Uchafu mitaani Dar: Nani alaumiwe?

Mimi hii mada inanipa matatizo kidogo. Naona kama vile inaelekea kule kule kwenye mtazamo wa kuwa waafrika ndivyo walivyo. Hii inaonyeshwa kwenye misemo kama mtu mchafu mchafu tu. Mimi pengine ni naive lakini siamini kama kuna mtu mwenye akili timamu anayependa kuishi katika mazingira kama hayo tuliyoonyeshwa kutoka Mwanza. Kinachotokea ni kukubali hali kwa sababu hakuna njia mbadala iliyoainishwa.

Hii tabia ya kuwalaumu wananchi ni manifestation ya self-hatred ambayo imetutawala kama jamii. Tunawalaumu watu kuwa na taka mbele ya nyumba zao wakati mahali pa kutupia taka hakuna! Mbona Naples ambao ni wazungu suala la taka nao limewashinda?

Tunawasema wananuka vikwapa bila kuangalia mazingira wanayoishi. Joto lenye humidity kiasi cha juu ambacho mtu ni lazima atoke jasho. Tuambiane ukweli hao wazungu wanaoga mara ngapi kwa WIKI? Ingekuwa kwao kama ni kwetu si tungeipata hiyo harufu. Pamoja na kutokuwapa maji ya uhakika watanzania wanaoga mara nyingi kuliko hao wazungu. Watanzania wanatumia mawe kujisugua kuondoa uchafu. Leo, ndugu zangu, mnawakebehi kuwa wananuka vikwapa? Hao wazungu wangekuwa na joto kama letu na wasingekuwa na pafyumu hali ingekuwaje?

Huko katika nchi tunazozionea wivu, ni nani anayewajibika katika masuala ya usafi katika public spaces? Serikali itakayoamka na kumwambia mwananchi kuwa yeye ni wajibu wake kusafisha barabara na kuzibua mitaro haitachukua raundi. Wote tunajua hilo maana wengi wetu tumewahi kuishi huko. Leo huyu mtanzania ambaye anakamuliwa kinachoitwa kodi ya maendeleo na utitiri wa kodi nyingine, bado anatakiwa ahakikishe si nyumbani kwake peke yake bali mazingira ya nje yawe safi bila kuambiwa wapi huo uchafu atakaoukusanya aupeleke. Leo tunasema kuwa tuna haja ya kuwafundisha watu usafi kana kwamba ni kitu kigeni kwao. Nenda kwenye nyumba zao, vyumba vyao uone wanavyojitahidi kuvipamba kwa vitambaa wanavyoshona wenyewe, picha wanazotoa katika magazeti, kalenda n.k. bila kuwa na theluthi ya zana walizokuwa nazo wenzetu.

Mimi bado naamini kuwa inabidi wale walio katika nafasi ya uongozi wawajibike kwanza kwa kuhakikisha kuwa nyenzo, sehemu,mazingira na taratibu zinawekwa za kuhakikisha usafi katika miji yetu. Wawe wabunifu katika kukusanya na kuongeza mapato yatakayowawezesha kutoa huduma kama inavyotakikana. Tuanze kudai wale waliopata uongozi waongoze kweli na wanaposhindwa wawajibike.
 
Chicken has come home to roost!

Naomba nitumie hii nukuu kutoka kwa Michuzi. Hivi tutamlaumu nani? Mwenye nyumba, diwani, katibu kata, meya, halmashauri, mbunge, DC, mkuu wa mkoa Waziri wa afya, Nyumba, Tamisemi, Mazingira, miundombinu, Waziri Mkuu au Raisi?

Hivi tukipata mlipuko wa kipindupindu tutapona?

http://issamichuzi.blogspot.com/2008/03/mjadala-pepe.html

Mwenye utaalamu wa kuweka picha hii ya maji machafu mtaani Mwananyamala baada ya mvua naomba aiweke hapa ukumbini!

