Uchaguzi Zanzibar itakuwaje 2010?

Side,
Naungana na pointi zako hapo juu, kuhusu hayo matamko ya sisiemu na watu wake. Kwa mtu anayedai kwamba nchi ilipatikana kwa mapanga, na hivyo anayeitaka naye apite njia hiyo hiyo nadhani haitakii mema Zanzibar na watu wake na ni mwehu! Kama hakutaka nchi ipatikane kwa "MAKARATASI" (kura) nadhani wangeondoa kabisa suala la uchaguzi, ambao aghalabu huwa wa tiktak ama mazingaombwe. Ndio yale yale ya kura za maruhani.
Suala la wizi wa kura kwa chaguzi za visiwani huwa si la kujadiliwa ama kuumiza vichwa sana, kwani linatambulika. Na mpaka kesho sijajua wale jamaa waliokimbia na maboksi ya kura mwaka 2000 na kwenda kubadili matokeo porini wamechukuliwa hatua gani!
Tungepata ufumbuzi wa hili suala tata nadhani tungekuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuchambua suala hili. Mlio na taarifa za suala hili tunaziomba.
 
'Suala la wizi wa kura kwa chaguzi za visiwani huwa si la kujadiliwa ama kuumiza vichwa sana, kwani linatambulika. Na mpaka kesho sijajua wale jamaa waliokimbia na maboksi ya kura mwaka 2000 na kwenda kubadili matokeo porini wamechukuliwa hatua gani!
Tungepata ufumbuzi wa hili suala tata nadhani tungekuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuchambua suala hili. Mlio na taarifa za suala hili tunaziomba.'


IDIMI umenifanya nicheke saaana mkuu. Lile changa la macho tu, kuonyesha jamaa wapo makini na uchanguzi, jamaa ni wao wenyewe na walipanga nao. Watu wale wapo mitaani kama kawaida hawaijui Jela wala Rumande. (kinyume chake wanasifiwa kwa kufanikisha kazi waliyotumwa).
 
'Suala la wizi wa kura kwa chaguzi za visiwani huwa si la kujadiliwa ama kuumiza vichwa sana, kwani linatambulika. Na mpaka kesho sijajua wale jamaa waliokimbia na maboksi ya kura mwaka 2000 na kwenda kubadili matokeo porini wamechukuliwa hatua gani!
Tungepata ufumbuzi wa hili suala tata nadhani tungekuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuchambua suala hili. Mlio na taarifa za suala hili tunaziomba.'


IDIMI umenifanya nicheke saaana mkuu. Lile changa la macho tu, kuonyesha jamaa wapo makini na uchanguzi, jamaa ni wao wenyewe na walipanga nao. Watu wale wapo mitaani kama kawaida hawaijui Jela wala Rumande. (kinyume chake wanasifiwa kwa kufanikisha kazi waliyotumwa).

Si utani mkuu, kama mambo ni hivi basi safari ya kwenda kwenye kitu "Demokrasia" ya kweli ni ndefu isiyo na kifani.
Ila kuna siku isiyo na jina kitaeleweka tu. Za mwizi arobaini!

Kumbuka kitabu cha KULI, "Yana mwisho haya"
 
Mmesema mengi wakuu, lakini tukubali kuwa chanzo cha vurugu Zanzibar sio Seif Sharif Hamad, chanzo ni wizi wa kura. Lakini sasa jumuiya ya kimataifa inatakiwa kuwa makini sana, kwani hiyo sumu ya CCM imeanza kuenea kwenye sehemu nyingine za Afrika.
2010 naweza kusema story will be the same, Siefu na CUF watashinda, wapemba kama 20 watauawa wengine watafungwa, utaitishwa muafaka mpya ambao utaendelea mpaka 2015, lakini 2015 sidhani kama seifu atakuwepo tena kwenye kugombea urais, huenda Haji Duni ataingia kwenye ulingo.
Lakini mbuni ya CCM sasa tunaona inakuwa na spill over effect!
 
Bila shaka sisiemu wamemuambukiza upumbavu Mwai "Kibaka". Inasikitisha sana kuona ndugu zetu wa Kenya wanauawa kwa kuchagua kile wanachokipenda. Hata ningekuwa ni mimi, ningekufa kwa kutetea haki na maamuzi yangu ya kutokubali kuibiwa.
Naamini haki itapatikana Kenya, hata kwa mabavu.
 
