Uchaguzi wa Magogoni Zanzibar

Status
Not open for further replies.

Kibunango

Platinum Member
Aug 29, 2006
8,419
2,270
Naona macho na masikio ya JF yapo huko Busanda tu, kwa taarifa kesho katika Jimbo la Magogoni kuna uchaguzi wa Mbunge vile vile..

Kampeni za Jimbo la Magogoni Z'bar kuhitimishwa Ijumaa

FAINALI ya kampeni za kunadi wagombea wa nafasi ya uwakilishi wa jimbo la Magogoni kisiwani Unguja itakuwa leo wakati vyama pinzani vya CUF na CCM vitakapofanya mikutano yao ya hadhara kwenye viwanja tofauti kurusha karata zao za mwisho kabla ya upigaji kura utakaofanyika kesho.

CCM, ambao wanatetea kiti hicho, watahitimisha kampeni zao kwa kufanya mkutano kwenye viwanja vya Daraja Bovu, ambako mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama hicho, Dk Ali Mohamed Shein atakuwa mgeni rasmi, wakati CUF itakuwa kwenye viwanja vya Kwa Mabata, ambako makamu mwenyekiti wa chama hicho, Machano Hamisi Machano atakuwa mgeni rasmi.

SAU, chama kingine kilichosimamisha mgombea kwenye uchaguzi huo, kitahitimisha kampeni zake kwenye uwanja wa Diwani.

Asha Mohamed Hilal atakuwa akijaribu kukirejesha kiti hicho CCM baada ya mwakilishi wa jimbo hilo, Daud Hassan Daud kufariki dunia mwaka jana, wakati CUF imemsimamisha Hamad Ali Hamad na SAU imemsimamisha Khamis Msele Omar.

Kampeni hizo za uchaguzi zilizoanza tangu Mei 9 zimekuwa zikitawaliwa na malalamiko na vijembe na jana Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) ulitangaza kuwa vijana watakaowapigia kura wapinzani watakuwa wanasaliti mapinduzi ya mwaka 1964 na uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961.

Naibu katibu mkuu wa UVCCM-Zanzibar, Mohamed Hassan Moyo alitoa kauli hiyo jana wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi mgombea wake, Asha Mohamed Hilal.

Moyo alisema kuwa mapinduzi ya 1964 na juhudi za kuleta uhuru wa 1961 mikakati yake ziliandaliwa na kutekelezwa na kundi la vijana, hivyo ni lazima heshima ya vijana wa ASP na TANU zilindwe na kuthaminiwa na wote.

Alisema itakuwa ni aibu na usaliti dhidi ya juhudi za wanamapinduzi na wapigania uhuru ikiwa kada ya vijana nchini walioelimishwa na kujengeka katika afya bora chini ya Serikali za Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakivipigia kura vyama vya upinzani.

“Vijana wa TANU na ASP hawakuwa na hofu, woga wala usaliti hivyo vijana walio chini ya UV-CCM nao pia wanapita katika nyayo hizo kwa vitendo na ujasiri,” alisema Moyo ambaye ni mtoto wa mwanamapinduzi, Hassan Nassor Moyo.

Naibu katibu mkuu huyo alisema vyama vya upinzani havistahili kupewa ridhaa ya kuongoza kwa sababu ni vyama vya kihuni vinavyohubiri shari na uvunjaji wa amani badala kujijenga kisiasa hadi vijijini.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi limewatahadharisha wapiga kura kuhakikisha amani na utulivu wakati watakapokuwa wakipiga kura kesho kumchagua mwakilishi wa jimbo la Magogoni.

Kamanda wa mkoa wa Mjini Magharib, Bakari Khatib Shaaban alitoa tahadhari hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Zanzibar.

Nayo Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imewataka wananchi wa jimbo hilo waliothibitishwa kuwa ni wapiga kura halali kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi huo.

Taarifa ya tume hiyo ambayo ilisambazwa kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa, tume itahakikisha kila aliyekuwa na haki anapewa nafasi ya kupiga kura katika uchaguzi huo. Taarifa hiyo inaeleza kuwa vituo vitafunguliwa kuanzia saa 12:00 asubuhi na vitafungwa saa 12:00 jioni.

