Uchafu mitaani Dar: Nani alaumiwe?

FM,

Lete solutions zako za mjini sasa, maana kulalamika tumesikia, na tatizo liko pale pale. Unayeona kuna solutions za vijijini na zile za mjini, basi tuletee za mjini.

Watu wanaendelea kufa kwa magonjwa yatokanayo na uchafu, kwanini tusitafute solution?

Wakipewa Wazungu hayo maeneo, watapata solution, huku Watanzania bado tunasubiri serikali ije utuokoe. Kama mnaweza itoeni hiyo serikali, lakini
kama hamna uwezo wa kuitoa serikali mtafanya nini? Mtaendelea kuzungukwa na uchafu?

Naona Mkuu haukusoma zaidi ya pale niliposema nimetofautiana na wewe! Ungeendelea ungekuta yafuatayo:

Tukitazama hili la uchafu, hata wananchi wa Manzese wafanye nini bila kuwa na chombo kitakachoweza kuukusanya huo uchafu na kwenda kuutupa mahali panapostahili, juhudi zao zitakuwa bure. Mfano angalia vile vitrela vya kuchukua uchafu vinavyo overflow. In desperation wananchi wamefikia hatua ya kuchoma bila kuangalia madhara ya moshi ulio na sumu! Wengine wanawalipa watoto wa mjini kuchukua na kwenda kutupa taka hizo sehemu wanazojua wao.

Hii ndiyo inayonipelekea kusema kuwa katika mazingira ya miji ni lazima utawala uwajibike kwa kuweka nyenzo na system za kushughulikia suala la uchafu. Wakishafanya hivyo, ndiyo waweke bye-laws zitakazomwadhibu yeyote ambaye atasababisha uchafu maana hatokuwa na sababu. Singapore unalipa faini kama unatupa Big G chini, kama hauflush public toilet kwa sababu mapipa na vyoo havikosi maji kwa hiyo hauna sababu ya kufanya vinginevyo. Sehemu nyingi Ulaya wenye mbwa wana wajibika kukusanya choo cha mbwa wao kwa sababu sehemu ya kukitupia kiko kila sehemu. Mtu anayeacha kinyesi cha mbwa wake bila kukikusanya anaadhibiwa!

Utamlaumu vipi mtu kujisaidia nyuma ya mti kama hamna huduma ya vyoo vya umma? Utamlaumu vipi mtu kutupa maganda ya ndizi chini kama hamna sehemu ya kutupia? Na zaidi ya haya, utawalaumu vipi wote hawa kama hauwaadhibu wakifanya hivyo wakati vyoo vipo na vipipa vipo?

Miji inahitaji utawala unaowajibika ili ifanye kazi. Hili sidhani kama tunaweza kukwepa.

Uwajibikaji wa mtu binafsi ni muhimu lakini ina mwisho wake ndiyo maana tunakua na serikali za mitaa. Sasa Mkuu, hilo lundo la uchafu watalipeleka wapi kama serikali ya mtaa haijatenga sehemu maalum ya kutupia taka? Inabidi wa wajibishwe na hao waliowaweka yaani wananchi wenyewe. Nchini mwetu tumefikia hatua ya ukipigwa na kibaka polisi wanakwambia kamkamate umlete! Siku nyingine si nitapiga kelele ili waje watu na mafuta ya taa na matairi? Ni lazima uwajibikaji wa viongozi uwepo.
 
Nchi hii ni muda mrefu sana hatujapata mtu wa kukosha nyoyo zetu. Labda miaka ya sabini waliyokuwepo walishuhudia idadi kubwa ya viongozi na mfumo wa kazi wa uwajibikaji.
Leo hii mimi naishi Mwenge ni kama nipo Peponi maana Serikali yangu haitambuwi mahala nilipo. Si kiongozi wa kitongoji, kijiji, kata, tarafa wala wilaya. Utaona karatasi ya Kata siku wakitaka kula pesa zetu kwa kigezo cha kupuliza dawa.
Je, katika mazingira ambayo viongozi ngazi ya kata hawawajibiki kwa wananchi ndani ya eneo lao ni kwa namna gani mwananchi atasimamia swala zima la usafi?
Sijafika ulaya lakini kichwa changu kinafanya kazi. Kama Baba mwenye Nyumba hatambui ongezeko la wageni kwenye nyumba yake ni namna ghani anakuwa kiongozi wa familia?
Wakati wa Mwalimu tulikuwa maskini kutokana na maliasili nyingi kuwa Iddle lakini hatukuwa na idadi kubwa ya viongozi uchwara.
Ni wakati wa mfumo wa chama ulikuwa uhami wala kuhamia sehemu bila Balozi wako kubariki. Ilikuwa ni kosa kumpokea mgeni pasipo kumtambulisha kwa balozi. Mitaa ilikuwa ni misafi maana sera ya kujitegemea ilitumika vizuri lakini leo hii serikali sijui ipo na inafanya nini.
Nchi yetu ndipo mahali wananchi wanatangulia mbele serikali nyuma yao. Tunavamia kwanza maeneo ya kuishi ndo serikali inakuja kupima na kubomoa. Tabata Dampo, ni mfano. Je, uchafu ule mwananchi alaumiwe vipi? Tambua sisi ni wanyama ni kwa kuwapa watu fulani dhamana ya kuelekeza fikra zao katika kuwasimamia wengine ndipo ubinadamu wetu unatofautiana na wanyama wengine.
Hakika Serikali inapaswa kubeba lawama imetuacha tuwe wanyama badala ya kuwa binadamu.
Mimi natupia lawama viongozi. Nchi zote ambazo sasa hivi tunaona kuwa ni kioo cha usafi, hazikuwa siku zote hivi. Singapore ilikuwa bandari masikini na chafu kwa kila jinsi walipopata uhuru. Ni uongozi wao waliochukizwa na hali hiyo na kuweka sheria ambazo zilimwadhibu raia yeyote atakayeendekeza uchafu. Miji ya uingereza, ufaransa yote nayo ilikithiri kwa uchafu mpaka utawala ulipopitisha sheria ili kukabiliana na milipuko ya magonjwa iliyokuwa kama tija wakati ule. Ni mlipuko wa mara kwa mara wa Cholera ndiko kuliwafanya wenzetu wapitishe sheria ambazo kwanza zililazimishe local authorities wajenge sewer systems na wakazi wote wa mjini kuunganisha kwenye hizo sewers! Wananchi walipinga sana wakiona kuwa ni utawala wa ubabe lakini utawala ulishinikiza mpaka hali ikakubalika. Bila uongozi ulioamka hamna kitakachofanyika.

Hali hii ya uchafu kukithiri mara nyingi ni mijini na sio vijijini. Vijijini kila mwenye nyumba anawajibika katika sehemu yake na hapo awali sehemu kubwa ya uchafu uliokuwa ukizalishwa ulikuwa ni bio-degradable. Hapa mjini hakuna mwenye mji na bila uongozi kuweka sehemu na taratibu za kukabiliana na hali hii hakuna ambacho mwananchi wa kawaida anachoweza kufanya. Kama hakuna taratibu za kukusanya taka, mwananchi aishie katikati ya mji ni vigumu kuchimba shimo la kutupia taka zake. Ziwekwe taratibu na kuhakikisha kuwa zinafuatwa. Bahati mbaya taratibu hizo zinafanywa dili kiasi cha kumuondolea mwananchi hamu ya kuzitumia!
 
