Ubalozi China wagomea Risala kwa Kikwete

Nimeiona na kuisoma hiyo risala. Kimsingi ina mambo mengi ya maana kama unazungumzia ukweli wa jumla na ujumla wa mzungumzaji (yaani isingekuwa imetoka specifically kwa wanafunzi wenye mahitaji yao maalum kama wanafunzi). Lakini kama ni matumizi bora ya fursa (namaanisha rational utilization of opportunities, neno "rational" badala ya "bora" sina kiswahili chake), wanafunzi hapa walihitaji ushauri zaidi. Nasema hivyo kwa maana kuwa fursa ya kukutana na rais ingefaa wao kuyatatua yale immediate issues zinazowakwaza kimasomo, kama hayo ya upungufu wa hela, matatizo ya matibabu, mahitaji ya kompyuta nk, sasa hayo mengine ya EPA na Richmond wangeweza kumwandikia na kumtumia kwa njia ya posta. Unapomdai mkubwa haki fulani, unaweza kuchomeka siasa kidogo kumuonesha una taarifa na uko pamoja nae katika jitihada za kujenga nchi, lakini usizidishe sana hadi ukaonekana kuwa hoja yako ni kumpinga huyo unayemtaka akupatie unachodai. Naona hawa wadogo zangu (na wengine wanangu) wamezidisha pilipili sasa chakula kikawa hakiliki! Ukichukua hii risala, ukafuta kichwa cha habari na kuwakabidhi watu 10, ukawaambia kila mmoja atoe maudhui au hoja kuu ya risala hiyo unadhani wangesema ni nini? Mahitaji yao halisi hawa vijana wameyafanya yakafunikwa na hoja za ufisadi ambazo kuna watu wengine wenye nafasi zaidi ya kupambana nazo kuliko hao wanafunzi, tupo sisi, wabunge wazuri tu kina Mwakyembe, Slaa, Zitto, Kilango na wengine, nk nk, ndio mgawanyo wa kazi, sasa wadogo zetu hawa wanataka wamalize kila kitu kwenye risala moja?

Ninapingana na uamuzi wa ubalozi kuwazuia kusoma risala hiyo. Badala yake wangewashauri tu jinsi ya kuiweka vizuri (unless wamepewa ushauri huo wakakataa), au wangewaonesha maneno wanayoona hayapendezi. Sasa ikitokea kuwa hayo maeneo ubalozi unayokataa ndio maslahi halisi ya wanafunzi, basi hapo ndio wasaa wa kupiga kelele, na kumuwahishia Field Marshal ES amfikishie muungwana. Risala hii kama ilivyo kwa sasa inafanana na hotuba anayosoma mtu dhidi ya mpinzani wake wa kisiasa, mfano unapomhoji rais kuhusu ajira milioni 1 alizoahidi, sasa sijui ndio unamsuta au ni nini? Na hapo hapo unamwomba akuongezee fedha za kujikimu nk, sasa wewe kipaumbele chako kipi, uongezewe hela za kujikimu au rais atimize ahadi yake ya ajira milioni 1? Vipaumbele, na matumizi rational ya fursa mbalimbali (kama hii waliyopata ya kukutana na mkulu) ndio vinavyowaangusha hawa vijana.

Mkuu mimi sijaiona lakini kama ilikuwa inauliza mambo ya EPA na RICHMOND sion tatizo, tabaka la wasomi ndo wanaitaji kuoji zaidi mnakata haoji nani kama sio wasomi, wale sio watoto wa shule ya msingi na sekondari, ni watu wazima wana haki ya kujua kinachoendelea kwenye nchi yao.
Hili tatizo mkuu la wasomi wetu kukaa kimya ndo linamaliza vyuo vyetu vikuu, haviwezi kuoji kitu siku tofauti na zamani wasomi wa mlimani wakioji watu wakawaida wanafurahi kuwa wamewakilishwa na chuo chao.
 
mi sishangai saana, unyanyasaji wa ndugu zetu waliopo vyuo vya nje ni mkubwa sana. ukikumbuka waliofanyiwa wale wa ukraine utalia, inaniuma sana kwani ilibaki kidogo nami niwe mhanga.

siku mnyonge akichoka,dunia haitakalika
 
Ingekuwa ni vigumu kwa balozi yeyote kukubali hii risala isomwe mbele ya Raisi, lets be realistic. Nani anayependa kuona kitumbua chake kinatiwa changa na vitoto vya shule?
KATOTO CHA MZUNGU{kana ka nsungu}ni kweli kabisa hakuna ambaye angekubali hii ilikuwa ni noma ila tusubiri kama mwanaforum aliyesema atapeleka kwa jk.
 
