Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Mr James Olle Millya
CCM wanadai kuwa Millya kajitoa kisa alichujwa kugombea EALA.........hiii kauli ya wanamagamba inanifanya niangalie wale ambao kamati kuu ya ccm iliwapitisha........na nikabaini wengi wao ni wazee ambao wamevuruga sekta za umma walizopewa dhamana na sasa wanakwenda EALA kupumzika na kulinda ugali waliopora..........Vigogo wang'ara ubunge Afrika Mashariki........na vijana ambao ccm inaona wanafaa ni wale ambao wazazi wao walishika nyadhifa za juu ndani ya ccm na serikalini..........
Nafasi tatu za bara................uteuzi wa Kimbisa, Murunya na Makongoro una walakini mkubwa..................Kiimbisa alilitafuna sana jiji la Dar, Murunya alitafuna Hifadhi ya Ngorongoro na watajwa hawa wawili walitumia kikamilifu pesa walizopora kwenye taasisi za umma kununua ubunge wa EALA...............na sasa wanaonekena kuwa mashujaa.................naye Makongoro hakuwa na cha kuhonga lakini kwa chama makini hakingeliweza kumpitisha mlevi huyu ambaye maisha yake yote hana mchango wa maana kwenye jamii..................yote haya yamefanyika kwa kuwaachia vijana maumivu..............makali sana.
Nafasi za wanawake mbili zimenyakuliwa na akina Shyrose Bhanji na Angela Kizigha.................amabao umahiri wao hata wa kujieleza unatia shaka na wako wanawake wengineo wasomi na walijieleza vizuri lakini kwa sababu hawana mkate wa kuwahonga wabunge wa ccm hawakupewa nafasi ya kwenda kutuwakilisha................
Waliofanya uteuzi mzuri ni NCCR-MAGEUZI pekee yao.....................na Bi. Dr. Nderakindo Perpetua Kessy ana upeo wa kuwazidi wateuliwa wote saba wa ccm na huyo ndiye ninamtarajia kung'ara kwenye bunge la EALA..............na Chadema mikakati yao ilikuwa aibu tupu........na inanipa wasiwasi wa ya kuwa kama hawatajirekebisha na kuajiri wataalamu wa kuwashauri vizuri basi wataanza kupoteza mwelekeo.........mgombea wao alikuwa dhaifu na sielewi kwa nini hawakuwa na majina mengine katika nafasi nyinginezo..........
Ushauri kwa vijana.
Kura zenu msizipoteze na kuwapa ccm kwa sababu hicho ni chama cha wazee hususani wastaafu na vijana ambao wazazi wao walikwishaula ndani ya hicho chama..........
Kura zenu pelekeni vyama vya upinzani na kuhakikisha kiburi cha ccm kinafikia ukomo uchaguzi wa 2015 kwa kunyang'anywa Uraisi na uwingi wao Bungeni...........bila ya kufanya maamuzi haya magumu mtaendelea kuwasindikiza wachovu kwenda kukata kidali yao ya dhuluma tu.............
Bunge la 2015 litusaidie kurekebisha utaratibu wa kuwateua wabunge wa EAC kwa kuwarudishia raia waifanye kazi hii moja kwa moja..............wabunge wa Bunge la Muungano kazi hii hawaiwezi zaidi ya kuitumia kuwajaza maswahiba wao ambao wanawahonga au wanaweza kuwatumia kufanikisha miradi yao ya kisiasa........