Maalim Seif alianzia mbali katika kupandikiza mbegu mbaya ambayo kwa sasa anaijutia. Tokea akiwa waziri wa elimu katika SMZ aliweza kubagua wananchi wa visiwa hivyo na aliendelea hata alipokuwa waziri kiongozi. Fainali ni pale alipoanza kampeni zake kabla hata ya mfumo wa vyama vingi kuingia tz.

Kauli za nchi ilipinduliwa na haiwezi kutolewa kwa makaratasi, ni maneno ya kwenye maskani na baraza za kahawa. Iwapo mwakilishi alisema hivyo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi huo utakuwa ni utashi wake binafsi... kwani huko kuna mengi ya kushangaza, kuna mwakilishi mmoja aliitaka wizara ya Utalii kuwapaka kobe rangi, ili waweze kuvutia zaidi watalii.

Wizi wa kura visiwani upo si kwa CUf wala CCM, wote wamekuwa wakitumia njia chafu katika kupata ushindi. wanacuf wengi hupiga kula zaidi ya kituo kimoja... 2000 wakati CCM ikiwaajili wanajeshi wa SMZ kwa kuwafungulia makambi huko Pemba, CuF wao waliwapakia watu kibao toka Tanga na Mombasa kwenye majahazi kenda kupiga kura.
 
Maalim Seif alianzia mbali katika kupandikiza mbegu mbaya ambayo kwa sasa anaijutia. Tokea akiwa waziri wa elimu katika SMZ aliweza kubagua wananchi wa visiwa hivyo na aliendelea hata alipokuwa waziri kiongozi. Fainali ni pale alipoanza kampeni zake kabla hata ya mfumo wa vyama vingi kuingia tz.

Kauli za nchi ilipinduliwa na haiwezi kutolewa kwa makaratasi, ni maneno ya kwenye maskani na baraza za kahawa. Iwapo mwakilishi alisema hivyo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi huo utakuwa ni utashi wake binafsi... kwani huko kuna mengi ya kushangaza, kuna mwakilishi mmoja aliitaka wizara ya Utalii kuwapaka kobe rangi, ili waweze kuvutia zaidi watalii.

Wizi wa kura visiwani upo si kwa CUf wala CCM, wote wamekuwa wakitumia njia chafu katika kupata ushindi. wanacuf wengi hupiga kula zaidi ya kituo kimoja... 2000 wakati CCM ikiwaajili wanajeshi wa SMZ kwa kuwafungulia makambi huko Pemba, CuF wao waliwapakia watu kibao toka Tanga na Mombasa kwenye majahazi kenda kupiga kura.

kibunango hapa umetupa maelezo mepya maalim

mie sina uhakika kama kuna wanaotoka tanga na mombasa kupigia kura cuf, ila haya huenda ni sawa na siasa inayotokea huko kenya kila kundi kujenga hoja kuwa wenzao ndio wizi.

sasa jee ni lipi lifanyike kuzuia manun'guniko pande zote?

au ndio tuseme hakuna dawa
 
CCM kushindwa bara itakuwa kama miaka 50 au 100 ijayo,kwa hiyo Zanzibar wasahau kabisa suala la uchaguzi wa kidemokrasia.Nasema hivyo kwa kuwa huku bara kuna maradhi makubwa ya kutoelewa mambo kwa jumla.Pia kuna suala la katiba ambayo bado inaonekana kama bado ya chama kimoja.
Kama kuna jinsi ya kubadili mambo kwanza ni kuhamsisha wananchi ili katiba ibadilike na kukidhi haja ya kiwepo chaguzi za haki.
 
Yote semeni lakini Pemba kunatisha,wapemba wacheni mchezo wanatisha,na wanaua na kuchinja kama kuku ,polisi nasikia wanajua kilichowatokea kule,na ni watu wa ajabu sana wanaweza kumtrace polisi muuaji na kumnadia mwizi nasikia walimfuata waliemjua na kumnadia mwizi na kumchoma hapo Unguja.Bora wapewe Baseifu awe ndio raisi wao.
Nasikia Kigoma inataka kujitenga ?
 
Maalim Seif kwa upande wa siasa za visiwani ndie mhusika mkuu wa fujo zote baada ya chaguzi, kwa madai ya kuibiwa kura(inawezekana ni kweli). Njia ambayo anatumia kufikisha ujumbe kwa wafuasi na wapenzi wa chama chake imejaa shari hivyo kuwafanya wafuasi wake wawe washari vilevile, huku yeye katulia tuli nyumbani kwake mtoni.