Source: Mwananchi
 
Last edited by a moderator:
Naona macho na masikio ya JF yapo huko Busanda tu, kwa taarifa kesho katika Jimbo la Magogoni kuna uchaguzi wa Mbunge vile vile..

Kampeni za Jimbo la Magogoni Z'bar kuhitimishwa Ijumaa

FAINALI ya kampeni za kunadi wagombea wa nafasi ya uwakilishi wa jimbo la Magogoni kisiwani Unguja itakuwa leo wakati vyama pinzani vya CUF na CCM vitakapofanya mikutano yao ya hadhara kwenye viwanja tofauti kurusha karata zao za mwisho kabla ya upigaji kura utakaofanyika kesho.

CCM, ambao wanatetea kiti hicho, watahitimisha kampeni zao kwa kufanya mkutano kwenye viwanja vya Daraja Bovu, ambako mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama hicho, Dk Ali Mohamed Shein atakuwa mgeni rasmi, wakati CUF itakuwa kwenye viwanja vya Kwa Mabata, ambako makamu mwenyekiti wa chama hicho, Machano Hamisi Machano atakuwa mgeni rasmi.

SAU, chama kingine kilichosimamisha mgombea kwenye uchaguzi huo, kitahitimisha kampeni zake kwenye uwanja wa Diwani.

Asha Mohamed Hilal atakuwa akijaribu kukirejesha kiti hicho CCM baada ya mwakilishi wa jimbo hilo, Daud Hassan Daud kufariki dunia mwaka jana, wakati CUF imemsimamisha Hamad Ali Hamad na SAU imemsimamisha Khamis Msele Omar.

Kampeni hizo za uchaguzi zilizoanza tangu Mei 9 zimekuwa zikitawaliwa na malalamiko na vijembe na jana Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) ulitangaza kuwa vijana watakaowapigia kura wapinzani watakuwa wanasaliti mapinduzi ya mwaka 1964 na uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961.

Naibu katibu mkuu wa UVCCM-Zanzibar, Mohamed Hassan Moyo alitoa kauli hiyo jana wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi mgombea wake, Asha Mohamed Hilal.

Moyo alisema kuwa mapinduzi ya 1964 na juhudi za kuleta uhuru wa 1961 mikakati yake ziliandaliwa na kutekelezwa na kundi la vijana, hivyo ni lazima heshima ya vijana wa ASP na TANU zilindwe na kuthaminiwa na wote.

Alisema itakuwa ni aibu na usaliti dhidi ya juhudi za wanamapinduzi na wapigania uhuru ikiwa kada ya vijana nchini walioelimishwa na kujengeka katika afya bora chini ya Serikali za Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakivipigia kura vyama vya upinzani.

“Vijana wa TANU na ASP hawakuwa na hofu, woga wala usaliti hivyo vijana walio chini ya UV-CCM nao pia wanapita katika nyayo hizo kwa vitendo na ujasiri,” alisema Moyo ambaye ni mtoto wa mwanamapinduzi, Hassan Nassor Moyo.

Naibu katibu mkuu huyo alisema vyama vya upinzani havistahili kupewa ridhaa ya kuongoza kwa sababu ni vyama vya kihuni vinavyohubiri shari na uvunjaji wa amani badala kujijenga kisiasa hadi vijijini.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi limewatahadharisha wapiga kura kuhakikisha amani na utulivu wakati watakapokuwa wakipiga kura kesho kumchagua mwakilishi wa jimbo la Magogoni.

Kamanda wa mkoa wa Mjini Magharib, Bakari Khatib Shaaban alitoa tahadhari hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Zanzibar.

Nayo Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imewataka wananchi wa jimbo hilo waliothibitishwa kuwa ni wapiga kura halali kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi huo.

Taarifa ya tume hiyo ambayo ilisambazwa kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa, tume itahakikisha kila aliyekuwa na haki anapewa nafasi ya kupiga kura katika uchaguzi huo. Taarifa hiyo inaeleza kuwa vituo vitafunguliwa kuanzia saa 12:00 asubuhi na vitafungwa saa 12:00 jioni.

