Ubora wa vyuo vikuu duniani: Oxford chaongoza duniani, Cape Town chaongoza bara la Afrika

bryan2

JF-Expert Member
Jun 8, 2016
3,323
4,667
_91344199_9ba38105-603d-4b23-a9e8-852c43503e00.jpg


Chuo kikuu cha Oxford kimeibuka kidedea katika orodha ya vyuo vikuu bora duniani ya Times Higher Education. Hi ni mara ya kwanza kwa chuo kikuu cha Uingereza.

Oxford imeisukuma katika nafasi ya pili, California Institute of Technology, ambayo imekuwa ikiongoza orodha hiyo kwa miaka mitano iliopita .

Katika orodha ya vyuo vikuu bora barani Afrika, chuo kikuu cha Cape Town kimeibuka wa kwanza kutoka Afrika kusini kwenye orodha hiyo ya Times Higher Education.

Inadhihirisha umahiri wa taifa hilo, ambalo vyuo vyake vikuu 6 vipo katika nafasi za vyuo vikuu 15 bora kikwemo chuo cha Witwatersrand katika nafasi ya pili, Stellenbosch nafasi ya tatu, tChuo kikuu cha KwaZulu-Natal katika nafasi 5 na chuo kikuu cha Pretoria katika nafasi ya sita.

Makerere kilichopo Uganda ndiyo chuo kikuu nje ya Afrika kusini kufanikiwa kuwa atika nafasi ya nne.

Vyengine ni chuo kikuu cha Ghana katika nafasi ya 7, na chuo kikuu cha Nairobi katika nafasi ya 8.

Orodha ya Times Higher Education duniani inapima vitu kama mafunzo, utafiti, na mtazamao wa kimaaifa - kwa mfano, idadi ya wanafunzi wanaotoka nje na wafanyakazi.

Nico Cloete, mkurugenzi wa taasisi ya Higher Education Trust na mratibu wa utafiti wa elimu ya juu na Advocacy Network in Africa, anasema taasisi hizo nne katika orodha ya Afrika - Cape Town, Makerere, Nairobi na Ghana - "zimeidhinisha mipango ya kuwa vyuo vikuu vinavyoongoza kwa utafiti" nchini mwao na vimeshuhudia "ongezeko kubwa kwa wanaofuzu kwa ushahada ya uzamifu na kuunda taasisi za utafiti katika miaka mitano iliopita".


Chanzo: BBC Swahili

Vyuo 30 bora Afrika.

Rank
1 University of Cape Town - South Africa
2 University of the Witwatersrand - South Africa
3 Makerere University - Uganda
4 Stellenbosch University - South Africa
5 University of KwaZulu-Natal - South Africa
6 University of Port Harcourt - Nigeria
7 University of the Western Cape - South Africa
8 University of Nairobi - Kenya
9 University of Johannesburg - South Africa
10 University of Marrakech Cadi Ayyad - Morocco
11 University of Pretoria - South Africa
12 University of Ghana - Ghana
13 University of South Africa - South Africa
14 Suez Canal University - Egypt
15 University of Hassan II Casablanca - Morocco
16 Addis Ababa University - Ethiopia
17 Rhodes University - South Africa
18 University of the Free State - South Africa
19 North-West University - South Africa
20 University of Tunis - Tunisia
21 Ecole Nationale d’Ingénieurs de Sfax - Tunisia
22 Université Mohammed V – Agdal - Morocco
23 American University in Cairo - Egypt
24 Nelson Mandela Metropolitan University - South Africa
25 South Valley University - Egypt
26 Alexandria University - Egypt
27 Assiut University - Egypt
28 University of Sfax - Tunisia
29 University of Yaounde I - Cameroon
30 Minia University - Egypt
 
Wasalaam wanajukwaa.

Katika orodha ya vyuo bora Africa iliyotolewa mwaka huu 2016 na mtandao wa Times Higher Education (THE), Tanzania haina chuo hata kimoja katika orodha hiyo tofauti na miaka ya nyuma.

Orodha ya Times Higher Education duniani inapima vitu kama
=>mafunzo,
=>utafiti,
=>na mtazamo wa kimataifa.
Kwa mfano, idadi ya wanafunzi wanaotoka nje na wafanyakazi.

Nico Cloete, mkurugenzi wa taasisi ya Higher Education Trust na mratibu wa utafiti wa elimu ya juu na Advocacy Network in Africa, anasema taasisi hizo nne katika orodha ya Afrika - Cape Town, Makerere, Nairobi na Ghana - "zimeidhinisha mipango ya kuwa vyuo vikuu vinavyoongoza kwa utafiti" nchini mwao na vimeshuhudia "ongezeko kubwa kwa wanaofuzu kwa ushahada ya uzamifu na kuunda taasisi za utafiti katika miaka mitano iliopita".

Je, sisi kama Tanzania tunakwama wapi? Na nini kifanyike ili elimu ya vyuo vikuu vyetu ipande katika viwango vya kimataifa?

Top 30 African universities: Times Higher Education reveals snapshot university ranking

Je unavitambua vyuo vikuu bora duniani? - BBC Swahili
 
UDSM imezorota siku za karibuni. Kiashiria kimoja ni website yao. Zamani ilikuwa imekaa vizuri, lakin sasa inatisha. Pull-down menu zake hazikupeleki popote penye habari za maana. Haikuwa hivyo miaka michache iliyopita.

Kama Makerere inaweza kwanini sisi tushindwe kufanya vizuri?

Ukiacha shule chache za binafsi, elimu imedorora sana Tanzania kwa ujumla. Maana inabidi kujenga toka kwenye msingi na sio kuanzia chuo kikuu. Hatua moja kubwa ya kwanza ni kurudisha HADHI ya waalimu katika jamii. Mwalimu anapashwa kuwa na hadhi sawa na daktari. That is the case in China. We can start by doubling or trebling the salaries of teachers. Inabidi tuanze sasa kutenga asilimia 27 - 30 ya bajeti iwe ya elimu. Na tufanye hivyo kweli, sio kudanganya hadharani kisha fedha hazitolewi. If you think education is expensive, try ignorance.
 
UDSM imezorota siku za karibuni. Kiashiria kimoja ni website yao. Zamani ilikuwa imekaa vizuri, lakin sasa inatisha. Pull-down menu zake hazikupeleki popote penye habari za maana. Haikuwa hivyo miaka michache iliyopita.

Kama Makerere inaweza kwanini sisi tushindwe kufanya vizuri?

Ukiacha shule chache za binafsi, elimu imedorora sana Tanzania kwa ujumla. Maana inabidi kujenga toka kwenye msingi na sio kuanzia chuo kikuu. Hatua moja kubwa ya kwanza ni kurudisha HADHI ya waalimu katika jamii. Mwalimu anapashwa kuwa na hadhi sawa na daktari. That is the case in China. We can start by doubling or trebling the salaries of teachers. Inabidi tuanze sasa kutenga asilimia 27 - 30 ya bajeti iwe ya elimu. Na tufanye hivyo kweli, sio kudanganya hadharani kisha fedha hazitolewi. If you think education is expensive, try ignorance.

Ungekuwa una elimunzuri ungefahamu kuwa orodha ya vyou vikuu bora duniani hutolewa na taasisi nyingi tu sio hao 'times' peke yao. Kabla hujafikia conclusion ungetafuta orodha ya taasisi nyingine pia na pengine ungetambua vigezo vyao ni vipi. Usiwe kama wengine wanasema eti wahitimu hawajui kiingereza. Kuna wataalamu huko Japan hata maneno kumi ya kiingereza hana lakini hatari hao, usipime.Kufikiri na kufanya 'analysis' kuna hitaji weledi na sio papara kama hivi. Harvard, Stanford na Yale nivya ngapi katika hiyo list yenu?
 
natofautiana sana na Mzee LOWASA lakini kwenye maono yake ya elimu kuhusu taifa hili nampongeza sana. kama juzi alisema wazi yeye angeanza na walimu
Kwanini asisitize kuanza na walimu wakati jpm yeye kaanza na madawati na sizani kama anawaza maslahi bora ya Mwl
kwa nn nchi inashindwa kuwa angalia walimu sababu elimu bora inaanzia chini hapo ndo tutaweza kudumu
 
naona mmeshupalia udsm tu.mbona hamhoji hivyo vijivyuo uchwara vyenu?
 
Back
Top Bottom