Kiwanda cha bia TBL na kiwanda cha sigara havijawahi kuendeshwa kwa hasara. Actually hata kuna wakati Mwalimu alisema kuwa serikali ilikuwa inategemea zaidi kiwanda cha bia kwa fedha za matumizi yake. Tatizo la kiwanda cha bia lilikuwa ni management na si hasara. Bia ilikuwa haiivi na supply ilikuwa haikidhi demand. Actually walichofanya Makaburu baada ya akina Mwinyi kuwauzia ni wali flood soko la bia Tanzania na bia zao Castle, na hapo ndipo walipopata fedha za kukarabati mitambo ya TBL. Kaburu hakuweka hata senti tano ya Afrika kusini katika TBL wakati wa ubinafsishaji. Hii inaonyesha jinsi soko la bia Tanzania lilivyokuwa kubwa. Hata kama kilitoa kodi ya bilioni moja wakati huo. hakikuendeshwa kwa hasara na kilisaidia kuendeshea matumizi ya serikali na faida ilikuwa inaingizwa serikalini. Eniwei, umeshakumbatia uwekezaji na ubinafsishaji sitaki kukuondoa huko. Lakini ukweli hubaki pale pale.
Hilo ndio lilikuwa tatizo la mashirika mengi ya umma. Management, Bodi, na serikali kuingilia maamuzi ya bodi/management.
Mifano mizuri bado tunayo, TANESCO. Walipokuwa wanakuja NetGroup Solution, Management, Board na TUICO walipinga kwa nguvu zote mpaka wakamsomesha Waziri wa Nishati na Madini zama hizo Maokola Majogo na akawaelewa na kukubaliana na TANESCO kwamba NetGroup wasije. Mkapa alipoona home-boy wake Maokola Majogo ame-side na TANESCO, Majogo alitupwa ofisi ya Makamu wa Rais (Kuondoa Umasikini) akaletwa mwingine ili kuja kukamilisha deal. Kilichoendelea wote tunajua, na hata Richmond nayo hivyo hivyo, ni serikali kuilingilia kila kitu.
TPA na wao hawakuachwa, kuna siku DG wa TPA nimesahau jina lake, alimwambia Mkapa wakiwa Mtwara, kwamba kama yeye (DG wa TPA) angepewa mamlaka ambayo wanapewa wageni ya kufanya maamuzi bila kuingiliwa, ana uhakika TPA ingekuwa mbali. Tatizo la mashirika mengi ya umma, kila unachofanya lazima kipate approval kutoka wizarani, na huko wizarani wanaangalia kwanza maslahi. Hilo ndilo lililikuwa kikwazo kwa mashirika mengi sana. Utahangaa GM au DG yule yule aliyekuwa anaongoza shirika kwa hasara, once likibinafsishwa kampuni inaanza kutengeneza faida, hakuna cha kuongeza mtaji wala nini, na si ajabu hata teknolojia ni ile ile.