Uchaguzi CCM: Majonzi yatawala vigogo Zanzibar

bagwell

Senior Member
Sep 19, 2012
113
25
Uchaguzi wa CCM Zanzibar ilifanyika jana huku ukiacha majonzi kwa wanasiasa maarufu, akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Khamis Suleiman Dadi, wakianguka.

Mwanasiasa huyo maarufu katika siasa za Zanzibar aliagushwa na wagombea wenzake katika nafasi ya NEC kupitia Wilaya ya Chake Chake Kisiwani Pemba.

Vigogo wengine walioanguka Wilaya ya Mjini ni aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Mohamoud Thabiti Kombo; Mwakilishi wa Jimbo la Rahaleo, Nassor Salim Ali; Mbunge wa Jango’mbe, Hassan Mussa Mzee; aliyekuwa Mbunge wa Kikwajuni, Paramuk Singa Hogani, na kadawa chama hicho, Baraka Mohamed Shamte.

Wengine katika Wilaya ya Kati Unguja ni aliyekuwa Waziri wa Maji Ujenzi Nishati na Ardhi, Tafana Kassim Mzee na aliyekuwa Mbunge wa Mpendae, Issa Kassim Issa.

Vigogo wengine waliopiga mweleka ni Naibu Waziri wa Afya, Dk. Sira Ubwa Mamboya, ambaye aligombea kupitia Wilaya ya Dimani, wakati Naibu Spika Ali, Abdalla Ali, alianguka kupitia Wilaya ya Mfenesini.

Walioibuka kidedea katika katika Wilaya ya Chake Chake nafasi ya Mwenyekiti ni Kombo Ali Kombo. Wajumbe wa NEC ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza Mohamed Aboud Mohamed; Ali Issa Ali, Seif Shaaban Mohamed, Mbarak Said Rashid, Hamad Bakary Ali na Suleiman Farahan Said.

Wilaya ya Kati nafasi ya uenyekiti aliyeshinda ni Hassan Mrisho Vuai. Wajumbe NEC ni Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati, Ramadhan Abdalla Shaaban; Balozi Ali Karume, Asha Mshimba Jecha, Khalfan Salum Suleiman, Kombo Hassan Juma na Haji Mkema Haji.

Wilaya ya Wete Mwenyekiti ni Kombo Hamad Yussuf na Wajumbe wa NEC ni Maida Hamad Abdalla, Maua Abeid Daftari, Asiya Sharif Omar, Makame Said Juma, na Hamad Faki Juma.

Wilaya ya Amani Mwenyekiti ni Abdi Ali Mzee, Wajumbe wa NEC Vuai Ali Vuai, ambaye pia Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Juma Khamis Haji, Situmai Mohammed Msimbe, Muhamad Amour Chombo, Rashid Ali Juma ambaye ni Mkurugenzi wa Manispaa ya mji wa Zanzibar na Nadra Juma Mohamed.

Wilaya ya mjini Mwenyekiti ni Juma Faki wakati wajumbe wa NEC ni Hamad Yussuf Masauni, Burhani Saadati Haji, Asha Abdalla Juma, Talib Ali Talib, Sufiani Khamis Ramadhani na Omar Jastus Morris.

Wilaya ya Kaskazini A Menyekiti Ali Makame Dilunga na wajumbe wake NEC ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Haji Omar Kheir, Ali Juma Chepe, Ussi Yahya Haji, Ame Mati Wadi, Mussa Ame Silima na Khamis Mohamed Mahamoud.

Wilaya ya Kaskazin B Mwenyekiti ni Hilika Fadhir Khamis na wajumbe ni Abeid Mohamed Khamis, Mtumwa Pea Yssuf, Bahati Ali Abeid, Miraji Khamis Mussa, Abdulhamid Hassan Juma na Bhati Ali Abeid.

Katibu Mwenezi wa CCM Zanzibar, Issa Haji Gavu, alisema matokeo ya uchaguzi wa Wilaya zote 12 za Zanzibar wanatarajia kutangaza leo.
 
mambo ya nchi nyingine ni ya kuyaacha tu. unaweza kusababisha vita bure. napita km ifuatavyo.
 
Back
Top Bottom