Nimeiona na kuisoma hiyo risala. Kimsingi ina mambo mengi ya maana kama unazungumzia ukweli wa jumla na ujumla wa mzungumzaji (yaani isingekuwa imetoka specifically kwa wanafunzi wenye mahitaji yao maalum kama wanafunzi). Lakini kama ni matumizi bora ya fursa (namaanisha rational utilization of opportunities, neno "rational" badala ya "bora" sina kiswahili chake), wanafunzi hapa walihitaji ushauri zaidi. Nasema hivyo kwa maana kuwa fursa ya kukutana na rais ingefaa wao kuyatatua yale immediate issues zinazowakwaza kimasomo, kama hayo ya upungufu wa hela, matatizo ya matibabu, mahitaji ya kompyuta nk, sasa hayo mengine ya EPA na Richmond wangeweza kumwandikia na kumtumia kwa njia ya posta. Unapomdai mkubwa haki fulani, unaweza kuchomeka siasa kidogo kumuonesha una taarifa na uko pamoja nae katika jitihada za kujenga nchi, lakini usizidishe sana hadi ukaonekana kuwa hoja yako ni kumpinga huyo unayemtaka akupatie unachodai. Naona hawa wadogo zangu (na wengine wanangu) wamezidisha pilipili sasa chakula kikawa hakiliki! Ukichukua hii risala, ukafuta kichwa cha habari na kuwakabidhi watu 10, ukawaambia kila mmoja atoe maudhui au hoja kuu ya risala hiyo unadhani wangesema ni nini? Mahitaji yao halisi hawa vijana wameyafanya yakafunikwa na hoja za ufisadi ambazo kuna watu wengine wenye nafasi zaidi ya kupambana nazo kuliko hao wanafunzi, tupo sisi, wabunge wazuri tu kina Mwakyembe, Slaa, Zitto, Kilango na wengine, nk nk, ndio mgawanyo wa kazi, sasa wadogo zetu hawa wanataka wamalize kila kitu kwenye risala moja?


Ndugu kithuku:
unasema kwamba wanafunzi wangeitumia nafasi hiyo kutatua zile immediate issue zinazowakwaza kimasomo, umesema kama vile vitabu, kompyuta ,upungufu wa hela, na matibabu. hebu nikuulize ndugu kithuku, kama raisi au serikali itatimiza hizo immediate needs za hao wanafunzi je sivyema wanafunzi kuhoji mustakbali wa taifa lao?.

Ni nani anayepaswa kutoa majibu ya matatizo ya nchi husika vizuri zaidi kuliko mkuu wa nchi husika?

tatizo ni kwamba tunawaangalia wanafunzi kama watoto wadogo, hata kama wapo katika vyuo vikuu, nasikitika kwamba maadam mtu anaitwa mwanafunzi basi hisia za kwanza zinazokuja katika mawazo ya baadhi ya watu ni kwamba hao wanafunzi ni watu wasioweza kufanya maamuzi ya kujitegemea. ifahamike china kuna wanafunzi kuanzia wale wa degree ya kwanza mpaka p.h.d, lakini eti wote hawa kuhoji kuhusu hali halisi ya taifa lao ndugu kithuku unahisi wamekosea.

Kithuku unasema kazi ya kuhoji kuhusu mambo ya EPA tuwaachie kina zitto, na Mwakyembe!!!, kweli?.mimi ninadhani jukumu la kuhoji suala la EPA ni la watanzania wote wakiwemo hao wanafunzi wa China. hili suala si la chama cha upinzani wala la CCM hili ni suala la watanzania wote.

Laiti hii risala ingekuwa na ujumbe wa kumsifu kikwete kuhusu kukubali kujiuzulu kwa lowasa na hatimaye kuvunja baraza la mawziri, au ingekuwa ina zungumzia jinsi alivyounda tume ya madini, au jinsi alivyofanikisha ziara ya george bila kugusia masuala ya richmond na EPA sidhani kama ubalozi wangeizuia!

Lakini kwa nini ubalozi wawazuie watanzania kumweleza raisi kero zao?. kwa nini wao waone kwamba kumwambia raisi kero zao kupitia risala ni vibaya?.

Mimi na wewe ndugu kithuku tunaongea haya kupitia kwenye mtandao,lakini wanafunzi wameamua kwenda one step further kumweleza mkuu kero zao kama wananchi live, ndugu yangu unahisi kwamba hawajashauriwa vyema?.

Mimi ninadhani kwamba popote pale hata kama ni chuo kikuu cha mlimani wanafunzi wa kitanzania wakipatiwa nafasi nzuri, watamtwanga Muungwana hoja hizo hizo za richmond na EPA.

JUKUMU LA KUPAMBANA NA UFISADI SIYO LA GAMBA LA NYOKA AU ZITTO AU MWAKYEMBE PEKEE, NI JUKUMU LA WATANZANIA WOTE POPOTE PALE WALIPO KAMA SAUTI ZAO ZITASIKIKA BASI HAWANA BUDI KUZITOA!.
 
Ingekuwa ni vigumu kwa balozi yeyote kukubali hii risala isomwe mbele ya Raisi, lets be realistic. Nani anayependa kuona kitumbua chake kinatiwa changa na vitoto vya shule?

hivi, wanaosoma china wote ni watoto!! anyway, risala ilikua a bit too strong.madenti wana jazba kidogo but its understandable, thats what u get when you corner a cat(simaanishi hao madenti ni cats).ishu kama ya EPA si kesi inaandaliwa jamani, na ishu ya shule za msingi vijijini, its hard zile shule zikalingana na za China au zikawa kama za private za tizii.kauchumi kadogo afu ukiplus na mafisadi basi ndo balaa.

Many words were not chosen carefully.Kuna maneno huwezi kuyatumia kwenye speech.Lakini messages zipo, tena zipo clear.wahusika wawajibishwe, hakuna kitu kibaya kama unyanyasike ughaibuni kwa kukosa pesa.Afu bora nchi za west madenti huwa wanapata kazi za kujishkiza, china box halibebeki, wenyewe tu wapo teele
 
Ahsante saana HuXiang na wachangiaji wotee
Kwanza kabisa nikuwa nawaomba wakuu HuXiang na wengine munapotumia hayo maneno ya kichina munafanya baadhi wasielewe mwakusudia nini,nimejaribu kutafsiri haya machache ila mkiweka mengine ni vema kuyatafsiri.
1.mian tiao=nodles
2.du lo jie=duo lo street
3.jiao 10=senti 10 RMB(YUAN)
4.chao fan=fried rice
5.dou fu=eggplants(BILINGANI)

.Anyway,si vema kurudiarudia yaliokwisha eleza ila huyu mama nastahiki kuwa fired kutokana na dhuluma anazotufanyia wanafunzi,yaani tunaishi kama wapweke ,nina matukio kadhaa ya kuongezea.

.Kuna MD students mmoja wa EASTCHINA medical University kaibiwa laptop,pesa etc bwenini kwake,kwa mujibu taratibu za ulinzi wa foreign students residents huu ni uzembe ambao university husika yapaswa kulipa maana vimeibiwa chumbai during class hours na hakuna security camera,huyu victim alipoomba msaada ubalozini hakuna hata alichosaidiwa even kumpa pole sijui kama walifanya.Ila naamini kama balozi zingine zinazojali watu wao hizi Chinez zingelipa.


.Kuna ndugu mwingine Huazhong University- Wuhan,kapata ajali ya pikipiki,huyu ilipaswa asaidiwe na University kugharamia matibabu kwa sababu tuna bima ,shule ikaleta ugumu kidogo,akaomba msaada ubalozini akaambiwa mumeambiwa musi drive-OK,for precautions huenda kuto drive ni bora zaidi ila ndio limeshatokea tayari,na katika sheria za hiyo bima hakuna kipengele kama hicho.

Hapo nimeonesha kila kitu twawaambia ubalozi ni kutokana na nature ya wachina,mara nyingi wakiona issue complicated kidogo tu huwa wanataka comments from ubalozi.Nilisikia huko HUNAN wanafunzi walihitaji ubalozi wapige simu chuoni ili wasainiwe forms za mkopo.


.Huyu Mama alishawahi kutujibia kwa wizara ya elimu ya juu kuwa wanafunzi wa schorlaship hatuhitaji nyongeza ya pesa za mkopo maana hizi tunazopewa zatosha kabisa hali ya kuwa watu twapiga pasi ndefu ama kushindia mian tiao.



Nasisitiza ombi letu la computer,kama wanahisi kuwa twahitaji pesa basi watuletee complete set,maana huku major kila kitu ni computer,internet,,-sijui ndio huko kuendelea China maana wanatunyanyasa sana sisi watoto wa wakulima,yaani timetable,notes,matangazo,recommended books ni katika NET tu,even ku submit reports kwa proffesor,pia yawasaidia saana wale wanaosoma kwa kichina kufanya translation kwa kutumia softwares.Yashangaza saana au sijui huyu mama kakalia hizo pesa?maana hili lilitiwa baraka na mheshimiwa balozi na kuthibitisha kuwa hata yeye watotowake ilibidi awanunulie,na ali promise kuwa atalifiksha rasmi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom