Joseph Kabila ni mtaalam wa kuchakachua yule. Huyo Chisekeli aliye tu.
Wana JF,
Nimebahatika kupata matokeo yasiyo rasmi ya awali katika Uchaguzi Mkuu wa DRC.
Hali inaonekana kuwa mbaya kwa Rais Kabila.
Source: RADIO VATICAN.
Date: 30 Novemba 2011
KABILA TSHISEKEDI JIMBO % % Kinshasa 11 74 North Kivu 36 27 South Kivu 27 20 Maniema 48 45 Katanga 42 41 Bas Congo 11 69 Bandundu 27 59 Orientale 39 36 Kasai Occidental 5 89 Kasai Oriental 7 87 Equateur 25 50 JUMLA 25.49 54.27
....Kutokana na halihalisi ya mambo tumelazimika kweka kambi makao makuu ya tume ya uchaguzi kwa kazi moja tu ya kubadili matokeo, nitawaomba niwape habari baada ya kutangazwa matokeo ila kwa wale wana jf mliopo Congo naomba endeleeni kutoa matokeo!
Mambo ni mazito lakini tutafanya kile tulichotumwa vuteni subira!
Na wewe ndo walewale,ulichotumwa na nani?unashiriki kuiba haki za watu?Mambo ni mazito lakini tutafanya kile tulichotumwa vuteni subira!
Sawa mkuu, mie ni mmoja wa waliobishi. Basi nimeamini! endelea kutujuza! hii ndiyo africa.Nipo kinshasa kusimamia uchaguzi hapa kongo! Hali ya usalama ni nzuri na watu wanaendelea kupiga kura bila hofu yoyote!
Nitawajuza kila kitu kitakachoendelea hapa Kongo!!
Updates:
Nipo jimbo la Katanga mida hii watu bado wapo kwenye vituo na upigwaji wa kura unaendele na sijajua saa ngapi utaisha!
Kulikuwa na rabsha za hapa na pale kule kinshasa lakini mungu anasaidia vikosi vya usalama viko imara, binafsi kwa mtazamo wa wapigakura japo kuhesabiwa kura bado taswira nyingi za wakongomani zinatoa ushindi kwa Kabila!
Uwepo wangu huku ni kwa kazi moja tu nayo ni kuhakikisha Joseph Kabila anashinda hiyo ni kwa mujibu wa agizo la magogoni!
Ningewapa picha ila mtanisamehe hii ni kwa mjibu wa taratibu za kazi yangu ya kiusalama japo ninasimu yenye kamera!
Endelea kufuatilia kila hatua ya kumrudisha madarakani kabila!!
UPDATES
Naaam ndugu wanajf niasubuhi kumekucha pilika ni nyingi hapa kongo, hali ya usalama siyo mbaya japo jana mapigano ya ghafla yalizuka na kusababisha watu watano kupoteza maisha kule kinshasa!
Shuguli za kuhesabu kura zinaendelea katika vituo karibu vyote!
Mida ya saa nne na nusu asubuhi za hapa nitalazimika kurudi kinshasa kwa mkutano wa dharura na Kabila! Usi log off jf upate yatakakuwa yameongelewa!
Updates
Jana majira ya saa sita kasoro maafisa usalama toka tz tulikutana mgombea wa upinzani ndugu Etienne Tshisekedi kutaka kujua mtazamo wake kuhusu uchaguzi na matokeo yajayo! Kwa hakika alionyesha kujiamini na akatuahidi kuyapokea matokeo yoyote yale ya haki. Ingawa aliosha kulalamikia dalili za hujuma ambozo ni kweli zipo, hakusema atapinga matokeo.
UPDATES
Mtanisame net inasumbua sana hapa!
Kwa wale wenye kubeza siwashangai kwakuwa nililitarajia hili! Naamini wengi hamjui misheni za kiusalama!
Kuna haja ya kuanzisha mafunzo hapa jf ili kupunguza ubishi usio na maana!
Kutokana na halihalisi ya mambo tumelazimika kweka kambi makao makuu ya tume ya uchaguzi kwa kazi moja tu ya kubadili matokeo, nitawaomba niwape habari baada ya kutangazwa matokeo ila kwa wale wana jf mliopo Congo naomba endeleeni kutoa matokeo!