UKIONA kwa mwenzio kunaungua ujue kwako kunateketea. Hiyo ni kauli iliyodhihiri jana baada ya uchaguzi wa wabunge wa viti maalumu wa Chadema, kufutwa baada ya kutokea vurugu zilizohusisha utoaji wa rushwa na upendeleo kwa baadhi ya wagombea.
Uchaguzi huo ambao ulikuwa ufanyike juzi, ulisitishwa usiku wa kuamkia jana baada ya wajumbe zaidi ya 25 wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), kuzuiwa kupiga kura kwa madai kuwa walikuwa wanatoka mikoa na wilaya mpya zilizotangazwa hivi karibuni.
Aidha, vurugu hizo zinadaiwa kusababisha madhara zaidi baada ya mjumbe mjamzito kujifungulia njiani na mwingine mimba kuharibika.
Mjumbe anayedaiwa kujifungulia njiani, alikuwa akitoka Kigoma kwenda katika uchaguzi huo na alijifungua baada ya kushtuka kutokana na kusikia kutokea kwa vurugu hizo.
Mwingine ni mjumbe kutoka Pemba ambaye alikuwa ukumbini katika Viwanja vya maonesho ya biashara Sabasaba, Dar es Salaam ambapo inadaiwa ujauzito wake uliharibika alipotolewa nje ya mkutano na kuzuiwa kushiriki kuchagua wabunge, jambo lililosababisha
kukimbizwa katika zahanati moja jijini Dar es Salaam.
Kutokana na vurugu hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alifika saa 2.15 usiku eneo la tukio kwa lengo la kusimamia uchaguzi ndipo alipogundua kuwapo kasoro hizo.
Ilidaiwa kuwa wajumbe waliohesabiwa walikuwa 182 huku idadi iliyokuwa ikitakiwa ikiwa ni wajumbe 139, jambo lililosababisha vurugu baada ya baadhi yao kuanza kutolewa katika ukumbi wa mkutano.
Karatasi zilianza kugawiwa kwa wajumbe saa 3.15 usiku na baadhi ya wajumbe kukosa na waliotolewa nje kulazimisha kuingia jambo lililosababisha Kabwe aingilie kati ili haki itendeke.
Hata hivyo Zitto alikiri kuwapo matatizo na kuwaarifu wagombea kuwa uchaguzi hauwezi kuendelea hadi atakaposikiliza wanachama wake.
Baada ya vurugu za juzi, mkutano huo ulihamishiwa Mbezi Beach katika ukumbi wa Kiramuu, ambako hadi jana jioni wajumbe walikuwa hawajaanza kupiga kura kutokana na wasimamizi wa uchaguzi huo kuhudhuria kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.
Ilipofika jioni, wajumbe hao wa Kamati Kuu waliwasili mkutanoni akiwamo Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe na waandishi wa habari kutakiwa kutoka nje ya mkutano ili kutoa nafasi ya kujadili mambo yao kwa siri.
Mwandishi wa habari hizi, alilazimika kuzungumza na wajumbe waliokuwa wakienda msalani na kupata habari kuwa mkutano huo umefutwa na Mbowe.
Wajumbe hao walidai kuwa Mbowe alituhumu kuwa uchaguzi huo ulinuka rushwa. Hata hivyo, baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa moja usiku jana, Mbowe alitoka na hakutaka kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu kilichokuwa kikijadiliwa.
Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk. Kitila Mkumbo, alikiri kuvunjwa kwa mkutano huo na kuongeza kuwa hatima ya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu itajadiliwa kesho katika kikao cha Kamati Kuu na Baraza Kuu la Chadema na katika Mkutano Mkuu keshokutwa.
Aidha wajumbe wote ambao si wa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, walitakiwa kurudi majumbani kwa kuwa mkutano wa Bawacha hautafanyika tena wala hautakuwa na nguvu ya kuchagua wabunge wa viti maalumu.
Habari zilizopatikana baadaye jana kutoka miongoni mwa wajumbe wa mkutano wa Bawacha, zilisema kuna watu wanaopendelewa na viongozi wa kitaifa na hali yao ya kukubalika ni mbaya na ndiyo maana ya kufuta uchaguzi huo ili kupanga jinsi ya kuwabeba.
Hii ni mara ya pili kwa Chadema kuahirisha mikutano ya Bawacha na ya vijana - Bavicha, ambapo mwaka jana, kulitokea mvutano kati ya kambi za Mbowe na Zitto na hivyo uchaguzi kuahirishwa.
