzani bungeni Pindi wapinzani wanaposhindwa kukubaliana tena kwa hoja hafifu.

Inasikitisha sana kuona chadema wanaposema CUF sio chama cha Upinzani kwa sababu tu wameungana kuunda serikali ya mseto zanzibar. Lakini wanasahau kuwa Serikali inaanzia katika ngazi za mitaa na kuendelea mpaka kwenye halmashauri, manispaa na majiji.

sasa vipi huko kwenye ngazi za wilaya wao wanaungana na CCM kuunda mabaraza ya madiwani. kwanini wasijitoe na huko.

Uroho tu na ukabila, udini umewajaa.

 
Niliiwahi kusema na narudia tena,haki haiombwi,na kwa kadri tunavyozidi kunyamaza ndivyo ccm wanatake advantage,swala la haki nchini si la chadema ni la watu wote,ndugu zangu tuingie mitaani tukomeshe uhuni huu.
 
Wakati tuliokuwa tukiusubiri kuona CCM wanavyojarbu kuupiga vita upinzani mahiri wa CHADEMA ni sasa, nadhani watanzania wale wote wanaotaka kufahamu nyendo na matendo yanayotendwa na CCM kila siku, jana wameshuhudia ni kitu gani kimeanza, Mimi nachoomba kwa wana JF na watanzania wote kufaham ni kwamba madai yote yanayotafutwa na CCM kutaka vyama vyote pinzani kujiunga si kwa nia nzuri, wamejaribu hata kuchakachua na kuongeza kanuni ambazo hata hazikuwepo wakidhania kuwa CHADEMA hawatoona. Na tufahamu kuwa CCM na CUF ni kitu kimoja mpaka sasa kwa hiyo wanajaribu kuingiza mashushu na wasaliti kupitia shati la Upinzani, Chonde chonde CHADEMA kataeni hiyo sumu!!!!, hata kwa kuandamana mjengoni huko huko, bunge ni la kwetu wananchi na wala si la CCM na CUF, pigeni ngumi hizo meza mpaka zipasuke lakini kieleweke!!!,. Wasomeni machoni mwao kuna tabasam la kinafiki! huo urafiki wa kutaka kutujengea uadui ndani yetu hatuutaki hatuutaki!!, Halafu kwa nini wanatudharau kiasi hichoo? wapuuzi kweli!, hivi wanadhania kuwa mpaka tukaamua kufanya hivyo tulikuwa hatujui kuwa tunazuia nini na ni kwa sababu gani, mi nawashauri CCM wajinge na CUF kwani ni ndugu tayari useme tu walikuwa hawajafahamiana coz dingi yao alichelewa kuwatambulisha!!, ni vyama viwili tayari vilivyoko madarakani, wakifanya hivyo watuache, kisha CHADEMA itajiunga na vyama pinzani vingine viliyobaki. kama si hivyo CHADEMA endelei kuwa CHADEMA hivyo hivyo, ukizingatia si nyie bali ni umma mkubwa wa watanzania uliopo nyuma yenu, tafadhrini sana CCM na CUF waacheni hao wawakilishi wetu, la sivyo wote tutaingia bungeni coz mmeshindwa kuwasikiliza na kuwatii wao.CHADEMA kuweni makini na huyo mama, naye ni kibaraka wa ccm na CUF, kwani hatumwamini kuwa ataisimamia haki kama inavyotakiwa, lakini kwa muundo wa Tundu Lisu, atajiuzuru ngazi hiyo wakati akienda kutibiwa PRESHA hukoooo!! Big up Tundu, tunakukubali, endelea kupiga hizo meza, but kuwa makini coz ipo day waweza kushtakiwa kuwa umeua kwa kumsababishia presha huyo mama!!, coz hayuko fresh kiafya, lakini usijali coz kayataka mwenyewe!! RAi yangu kwa vyama vingine tofauti na hivi vyama viwil tawala ni kwamba anakayetaka kwenda nasi na auvue na kuupiga vita huo uovu kwanza!!.

haya yooooote kwa Chadema ni DHAMBI YA UBAGUZI wa kidini, Kikanda na bado msipoangalia dhanbi hii itawamaliza wenyewe.
 
Kabla hata hatujasahau uchakachuaji wa kura za uraisi wa JK, kura za wabunge wa CCM, umeya wa jiji la Arusha, CCM sasa wameendeleza kufuru ya uchakachuaji wa waziwazi wa kanuni za Bunge. Ukisoma kanuni za kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni huwezi kuja na tafsiri ya kambi rasmi eti maana yake ni vyama vyote vya upinzani kama alivyosikika Anna Makinda akitamka uchakachuaji huo.

Kanuni za bunge za kuunda kambi ya upinzani lazima zijitosheleze bila ya kujipinga zenyewe. Tangu mwanzo kanuni inaanza kwa kutoa mwongozo kuwa kambi rasmi ya upinzania itaundwa pale ambapo vyama vya upinzani vimefisha asilimia 12.5 ya wabunge wote. Na kwamba chama cha upinzania hakitakuwa na haki ya kuunda kambi ya upinzania hadi kiwe na wabunge wasiopungua asilimia 12.5. Na kwamba kama vyama viwili vinawabunge waliofikia asilimia 12.5, basi kile chenye wabunge wengi ndicho kitakachochagua kiongozi wa kambi ya upinzani na naibu wake. Kanuni inaeleza wazi kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani ndiye mwenye uwezo wa kuchagua wabunge wa chama chake au kambi rasmi ya upinzania kuwa wasemaji wa wizara.

Tafsiri ya kambi rasmi ya upinzani haiwezi kuwa ya vyama vyote ikiwa kuna chama kinajitosheleza kwa wabunge kuunda kambi ya upinzani. Tafsiri hii inaweza kutumika pale tu ambapo hakuna chama cha upinzani kina wabunge wanaofikia asilimia 12.5, ambapo vyama vinalazimika kujiunga pamoja na kufikisha asilimia 12.5. Lakini kama kuna chama cha upinzani kimefikisha aslimia 12.5 na kimevipita vyama vingine kwa idadi ya wabunge ndicho chenye haki ya kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni. Si haki, na uchakachuaji huu wa makusudi wa CCM na spika wa bunge Anna Makinda haukubaliki kabisa na ni juu ya Chadema na Watanzania kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu wa kulichezea bunge la Tanzania. Kutafsiri kanuni ya bunge kwa kupotosha wakati kanuni zinajieleza wazi ni uhaini mkubwa sana.

Chadema na Watanzania tuchukue hatua za haraka sana za kisiasa, kisheria n.k. leo hii na si kesho ili kulinda na kurudisha heshima ya bunge letu.

Kanuni za Kuunda kambi ya upinzania
14.
-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwa
chini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasili za Kanuni hii
zinazofuata.
(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi
ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na
mbili na nusu ya Wabunge wote.
(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya
Wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge
wote.
(4) Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimoja
ambavyo kila kimoja kina Wabunge asilimia kumi na mbili na nusu
au zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kuliko
vingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwili
au zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimia
kumi na mbili na nusu, Wabunge wa vyama vinavyohusika
watachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibu
watakaokubaliana wenyewe.
15
.-(1) Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi
ya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi wa
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
(2) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateua
Wabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi ya
Upinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi ya
Upinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.

Huhitaji kuwa mtaalamu wa hermeneutics kuelewa hizo kanuni zinaeleza nini. Kanuni hizo zipo wazi na hazihitaji maelezo zaidi au vifungu vingine vya kanuni.
 
Kanuni za Kuunda kambi ya upinzania
14.
-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwa
chini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasili za Kanuni hii
zinazofuata.
(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi
ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na
mbili na nusu ya Wabunge wote..


kweli hesabu ugonjwa wa taifa!!!!!!!!!
ukiambiwa idadi si chini ya 12.5% .... Maana yake wawe 12.5% au zaidi.