1995 alijitangaza kuwa ndie mshindi wa uprez, masaa 24 kabla ya matokeo rasmi kutoka, matokeo yake yakawa ni vujo mitaani. Haya tumeona vile vile mwaka jana huko Kenya.

2000, mapema alishasema kuwa hatokubaliana na matokeo ya uchaguzi, hata kabla ya yeye mwenyewe kwenda kupiga kura, kauli hii iliwajaza jazba wafuasi wake na kusababisha vujo.

Mara zote baada ya makesheshe huja na kuwatuliza wafuasi wake kwa kuwataka wavute subira na kujiandaa na chaguzi zinazokuja. Hii inaonyesha wazi jinsi anavyozikilizwa vema na wanachama wake. Hivyo basi ni yeye mwenye uwezo wa kuzuia ama kuleta vujo hapo 2010


..lakini si kweli miaka yote hiyo CCM(mafisadi) wanaiba kura au na hili unataka kubisha,komandoo kawaletea nini zaidi ya njaa tuu na migawanyiko...amkeni nyie,haki ni muhimu kwa maendeleo na utaifa hata kama anayechaguliwa humtaki
 
Hakuna la kufanyika Zanzibar ni moyo wa CCM liwalo na liweko lakini upinzani kushika dola ya Zanzibar ni mwiko,hilo mkae na kulijua.

..mawazo kama haya tena humu JF yanatia uchungu sana,lakini sampuli hii ya mawazo na watu kama hawa mwisho wa siku wanajikomoa wenyewe na vizazi vyao vijavyo na huwezi kuamini watu kama hawa kwa lolote.
 
kibunango hapa umetupa maelezo mepya maalim

mie sina uhakika kama kuna wanaotoka tanga na mombasa kupigia kura cuf, ila haya huenda ni sawa na siasa inayotokea huko kenya kila kundi kujenga hoja kuwa wenzao ndio wizi.
Mtu wa Pwani hayo sio maelezo mepya, Ni mambo yaliyotokea huko visiwani. Mwaka 1995, CCM ilishangazwa sana na wingi wa kura walizopata CUF na wingi wa viti katika Baraza la Wawakilishi. Hawakutegemea hayo kwani walitegemea nguvu za Marehemu Dr Omar Ali Juma angeweza kuvuta jamaa wengi wa kisiwa cha pili, hata hivyo ilikuwa ni kinyume chake. Marehemu huyo sana sana aliweza kuwaondoa Wapemba wengi hasa wale wafanyakazi SMZ toka CCM kwenda CUF, hii ilitokana na hotuba zake...

Ili kudhibiti wingi wa viti Barazani, CCM walikuja na njia ya kuyagawa majimbo ya uchaguzi. CUF kuona hivyo waliwataka wanachama wake waliokuwa katika majimbo yaliyomegwa kwa manufaa ya CCM kutopiga kura humo, badala yake wahamishie nguvu zao kwenye majimbo mengine yenye ushindani mkubwa.

Kila CCM inapofanya janja katika chaguzi nao CUF hujibu mapigo. Tatizo lao hawaishii hapo, kwani wanaposhindwa huanzisha vujo. Vitendo kama vya kupaka vinyesi kwenye skuli, kujisaidia kwenye visima vya maji, kushambulia polisi na wakereketwa ni mojawapo ya vujo za CUF pale njia zao za kuizidi CCM zinapokwama.
 
mzee kibunango una maana dr omar alikuwa akiifanyia kazi CUF?

pili unataka kunithibitishia wote CCM na CUF wanacheza rafu, ila huyu mmoja akizidiwa ndio hupiga kelele?

sasa jee nn kifanyike ili tuweze kufanya uchaguzi usio na mizengwe nakila chama kiuze sera na wananchi waamue kwa kupiga kura tu
 
mzee kibunango una maana dr omar alikuwa akiifanyia kazi CUF?

pili unataka kunithibitishia wote CCM na CUF wanacheza rafu, ila huyu mmoja akizidiwa ndio hupiga kelele?

sasa jee nn kifanyike ili tuweze kufanya uchaguzi usio na mizengwe nakila chama kiuze sera na wananchi waamue kwa kupiga kura tu

Naam... Dr.Omar alichangia sana bila yeye kujua hilo. Kila mkutano wa kampeni aliohotubia uliondoa wapemba wengi ndani ya CCM. Mwingine aliyekuwa akichochoea ni yule ndumila kuwili Awesu Dadi.