240308terffo5.jpg


Wa-kulaumiwa ni serikali itakubali vipi raia wake waishi katika mazingira machafu kama haya wakati wanalipa kodi?
 
Nionavyo mimi wa kulaumu ni Madiwani na Halmashauri yao pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri hizo ambao ndiyo watendaji wakuu. Kwa mkoa wa DSM Mkuu wa Mkoa na Madc wa wilaya zote tatu wamekuwa wanasema na kukemea lakini wapi. Hizi Halmashauri zina kiburi sana kwa sababu wanalelewa na TAMISEMI. Ukiangalia muundo wao ni wa kulindana na kuneemeshana. Ni Hatari kubwa. Hebu tusubiri ripoti kuhusu bomoa bomoa ya Tabata kama kuna lolote la maana litafanyika.

Suala la uchafu linatakiwa lishughulikiwe katika ngazi ya mtaa. Lakini again ukiangalia size ya mitaa utagundua ni mikubwa mno. Kwa hiyo the best system that can work ni ya nyumba kumi. Kwa sababu usafi ungefanywa na wakazi wa kila barabara au street inayohusika.
 
Taifa la watu waliozoea uchafu, ni taifa la watu wachafu hata kama wananukia manukato

Mkuu MMJ,

Very strong quote, I like it! Nina wasi wasi kuwa ustaarabu wa uchafu tumeurithi toka kwa wahindi au waarabu, maana ukienda huko hutaaamini utakayoyaona kuhusu uchafu, pamoja na kwamba hali yao ya hewa sio kama yetu, kisiasa matatizo mengi ya taifa huanzia majumbani mwa wananchi wa lile taifa, kama taifa letu ni chafu, basi sisi wananchi ni wachafu tenma zaidi ya taifa, hakuna way out au around it!
 
Mkuu MMJ,

Very strong quote, I like it! Nina wasi wasi kuwa ustaarabu wa uchafu tumeurithi toka kwa wahindi au waarabu, maana ukienda huko hutaaamini utakayoyaona kuhusu uchafu, pamoja na kwamba hali yao ya hewa sio kama yetu, kisiasa matatizo mengi ya taifa huanzia majumbani mwa wananchi wa lile taifa, kama taifa letu ni chafu, basi sisi wananchi ni wachafu tenma zaidi ya taifa, hakuna way out au around it!

great point mzee, lakini siamini kwamba haya matatizo tumeyarithi, ni kwamba hivyo ndivyo watanzania tulivyo ! na usafi/uchafu has no excuse ! Everyone should bare the blame !
 
great point mzee, lakini siamini kwamba haya matatizo tumeyarithi, ni kwamba hivyo ndivyo watanzania tulivyo ! na usafi/uchafu has no excuse ! Everyone should bare the blame !

Kuna siku Mwl. Augustine Moshi aliandika hapa kuhusu safari yake ya Nigeria....alisema amewahi kushuhudia Wapopo wakijisaidia nje nje kwenye mabarabara yao bila aibu!! Kwa hiyo mimi nadhani si tu Watanzania Ndivyo Tulivyo bali ni Waafrika Ndivyo Tulivyo!!
 
Jamani uchafu tumejitengenezea wenyewe:
  • Ukiritimba wa kutoa viwanja vilivyopimwa
  • Rushwa
  • Ongezeko la wahamiaji mijini

Katika ukiritimba wa upimaji na utoaji wa viwanja kumesababisha wengi kuvamia maeneo na kuanza kujenga pasipo kusubiri serikali. Hali hii imesababisha ujenzi holela ambapo maeneo hayo kukosa miundo mbinu.

Rushwa, katika asasi za ardhi na upimaji(mipango)zimeweza kupangua mipango ya miji kwa kuweza kutoa viwanja katika maeneo ambayo yalitengwa kwa shughuli zingine... Tunakumbuka vilipoanza vioski ambavyo vingi vilijengwa mita chache toka barabarani, zaidi vilichangia kiasi kikubwa katika kuchafua miji kutokana na taka walizokuwa wakizalisha kukosa kuchukuliwa. Vilevile vingine vilijengwa katika secondary road hivyo kukosesha huduma za ukusanyaji wa taka katika maeneo ya ndani zaidi ya vitongoji.