Nchi hii ni muda mrefu sana hatujapata mtu wa kukosha nyoyo zetu. Labda miaka ya sabini waliyokuwepo walishuhudia idadi kubwa ya viongozi na mfumo wa kazi wa uwajibikaji.
Leo hii mimi naishi Mwenge ni kama nipo Peponi maana Serikali yangu haitambuwi mahala nilipo. Si kiongozi wa kitongoji, kijiji, kata, tarafa wala wilaya. Utaona karatasi ya Kata siku wakitaka kula pesa zetu kwa kigezo cha kupuliza dawa.
Je, katika mazingira ambayo viongozi ngazi ya kata hawawajibiki kwa wananchi ndani ya eneo lao ni kwa namna gani mwananchi atasimamia swala zima la usafi?
Sijafika ulaya lakini kichwa changu kinafanya kazi. Kama Baba mwenye Nyumba hatambui ongezeko la wageni kwenye nyumba yake ni namna ghani anakuwa kiongozi wa familia?
Wakati wa Mwalimu tulikuwa maskini kutokana na maliasili nyingi kuwa Iddle lakini hatukuwa na idadi kubwa ya viongozi uchwara.
Ni wakati wa mfumo wa chama ulikuwa uhami wala kuhamia sehemu bila Balozi wako kubariki. Ilikuwa ni kosa kumpokea mgeni pasipo kumtambulisha kwa balozi. Mitaa ilikuwa ni misafi maana sera ya kujitegemea ilitumika vizuri lakini leo hii serikali sijui ipo na inafanya nini.
Nchi yetu ndipo mahali wananchi wanatangulia mbele serikali nyuma yao. Tunavamia kwanza maeneo ya kuishi ndo serikali inakuja kupima na kubomoa. Tabata Dampo, ni mfano. Je, uchafu ule mwananchi alaumiwe vipi? Tambua sisi ni wanyama ni kwa kuwapa watu fulani dhamana ya kuelekeza fikra zao katika kuwasimamia wengine ndipo ubinadamu wetu unatofautiana na wanyama wengine.
Hakika Serikali inapaswa kubeba lawama imetuacha tuwe wanyama badala ya kuwa binadamu.


Mafanikio uliyoona miaka ya zamani yalikuwa ni yale ya serikali za mitaa alizoacha mkoloni. Kuanzia 1972 ni kichwa cha mwenda wazimu.
 
Mafanikio uliyoona miaka ya zamani yalikuwa ni yale ya serikali za mitaa alizoacha mkoloni. Kuanzia 1972 ni kichwa cha mwenda wazimu.

So what happened? why regress and not progress? It seems somewhere after several years of self autonomy and our independence, we changed the direction on everything! Look at Production, Education, Cleanliness, Morals, Accountability, Efficiency, Motivation, following Law and Order etc.

We need to examine what happened and why it is affecting us to the point we are just cool with everything, the Que Sera Sera, Ndivyo tulivyo attitude!

I think it is time we sit down and not writing up new plans and policies but revisit everything we have done from the day Mkoloni left todate and do a thorough analysis that can provide constructive feedback to correct our ills and short comings.

If we fail to make effort to do that, we will never make any progress and our efforts will be similar to a dog trying to bite its own tail!
 
uchafu ni suala personal, dont expect mtu anye nje then aexpect serikali ije izoe ma*vi yake !

Kama uchafu wa taka taka, watanzania saa nyingine tunakuwa nyuma katika usafi wenyewe, najua kwamba kuna magari ya manispaa na city ambayo hupitia taka katika maeneo fulani si chini ya mara 2 kwa wiki, lakini utakuta watu bado tu wanatupa taka ovyo !

Kwa mbongo mazoea yana tabu, hata ukiweka tank ya kunywa maji safi, yeye atataka tu maji ya bombani, ukileta magari ya taka yeye atatupa tu taka anapojua yeye, hata ukimjengea uwanja safi wa soka, basi watavunja tu viti ili mradi wakae chini, SABABU ? eti wamezoea kuangalia mechi wakiwa wamekaa chini. Angalieni watu walivyochafua vyoo siku ile kwenye mechi iliyochezwa katika wanja jipya ! Watu walihara balaaaaaaa, na wengine wakadiriki hata kupaka ukutani na wengine kuweka machata yao, we have a longggg way to go folks !

SASA NANI ALAUMIWE ??
 
Kachimbe jalala....

kuna mitaa majalala hatachimbiki,licha ya kwamba nyumba za mitaa hiyo zinakaliwa na wapangaji wasio na mamlaka ya kufukuafukua eneo la mwenyewe,hata pa kuchimba hamna,nyumba zimashonana ukuta na ukuta,watu wanaingia vyumbani mwao kiubavu ubavu.Hujasikia jiji kama Dar takribani asilimia 30 ya nyumba ndio zimejengwa kwa kufuata ramani za mipango miji,zilizobaki ni kiasi cha kuunganisha tu mchanga na saruji.
 
Kuna ubaya gani wa kuanzisha magari taka ambayo yatasomba takataka zilizowekwa kwenye mifuko maalum angalau mara moja kwa wiki badala ya kuitupa uwani au upenuni.

faida ya hiyo:

a. Biashara ya mifuko
b. Biashara ya taka (waste energy etc)
c. Mazoea mapya ya kupenda usafi
d. Ajira kwa madereva na wasomba taka

Kwa jiji kama la Dar, kila siku moja ya wiki upande mmoja unachukuliwa Taka

Jumatatu na Jumanne (Temeke)
Jumatano na Alhamisi (Kinongondi)
Ijumaa na Jumamosi (Ilala)

Tatizo la misongamano ya nyumba. Kwa vile hatuna mitaa ambayo magari makubwa yanaweza kupita basi tunaweza kuwa na magari madogo ya saizi ndogo ambayo yatasimama mwishoni mwa mtaa/au mwanzoni kwa masaa kadhaa ili watu walete uchagu wao ukiwa umewekwa na kufungwa kwenye mifuko rasmi inayokubalika (jinsi wataileta hilo lwao wanaweza kuibeba kichwani wakitaka alimradi isimwagike)

Mtu ambaye atajulikana ametupa uchafu analimwa faini; anayeweka uchafu bila ya kuufunga vizuri analimwa faini vile vile, na faini hiyo inatumika kulipia huduma za magari hayo.

Gharama ya huduma hiyo kutoka kwenye halmashauri au watu binafsi inalipwa kama kodi ya huduma za taka (waste products levy). Kila wilaya au halmashauri inaweza kujipangia kiwango chake na wananchi wote (wakazi wa eneo) wanalipia huduma hiyo.

Sasa, kwa wale wanaoishi kwenye nyumba za kupanga, Basi kodi yao inaendana na idadi ya wapangaji ikigawanywa kwa siku za wiki.

Kwenye maeneo ambayo yana wapangaji wengi (vyuoni, mashule, n.k) wanajiwekea utaratibu tofauti na ule wa maeneo ya makazi.

Hata hivyo, jambo la kwanza la kushughulikia ni kuhakikisha kuna mahali ambapo taka hizo zitaweza kutupwa bila kusababisha madhara kwa jamii au maji na pia kuona kama kunaweza kuwa na kiwanda cha kutumia taka kutengeneza nishati (waste energy).

Lakini njia ya pili (ukiondoa hiyo ya magari kuzunguka mtaani kila siku ya wiki tunaweza kuanzisha huduma ya kukusanya taka kwa mkaa ambapo unaweka "collection bin" ambapo kila mtaa unakuwa na moja na kama mtaa ni mrefu au una wakazi wengi basi unaweza kuwa na zaidi ya moja, hizo collection bins zinawekwa mahali ambapo gari la taka linaweza kufika angalau mara moja kwa wiki kuzikusanya kwenye "collection trucks".

Kwenye somo hili naweza kusema mengi.. niwaache wengine waendelee kupendekeza suluhisho..
 
uchafu ni suala personal, dont expect mtu anye nje then aexpect serikali ije izoe ma*vi yake !

Kama uchafu wa taka taka, watanzania saa nyingine tunakuwa nyuma katika usafi wenyewe, najua kwamba kuna magari ya manispaa na city ambayo hupitia taka katika maeneo fulani si chini ya mara 2 kwa wiki, lakini utakuta watu bado tu wanatupa taka ovyo !

Kwa mbongo mazoea yana tabu, hata ukiweka tank ya kunywa maji safi, yeye atataka tu maji ya bombani, ukileta magari ya taka yeye atatupa tu taka anapojua yeye, hata ukimjengea uwanja safi wa soka, basi watavunja tu viti ili mradi wakae chini, SABABU ? eti wamezoea kuangalia mechi wakiwa wamekaa chini. Angalieni watu walivyochafua vyoo siku ile kwenye mechi iliyochezwa katika wanja jipya ! Watu walihara balaaaaaaa, na wengine wakadiriki hata kupaka ukutani na wengine kuweka machata yao, we have a longggg way to go folks !

SASA NANI ALAUMIWE ??

Bongoyo kweli kwema! Gari la taka mara mbili kwa wiki!

Wengi wetu tukiachiwa tunakuwa wanyama. Hao football hooligans wa uingereza ni waafrika? Kwenye concerts nyingine za wazi watu mbona wanajisaidia ovyo? Nasikia wenye mashamba uingereza walianza kukataa kuwaruhusu vijana kutumia nafasi hizo kwa sababu hiyo hiyo ya uchafu kukithiri wakiondoka. Kuna sikukuu zao hata hao wazungu wanajisaidia ovyo barabarani! Cha msingi ni kuijua hali na kuipangia mikakati. Kwa mfano, ukienda kwenye vyoo vya umma vingi ulaya utakuta taa ni ya bluu. Hii ni kutokana na tabia ya mateja kutumia sehemu hizo kujidunga madawa ya kulevya. Taa ya bluu inafanya mishipa ya damu isionekane kwa urahisi. Vyoo na masinki katika sehemu zote za hadhara huwa zinakuwa vandal-proof ambavyo ni vigumu kung'oa au kuharibu. Rangi na vigae vya ukutani navyo hivyohivyo. Vinawekwa ili viwe rahisi kusafisha baadaye na si kwa ajili ya umaridadi. Badala ya kujazana kwenye mageti walishindwa kweli kuweka ulinzi kwenye vyoo na kutoza kiingilio? Kwenye hiyo stadium ya kisasa hakuna camera zinazomnasa mhalifu wakati akifanya tendo? Kwa nini hawakuzitumia? Mimi wasiwasi ni kuwa kwenye mradi huo tulijiingiza wenyewe kwenye mkenge. Kwa sababu za kisiasa za kuomba tutumie uwanja kabla ya practical completion ambapo kila kitu kinakaguliwa na consultants. Mnajuaje kuwa hivyo viti havikuwekwa kwa umadhubuti uliokusudiwa? Nani ali'snag' uwanja? Kuna muda (defect liability period) ambapo mkandarasi anawajibika kwa ubovu wowote utakaonekana kutokanana poor workmanship au inferior equipment. Kwa kuutumia uwanja kabla ya wakati tumempa loophole. Waingereza hawakuwa wajinga kusuburi mpaka uwanja wa Wembley ukamilike ndio waanze kuutumia.

Mimi nilipoambiwa kuwa Tanzania kuna sheria ya watu kuvaa safety belts wakati wakiendesha magari sikuamini kama wabongo ninaowajua watafanya hivyo. Mbona wengi wanafanya! Unadhani wanapenda au hawataki kutoa mchango kwa trafik?

Sijui kama bado ni kweli lakini kuna wakati jiji la Paris liljaa vinyesi vya mbwa. Lakini ukivuka mpaka ukienda ujerumani hukuti kinyesi cha mbwa barabarani. Tofauti iliyokuwepo ni kuwa ujerumani mwenye mbwa akionekana ameacha kinyesi cha mbwa wake bila kukizoa analimwa faini wakati Paris haikuwa hivyo. Wote wazungu hao. Unadhani wazungu wangeacha kuvuta sigara kwenye mabaa bila tishio la faini kubwa kwa mwenye baa? Thubutu!

Hali haitabadilika kwa kuweka mapipa tuu bila kupitisha sheria za kuhakikisha yanatumiwa. Siyo sisi wala sio hao wazungu. Ni baada ya matumizi ya muda mrefu ndiyo inakuwa tabia. Lakini mwanzo shurti tishio la kiboko liwepo.

Bin Maryam hakukosea aliposema kuwa tulikosea kwa kutothamini tulichoachiwa na mkoloni. Nakumbuka mantra moja iliyotawala wakati ule ni mtu usiwe mnyapara tukiamini kuwa kila mtu atajituma. Hapo ndipo tulipoanza kukosea.
 
uchafu ni suala personal, dont expect mtu anye nje then aexpect serikali ije izoe ma*vi yake !

Kama uchafu wa taka taka, watanzania saa nyingine tunakuwa nyuma katika usafi wenyewe, najua kwamba kuna magari ya manispaa na city ambayo hupitia taka katika maeneo fulani si chini ya mara 2 kwa wiki, lakini utakuta watu bado tu wanatupa taka ovyo !

Kwa mbongo mazoea yana tabu, hata ukiweka tank ya kunywa maji safi, yeye atataka tu maji ya bombani, ukileta magari ya taka yeye atatupa tu taka anapojua yeye, hata ukimjengea uwanja safi wa soka, basi watavunja tu viti ili mradi wakae chini, SABABU ? eti wamezoea kuangalia mechi wakiwa wamekaa chini. Angalieni watu walivyochafua vyoo siku ile kwenye mechi iliyochezwa katika wanja jipya ! Watu walihara balaaaaaaa, na wengine wakadiriki hata kupaka ukutani na wengine kuweka machata yao, we have a longggg way to go folks !

SASA NANI ALAUMIWE ??

Ilaumiwe serikali....
 
Jamii ya watu waliozoea kuona uchafu, na uchafu huo kwao haunuki tena, yaani wameuzoea kiasi kwamba harufu yake hainusiki tena; basi jamii hiyo huwa imezoea uchafu.

Mwanakijiji.. tutake radhi yaani sie sawa na hii picha
y1pIjS-ngexYeXGBi9Ve2_ZOREQibbxzii9BaH1fROPZxMbuzwY95PlI92B3pDuswKl9SDAULad-P4

Kuna ubaya gani wa kuanzisha magari taka ambayo yatasomba takataka zilizowekwa kwenye mifuko maalum angalau mara moja kwa wiki badala ya kuitupa uwani au upenuni.
Kuna wazo zuri ambalo sasa limewanufaisha wengi, lile ambalo katoa Mtanzania, kuwa kuna haya ya kuwatumia vijana wakao maskani kukusanya taka kwa kulipwa.

ILO katika miaka ya tisini mwishoni na mwanzoni mwa miaka ya elfu mbili walikuwa na kauli mbiu ya "Takataka ni mali" Waliweza kuwavuta vijana wengi hasa akinamama na kuweza kujipatia ajila kwa kukusanya taka toka majumbani.

Baadae wigo ulipanuka na wengi wakajiunga katika CBO za ukusanyaji wa taka. Ili kuongeza kipato walianza hata kufagia barabara. Manispaa na halmashauri ziliingia mikataba nao na nyingi bado zinafanya kazi kwa ufanisi mkubwa.

CBO ambazo zilikuja baadae ambazo zilipata misaada wakati wa uanzishwaji wake, kama vile magari ya kuzolea taka, wheelbarrows na vifaa vingine, hazikuweza kuendelea baada ya kufanya kazi chini ya miaka miwili.

Wachunguzi wa miradi wanasema Tatizo kubwa la kutoa vifaa vyote muhimu kwa vikundi vya taka vinawajengea tabia wazoaji taka kutothamini vifaa hivyo na mradi mzima, kwani wanakuwa wanajiona kama wameajiliwa, huku ni mradi kwa faida yao.

Kwa ufupi miradi mingi ya ukusanyaji na utupaji taka ambayo imefanikiwa ni ile ambayo ilianza bila ya kitu, kuliko hii ambayo imekuja na vitendea kazi.


y1pIjS-ngexYeUuAxERGmUhdUu1QjpK6C7x3yaQ_vPNiIQ8dCC8-2EkoO8GIUVEybbZMW2ldj5spog
Pichani moja ya CBO za kukusanya na kutupa taka ikiwa kazini, Hii ni kazi extra kwao kwani wao ukusanya taka nyumba kwa nyumba... Takataka za barabarani wameingia mkataba na Halmashauri ya Manipaa.
 
Hili ni tatizo la sisi wananchi kwanza, na baadaye viongozi, unahitaji kuchungulia kwa jirani zetu Zambia tu, maana ukipita vitongojini kwa wananchi wenye hali za chini huwezi kuta uchafu, the matter of fact wao sio wasafi tu, bali huwa siku zote wanazungusha wigo kwenye nyumba zao, hata iwe ya maboxi, kutakuwa na wigo na tangazo kuwa,".... Chenjeleni pali ne mbwa..." yaaani hatari kuna mbwa, hili neno lazima ulijue ukipita huko kwa jirani zetu,

Now wananchi wasafi, siku zote watakuwa na very strong standing point morally, kwenye kuilazimisha serikali yao, iwe kuu au ya mitaa not only kuwasaidia as a community ku-deal na ishus za usafi, bali wanaweza hata kuilazimisha pie kufanya watakayo.

