Elections 2010 Uchaguzi Viti Maalum Chadema Wakwama

Masonjo

JF-Expert Member
Aug 8, 2010
2,724
1,116
UKIONA kwa mwenzio kunaungua ujue kwako kunateketea. Hiyo ni kauli iliyodhihiri jana baada ya uchaguzi wa wabunge wa viti maalumu wa Chadema, kufutwa baada ya kutokea vurugu zilizohusisha utoaji wa rushwa na upendeleo kwa baadhi ya wagombea.

Uchaguzi huo ambao ulikuwa ufanyike juzi, ulisitishwa usiku wa kuamkia jana baada ya wajumbe zaidi ya 25 wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), kuzuiwa kupiga kura kwa madai kuwa walikuwa wanatoka mikoa na wilaya mpya zilizotangazwa hivi karibuni.

Aidha, vurugu hizo zinadaiwa kusababisha madhara zaidi baada ya mjumbe mjamzito kujifungulia njiani na mwingine mimba kuharibika.

Mjumbe anayedaiwa kujifungulia njiani, alikuwa akitoka Kigoma kwenda katika uchaguzi huo na alijifungua baada ya kushtuka kutokana na kusikia kutokea kwa vurugu hizo.

Mwingine ni mjumbe kutoka Pemba ambaye alikuwa ukumbini katika Viwanja vya maonesho ya biashara Sabasaba, Dar es Salaam ambapo inadaiwa ujauzito wake uliharibika alipotolewa nje ya mkutano na kuzuiwa kushiriki kuchagua wabunge, jambo lililosababisha
kukimbizwa katika zahanati moja jijini Dar es Salaam.

Kutokana na vurugu hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alifika saa 2.15 usiku eneo la tukio kwa lengo la kusimamia uchaguzi ndipo alipogundua kuwapo kasoro hizo.

Ilidaiwa kuwa wajumbe waliohesabiwa walikuwa 182 huku idadi iliyokuwa ikitakiwa ikiwa ni wajumbe 139, jambo lililosababisha vurugu baada ya baadhi yao kuanza kutolewa katika ukumbi wa mkutano.

Karatasi zilianza kugawiwa kwa wajumbe saa 3.15 usiku na baadhi ya wajumbe kukosa na waliotolewa nje kulazimisha kuingia jambo lililosababisha Kabwe aingilie kati ili haki itendeke.

Hata hivyo Zitto alikiri kuwapo matatizo na kuwaarifu wagombea kuwa uchaguzi hauwezi kuendelea hadi atakaposikiliza wanachama wake.

Baada ya vurugu za juzi, mkutano huo ulihamishiwa Mbezi Beach katika ukumbi wa Kiramuu, ambako hadi jana jioni wajumbe walikuwa hawajaanza kupiga kura kutokana na wasimamizi wa uchaguzi huo kuhudhuria kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.

Ilipofika jioni, wajumbe hao wa Kamati Kuu waliwasili mkutanoni akiwamo Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe na waandishi wa habari kutakiwa kutoka nje ya mkutano ili kutoa nafasi ya kujadili mambo yao kwa siri.

Mwandishi wa habari hizi, alilazimika kuzungumza na wajumbe waliokuwa wakienda msalani na kupata habari kuwa mkutano huo umefutwa na Mbowe.

Wajumbe hao walidai kuwa Mbowe alituhumu kuwa uchaguzi huo ulinuka rushwa. Hata hivyo, baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa moja usiku jana, Mbowe alitoka na hakutaka kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu kilichokuwa kikijadiliwa.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk. Kitila Mkumbo, alikiri kuvunjwa kwa mkutano huo na kuongeza kuwa hatima ya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu itajadiliwa kesho katika kikao cha Kamati Kuu na Baraza Kuu la Chadema na katika Mkutano Mkuu keshokutwa.

Aidha wajumbe wote ambao si wa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, walitakiwa kurudi majumbani kwa kuwa mkutano wa Bawacha hautafanyika tena wala hautakuwa na nguvu ya kuchagua wabunge wa viti maalumu.

Habari zilizopatikana baadaye jana kutoka miongoni mwa wajumbe wa mkutano wa Bawacha, zilisema kuna watu wanaopendelewa na viongozi wa kitaifa na hali yao ya kukubalika ni mbaya na ndiyo maana ya kufuta uchaguzi huo ili kupanga jinsi ya kuwabeba.

Hii ni mara ya pili kwa Chadema kuahirisha mikutano ya Bawacha na ya vijana - Bavicha, ambapo mwaka jana, kulitokea mvutano kati ya kambi za Mbowe na Zitto na hivyo uchaguzi kuahirishwa.

Source: HabariLeo | Chadema hakieleweki
 
Kitila, tuhabarishe bwana. Wewe ndiye uliekuwa unasimamia uchaguzi huu. Kwani wale viti maalum mwaka 2005 mliwapataje? Hatukusikia haya wakati ule.
 
UKIONA kwa mwenzio kunaungua ujue kwako kunateketea. Hiyo ni kauli iliyodhihiri jana baada ya uchaguzi wa wabunge wa viti maalumu wa Chadema, kufutwa baada ya kutokea vurugu zilizohusisha utoaji wa rushwa na upendeleo kwa baadhi ya wagombea.

Uchaguzi huo ambao ulikuwa ufanyike juzi, ulisitishwa usiku wa kuamkia jana baada ya wajumbe zaidi ya 25 wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), kuzuiwa kupiga kura kwa madai kuwa walikuwa wanatoka mikoa na wilaya mpya zilizotangazwa hivi karibuni.

Aidha, vurugu hizo zinadaiwa kusababisha madhara zaidi baada ya mjumbe mjamzito kujifungulia njiani na mwingine mimba kuharibika.

Mjumbe anayedaiwa kujifungulia njiani, alikuwa akitoka Kigoma kwenda katika uchaguzi huo na alijifungua baada ya kushtuka kutokana na kusikia kutokea kwa vurugu hizo.

Mwingine ni mjumbe kutoka Pemba ambaye alikuwa ukumbini katika Viwanja vya maonesho ya biashara Sabasaba, Dar es Salaam ambapo inadaiwa ujauzito wake uliharibika alipotolewa nje ya mkutano na kuzuiwa kushiriki kuchagua wabunge, jambo lililosababisha
kukimbizwa katika zahanati moja jijini Dar es Salaam.

Kutokana na vurugu hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alifika saa 2.15 usiku eneo la tukio kwa lengo la kusimamia uchaguzi ndipo alipogundua kuwapo kasoro hizo.

Ilidaiwa kuwa wajumbe waliohesabiwa walikuwa 182 huku idadi iliyokuwa ikitakiwa ikiwa ni wajumbe 139, jambo lililosababisha vurugu baada ya baadhi yao kuanza kutolewa katika ukumbi wa mkutano.

Karatasi zilianza kugawiwa kwa wajumbe saa 3.15 usiku na baadhi ya wajumbe kukosa na waliotolewa nje kulazimisha kuingia jambo lililosababisha Kabwe aingilie kati ili haki itendeke.

Hata hivyo Zitto alikiri kuwapo matatizo na kuwaarifu wagombea kuwa uchaguzi hauwezi kuendelea hadi atakaposikiliza wanachama wake.

Baada ya vurugu za juzi, mkutano huo ulihamishiwa Mbezi Beach katika ukumbi wa Kiramuu, ambako hadi jana jioni wajumbe walikuwa hawajaanza kupiga kura kutokana na wasimamizi wa uchaguzi huo kuhudhuria kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.

Ilipofika jioni, wajumbe hao wa Kamati Kuu waliwasili mkutanoni akiwamo Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe na waandishi wa habari kutakiwa kutoka nje ya mkutano ili kutoa nafasi ya kujadili mambo yao kwa siri.

Mwandishi wa habari hizi, alilazimika kuzungumza na wajumbe waliokuwa wakienda msalani na kupata habari kuwa mkutano huo umefutwa na Mbowe.

Wajumbe hao walidai kuwa Mbowe alituhumu kuwa uchaguzi huo ulinuka rushwa. Hata hivyo, baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa moja usiku jana, Mbowe alitoka na hakutaka kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu kilichokuwa kikijadiliwa.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk. Kitila Mkumbo, alikiri kuvunjwa kwa mkutano huo na kuongeza kuwa hatima ya uteuzi wa wabunge wa viti maalumu itajadiliwa kesho katika kikao cha Kamati Kuu na Baraza Kuu la Chadema na katika Mkutano Mkuu keshokutwa.

Aidha wajumbe wote ambao si wa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, walitakiwa kurudi majumbani kwa kuwa mkutano wa Bawacha hautafanyika tena wala hautakuwa na nguvu ya kuchagua wabunge wa viti maalumu.

Habari zilizopatikana baadaye jana kutoka miongoni mwa wajumbe wa mkutano wa Bawacha, zilisema kuna watu wanaopendelewa na viongozi wa kitaifa na hali yao ya kukubalika ni mbaya na ndiyo maana ya kufuta uchaguzi huo ili kupanga jinsi ya kuwabeba.

Hii ni mara ya pili kwa Chadema kuahirisha mikutano ya Bawacha na ya vijana - Bavicha, ambapo mwaka jana, kulitokea mvutano kati ya kambi za Mbowe na Zitto na hivyo uchaguzi kuahirishwa.

Source: HabariLeo | Chadema hakieleweki

Hapo kwenye red: WHAT IS THIS MAN ACTUALLY DOING IN CHADEMA? DO CHADEMA PEOPLE REALLY KNOW THE INSIDE OF HIM? ANYWAY, FROM TODAY ONWARDS, I WONT UTTER A SINGLE WORD ON HIM, BUT TIME WILL TELL! KNOWING THE INSIDE OF A MAN IS VERY IMPORTANT, NOT HIS/HER WORDS!
 
Source: HabariLeo....mhariri Michuzi

Na Elizabeth Suleyman

MKUTANO wa kuwachagua wabunge wa viti maalum kwa tiketi ya Chadema jana ulivunjika tena kutokana na maadalizi mabovu na kuibuka kwa mapungufu kadhaa.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk Kitila Mkumbo aliliambia gazeti hili kuwa mapungufu yaliyojitokeza ni kuwa hakukuwepo na muongozo wa uchaguzi wa Chadema."Kukosekana kwa muongozo wa uchaguzi, kulisababisha, wagombea kutofuata maadili ya chama,'' alisema Dk Mkumbo.

Hata hivyo, Dk Mkumbo alisema uamuzi wa jinsi ya kuwapata wabunge wa viti maalumu utategemeana na maamuzi yatakayotolewa na katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa ambaye pia ni mgombea urais, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Katika hatua nyingine, leo Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) linakutana kujadili kiini cha kuvunjika kwa mkutano wa kuchagua wabunge wanawake wa viti maalumu.

Hali haikuwa shwari kwenye uteuzi huo tangu juzi. Siku hiyo, naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe aliahirisha uchaguzi kutokana na kujitokeza malalamiko mengi, ikiwemo baadhi ya wagombea wasio na wajumbe kupewa fursa ya kujipigia kura na wengine kutoruhusiwa.

Sababu nyingine ya kusitishwa kwa uchaguzi huo ni kitendo cha baadhi ya wajumbe zaidi ya 25 kutoka wilaya mpya zilizoanzishwa karibuni kuondolewa ukumbini na hivyo kunyimwa fursa ya kupiga kura, kuibuka kwa mamluki pamoja na makundi ambayo yanaonekana yanatokana na tofauti za viongozi wa ngazi za juu.

Uamuzi wa kuvunjwa kwa mkutano huo kuliwafanya baadhi ya wagombea kuingiwa hofu ya kuhisi kuwa huenda kamati kuu ya Chadema inaweza kuteua wagombea inaowataka na kuacha wengine wenye sifa.

Zitto alifafanua kuwa wameamua kusitisha mchakato huo na kwamba kamati kuu ya Chadema pamoja na viongozi wa Bawacha itakutana na kutoa maamuzi ya kurudiwa kwa uchaguzi na kwamba uko uwezekana wa kufanya uchaguzi leo. Aliongeza kuwa malalamiko ya kupungua kwa karatasi za uchaguzi, ni jambo ambalo halipaswi kujitokeza tena na kwamba ni vyema likafanyiwa marekebisho mapema.

"Isije ikaonekana Chadema ni chama ambacho hakina demokrasia ya kweli ya kuwajali wanachama wake," alisema Zitto. "Hatuwezi kuwaacha wajumbe waliotoka mikoani kwenye wilaya hizo mpya wasipige kura na pia wagombea ambao wasiokuwa na wajumbea walioruhusiwa kukaa ndani kupiga kura wapige na wengine wenye wajumbe kufungiwa nje," alisema. "Haitakuwa picha nzuri, kwani tutakuwa tunawanyima haki yao ya msingi ya kupiga kura," alisisitiza.

Source: Mwananchi

 
Na Elizabeth Suleyman

MKUTANO wa kuwachagua wabunge wa viti maalum kwa tiketi ya Chadema jana ulivunjika tena kutokana na maadalizi mabovu na kuibuka kwa mapungufu kadhaa.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk Kitila Mkumbo aliliambia gazeti hili kuwa mapungufu yaliyojitokeza ni kuwa hakukuwepo na muongozo wa uchaguzi wa Chadema."Kukosekana kwa muongozo wa uchaguzi, kulisababisha, wagombea kutofuata maadili ya chama,'' alisema Dk Mkumbo.

Hata hivyo, Dk Mkumbo alisema uamuzi wa jinsi ya kuwapata wabunge wa viti maalumu utategemeana na maamuzi yatakayotolewa na katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa ambaye pia ni mgombea urais, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Katika hatua nyingine, leo Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) linakutana kujadili kiini cha kuvunjika kwa mkutano wa kuchagua wabunge wanawake wa viti maalumu.

Hali haikuwa shwari kwenye uteuzi huo tangu juzi. Siku hiyo, naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe aliahirisha uchaguzi kutokana na kujitokeza malalamiko mengi, ikiwemo baadhi ya wagombea wasio na wajumbe kupewa fursa ya kujipigia kura na wengine kutoruhusiwa.

Sababu nyingine ya kusitishwa kwa uchaguzi huo ni kitendo cha baadhi ya wajumbe zaidi ya 25 kutoka wilaya mpya zilizoanzishwa karibuni kuondolewa ukumbini na hivyo kunyimwa fursa ya kupiga kura, kuibuka kwa mamluki pamoja na makundi ambayo yanaonekana yanatokana na tofauti za viongozi wa ngazi za juu.

Uamuzi wa kuvunjwa kwa mkutano huo kuliwafanya baadhi ya wagombea kuingiwa hofu ya kuhisi kuwa huenda kamati kuu ya Chadema inaweza kuteua wagombea inaowataka na kuacha wengine wenye sifa.

Zitto alifafanua kuwa wameamua kusitisha mchakato huo na kwamba kamati kuu ya Chadema pamoja na viongozi wa Bawacha itakutana na kutoa maamuzi ya kurudiwa kwa uchaguzi na kwamba uko uwezekana wa kufanya uchaguzi leo. Aliongeza kuwa malalamiko ya kupungua kwa karatasi za uchaguzi, ni jambo ambalo halipaswi kujitokeza tena na kwamba ni vyema likafanyiwa marekebisho mapema.

"Isije ikaonekana Chadema ni chama ambacho hakina demokrasia ya kweli ya kuwajali wanachama wake," alisema Zitto. "Hatuwezi kuwaacha wajumbe waliotoka mikoani kwenye wilaya hizo mpya wasipige kura na pia wagombea ambao wasiokuwa na wajumbea walioruhusiwa kukaa ndani kupiga kura wapige na wengine wenye wajumbe kufungiwa nje," alisema. "Haitakuwa picha nzuri, kwani tutakuwa tunawanyima haki yao ya msingi ya kupiga kura," alisisitiza.

Source: Mwananchi



Mhamasishaji Mkuu: ROSTAM A..
 
Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk Kitila Mkumbo aliliambia gazeti hili kuwa mapungufu yaliyojitokeza ni kuwa hakukuwepo na muongozo wa uchaguzi wa Chadema."Kukosekana kwa muongozo wa uchaguzi, kulisababisha, wagombea kutofuata maadili ya chama,'' alisema Dk Mkumbo.

Hata hivyo, Dk Mkumbo alisema uamuzi wa jinsi ya kuwapata wabunge wa viti maalumu utategemeana na maamuzi yatakayotolewa na katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa ambaye pia ni mgombea urais, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Katika hatua nyingine, leo Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) linakutana kujadili kiini cha kuvunjika kwa mkutano wa kuchagua wabunge wanawake wa viti maalumu.

Hali haikuwa shwari kwenye uteuzi huo tangu juzi. Siku hiyo, naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe aliahirisha uchaguzi kutokana na kujitokeza malalamiko mengi, ikiwemo baadhi ya wagombea wasio na wajumbe kupewa fursa ya kujipigia kura na wengine kutoruhusiwa.

Sababu nyingine ya kusitishwa kwa uchaguzi huo ni kitendo cha baadhi ya wajumbe zaidi ya 25 kutoka wilaya mpya zilizoanzishwa karibuni kuondolewa ukumbini na hivyo kunyimwa fursa ya kupiga kura, kuibuka kwa mamluki pamoja na makundi ambayo yanaonekana yanatokana na tofauti za viongozi wa ngazi za juu.

Uamuzi wa kuvunjwa kwa mkutano huo kuliwafanya baadhi ya wagombea kuingiwa hofu ya kuhisi kuwa huenda kamati kuu ya Chadema inaweza kuteua wagombea inaowataka na kuacha wengine wenye sifa.

Zitto alifafanua kuwa wameamua kusitisha mchakato huo na kwamba kamati kuu ya Chadema pamoja na viongozi wa Bawacha itakutana na kutoa maamuzi ya kurudiwa kwa uchaguzi na kwamba uko uwezekana wa kufanya uchaguzi leo. Aliongeza kuwa malalamiko ya kupungua kwa karatasi za uchaguzi, ni jambo ambalo halipaswi kujitokeza tena na kwamba ni vyema likafanyiwa marekebisho mapema.


OMG.... WTF.... KMA!!!!!

Kitila na wenzako, this is not good aisee, hebu wekeni mambo sawa na muwe organized; chadema sasa ni another level kwahiyo wekeni vitu sawa. Ikibidi ajirini full time people wawafanyie protocol and procedure management na kama mnao watoeni muweke wengine hao wamefeli!! hatujasahau ya kule kusini mlivyotolewa kwenye uchaguzi, fomu imechukuliwa kabla ya confirmation ya mgombea

WE LOOK TO YOU FOR QUALITY, CHANGE NOW!!!
 
Na Elizabeth Suleyman

MKUTANO wa kuwachagua wabunge wa viti maalum kwa tiketi ya Chadema jana ulivunjika tena kutokana na maadalizi mabovu na kuibuka kwa mapungufu kadhaa.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Dk Kitila Mkumbo aliliambia gazeti hili kuwa mapungufu yaliyojitokeza ni kuwa hakukuwepo na muongozo wa uchaguzi wa Chadema."Kukosekana kwa muongozo wa uchaguzi, kulisababisha, wagombea kutofuata maadili ya chama,'' alisema Dk Mkumbo.

Hata hivyo, Dk Mkumbo alisema uamuzi wa jinsi ya kuwapata wabunge wa viti maalumu utategemeana na maamuzi yatakayotolewa na katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa ambaye pia ni mgombea urais, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Katika hatua nyingine, leo Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) linakutana kujadili kiini cha kuvunjika kwa mkutano wa kuchagua wabunge wanawake wa viti maalumu.

Hali haikuwa shwari kwenye uteuzi huo tangu juzi. Siku hiyo, naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe aliahirisha uchaguzi kutokana na kujitokeza malalamiko mengi, ikiwemo baadhi ya wagombea wasio na wajumbe kupewa fursa ya kujipigia kura na wengine kutoruhusiwa.

Sababu nyingine ya kusitishwa kwa uchaguzi huo ni kitendo cha baadhi ya wajumbe zaidi ya 25 kutoka wilaya mpya zilizoanzishwa karibuni kuondolewa ukumbini na hivyo kunyimwa fursa ya kupiga kura, kuibuka kwa mamluki pamoja na makundi ambayo yanaonekana yanatokana na tofauti za viongozi wa ngazi za juu.

Uamuzi wa kuvunjwa kwa mkutano huo kuliwafanya baadhi ya wagombea kuingiwa hofu ya kuhisi kuwa huenda kamati kuu ya Chadema inaweza kuteua wagombea inaowataka na kuacha wengine wenye sifa.

Zitto alifafanua kuwa wameamua kusitisha mchakato huo na kwamba kamati kuu ya Chadema pamoja na viongozi wa Bawacha itakutana na kutoa maamuzi ya kurudiwa kwa uchaguzi na kwamba uko uwezekana wa kufanya uchaguzi leo. Aliongeza kuwa malalamiko ya kupungua kwa karatasi za uchaguzi, ni jambo ambalo halipaswi kujitokeza tena na kwamba ni vyema likafanyiwa marekebisho mapema.

"Isije ikaonekana Chadema ni chama ambacho hakina demokrasia ya kweli ya kuwajali wanachama wake," alisema Zitto. "Hatuwezi kuwaacha wajumbe waliotoka mikoani kwenye wilaya hizo mpya wasipige kura na pia wagombea ambao wasiokuwa na wajumbea walioruhusiwa kukaa ndani kupiga kura wapige na wengine wenye wajumbe kufungiwa nje," alisema. "Haitakuwa picha nzuri, kwani tutakuwa tunawanyima haki yao ya msingi ya kupiga kura," alisisitiza.

Source: Mwananchi


Read the literal contents of both papers and judge your self...my insistance in red
 
mmmh chama hakina muongozo wa namna ya kuchagua wabunge wake? kweli tutafika kwa namna hii?!
 
Kama kulikuwa na ukiukaji wa taratibu sio vibaya kufutwa kwa uchaguzi, lakini ni vizuri uchaguzi urudiwe na wajumbe wote wapate nafasi ya kuchagua na kuchaguliwa kwa haki.

Katu wakulu wa chama wasijichague majina kivyao kama ilivyokuwa 2005.
 
Huyu bundi alikuwepo siku nyingi sana.


......Katika hatua nyingine, mvutano mkubwa umeibuka ndani ya Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.
Mvutano huo umeibuka kutokana na kundi la Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na lile la Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe kutofautiana kuhusu wagombea wa viti maalum.

Wakati kundi la Mbowe linataka wabunge wa sasa wa viti maalum wachaguliwe, wakati kundi la Zitto linataka wateuliwe wapya kutoka maeneo mbalimbali kwa lengo la kusambaza chama.


Uchaguzi wa Viti Maalum Chadema uliingia dosari juzi baada ya baadhi ya wagombea kudaiwa kutoa rushwa ili wachaguliwe.

Tuhuma hizo na nyingine zilisababisha, wasimamizi wa uchaguzi kuvunja uchaguzi huo.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho, zinadai kwamba Mbowe alikemea vikali vitendo vya rushwa ndani ya Chadema kwa wagombea hao.


Miongoni mwa wagombea ambao walionekana kukataliwa ni pamoja na wabunge watatu wa viti maalum waliomaliza muda wao.
 
Mzee msekwa aliposema rushwa haiko CCM tu iko kila mahali alionekana mwehu..nadhani hii ni changamoto kama nilivyokwishachangia suala hilo.......hizo ndio politiks za bongo rushwa ipo na itachukua muda mrefu kuitokomeza...nilisema Miiko na Maadili ya Uongozi ianze kufatwa sasa na kizazi kipya ili kiikomboe nchi.
 
CHADEMA kama wanadhamira ya kweli kupata suluhisho la hili suala wanawake wapige kura kuchagua wawakilishi wao bungeni wanaume msijipe jukumu la kuwachagulia mtu ondokeni kwenye mfumo DUME , mnataka kuonyesha kuwa wanawake wenyewe hawawezi si kweli na si sahihi
 
CHADEMA mumefanya vizuri kualisha uchaguzi ili kutafuta njia bora zaidi ya kupata uwakilishi wa wanawake wekeni mipango mizuri na muitishe uchaguzi haraka iwezekanavyo ili isije ikaleta gumzo lisilo la lazima lakini kwa maamuzi yenu ni ditto
 
kwakweli ktk hili mmetuaibisha,m/kiti kuingilia uchaguzi wa wanawake si umwachie mkeo bac ashughulikie?lazima uende wewe?tumeamini CHADEMA bila uchaga haiwezekani!
 
Kama alivyosema Dr Slaa marupurupu ya wabunge ni makubwa sana, wekeni kanuni mbunge wa CHADEMA atoe 50% ya marupurupu yake kwa ajili ya shughuli za uhai wa chama tuone ni wangapi bado watataka huo ubunge.
 
Back
Top Bottom