Source: Mwananchi

Mkuu umeweka jina la CHADEMA kuuza thread nini? mbona sioni kokte iliko ongelewa chadema na uhoi wake? Nijuvye mkuu sijakupata kabisa!
 
Mkuu hiyo signature yako ingekuwa inatumika kwenye kampeni za huko Magogoni nadhani chama chako (ambacho hakiko hoi) kingekuwa hoi !!
 
Chadema hawana ubavu huko visiwani, Umaarufu wa Chadema visiwani ulikuwa mkubwa miaka ya tisini, hata hivyo wameshindwa kuuendeleza kiasi cha kushindwa kuweka mgombea katika Jimbo la Magogoni ambalo kwa namna moja ama nyingine lina ufahamu mkubwa katika kutathimini sera za vyama na sio mapenzi ya watu na itikadi zao kwa vyama, hali ambayo ipo kwenye majimbo mengi visiwani humo.

Hii inamaanisha kuwa Chadema pamoja na kuvuma sana huko Bara, ipo hoi bin taabani huko visiwani, tofauti na vyama kama CCM na CUF ambavyo vinatamba Tanzania nzima.
 
Hii inamaanisha kuwa Chadema pamoja na kuvuma sana huko Bara, ipo hoi bin taabani huko visiwani, tofauti na vyama kama CCM na CUF ambavyo vinatamba Tanzania nzima.

chama kinaweza vipi kuwa hoi mahali ambapo hakishindani? CUF ndiyo inaweza kuwa hoi au CCM huko visiwani! ama?
 
Chadema hawana ubavu huko visiwani, Umaarufu wa Chadema visiwani ulikuwa mkubwa miaka ya tisini, hata hivyo wameshindwa kuuendeleza kiasi cha kushindwa kuweka mgombea katika Jimbo la Magogoni ambalo kwa namna moja ama nyingine lina ufahamu mkubwa katika kutathimini sera za vyama na sio mapenzi ya watu na itikadi zao kwa vyama, hali ambayo ipo kwenye majimbo mengi visiwani humo.

Hii inamaanisha kuwa Chadema pamoja na kuvuma sana huko Bara, ipo hoi bin taabani huko visiwani, tofauti na vyama kama CCM na CUF ambavyo vinatamba Tanzania nzima.

Kwikwi.. CUF mnao wabunge wangapi bara wa kuchaguliwa vile...nnnnhh?
 
Chadema haina haja ya kuwa na nguvu sehemu ambayo wakazi wake wote hata hawafikii nusu ya wakazi wa Mwanza.Chadema ikijiimarisha bara inatosha sana
 
Chadema hawana ubavu huko visiwani, Umaarufu wa Chadema visiwani ulikuwa mkubwa miaka ya tisini, hata hivyo wameshindwa kuuendeleza kiasi cha kushindwa kuweka mgombea katika Jimbo la Magogoni ambalo kwa namna moja ama nyingine lina ufahamu mkubwa katika kutathimini sera za vyama na sio mapenzi ya watu na itikadi zao kwa vyama, hali ambayo ipo kwenye majimbo mengi visiwani humo.

Hii inamaanisha kuwa Chadema pamoja na kuvuma sana huko Bara, ipo hoi bin taabani huko visiwani, tofauti na vyama kama CCM na CUF ambavyo vinatamba Tanzania nzima.

Swali kaulizwa GT wewe unajibu!!! Ndio maana michango yako inafananafananana, ama kweli kazi kwelikweli.
 
Mmmhh siku hizi comparison ya maende unaweza kuifanya kwa mchele ( irrelevant comparison) sijui kama utapata unachokusudia; anauza jina la chadema tu huyo hana lolote
 
Mmmhh siku hizi comparison ya maende unaweza kuifanya kwa mchele ( irrelevant comparison) sijui kama utapata unachokusudia; anauza jina la chadema tu huyo hana lolote
Bahati mbaya jina la Chadema haliuziki huko Zenj...!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom