Mbala-mwezi
Member
- Sep 27, 2009
- 22
- 3
Hakuna chaguzi ngumu kwa vyama vya upinzani kushinda kama hizi za mitaa. Hata hivyo, katika hali inayoonesha mwanga mpya, majimbo matatu ya mkoa wa Kigoma yanaonesha kukubalimabadiliko ya kweli na Uhuru wa kweli...haya sio mengine..
kwanza ni jimbo la Kigoma mjini ambalo CHADEMA inaongoza kata7 kati ya 13, ambako kuna mitaa68, mitaa4 uchaguzi umevurugika. CHADEMA imeshinda mitaa33, CUF1.UMD1,CCM29...Mwaka 2004, jimbo hili lilikuwa na mitaa 200, ambapo CCM ilishinda mitaa 110, CHADEMA90....hayo ndio mabadiliko makubwa katika jimbo hilo ngome ya CHADEMA, ambayo mpaka sasa haijajulikana wazi nani anajipanga kuiongoza kupitia CHADEMA 2010, ingawa kuna mpambano mkali ndani ya CCM ambapo zaidi ya watu4 wameshaanza kupambana kila mmoja akitaka awe yeye kupitia CCM 2010.
Pili, ni jimbo la Kigoma kaskazini, ambalo lipo chini ya Zitto Kabwe, ambalo mwaka 2004, CHADEMA ilishinda vijiji2 tu kati ya 33...Leo, matokeo yaliyopatikana mpaka jioni hii, CHADEMA imeshinda vijiji12, CCM16, na vijiji 5 vilivyopo ukanda wa ziwa Tanganyika matokeo bado hayajapatikana kutokana na ukosefu wa mawasiliano ya simu, na zaidi ni usafiri mgumu kwani boti linachukua takribani masaa8 na zaidi..Haya ndio matokeo ya CHADEMA katika jimbo hili, ambalo Mh Zitto hakuweza kufanya kampeni hata siku moja, japo alichangia gharama za kampeni na kuamuru wanakijiji wapambane na kila aina ya mbinu chafu za CCM na serikali yake katika uchaguzi....
Tatu ni jimbo la Kigoma kusini ambalo mwaka 2004, upinzani ukiongozwa na CHADEMA, ukifuatiwa na NCCR na CUF kwa mbali ulifanikiwa kushinda vijiji27 kati ya 43....mpaka sasa vijiji 8 vilivyopo ukanda wa ziwa na ambako ni ngome ya CHADEMA matokeo hayajapatikana kutona na usafiri na mawasiliano duni...mpaka sasa CHADEMA imeshinda vijiji8, NCCR8,CUF2...hili ni jimbo ambalo kwa sasa kutoka upinzani linawaniwa na vijana wawili, Afisa Habari wa CHADEMA David Kafulila26, na Mdhamini wa chama, kijana wa kiasia, Muslim Asanary26....kutoka vyama vingine bado hakuna fununu kabisa hasa baada ya ngome ya NCCR iliyopo kata ya Nguruka kuwa nyuma ya David Kafulila..
kwanza ni jimbo la Kigoma mjini ambalo CHADEMA inaongoza kata7 kati ya 13, ambako kuna mitaa68, mitaa4 uchaguzi umevurugika. CHADEMA imeshinda mitaa33, CUF1.UMD1,CCM29...Mwaka 2004, jimbo hili lilikuwa na mitaa 200, ambapo CCM ilishinda mitaa 110, CHADEMA90....hayo ndio mabadiliko makubwa katika jimbo hilo ngome ya CHADEMA, ambayo mpaka sasa haijajulikana wazi nani anajipanga kuiongoza kupitia CHADEMA 2010, ingawa kuna mpambano mkali ndani ya CCM ambapo zaidi ya watu4 wameshaanza kupambana kila mmoja akitaka awe yeye kupitia CCM 2010.
Pili, ni jimbo la Kigoma kaskazini, ambalo lipo chini ya Zitto Kabwe, ambalo mwaka 2004, CHADEMA ilishinda vijiji2 tu kati ya 33...Leo, matokeo yaliyopatikana mpaka jioni hii, CHADEMA imeshinda vijiji12, CCM16, na vijiji 5 vilivyopo ukanda wa ziwa Tanganyika matokeo bado hayajapatikana kutokana na ukosefu wa mawasiliano ya simu, na zaidi ni usafiri mgumu kwani boti linachukua takribani masaa8 na zaidi..Haya ndio matokeo ya CHADEMA katika jimbo hili, ambalo Mh Zitto hakuweza kufanya kampeni hata siku moja, japo alichangia gharama za kampeni na kuamuru wanakijiji wapambane na kila aina ya mbinu chafu za CCM na serikali yake katika uchaguzi....
Tatu ni jimbo la Kigoma kusini ambalo mwaka 2004, upinzani ukiongozwa na CHADEMA, ukifuatiwa na NCCR na CUF kwa mbali ulifanikiwa kushinda vijiji27 kati ya 43....mpaka sasa vijiji 8 vilivyopo ukanda wa ziwa na ambako ni ngome ya CHADEMA matokeo hayajapatikana kutona na usafiri na mawasiliano duni...mpaka sasa CHADEMA imeshinda vijiji8, NCCR8,CUF2...hili ni jimbo ambalo kwa sasa kutoka upinzani linawaniwa na vijana wawili, Afisa Habari wa CHADEMA David Kafulila26, na Mdhamini wa chama, kijana wa kiasia, Muslim Asanary26....kutoka vyama vingine bado hakuna fununu kabisa hasa baada ya ngome ya NCCR iliyopo kata ya Nguruka kuwa nyuma ya David Kafulila..