Ni ukweli usiofichika kuwa CCM na CUF ni wacheza rafu kubwa katika chaguzi na hasa za visiwani. Wanaibiana ujuzi, mipango na mikakakati ya ushindi, kwani kila chama kina watu wake ndani ya chama kingine.

Cha kufanya sasa, kwanza ni kwa Wanzej wote kukubali kuwa wao ni wamoja,dhihaka ya upemba,unyamwezi,ungazija na mengine yawe historia. Ni kazi kubwa lakini ni lazima ifanywe.

Maalim Seif aombe sahamani kwa kuwa na sera ya utengano kwa wazenj wote.

Wenye ushawishi mkubwa na mapenzi ya wengi wawe tayali kukubali yanayofanywa na wengine katika kuleta maendeleo. Mfano Maalim Seif awe anakubali juhudi za dhati zinazofanywa na chama tawala, hali kadhalika chama tawala kipokee kwa dhati mapendekezo ya kimaendeleo toka CUF.

Wapemba wa waunguja wengi wamehusiana ni vema wakaanza kuondoa tofauti zao kisiasa ndani ya nyumba zao. Hii itasaidia kujenga taifa linaloangalia sera na sio chama.

SMZ chini ya idara ya utumishi iache tabia ya kuchunguza sana waombaji waliofuzu katika fani zao kama wamehusu kisiwa cha pili. Uwezo, ujuzi na taaluma vime ndio vigezo pekee katika kuajili na sio vinginevyo.
Aidha idara zingine zote zenye ukuritimba dhidi ya kundi au kabila fulani viache kufanya hivyo.

Zanzibar wakubali kuwa ndio Mji mkuu wa visiwa hivi. Hivyo wame tayali kupokea wahamiaji bila kuwadhihaki.

Sheria na Katiba ya nchi zifuatwe ipasavyo na sio kupindishwa kwa manufaa ya kundi fulani.

Vyama vyote vya Siasa viheshimu Mapinduzi ya mwaka 1964. Mapinduzi hayo ndio yaliyotufikisha hapa tulipo tukiwa vifua mbele kuringia Uzenj. Kwa kufanya hivyo kutaondoa misuguano ambayo ipo muda mrefu kiasi kwa sasa imekuwa kama ni silaha dhidi ya vyama vingine.
 
duh hivi wewe ndio yule KIBUNANGO ninayekujua a.k.a ........ ama nimekosea,kula tano kwa darasa safi kabisa.
 
Naam... Dr.Omar alichangia sana bila yeye kujua hilo. Kila mkutano wa kampeni aliohotubia uliondoa wapemba wengi ndani ya CCM. Mwingine aliyekuwa akichochoea ni yule ndumila kuwili Awesu Dadi.

Ni ukweli usiofichika kuwa CCM na CUF ni wacheza rafu kubwa katika chaguzi na hasa za visiwani. Wanaibiana ujuzi, mipango na mikakakati ya ushindi, kwani kila chama kina watu wake ndani ya chama kingine.

Cha kufanya sasa, kwanza ni kwa Wanzej wote kukubali kuwa wao ni wamoja,dhihaka ya upemba,unyamwezi,ungazija na mengine yawe historia. Ni kazi kubwa lakini ni lazima ifanywe.

Maalim Seif aombe sahamani kwa kuwa na sera ya utengano kwa wazenj wote.

Wenye ushawishi mkubwa na mapenzi ya wengi wawe tayali kukubali yanayofanywa na wengine katika kuleta maendeleo. Mfano Maalim Seif awe anakubali juhudi za dhati zinazofanywa na chama tawala, hali kadhalika chama tawala kipokee kwa dhati mapendekezo ya kimaendeleo toka CUF.

Wapemba wa waunguja wengi wamehusiana ni vema wakaanza kuondoa tofauti zao kisiasa ndani ya nyumba zao. Hii itasaidia kujenga taifa linaloangalia sera na sio chama.

SMZ chini ya idara ya utumishi iache tabia ya kuchunguza sana waombaji waliofuzu katika fani zao kama wamehusu kisiwa cha pili. Uwezo, ujuzi na taaluma vime ndio vigezo pekee katika kuajili na sio vinginevyo.
Aidha idara zingine zote zenye ukuritimba dhidi ya kundi au kabila fulani viache kufanya hivyo.