However, haya ya community na usafi, yanawezekana tu kukiwepo na elimu, yaani wananchi walioelimika, I am not sorry kwamba sisi wabongo hatujaelimika vya kutosha kuelewa umuhimu wa usafi wa mazingira yetu kama sio hata nyumba zetu. Sisi wananchi ni wachafu sana, ukingia kwenye basi la dala dala ni sawa kabisa na kuingia kwenye elevator pale NSSF, utasikia kikwapa kama mko kwenye zizi la wanyama, I mean sisi wananchi wachafu, wewe umeoan uwanja wa mpira mpya, yaaani nasikia wa-China mpaka leo hawaamini kuwa siku ya mechi ya kwanza pale na Mozambique, walioingia kuangalia mpira ule ni wananchi, yaaani in other words, bina-adam.

Nenda huko majuu, I mean nyumba zingine kweli ni safi za wabongo, lakini zingine ukiiingia utafikiri uko bongo, lakini mtu yuko majuu, kuna siku niliiingia nyumba moja ya mbongo majuu yaaani sikuamini kuwa Europe kunaweza kuwa na nyumba ndani inafanana hivyo, sasa what serikali has to do na this? Yaaani wabongo wachache sana utakuta ndani kwao ni bomba huko majuu, sasa kama wako majuu wako hivyo je wakirudi nyumbani itakuwaje?

Serikali has nothing to do na uchafu wetu wananchi, wananchi wasiokuwa na elimu ya kutosha kama sisi bongo, kamwe hatutaweza kuwa wasafi, as the results tutaishia kuwachagua viongozi wachafu kama sisi wananchi, guess what hili litakuwa tifa la uchafu kama tulivyo bongo. Hebu niambie ni lini usafi na uchafu wa mazingara yetu umewahi kuwa ishu kwenye kampeni zetu za ubunge au urais?

Wananchi wachafu hu-create serikali chafu kama yetu, uchafu wa nyumbani na mazingara ukizidi, mwisho huhamia na kwenye akili zetu.

Ahsante Wakuu!
 
mzee FMES

umenifanya nijiangalie mie mwenyewe mara mbili mbili, kumbe hili la kubadili tabia hata na mimi linanigusa.


kubadili tabia sio kwenye masuala ya ukimwi hata ktk uchafu kwa hio tujitahdini.

hata hivyo ktk mazingira ya public serikali ikiwa kuu au za mitaaa ijitahidi kutunga sheria za usafi na anaekiuka aadhibiwe huwezi amini ukitembea kwenye masoko yetu, sijui pengine weshabadilika hakuingiliki kwa harufu mbaya na matope hata ikiwa hakujanyesha mvua.


pia suala la elimu ya mazingira litiliwe maanani tokea mashuleni, sio siri watanzania wachafu hadi kwenye nyumba za ibada usiombe ukashikwa na haja na ukataka kwenda msikitni kujisaidia utatapika. sijui kanisani sijawahi kuingia.


ukienda kwenye sehemu ya starehe ndio usiseme.


kuna jamaa kanihaduthia kua hata wanawake wengi wa kibongo wazuri nje tu huenda viwalo vya ndani vina wiki kama si zaidi havijapata maji au kuwa mbali na mwili.


tujitahidini tubadilike na mm leo rasmi nitaongoza usafi humu nyumbani mwangu nione aibu
 
So what happened? why regress and not progress? It seems somewhere after several years of self autonomy and our independence, we changed the direction on everything! Look at Production, Education, Cleanliness, Morals, Accountability, Efficiency, Motivation, following Law and Order etc.

We need to examine what happened and why it is affecting us to the point we are just cool with everything, the Que Sera Sera, Ndivyo tulivyo attitude!

I think it is time we sit down and not writing up new plans and policies but revisit everything we have done from the day Mkoloni left todate and do a thorough analysis that can provide constructive feedback to correct our ills and short comings.

