Ubalozi wetu Pretoria una simu moja tu ya reception bila extension?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Jamani, leo nimeona comment kwenye Mwananchi nimeshangaa sana. Kulikuwa na comment kwamba balozi zetu za nje zipo kwa ajili ya kuomba misaada na kuratibu ziara za viongozi wa serikali katika nchi hizo, sio kusaidia Watanzania wanaokwama wakiwa nje. Ikatajwa kwamba ubalozi wetu wa Afrika Kusini pale Pretoria una simu moja tu ya reception, ukipiga simu kuhitaji msaada wa mtumishi fulani wa ubalozi unaambiwa wana simu moja tu ya mapokezi, acha namba yako watamwambia akupigie, na wala hawakupigii tena. Nashindwa kuelewa inakuwaje kwa wafanyabiashara wa Afrika kusini wakitaka habari toka ubalozi wanajisikiaje wakiambiwa hivi.

Mlioko Afrika Kusini hebu tuthibitishieni hili. Na kama una experience za huduma mbovu za balozi zetu hebu tueleze mambo yaliyokupata.
 
Back
Top Bottom