Zanzibar wakubali kuwa ndio Mji mkuu wa visiwa hivi. Hivyo wame tayali kupokea wahamiaji bila kuwadhihaki.

Sheria na Katiba ya nchi zifuatwe ipasavyo na sio kupindishwa kwa manufaa ya kundi fulani.

Vyama vyote vya Siasa viheshimu Mapinduzi ya mwaka 1964. Mapinduzi hayo ndio yaliyotufikisha hapa tulipo tukiwa vifua mbele kuringia Uzenj. Kwa kufanya hivyo kutaondoa misuguano ambayo ipo muda mrefu kiasi kwa sasa imekuwa kama ni silaha dhidi ya vyama vingine.

Mapinduzi hayo yamemsaidia nini kijana aliyezaliwa mwaka 1970 ambaye hana kazi, hana shamba na anaishia kuwa juha kwenye nchi yake?

Wazenji wanaotembea vifua mbele wako wangapi? Siku itafika mtakuja ondoka tu, mpende msipende. Ile ni nchi ya kila mtu na japo huko nyuma mlifanikiwa
kuiba kura, itafika siku wananchi watachukua mapanga kuwatoeni kama walivyomtoa mwarabu.
 
Mapinduzi hayo yamemsaidia nini kijana aliyezaliwa mwaka 1970 ambaye hana kazi, hana shamba na anaishia kuwa juha kwenye nchi yake?

Wazenji wanaotembea vifua mbele wako wangapi? Siku itafika mtakuja ondoka tu, mpende msipende. Ile ni nchi ya kila mtu na japo huko nyuma mlifanikiwa
kuiba kura, itafika siku wananchi watachukua mapanga kuwatoeni kama walivyomtoa mwarabu.

Jina lako kwanza linakusuta...

Mapinduzi hayo yamewasaidia wananchi wa visiwa hivyo kwa mapana na marefu. Hizo kauli za kejeli na kichochezi hazina nafasi kwenye nchi ya kimapinduzi.
 
Naam... Dr.Omar alichangia sana bila yeye kujua hilo. Kila mkutano wa kampeni aliohotubia uliondoa wapemba wengi ndani ya CCM. Mwingine aliyekuwa akichochoea ni yule ndumila kuwili Awesu Dadi.

Ni ukweli usiofichika kuwa CCM na CUF ni wacheza rafu kubwa katika chaguzi na hasa za visiwani. Wanaibiana ujuzi, mipango na mikakakati ya ushindi, kwani kila chama kina watu wake ndani ya chama kingine.

Cha kufanya sasa, kwanza ni kwa Wanzej wote kukubali kuwa wao ni wamoja,dhihaka ya upemba,unyamwezi,ungazija na mengine yawe historia. Ni kazi kubwa lakini ni lazima ifanywe.

Maalim Seif aombe sahamani kwa kuwa na sera ya utengano kwa wazenj wote.

Wenye ushawishi mkubwa na mapenzi ya wengi wawe tayali kukubali yanayofanywa na wengine katika kuleta maendeleo. Mfano Maalim Seif awe anakubali juhudi za dhati zinazofanywa na chama tawala, hali kadhalika chama tawala kipokee kwa dhati mapendekezo ya kimaendeleo toka CUF.

Wapemba wa waunguja wengi wamehusiana ni vema wakaanza kuondoa tofauti zao kisiasa ndani ya nyumba zao. Hii itasaidia kujenga taifa linaloangalia sera na sio chama.

SMZ chini ya idara ya utumishi iache tabia ya kuchunguza sana waombaji waliofuzu katika fani zao kama wamehusu kisiwa cha pili. Uwezo, ujuzi na taaluma vime ndio vigezo pekee katika kuajili na sio vinginevyo.
Aidha idara zingine zote zenye ukuritimba dhidi ya kundi au kabila fulani viache kufanya hivyo.

Zanzibar wakubali kuwa ndio Mji mkuu wa visiwa hivi. Hivyo wame tayali kupokea wahamiaji bila kuwadhihaki.

Sheria na Katiba ya nchi zifuatwe ipasavyo na sio kupindishwa kwa manufaa ya kundi fulani.