If we fail to make effort to do that, we will never make any progress and our efforts will be similar to a dog trying to bite its own tail!

Rev:

Kuna makosa tuliyafanya na tunaendelea kufanya. Moja ya makosa hayo ni kudharau matumizi ya financial resources na kuendelea kutumia zaidi physical resources.

Pesa ni conceptual wealth. Unapokuwa na noti yenye thamani ya dollar 100 siku kweli kuwa noti yenyewe ina thamani ya dollar 100. Lakini conceptually noti hiyo inaweza kununua vitu au huduma zenye thamani ya kiasi hicho.

Moja ya uvumbuzi mkubwa na unaosaidia sana maendeleo ya binadamu ni matumizi ya conceptual resource (Pesa). Na tofauti kati ya walioendelea na nchi masikini kwa kiasi kikubwa yanatokana na jinsi gani wanatumia resource hii.

Tukurudi kwenye mada. Mwananchi kujitolea kufanya usafi kwa nguvu zake ni matumizi ya physical resource ambayo kwa siku zote ayajatupeleka mahali popote. Hili usafi ufanyike ni lazima mwananchi huyo awepo pale physically. Mchukue daktari mwenye shifti ya usiku au mtu mwenye kufanya kazi ya kuchinja ng'ombe. Mtu huyu anaweza kufanya usafi wa ndani ya nyumba yake lakini usafi wa nje ni lazima vyombo vingine viingilie na kufanya kazi kwa niaba yake. Na hapo ndipo umuhimu wa pesa unapokuwepo.

Watu hawa wakitoa mchango kwa njia ya kodi wa kuwasaidia kufanya usafi, basi mchango huo unaweza kununua gari, kuajiri dereva na wataalamu wengine wa usafi na kufanya kazi kwa niaba yao.

Kuna kipindi watu wa Osterbay walikuwa wanajaza viroba vya uchafu kwenye magari yao na kwenda kuvitupa Magomeni au Jangwani. Hao ndio viongozi wa nchi. Kutumia gari lako (physical asset) na wewe mwenyewe kuendesha gari hilo (physcial resource) kwenda kutupa takataka ni kuendeleza matumizi ya physical resources. Kuhimiza wananchi kujitolea ni kuendeleza matumizi ya physical resources.

Kwa maoni yangu, tunaupungufu mkubwa wa watu wanaojua kukusanya na kutumia pesa kama resource za maendeleo. Ukiwa mwalimu usiwaangalie wanafunzi wako na kusema vijana hawa wameshiba sana basi wanaweza kusoma na kuzalisha chakula cha kujilisha. Na ukiwa kiongozi wa nchi, usifikiri kuwa watu watatoka kazini na baadaye wafanye kazi za kusafisha mitaa. Tunaishi mijini na miji yote imeendelea kwa kodi za watu. Na kama mji hauendelei basi kuna ulakini katika ukusanyi au matumizi ya kodi.
 
Kwa maoni yangu, tunaupungufu mkubwa wa watu wanaojua kukusanya na kutumia pesa kama resource za maendeleo. Ukiwa mwalimu usiwaangalie wanafunzi wako na kusema vijana hawa wameshiba sana basi wanaweza kusoma na kuzalisha chakula cha kujilisha. Na ukiwa kiongozi wa nchi, usifikiri kuwa watu watatoka kazini na baadaye wafanye kazi za kusafisha mitaa. Tunaishi mijini na miji yote imeendelea kwa kodi za watu. Na kama mji hauendelei basi kuna ulakini katika ukusanyi au matumizi ya kodi.

Haswa, Bin Maryam, haswa. Tulipangiwa zamu kulinda sungusungu wakati askari wapo! Kwa wenzetu watu wanajitolea kuongezea pale ambapo serikali imeshindwa au kama namna ya kuonyesha mshikamano na sio kuchukua nafasi ya serikali. Watu wanajitolea kufanya usafi mara moja kwa msimu, na institution husika zinasaidia kwa kutoa vitendea kazi na utaalamu kama unahitajika. Si kuwasukumizia mzigo wananchi. Wakifanya hivyo wanajua kuwa kibarua kitaota mbawa.
 
Back
Top Bottom