Ongezeko la wahamiaji:
Miji yote mikubwa ina tatizo hili. Lakini ukiritimba wa halmashauri zetu, uchache wa vifaa na uchache wa watendaji kulinganisha na idadi ya mahitaji ya viwanja kumesababisha ujenzi holela.

Ujenzi holela kwa kiasi kikubwa umechangia kuchafua mazingira ya halmashauri nyingi za miji yetu. Hii inatokana na serikali kwanza kushindwa kutambua maeneo hayo na hivyo kupeleka huduma muhimu.

Ni vema sasa serikali kuweza kutambua informal settlement na kuanza kutafuta namna ya kuweza kuondoa matatizo ya maji taka, na taka ngumu katika maeneo hayo. Kuvunja nyumba zao sio suluhu uwapo bado serikali hiyohiyo haina maeneo yaliyopimwa kukidhi mahitaji ya wananchi.

Ipo mifano mingi ya informal settlement ambayo imeweza kwa namna moja kupunguza matatizo ya uchafu wa mazingira yao. Kwa Dar es Salaamu kitongoji cha Hanna Nassif Kinondoni ni mfano mzuri katika namna ya kuondoa ama kupunguza uchavuzi wa mazingira. Kule Zenj katika kitongoji cha Maili Nne na Mtaa wa Jang'ombe ni vielelezo tosha kwa namna gani wananchi wanaweza kuondoa matatizo yao usafi pale tu serikali inapoweza kutambua informal settlement.

Iringa kuna mifano mingi zaidi na asasi ya ISP ishukuliwe kwa kuweza kuwabana serikali na kuweza kuchangia katika kuweka miundo mbinu katika maeneo yaliyovamiwa.
 
`Most Dar houses direct sewage into rivers, ocean during rains`

2008-04-01 08:59:59
By Angel Navuri


Most residential houses in Dar es Salaam reportedly drain their sewage to rivers and streams that lead to the ocean during the rainy season due to lack of main chambers, `The Guardian` has learnt.

A week-long survey carried out in various parts of the city, including Sinza, Kinondoni, Manzese, Mbezi Beach and Buguruni has shown that a large per cent of city dwellers drain sewage from their houses through small chambers, something which experts say is not technically advisable.

In an interview, Omar Hassan, a resident of Manzese admitted that most houses lack main chambers for sewage disposals, and are reluctant to pay for hired draining facilities.

``As a way of avoiding the cost of draining the facilities, these people have developed a disposing off sewage during the rain season,`` he said.

People who have constructed main sewage chambers, according to Hassan, are also involved in draining wastes during the rain season, he added.

Mariam Mhina, who resides at Mbezi Beach explained that landlords who build main chambers, but do not drain sewage through the system, but wait until the rain season to flush them.

observers say this careless diposal of sewage could be the main cause of diseases such as cholera and diahrea.

``House owners are not ready to incur costs of draining the chamber it is because of this that they do it during rain seasons, causing environmental pollution and other related problems,`` said Mhina.

Buguruni resident, Mohamed Saidi, blamed the Dar es Salaam City Council and the Ministry of Lands and Housing Settlements for the unplanned construction and the eventual sub standards structures in Dar es Salaam.

The survey has also extablished that it has always been a problem to control those who liter the city environs through this form of sewage disposal.

Tomson Msangi from Kinondoni told this paper that thorough and weekly-inspections by public health officers of the environs was crucial to enable people live in tidy circumstances.

``At the moment, public health officers are not doing their work. That`s why the problem has been going on unabated,`` he said.

Responding to this state of affair, Health and Social Welfare deputy minister Aisha Kigoda explained that serious measures would be taken against people found draining sewages during the rain season.

Kigoda explained that the government was aware of the problem but was waiting for amendment of the Public Health Act 2007, expected to incorporate related issues.

SOURCE: Guardian

Hivi hii Chamber wanazozungumzia ni zipi? Na zinatakiwa kuwa drained vipi? Maana inaelekea zinakusanya sewage mpaka mvua zinapokuja ndio wanapoziachia!
 
Ni chamber baada ya septic tank,(note sio seepage tank) ambayo mara nyingi huwa na maji tu without sludge..
 
Ni chamber baada ya septic tank,(note sio seepage tank) ambayo mara nyingi huwa na maji tu without sludge..

Itakuwa ni Soak Pit? Au ni tanki tu la kukusanya yatokayo kwenye septic tank bila kuyaruhusu yasambae kwenye udongo? Soak pit bila weep holes!
 
Itakuwa ni Soak Pit? Au ni tanki tu la kukusanya yatokayo kwenye septic tank bila kuyaruhusu yasambae kwenye udongo? Soak pit bila weep holes!

Sawa sawa...!

Huku kwetu watu hupenda kuita chamber... naona hata waandishi wa habari wameingia kwenye mkumbo huo.
 
In an interview, Omar Hassan, a resident of Manzese admitted that most houses lack main chambers for sewage disposals, and are reluctant to pay for hired draining facilities.
DSC00673.JPG
 
Wana Jf Kwa Kweli Hali Ya Usafi Katika Miji Yetu Inatisha. Miji Imejaa Takataka Kila Sehemu. Mifuko Ya Plastic Imezagaa, Karatasi Zimetupwa Ovyo, Watu Wanadiliki Kula Vitu Kama Ndizi Mbivu, Miwa, Mahindi Yaliyopikwa Au Kuchomwa Na Kutupwa Ovyo Bila Kujali Usafi, nimeona hata wengine wakila pipi na kutupa vijikarasi vyake ovyo, wengine ununua hata karanga na kutupa vijigazeti vilivyofungia karanga hizo. Miji Mingi Haina Vifaa Vya Kuwekwa Takataka Hivyo Kila Mtu Utupa Taka Taka Popote Alipo. Watu Hawaoni Tena Kama Kuna Sababu Ya Kujali Usafi Wa Miji Yetu. Miji Mingi Haifagiliwi Na Ile Inayofagiliwa Hii Ufanyika Mchana Na Kuleta Usumbufu Kwa Wapita Njia. Kuna mji ambao nilikuta maji taka yakiachiwa kutiririka katika barabara na katika mitaa na makazi ya watu. Je Usafi Wa Miji Yetu Tanzania Inahitaji Pesa Za Kigeni? Halmashauri Za Miji, Manispaa Za Miji Pia, Na Hata Majiji Mwafanya Nini Kama Uchafu Umesambaa Kila Mahali? Tufanye Nini Ili Tutunze Usafi Wa Miji Yetu? Hili Linanikera
 
Wana Jf Kwa Kweli Hali Ya Usafi Katika Miji Yetu Inatisha. Miji Imejaa Takataka Kila Sehemu. Mifuko Ya Plastic Imezagaa, Karatasi Zimetupwa Ovyo, Watu Wanadiliki Kula Vitu Kama Ndizi Mbivu, Miwa, Mahindi Yaliyopikwa Au Kuchomwa Na Kutupwa Ovyo Bila Kujali Usafi, nimeona hata wengine wakila pipi na kutupa vijikarasi vyake ovyo, wengine ununua hata karanga na kutupa vijigazeti vilivyofungia karanga hizo. Miji Mingi Haina Vifaa Vya Kuwekwa Takataka Hivyo Kila Mtu Utupa Taka Taka Popote Alipo. Watu Hawaoni Tena Kama Kuna Sababu Ya Kujali Usafi Wa Miji Yetu. Miji Mingi Haifagiliwi Na Ile Inayofagiliwa Hii Ufanyika Mchana Na Kuleta Usumbufu Kwa Wapita Njia. Kuna mji ambao nilikuta maji taka yakiachiwa kutiririka katika barabara na katika mitaa na makazi ya watu. Je Usafi Wa Miji Yetu Tanzania Inahitaji Pesa Za Kigeni? Halmashauri Za Miji, Manispaa Za Miji Pia, Na Hata Majiji Mwafanya Nini Kama Uchafu Umesambaa Kila Mahali? Tufanye Nini Ili Tutunze Usafi Wa Miji Yetu? Hili Linanikera

Hili swala litashughulikiwa kwa makini zaidi na serikali za mitaa kuliko serikali kuu.
 
charity begins at home. wangapi waamka na kundoka bila kutandika kitanda? wangapi wanaacha vyombo vichafu mezani ama vimelundikana kwenye sinki? wangapi wanakula bila kunawa? ( the opposite is quite funny: kunawa bila kula!)? wangapi wanatoka msalani na kuendelea na shughuli zao bila kunawa? wangapi wanaenda msalani na kutoka bila kuflash?

tujikumbushe singapore: baada ya udhia na kadhia iliyosababishwa na jojo (chewing gum) serikali iliamua kupitisha na kutekeleza kwa ukali sheria iliyopiga marufuku jojo singapore. umeshawahi kukalia kiti cha daladala na kusimama na mnato wa jojo kwenye makalio?

tukubaliane kwamba usafi ni kigezo kimojawapo cha kuzingatia wakati wa ku design makazi na namna ya kuishi. nimebahatika kutembelea 'mahekalu' kibao yaliyojengwa dar es salaam. good design and everything. lakini uchafu kuanzia barabara mbovu, mifereji iliyoziba, bustani zisizo na mbele wala nyuma na masinki meupe yaliyogeuka rangi ya 'ugoro'.i.e. deep brown! halafu mtu mzima na akili zake ndipo anapotokea hapo kila kukicha na suti ya kufa mtu, driving a bmw.nini kinamzuia asishushe kioo na kutema mate au kupenga kamasi barabarani? afterall alipotoka msalani asubuhi hakuflashi! hana utamaduni huo!!

je leo hii twaweza kutamba kifua wazi ( ladies this option not for you!!) kwamba 'tanzania bila kipindupindu yawezekana'? i can here a very loud msonyo...'thubutu'!!!!!
 
charity begins at home. wangapi waamka na kundoka bila kutandika kitanda? wangapi wanaacha vyombo vichafu mezani ama vimelundikana kwenye sinki? wangapi wanakula bila kunawa? ( the opposite is quite funny: kunawa bila kula!)? wangapi wanatoka msalani na kuendelea na shughuli zao bila kunawa? wangapi wanaenda msalani na kutoka bila kuflash?

tujikumbushe singapore: baada ya udhia na kadhia iliyosababishwa na jojo (chewing gum) serikali iliamua kupitisha na kutekeleza kwa ukali sheria iliyopiga marufuku jojo singapore. umeshawahi kukalia kiti cha daladala na kusimama na mnato wa jojo kwenye makalio?

tukubaliane kwamba usafi ni kigezo kimojawapo cha kuzingatia wakati wa ku design makazi na namna ya kuishi. nimebahatika kutembelea 'mahekalu' kibao yaliyojengwa dar es salaam. good design and everything. lakini uchafu kuanzia barabara mbovu, mifereji iliyoziba, bustani zisizo na mbele wala nyuma na masinki meupe yaliyogeuka rangi ya 'ugoro'.i.e. deep brown! halafu mtu mzima na akili zake ndipo anapotokea hapo kila kukicha na suti ya kufa mtu, driving a bmw.nini kinamzuia asishushe kioo na kutema mate au kupenga kamasi barabarani? afterall alipotoka msalani asubuhi hakuflashi! hana utamaduni huo!!

je leo hii twaweza kutamba kifua wazi ( ladies this option not for you!!) kwamba 'tanzania bila kipindupindu yawezekana'? i can here a very loud msonyo...'thubutu'!!!!!