Vyama vyote vya Siasa viheshimu Mapinduzi ya mwaka 1964. Mapinduzi hayo ndio yaliyotufikisha hapa tulipo tukiwa vifua mbele kuringia Uzenj. Kwa kufanya hivyo kutaondoa misuguano ambayo ipo muda mrefu kiasi kwa sasa imekuwa kama ni silaha dhidi ya vyama vingine.

kuna maeneo mengi hapa nnakuunga mkono.

niliwahi kusikia pahali fulani kuwa CUF imekubali kuyaheshimu mapinduzi ya 64 na pia niliwahi kushuhudia wafuasi wa CUF wakihudhuria sherehe moja ya mapinduzi kule amani


lakini hayo mengine yanapaswa kuzingatiwa na pande zote mbili, nnategemea inshaallah tutafika tu
 
Alianza Baba, akaja Kaka, sasa mie, ...and then atakuja FATUMA mwanasheria aliyebobea



Na Salma Said, Zanzibar

BALOZI Ali Abeid Karume ameamua kutangaza mapema kuwa ataingia kwenye kinyanganyiro cha urais wa Zanzibar mwaka 2010.


Balozi Karume ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Itali na mdogo wa Rais wa sasa wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Amani Abeid Karume aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa jana kuwa ameamua kutanga mapema msimamo wake huo.


"Nitachukua fomu za kugombea Urais wa Zanzibar mwaka 2010 tena sina utani katika hilo, kwani sifa zote 13 zilizomo kwenye katiba na mwongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ninazo, hivyo sioni sababu ya kwa nini nisigombee nafasi hiyo," alisema Balozi Karume.


Mwanadiplomasia huyo amepinga hoja zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa kuwa haitapendeza tena kwa watoto wa viongozi waliowahi kuongoza nchi kujitokeza katika uchaguzi wa mwaka 2010.


"Kuna fitina za kisiasa kuwa haiwezekani na wala haipendezi rais ajaye wa Zanzibar atoke katika mfamilia moja. Mimi nasema hoja hiyo haina msingi kwa sababu kinachotakiwa ni sifa," alisema Balozi huyo.


Balozi Karume alitoa mfano wa nchi ya Singapore ambayo iliwahi kuongozwa na watu kutoka katika familia moja katika nyadhifa mbali mbali, lakini halikuwa tatizo kwa kuwa jambo muhimu ni sifa na kukubalika na wananchi na siyo suala la familia.


Alisema hata Baba wa Taifa hili, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alisisitiza umuhimu wa kiongozi kuwa na sifa zinazotakiwa na sio suala jengine.


Balozi Karume ambaye aliwahi kugombea urais wa Tanzania mwaka 2005 alisema ni muhimu chama kikamtendea haki mwanachama wake bila ya kuangalia anatoka katika familia gani.


"Mimi niliingia kwenye chama hiki (CCM) si kwa dharura, niliingia kwa uzalendo tangu hata havijaungana ASP na TANU kuzaliwa CCM. Nitasikitika sana kuona kama chama kitampa mtu ambaye hata kadi yake kachukua juzi tena wino wake haujakauka," alisema


Balozi huyo aliwaponda wanasiasa wanaotajwa kuwa na dhamira ya kugombea kiti cha urais wa Zanzibar mwaka 2010 kuwa wengi wao hawana sifa zinazotakiwa na CCM.


"Msije mkafanya kosa kumchagua mtu mwenye sifa ya usomi, lakini kumbe kusomea kwenyewe ni kupiga kinanda au kwa mfano mtu kasomea kusonga ugali aje kuwa mgombea. Kwa nini asitafutwe mtu kama Balozi Karume aliyesomea Uchumi, Diplomasia na Utawala katika Biashara na kumpa nchi, kuliko kumtafuta dereva wa teksi," alibeza Karume.


Hii ni mara ya pili kwa mtoto wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Abeid Amani Karume kujitosa katika mbio za kusaka nafasi ya juu ya uongozi katika visiwa vya Zanzibar.


Baadhi ya watu wamekuwa wakisema kuwa haitakuwa busara kwa watoto wa viongozi waliotawala Zanzibar kujitokeza kugombea nafasi hiyo kwani inaweza kuwanyima fursa wananchi wengine kushika nafasi hiyo.
 
Hivi ni dalili za kurudisha tawala za kitemi....kwanini asiachie wengine karume karume karume nasikia waziri wa mambo ya muungano naye Dr Hussein Mwinyi is another contender for presidential post huko Zanzibar 2010 tawala za jadi mtoto wa kiume kurithi madaraka duuuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom