X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Ahadi mbalimbali za wagombea urais 2010
Saturday, 09 October 2010 21:34 |
Jakaya Kikwete 1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora 2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini 3.Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga 4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga 5.Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma 6.Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini 7. Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma 8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera 9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera 10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini 11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini 12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera 13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera 14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera 15. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya 16. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera 17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali 18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza 19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza 20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita 21. Kulinda muungano kwa nguvu zote-Pemba 22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro 23.Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini 24.Kujenga bandari Kasanga –Rukwa 25.Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo – Songea 26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya 27. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga 28.Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa 29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro 30. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini 31. Kuboresha barabara za Igunga -Tabora 33.Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu 34. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini 35. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara 36. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma 37. Kulinda haki za walemavu- Makete 38.Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini 39.Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha 40.Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini 41.Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora 42. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini 43.Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma 44.Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga 46.Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini 47.Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, . 48.Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido 49.Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro 50.Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara 51.Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini 52.Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini 53.Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa 54.Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa 55. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa 56. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda 57.kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara 58.kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo ,Iringa 59.ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar 60.Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar 61. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti Maalimu Seif Sharif Hamad 1. Zanzibar kuwa kama Hong Kong – Unguja 2.Kuendeleza mashamba ya Karume- Kibanda maiti 3. Kubadilisha katiba na kuunda katiba mpya ya muungano na Zanzibar- Pemba 4.Kubadilisha mfumo wa uteuzi makamishna wa tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC)- Unguja 5. Kuwaunganisha wazanzibari ili kujenga umoja, udugu na ushirikiano-Pemba 6. Kuwasilisha hoja ya kubadili katiba ya Zanzibar na ya Muungano-Viwanja vya Kibanda Maiti 7. Kuondoa bajeti ya ZEC isiwe chini ya waziri kiongozi na badala yake kuwa inajitegemea yenyewe- Pemba 8. Kuondoa ulazima wa mwenyekiti wa tume kuwa jaji na badala yake awe mtu anayejua sheria-Unguja 9. Serikali kuundwa na vyama vyote vilivyopata ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi- Unguja 10.Kujenga jamii yenye maelewano na umoja -Pemba 11.Kutokochagua kiongozi kwa urafiki bali kwa uwajibikaji na uadilifu -Unguja na pemba 12.Kudhibiti vyombo vya dola vinavyofanya kazi kwa matakwa ya watu binafsi -Kibanda maiti 13.Kukomesha rushwa-Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba 14.Kuhakikisha ununuzi wa zabuni unakuwa wazi na wananchi kuruhusiwa kuhoji kuhusu zabuni-Jimbo la ole Pemba 15.Kuongeza kima cha chini cha mshahara hadi Sh150,000-Mkanyageni Pemba 16.Kubadili vikosi vyote vya usalama na kulipwa mishahara kima cha chini kulipwa Sh180,000-Chakechake Pemba 17.Kubadilisha kikosi cha KMKM kuwa kikosi cha mwambao-Wawi 18.Wazee kupanda daladala bure na wale wasiokuwa na watoto kulelewa bure-Majimbo ya Chakechake 19.Kufuta michango yote ya shule za msingi na sekondari, kila mwanafunzi kuwa na kompyuta na badala ya kuishia darasa la saba sasa kuishia kidato cha sita-Hoteli ya Bwawani 20.Kutoa kitambulisho cha kila Uzanzibari na kufuta cha Mzanzibari mkaazi- Uwanja wa Hospitali ya Mnazi Mmoja 21.Kila mzanzibar kupata pasi ya kusafiria- Hoteli ya bwawani Zanzibar 22.Kuanzisha shirika la ndege Zanzibar -Viwanja vya Kibanda maiti 23.Kupandisha uchumi wa Zanzibar kutoka 6.8 hadi 15 kila mwaka kwa Zanzibar -Unguja 24.Kutoa uhuru zaidi kwa vyombo vya habari pamoja na kusaidia uanzishwaji wa Baraza la Habari Zanzibar-Unguja na Pemba 25. Kuweka hadharani nambari yake ya simu - Viwanja vya Kibanda miti 26. Kubadili sheria ya uwekezwaji-Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar 27.Kila mwanafunzi kuwa na komputa yake-Viwanja vya Kibanda maiti 28.Akiwa rais hata waziri au mkewe atafungwa akiwa ametenda kosa-Viwanja vya Tibirizi Kisiwani Pemba 29.Kujenga bandari ya Mkokoto na Pemba ili kuweka usafiri wa haraka wa boti ziendazo kasi-Tibirizi Kisiwani pemba. Profesa Ibrahim Lipumba 1.Kubadili katiba na kumteua Dk, Mohamed Shein kuwa makamu wa Rais –Unguja 2.Elimu ya bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu -Tanga 3.Kubana matumizi kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri-Tanga 4.Kuunda serikali shirikishi-Mtwara 5.Kusimamia rasilimali –Tanga 6.Kuimarisha miundombinu-Kidongo chekundu 7. Kusimamia na kuboresha afya-Kidongo Chekundu,Dar 8. Kuboresha kilimo, viwanda na uwekezaji-Mtwara 9.Kudhibiti uuzaji wa zao la korosho-Mtwara 10 Mfuko maalumu wa kusomesha walemavu-Tanga Dk Willibrod Slaa 1.Kurudisha pesa za mradi wa Rada-Moshi 2. Kushughulikia suala la taasisi ya kuweka na kuvuna pesa(DECI)-Uwanja wa mashujaa Moshi 3. Kujenga nchi isiyo na ufisadi-Mwanza 4.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar-Ifakara 5.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo –Arusha 6.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais-Mwanza 7.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15-Arusha 8. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho-Kilimanjaro 9. Kutoa huduma bora za afya bure-Mwanza 10. Kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi-Tarime 11.Kufuta walimu wote wa cheti na stashahada shule za sekondari na kuleta walimu walio na shahada –Arusha 12. Kutoa elimu bure kuanzia shule ya awali hadi kidato cha sita -Morogoro 13.Kutoa huduma za afya bure kuanzia kituo cha afya hadi hospitali ya rufaa-Mwanza 14.Kutoa ruzuku taasisi za kidini-Ifakara 16.Kusambaza magari aina ya shangingi kwa jeshi la polisi ili wakamatie wahalifu,badala ya mawaziri kuyatumia-Ifakara Dk Mohammed Shein 1) Kuboresha maisha ya wavuvi-Chakechake Pemba 2) Kusomesha wafanyakazi-Mnazi mmoja 3) Kipaumbele katika elimu -Unguja na Pemba 4) Kipaumbele katika afya-Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba. 5) Kuulinda Muungano- Wawi kisiwani Pemba 6)Kuleta mabadiliko Zanzibar-Pemba na Unguja 7)Kuboresha Bandari ya Zanzibar kwa kuijenga upya-Kibandamaiti 8)Kuboresha Maendeleo Zanzibar- Jimbo la Wete, Pemba 9.Ujenzi wa maktaba kubwa na nzuri Kisiwani Pemba- Mtambwe 10.Kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu Zanzibar- Kijiji cha Kambini Mchangamdogo 11.Kuimarisha miundombinu Kisiwa cha Pemba- Kijiji cha Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba 12.Kuhamasisha wawekezaji kuwekeza Pemba katika miradi mbalimbali-Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba. 13.Ahadi eneo la Micheweni kuwa maeneo huru ya uchumi- Micheweni Kaskakzini Pemba 14. Kumaliza matatizo ya maji mkoani -Mkoani 15.Kujenga Bandari ya kisasa katika eneo la Mpiga Duri Unguja- Mkoani 16.Kuiamrisha makazi bora kwa wazanzibar- Mkoani Imeandaliwa na Hussein Issa |