Kaiyulankuba,
Nashukuru kwa mchango wako. Unalosema ni kweli. Hata mimi nimeshagundua kuwa hata watanzania sisi wenyewe hatujawa na utaratibu wa kuweka mazingira katika usafi. Uliyosema yote ni kweli. Sasa tukubaliane kwamba uchafu ni shida ya wananchi na hivyo imeambukizwa mpaka viongozi wetu siyo??????? Siku zote naamini kwamba kila kitu kinategemea uongozi na muelekeo wake, ukielekea kubovu, wananchi wanaelekea kule kule. Tusijaribu kuwavua wajibu viongozi wetu. Uchafu unaanzia kwao.
Je uongozi wa miji yetu kwa nini usiwajibishwe? Unaona hakuna anayejali. Leo hii kama anakuja kiongozi wa nchi katika mji fulani basi utaona jinsi watu wanavyoshughulika kusafisha mazingira na kupamba mji, lakini, baada ya hapo uchafu unabaki pale pale. Hii ni aibu kwetu. Je hata kuweka vifaa vya kutupa taka ndani yake inashindikana? je hata kutunga sheria ndogo za kuwajibisha wachafuzi wa mazingira inashindikana?
 
Hili swala litashughulikiwa kwa makini zaidi na serikali za mitaa kuliko serikali kuu.[/QUOTE]

Na kama miji haiwajibiki je, nani awawajibishe? tukae kimya? nani anawajibika uongozi wa miji unapokuwa haukufanya maukumu yake? Je ni hawa madiwani ambao wanashabikia mambo ya siasa tu bila kujali majukumu yao mengine? Nani tumuwajibishe kuhusiana na uchafu uliokithiri mijini?
 
viongozi hawawezi kukwepa jukumu lao katika hili. 'hapo zamani za kale' idara za afya zilikuwa na watu wanaitwa 'mabwana afya' ambao kazi yao ilikuwa ni kukagua usafi (hygiene) na kusimamia sheria ndogo ndogo za halmashauri kuhusiana na swala hilo. hawa watu siku hizi wako wapi? hivi wenyeviti wa vitongoji, maofisa watendaji (vijiji/kata), wakurugenzi wa halmashauri...wanapofanyiwa 'perfomance assessment' wanazingatia vigezo gani? hili la afya na mazingira safi limo? that is assuming kuna kitu kinaitwa perfomance assessment! badala yake tunaona watu wanapandishwa vyeo kutokana na jinsi walivyoweza kudhibiti wapinzani! badala yake tunaona serikali kuu 'ikiminya' ruzuku na kuneglect wilaya ambazo zimepigia kura upinzani. kuna baadhi ya halmashauri ambazo huingia mkataba na wananchi ( perfomance contract for service delivery) and every year they are assessed based on that. of course this is not tanzania, ingawa wenzetu wamasai (was it longido or arumeru?) walisha tuonyesha njia kwa kugoma kulipa kodi na ushuru mbali mbali wa halmashauri kwa kupinga huduma mbovu( afya, barabara, maintanance ya majosho). the fact that the majority of these people hata hawakuwahi kwenda shule, showed that with determined commuity organization watu wa kawaida kabisa kuonyesha njia katika kuiwajibisha serikali.
 
Hivi haya mabango yanayowekwa mjini kila kona bila mpangilio ndio nini?

Najua jiji wanataka kukusanya revenues lakini naona sasa yataanza kusababisha ajali barabarani. Hivi kwa nini wasiweke standards na kuwalazimisha kuweka dimensions zinazoeleweka na zaidi ya hayo kuwauliza local councils na wananchi kabla hawajaweka residential areas
 
Back
Top Bottom