Source: HabariLeo | Chadema hakieleweki
Uchaguzi huo ambao ulikuwa ufanyike juzi, ulisitishwa usiku wa kuamkia jana baada ya wajumbe zaidi ya 25 wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), kuzuiwa kupiga kura kwa madai kuwa walikuwa wanatoka mikoa na wilaya mpya zilizotangazwa hivi karibuni.
Aidha, vurugu hizo zinadaiwa kusababisha madhara zaidi baada ya mjumbe mjamzito kujifungulia njiani na mwingine mimba kuharibika.
Mjumbe anayedaiwa kujifungulia njiani, alikuwa akitoka Kigoma kwenda katika uchaguzi huo na alijifungua baada ya kushtuka kutokana na kusikia kutokea kwa vurugu hizo.
Mwingine ni mjumbe kutoka Pemba ambaye alikuwa ukumbini katika Viwanja vya maonesho ya biashara Sabasaba, Dar es Salaam ambapo inadaiwa ujauzito wake uliharibika alipotolewa nje ya mkutano na kuzuiwa kushiriki kuchagua wabunge, jambo lililosababisha
kukimbizwa katika zahanati moja jijini Dar es Salaam.
Kutokana na vurugu hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alifika saa 2.15 usiku eneo la tukio kwa lengo la kusimamia uchaguzi ndipo alipogundua kuwapo kasoro hizo.
Ilidaiwa kuwa wajumbe waliohesabiwa walikuwa 182 huku idadi iliyokuwa ikitakiwa ikiwa ni wajumbe 139, jambo lililosababisha vurugu baada ya baadhi yao kuanza kutolewa katika ukumbi wa mkutano.
Karatasi zilianza kugawiwa kwa wajumbe saa 3.15 usiku na baadhi ya wajumbe kukosa na waliotolewa nje kulazimisha kuingia jambo lililosababisha Kabwe aingilie kati ili haki itendeke.
Hata hivyo Zitto alikiri kuwapo matatizo na kuwaarifu wagombea kuwa uchaguzi hauwezi kuendelea hadi atakaposikiliza wanachama wake.
Baada ya vurugu za juzi, mkutano huo ulihamishiwa Mbezi Beach katika ukumbi wa Kiramuu, ambako hadi jana jioni wajumbe walikuwa hawajaanza kupiga kura kutokana na wasimamizi wa uchaguzi huo kuhudhuria kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.
Ilipofika jioni, wajumbe hao wa Kamati Kuu waliwasili mkutanoni akiwamo Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe na waandishi wa habari kutakiwa kutoka nje ya mkutano ili kutoa nafasi ya kujadili mambo yao kwa siri.
Mwandishi wa habari hizi, alilazimika kuzungumza na wajumbe waliokuwa wakienda msalani na kupata habari kuwa mkutano huo umefutwa na Mbowe.
Wajumbe hao walidai kuwa Mbowe alituhumu kuwa uchaguzi huo ulinuka rushwa. Hata hivyo, baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa moja usiku jana, Mbowe alitoka na hakutaka kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu kilichokuwa kikijadiliwa.
Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk. Kitila Mkumbo, alikiri kuvunjwa kwa mkutano huo na kuongeza kuwa hatima ya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu itajadiliwa kesho katika kikao cha Kamati Kuu na Baraza Kuu la Chadema na katika Mkutano Mkuu keshokutwa.
Aidha wajumbe wote ambao si wa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, walitakiwa kurudi majumbani kwa kuwa mkutano wa Bawacha hautafanyika tena wala hautakuwa na nguvu ya kuchagua wabunge wa viti maalumu.
Habari zilizopatikana baadaye jana kutoka miongoni mwa wajumbe wa mkutano wa Bawacha, zilisema kuna watu wanaopendelewa na viongozi wa kitaifa na hali yao ya kukubalika ni mbaya na ndiyo maana ya kufuta uchaguzi huo ili kupanga jinsi ya kuwabeba.
Hii ni mara ya pili kwa Chadema kuahirisha mikutano ya Bawacha na ya vijana - Bavicha, ambapo mwaka jana, kulitokea mvutano kati ya kambi za Mbowe na Zitto na hivyo uchaguzi kuahirishwa.
Source: HabariLeo | Chadema hakieleweki