CDM wako 12.5% kwa nini wasianzishe kambi yao?
CCM wako zaidi ya 12.5% ndo maana wako wenyewe.

Hivi kweli kama Spika hapa umeshindwa kuelewa hili,
KATIBA SI NDO TUTAPELEKWA CHAKA LA HATARI.


 
Ahsante sana ndugu yagu. lakini kumbuka Pia Spika ana nafasi nzito katika kubalisha kanuni za Bunge.

Pitia kanuni ya Kifungu cha 152 (3) ambacho kinasema bayana kuwa Spika akishauriana na kamati ya kanuni za Bunge atakuwa na madaraka ya kuzifanyia marekebisho au mabadiliko, nyongeza za kanuni za bunge kulingana na mahitaji ya wakati, kadri atakavyoona inafaa.


Kwa msingi huo Sasa ni wakati muafaka kuondoa Hilo neno RASMI ili kuwepo na uakilishi mahiri wa upinzani bungeni Pindi wapinzani wanaposhindwa kukubaliana tena kwa hoja hafifu.

Inasikitisha sana kuona chadema wanaposema CUF sio chama cha Upinzani kwa sababu tu wameungana kuunda serikali ya mseto zanzibar. Lakini wanasahau kuwa Serikali inaanzia katika ngazi za mitaa na kuendelea mpaka kwenye halmashauri, manispaa na majiji.

sasa vipi huko kwenye ngazi za wilaya wao wanaungana na CCM kuunda mabaraza ya madiwani. kwanini wasijitoe na huko.

Uroho tu na ukabila, udini umewajaa.


naomba mfano wa halmashauri ambapo CDM wameungana na CCM kuunda baraza la madiwani? if you do not have any, delete this shit of yours!!
 
Ahsante sana ndugu yagu. lakini kumbuka Pia Spika ana nafasi nzito katika kubalisha kanuni za Bunge.

Pitia kanuni ya Kifungu cha 152 (3) ambacho kinasema bayana kuwa Spika akishauriana na kamati ya kanuni za Bunge atakuwa na madaraka ya kuzifanyia marekebisho au mabadiliko, nyongeza za kanuni za bunge kulingana na mahitaji ya wakati, kadri atakavyoona inafaa.


Kwa msingi huo Sasa ni wakati muafaka kuondoa Hilo neno RASMI ili kuwepo na uakilishi mahiri wa upinzani bungeni Pindi wapinzani wanaposhindwa kukubaliana tena kwa hoja hafifu.

Inasikitisha sana kuona chadema wanaposema CUF sio chama cha Upinzani kwa sababu tu wameungana kuunda serikali ya mseto zanzibar. Lakini wanasahau kuwa Serikali inaanzia katika ngazi za mitaa na kuendelea mpaka kwenye halmashauri, manispaa na majiji.

sasa vipi huko kwenye ngazi za wilaya wao wanaungana na CCM kuunda mabaraza ya madiwani. kwanini wasijitoe na huko.

Uroho tu na ukabila, udini umewajaa.

Hapa tatizo ni kwamba, tafsiri ya kuchakachua ya CCM inapinga kanuni za msingi zinazoelekeza kuwa chama cha upinzania kinapata haki ya kuunda au kuwa katika kambi rasmi ya upinzani ikiwa kimefikisha asilimia 12.5 ya wabunge wote. Kama vyama vyote havina idadi hiyo ndio vinaungana kupata asilimia 12.5 na kuunda kambi rasmi. Chadema inajitosheleza kuunda kambi rasmi, na vyama vingine kulingana na kanuni havina haki ya kuwemo katika kambi rasmi ya upinzani. Hivyo kulingana na kanuni Chadema yenye wabunge wengi hailazimiki kuingiza wabunge wa vyama vingine kwenye kambi rasmi ya upinzani. Hiyo tafsiri ya kuchakachuwa ya CCM si halali kwa namna yeyote ile na haikubaliki. Inadhalilisha bunge na kuwa kama kilabu cha pombe.
 
Back
Top Bottom